Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Kwa nini Tanzania bado ni Taifa masikini Duniani?

    Report Post
    Results 1 to 17 of 17
    1. #1
      Kabaridi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 15th November 2011
      Location : Laikipia
      Posts : 1,758
      Rep Power : 699
      Likes Received
      462
      Likes Given
      591

      Default Kwa nini Tanzania bado ni Taifa masikini Duniani?

      WIKI kadhaa zilizopita nilialikwa katika mkutano wa vijana uliofanyika Arusha, ambako nilikwenda kama mzungumzaji.

      Katika mazungumzo yetu, kijana mmoja aliuliza swali kuhusu sababu za Tanzania kuendelea kuwa taifa masikini.

      Bila shaka hata wewe unayesoma makala haya, ni kati ya Watanzania ambao wamekuwa wakijiuliza; kwa nini Taifa hili bado ni duni? Achilia mbali Tanzania bara ambalo ni eneo kubwa, vipi kuhusu eneo dogo kama Zanzibar?

      Unakuta eneo fulani lina utitiri wa viongozi kuanzia balozi wa nyumba kumi, Mwenyekiti wa Serikali za Mtaa, Mtendaji wa Kata, Diwani, Mbunge, Mkuu wa Wilaya, Mkuu wa Mkoa, Mwenyekiti wa Halmashauri na viongozi wengine, lakini bado eneo linaendelea kuwa duni. Tatizo ni nini?

      Hivi ni kwa nini maeneo mengi ya Zanzibar kasi ya wasio na ajira ni kubwa, wakati kisiwa hicho kikiwa na wakazi wachache? Ni swali ambalo kila mwenye akili timamu anaweza kujiuliza.

      Hata Tanzania bara, bado tunaweza kuendelea kujiuliza kwa nini hali ya maisha ya walio wengi ni duni wakati tumekuwa tukiahidiwa mengi hasa nyakati za kampeni?

      Nafikiri shida kubwa iliyoko Tanzania ni kushindwa kuthubutu; kuna Watanzania wengi ambao hawajiamini kuanzisha mambo.

      Kwa mfano, wahitimu wengi wanafikiri kilicho muhimu kwao ni kuajiriwa. Mtu anaweza kusomea sheria, lakini yuko tayari kufanya kazi hata ya kuuza duka kwa sababu ndio kazi aliyopata ya kuajiriwa.

      Wengi wanafikiri kuajiriwa ndio maisha lakini tafiti mbalimbali zinaeleza kuwa watu ambao maisha yako yote wanategemea ajira, ndio ambao hufa wakiwa maskini.

      Kwa nini? Nakubaliana na hili kwani ni ukweli kuwa baada ya kumaliza ajira, kinachofuatia ni kupewa posho zako na kurudi nyumbani. Hakuna njia nyingine ya kuweza kuishi zaidi ya kusubiri kifo, huku ukila mafao yako.

      Hata kama wewe ni Mbunge, Mkuu wa Wilaya au Mkuu wa Mkoa, kazi hiyo bado haina chochote kama hutakuwa na kitu kingine cha kufanya.

      Kuna watu ambao walikuwa wakuu wa wilaya, leo hii wanafanya biashara ya mama ntilie. Kuna watu walikuwa wana fedha, leo hii hata nauli ya daladala kwenda huku na kule ni shida.

      Ndugu yangu ni lazima kuwa makini na kufikiria kuanzisha miradi yenye maana. Miradi mizuri zaidi, miradi ambayo inaweza kweli kusaidia kukufanya kuwa na mafanikio zaidi.

      Ni vigumu kufikiri kwamba unaweza kuwa na maendeleo makubwa, ikiwa fikra zako za aina ya miradi ni kuhusu miradi yenye kukuletea mafanikio madogo.

      Ni kwamba unaweza kuanza kwa miradi yenye fedha ndogo, nikimaanisha kwamba anzisha mradi kulingana na fedha ulizonazo, lakini lililo la msingi ni kuangalia aina ya miradi ambayo inaweza kuleta mafanikio makubwa zaidi mbele.

      Ninachotaka kueleza hapa ni kwamba sababu kubwa ya Tanzania kuendelea kuwa maskini ni wananchi wenyewe kutokuwa na uelewa wa nini ambacho wanatakiwa kufanya ili kuwa na maendeleo. Katika hili inawezekana hata walio madarakani nao hawakuwa na uelewa juu ya hilo.

      Hata baada ya baadhi ya viongozi kuanza kufahamu umuhimu wa namna ya kuwafanya wananchi kuwa na maendeleo ya haraka, wengi walishindwa kufanya mikakati hiyo kwa staili inayotakiwa.

      Uongozi usiofaa au viongozi wasiofaa, kwa maana ya kuwa na watu ambao wanashindwa kuwaendeleza wengi, ni kati ya sababu za msingi za kudumaa kwetu kimaendeleo.

      Kwa nini tumsifie mwalimu kuwa anajua kufundisha ikiwa idadi kubwa ya wanafunzi wake wanafeli mitihani?

      Hata kama labda mtoto mwenyewe anayefundishwa, kichwani anasumbuliwa na kero nyingi na kusababisha ashindwe kusoma vizuri, bado hatuwezi kusahau mchango wa mwalimu kwa kufeli mwanafunzi huyo.

      Ndiyo maana nasema kwamba umasikini unaoendelea Tanzania unachangiwa na viongozi wasio na huruma na wananchi. Hawana mikakati mahsusi katika kusaidia maendeleo katika maeneo wanayoyaongoza.

      Aidha, Watanzania wengi bado ni wazito katika kupambanua mambo. Msingi hasa wa kuwa na maendeleo ni pamoja na kutokuwa na urafiki wa kudumu au uadui wa kudumu na wanasiasa.Mataifa mengi yaliyoendelea tabia zao ni kwamba hawana urafiki wa kudumu wala uadui wa kudumu.

      Kwa mfano, kinachoendelea Zanzibar sio sahihi hata kidogo, kwamba kila uchaguzi, ni lazima kuona Pemba inachukuliwa na CUF, Unguja inachukuliwa zaidi na CCM. Au hata kwa Tanzania bara, ni makosa mno kukubali kuendelea kukipigia kura chama fulani miaka nenda miaka rudi.

      kwa mfano, kama katika uchaguzi uliopita ulikipigia kura Chadema, TLP au CCM, ni muhimu katika uchaguzi ujao, kumpima kiongozi alifanya nini kabla ya kupiga kura yako.

      Kama hajafanya chochote, hakuna sababu ya kukipigia kura wala kumpigia kura mgombea wake ambaye ameshindwa kutekeleza ahadi alizotoa katika uchaguzi uliopita.

      Chanzo: hapa


    2. FemaTV & Radio

    3. tz1
      #2
      tz1's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 19th March 2011
      Posts : 2,048
      Rep Power : 827
      Likes Received
      406
      Likes Given
      317

      Default Re: Kwa nini Tanzania bado ni Taifa masikini Duniani?

      kibaridi mbona umejijibu swali lako.
      hatuna cha kuchangia.
      [email protected]

    4. #3
      mwanapolo's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 29th March 2011
      Location : Mererani, Manyara
      Posts : 184
      Rep Power : 448
      Likes Received
      41
      Likes Given
      8

      Default Re: Kwa nini Tanzania bado ni Taifa masikini Duniani?

      Heading ingekuwa "Sababu ya watz na tz kuwa masikini" ingeleta maana ya stori nzima

    5. #4
      cmoney's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 14th October 2011
      Posts : 363
      Rep Power : 456
      Likes Received
      73
      Likes Given
      51

      Default Re: Kwa nini Tanzania bado ni Taifa masikini Duniani?

      dah imeni-touch kweli

    6. #5
      Hute's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 25th November 2010
      Posts : 1,402
      Rep Power : 710
      Likes Received
      354
      Likes Given
      23

      Default Re: Kwa nini Tanzania bado ni Taifa masikini Duniani?

      kwani sababu ya wakenya kuwa masikini nin nini...wakenya mbona mbunye sana hawa, yaani umasikini wa machokoraa kula majalalani, umasikini wa wapwani waliowatenga hadi leo wanataka kujingátua, umasikini wa maeneo yote isipokuwa nairobi hauoni, anakuja kutuchunguza sisi wabongo...haujauona umasikini wenu? nyine wakenya mnaangalia vya wenzenu tu kumba madudu ya kwenu hamyaoni...nyani haoni kundule...akili kubwa ya mkenya huwa anajiona yeye nchi yake imeendelea sana, nchi yake ni tajiri, nchi zingine ni masikini...ni ujinga wa kupindukia,,,hata mjusi au kenge angebadilishwa kuwa mkenya, asingekuwa na akili kama za hawa nyangáu....after all, huwa nafurahia kuwatungua kwa risasi pindi tunapowawinda kama majambazi wakija kwetu arusha kuhemea....majambazi wakubwa nyie...
      Bantugbro and NDINDA like this.
      Kama huna meno,usile bisi, kula Bwimbwi yaani kimbugi. Uongozi ukikushinda waachie wanaoweza!

    7. Miaka 50

    8. #6
      Kabaridi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 15th November 2011
      Location : Laikipia
      Posts : 1,758
      Rep Power : 699
      Likes Received
      462
      Likes Given
      591

      Default Re: Kwa nini Tanzania bado ni Taifa masikini Duniani?

      Watz niliweka makali hii ili tuangalie kwanini umaskini unazidi Afrika mashariki. Hute munasema eti CCM ndio jinamizi inayoila TZ na kueneza/kusambaa haraka kwa umaskini. Mimi naona hii dhana ni kinyume. Alivosema Mw. Nyerere, mungu amlinde peponi, kila mkenya ni "nyangau" na lazima atupiwe macho/darubini. Hii ndio "mindset" ambao inaila Tz kama cancer. Mtz amesalia tu kuona mtu ambaye hana uraia wa tz kama "nyangau"

      ..........kwanza Kwa nini tusiseme umaskini tz /umeenea kwa kukosa ushirikiano, hasa katika misingi za elimu/kusawazisha/kustandardize, kuboresha/privatization ya usambazaji wa huduma muhimu ambazo serikali ya siku inshindwa kutekeleza. Hapo ndipo private sector huingilia kuziba ufa. Mbona tusiwaachie waafrika nafasi bila kujali uraia wake, maana tunaotegemea wazungu, tumegundua ni wanyonyaji. Waganda hapa wanapiga watz bao ikija kwa masuala ya kushirikiana au kuiga miradi ya maendeleo. Mimi sikutaka tujadili mengi lakini kuna sehemu ambayo inahuzunisha.

      Baada ya jubilee, bado waliohitimu wameshindwa kupata ajira kutokana na mafunzo waliopata vyuo vikuu..........Mtu ambaye ana shahada la sheria, anaingilia kazi ya kuuza dukani....Swali ni alienda chuoni kupokea shahada kwa lengo gani? .............Afadhali angetumia pesa hizo katika matumizi mengine, labda akanunue shamba na mifugo ya kulea.................. Hii picha ina maanisha nini kwa kuzingatia umoja wa EAC?


    9. #7
      Hute's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 25th November 2010
      Posts : 1,402
      Rep Power : 710
      Likes Received
      354
      Likes Given
      23

      Default Re: Kwa nini Tanzania bado ni Taifa masikini Duniani?

      the point is, wewe masikini na chokoraa wa kenya, una ubavu gani kuja kujadili umasikini wa tz wakati umasikini wa kwako umeuacha kule kenya?....ondoa kamasi zako hapa, hua point....shughulikia matatizo yako kwanza, ndio uje kwa haya ya kwetu kama bado yatakuwepo.......
      Kama huna meno,usile bisi, kula Bwimbwi yaani kimbugi. Uongozi ukikushinda waachie wanaoweza!

    10. #8
      Nairoberry's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 7th March 2012
      Posts : 546
      Rep Power : 472
      Likes Received
      176
      Likes Given
      1

      Default Re: Kwa nini Tanzania bado ni Taifa masikini Duniani?

      heheheh kabaridi umewaweza huyu hute ni jangili tu
      janjez likes this.

    11. #9
      Bantugbro's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 22nd February 2009
      Posts : 2,409
      Rep Power : 1002
      Likes Received
      487
      Likes Given
      1490

      Default Re: Kwa nini Tanzania bado ni Taifa masikini Duniani?

      Quote By Kabaridi
      WIKI kadhaa zilizopita nilialikwa katika mkutano wa vijana uliofanyika Arusha, ambako nilikwenda kama mzungumzaji.
      Chanzo: hapa
      Kabaridi acha uchokozi, tafadhali nenda ukaimarishe ile sub-forum mpya tuliyowatengenezea...
      Chamoto, Askari Kanzu and Kabaridi like this.
      Just because presidents screws around, it doesn't make a president for screwing around..

    12. #10
      Kabaridi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 15th November 2011
      Location : Laikipia
      Posts : 1,758
      Rep Power : 699
      Likes Received
      462
      Likes Given
      591

      Default Re: Kwa nini Tanzania bado ni Taifa masikini Duniani?

      Quote By Bantugbro
      Kabaridi acha uchokozi, tafadhali nenda ukaimarishe ile sub-forum mpya tuliyowatengenezea...
      Bantugbro, huu si uchokozi....Ni hali ya kujaribu kujadili kiustarabu..Na niseme wazi mijadala kama hii huaribiwa na watu wasio na hoja...Nitaweka makala ya umaskini kenya baada ya uzi huu...lakini kwanza wacha tujadili TZ.


    13. #11
      Kabaridi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 15th November 2011
      Location : Laikipia
      Posts : 1,758
      Rep Power : 699
      Likes Received
      462
      Likes Given
      591

      Default Re: Kwa nini Tanzania bado ni Taifa masikini Duniani?

      Quote By Hute
      the point is, wewe masikini na chokoraa wa kenya, una ubavu gani kuja kujadili umasikini wa tz wakati umasikini wa kwako umeuacha kule kenya?....ondoa kamasi zako hapa, hua point....shughulikia matatizo yako kwanza, ndio uje kwa haya ya kwetu kama bado yatakuwepo.......
      Hute wewe ni mmoja wa watz ambao munadhihirisha uzalendo thabiti lakini ambao haujakomaa...Kuna pointi ambazo tunaeza jifunza na siyo kujaribu tu kuharibu mijadala...This is a very weak character kutoka kwako na naomba kuwa baadhi ya watu kama ninyi tz ni wachache.


    14. #12
      Bantugbro's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 22nd February 2009
      Posts : 2,409
      Rep Power : 1002
      Likes Received
      487
      Likes Given
      1490

      Default Re: Kwa nini Tanzania bado ni Taifa masikini Duniani?

      Quote By Kabaridi
      Bantugbro, huu si uchokozi....Ni hali ya kujaribu kujadili kiustarabu..Na niseme wazi mijadala kama hii huaribiwa na watu wasio na hoja...Nitaweka makala ya umaskini kenya baada ya uzi huu...lakini kwanza wacha tujadili TZ.
      Haya Mkuu, tunasubiri uweke hiyo ya umaskini wa Kenya maana hii ya TZ haina wachangiaji wengi.
      Just because presidents screws around, it doesn't make a president for screwing around..

    15. #13
      mtotowamjini's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 23rd April 2012
      Location : None of Your Business
      Posts : 4,531
      Rep Power : 1262
      Likes Received
      1109
      Likes Given
      28

      Default Re: Kwa nini Tanzania bado ni Taifa masikini Duniani?

      tatizo watanzania wengi hasa wa vijijini bado hawajaelimishwa vizuri kujua haki yao ya kimsingi. Tumeshazoea uonevu na kukubali kila kitu tunachoambiwa. Mtu anaona yeye kwa vile ni ccm basi lazima uchaguzi ampe kura ccm au chadema hivyo hivyo. Nchi za ulaya utakuta mtu ni mwanachama wa chama fulani lakini wakati wa uchaguzi kama anamuona mgombea wa chama chake hafai basi atachagua mgombea wa chama kingine ambae anamuona anafaa. Hiyo kitu inabidi iingie kwenye akili ya watanzania kutumia haki yao ya kupiga kura vizuri na waache kulainishwa na baiskeli,khanga na shs 10000
      Every saint has a past, every sinner has a future' ...Oscar Wilde

      One man's good fortune is another man's misfortune


    16. #14
      Smatta's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 5th November 2008
      Location : NAIROBBERY
      Posts : 1,744
      Rep Power : 885
      Likes Received
      261
      Likes Given
      568

      Default Re: Kwa nini Tanzania bado ni Taifa masikini Duniani?

      Watanzania warudi shule tu, hiyo ndio dawa ya kupunguza umaskini.
      Bukyanagandi likes this.
      Daima Mimi Mkenya, Mwananchi Mzalendo.

    17. #15
      Smatta's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 5th November 2008
      Location : NAIROBBERY
      Posts : 1,744
      Rep Power : 885
      Likes Received
      261
      Likes Given
      568

      Default Re: Kwa nini Tanzania bado ni Taifa masikini Duniani?

      na hatutaki hio sub forum ya Kenya, if we want to discuss issues with Kenya we post at Kenyan sites, hapa jf tunataka kujadili na watanzania. kama mnatufukuza mtupatie permanent ban, hii yakutufukuza polepole hatutakubali
      Bantugbro and Bukyanagandi like this.
      Daima Mimi Mkenya, Mwananchi Mzalendo.

    18. #16
      adolay's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 8th December 2011
      Posts : 1,635
      Rep Power : 771
      Likes Received
      490
      Likes Given
      498

      Default Re: Kwa nini Tanzania bado ni Taifa masikini Duniani?

      Kwanza tuna viongozi :-
      1. Wasio na uchu wa maendeleo
      ukiachia mbali mwl nyerere na mzee ruksa, kuanzia kipindi cha mkapa tumekuwa na janga la kitaifa. Kwa kuwa na viongozi wafanya biashara na wanajikuta kushindwa kuwachukulia hatua wa chini yao kwa hofu ya kuanikwa mazambi yao.

      Matokeo yake wote wanakuwa wezi kuanzia juu mpaka chini, makusanyo ya kodi na kila kitu wanajimilikisha- serikari inakosa fedha.

      2. Viongozi wasio na vision wala mikakati ya dhati kuwakombowa watz, mkukuta, mkurabita, kilimo kwanza, wizi tu!!

      3. Hawako teyari kuiamsha, kuielimisha na kuindeleza jamii.

    19. #17
      Bukyanagandi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 24th June 2009
      Location : DSM
      Posts : 1,948
      Rep Power : 920
      Likes Received
      704
      Likes Given
      1475

      Default Re: Kwa nini Tanzania bado ni Taifa masikini Duniani?

      Quote By Hute
      the point is, wewe masikini na chokoraa wa kenya, una ubavu gani kuja kujadili umasikini wa tz wakati umasikini wa kwako umeuacha kule kenya?....ondoa kamasi zako hapa, hua point....shughulikia matatizo yako kwanza, ndio uje kwa haya ya kwetu kama bado yatakuwepo.......
      Mkuu wala husipoteze muda kujadiliana nao maswala ambayo yako obvious, si rahisi kubadirisha mind set za baadhi yao. Mkuu, baadhi ya hawa jamaa wana malengo fulani katika forum hii na wako well organized, wanafikili wakisema sema Tanzania basi hilo tu litatufanya tubadirishe misimamo yetu thabiti kuhusu certain issues ambazo wanaona tulisha washtukia siku nyingi na siku hizi tumewazidi kete, wanatuona kero kweli kweli. Kuikasikilia TANZANIA kunatokana na msimamo wetu huo wa kukataa shotgun wedding ya Federation vile vile na kutokubali ku-sign an open ended clauses zilizo wekwa kimaksudi kula kwetu.

      Nilisha sema siku nyingi tu kwamba TANZANIA ni nchi huru - nyie fanyeni mambo yenu huko kwenu na wala sidhani kama kuna Mtanzania yeyote in his/her right mind anayeweza kuwa-bothered na mambo mnayo yafanya HUKO kwenu; mkitaka tubadilishane mawazo kwa heshima tutawasikiliza lakini mkileta mambo ya ukoloni ya kufikilia Watanzania ni shambaboy tutawapa wakati mgumu kweli kweli. Mkituomba msaada kwa kuheshimiana tutawapa, mifano tunayo:

      * CHAKULA wakati wa baa la njaa nchini mwenu mwaka jana - hiyo ndio maana alisi ya ujirani mwema, siyo ujirani wa hila.

      * Rais Jakaya Kikwete alipo tumia busara zake kuwasuluhisha wakati wa mapigano ya wenyewe kwa wenyewe - je kama ingekuwa Tanzania mgetoa usuluhishi wowote kweli?

      Back to the point, Mkuu we soma post yake No6 para No.2 ndiyo utagunduwa lengo lake lilikuwa ni nini hasa, kumbuka kahanzia mbali kwa ku-quote gazeti fulani; baadae kabisa ndiyo ka andika ya kwake-mambo mengine aliyo andika yalikuwa ni kupoteza lengo tu, madhumuni yake hasa hasa ni hayo aliyo andika paragraph No.2 post No.6-jamaa huyu yuko hell bent kuikandia Tanzanai-and 4what reason one may ask?

      East Africa kuna nchi zaidi ya TANO na nyingine zinataka kujiunga, chukulia mfano wa nchi kama Uganda, Rwanda, Burundi na wale wengine ambao wanataka kujiunga na Africa Mashariki, katika nchi hizi zote tajwa hakuna nchi yoyote ambayo ina some kind of deluded axe-to-grind with TANZANIA zaidi ya baadhi ya raia wa Kenya - nimesema baadhi (some) sio wote, yaani chuki za baadhi yao mtu unaweza kufikili TANZANIA iliwahi kupigana vita na Kenya!

      Mwisho, labda nisema mimi nimepata bahati ya kutembela nchi yenu na kuona kila kitu, leo hii nikimuona MKenya yeyote anaicheka/kubeza TANZANIA kuhusu umasikini ntamshangaa sana, nyiyi mna kitu gani cha kujivunia kuhusu kujali raia wenu masiki wa kutupwa; mimi nafikili ulipitiwa kidogo you didn't mean IT, kwa sababu tukianza kuchambua nulicho kiona huko kwenu KENYA hapa patakua hapakaliki nimeamua kumezea tu.

      Leteni mambo ya kujenga kwenye FORUM hii na sio ridiculous rhetoric ambazo hazisadii chochote Tanzania, Kenya au wana JF, mimi binafsi sipendi mambo ya kutuniana misuri kama wendawazimu.
      Last edited by Bukyanagandi; 12th June 2012 at 01:17. Reason: God forgives I don't!!
      Kabaridi likes this.

    20. Study Abroad

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...