Wana JF,
Taarifa nilizozipata muda si mrefu zinasema kwamba mwanamuziki mwimbaji maarufu wa muziki wa dansi Ally Pugi amefariki dunia usiku wa kuamkia jana (12/6/2010) huko Morogoro alikokuwa amekwenda kusalimia ndugu zake. Marehemu Ally ambaye mpaka wakati kifo kinamkuta alikuwa mwimbaji wa bendi ya BRC (Bendi ambayo uwa inatumbuiza pale Port View siku ya Ijumaa) alikuwa akifanya shughuli za Muziki huko nchini Botswana kabla ya kujiunga na BRC January 2009. Marehemu Ally tayari amezikwa huko huko Morogoro.
RIP Ally.
Tiba

Reply With Quote


Follow Us Here