Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Bakwata yaishtukia serikali

    Report Post
    Page 1 of 3 123 LastLast
    Results 1 to 20 of 41
    1. Ami is offline
      Ami
      #1
      Ami's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th April 2010
      Location : SPACE STATION
      Posts : 1,857
      Rep Power : 621
      Likes Received
      303
      Likes Given
      149

      Default Bakwata yaishtukia serikali

      Mkutano ulioitishwa na ofisi ya waziri mkuu kati yake kwa niaba ya serikali na viongozi wa dini uliingia dosari hapo jana na kushindwa kuendelea baada ya ujumbe wa waislamu uliowashirikisha Bakwata tu kutilia shaka mwaliko huo.

      “Mheshimiwa mwenyekiti naomba uwakilishi wa Waislam katika mkutano huu uongezeke... tukitizama uhalisia, idadi ya Waislam na Wakristo haitofautiani sana, lakini ndani ya mkutano huu Waislam tupo 15 wakati wenzetu wapo zaidi ya 40! “...Nasema hivi kwa sababu na sisi Waislam tunayo Jumuiya ya Taasisi za Kiislamu ambazo hazipo BAKWATA nao wana waumini wao na ninyi mlivyotuletea mwaliko mmeweka idadi ya viongozi 15 tu, sasa kwa mantiki hii lengo lenu kwa upande wetu halitatimia,” alisema Sheikh Lolila.
      .............................. .............................. .............................. .................
      Huu ni upendeleo wa wazi ambao hata hao waliokuwa wakipendelewa ili kujenga tabaka wameshtuka.
      Last edited by Ami; 6th July 2011 at 18:27.


    2. #2
      Luteni's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 9th January 2010
      Posts : 2,270
      Rep Power : 947
      Likes Received
      239
      Likes Given
      73

      Default Re: Bakwata yaishtukia serikali

      Hawana hoja kazi kutafuta conflicts zisizo na msingi, idadi ya wajumbe inahusiana nini na michango ya mawazo kwani wanakwenda kupiga kura, kama wana hoja za nguvu hata wajumbe wawili wanatosha kuwakilisha kwa vile hazimnamo wanafikiri uwingi wa wajumbe ndiyo hoja, hovyooo.
      Luteni is a True Revolutionist.

    3. #3
      blackpepper's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 19th January 2010
      Posts : 377
      Rep Power : 554
      Likes Received
      6
      Likes Given
      3

      Default Re: Bakwata yaishtukia serikali

      inferiority complex tu

    4. SMU is offline
      SMU
      #4
      SMU's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 14th February 2008
      Location : Mavurunza
      Posts : 4,604
      Rep Power : 3828
      Likes Received
      1349
      Likes Given
      1987

      Default Re: Bakwata yaishtukia serikali

      Mimi sidhani kama ni inferiority complex. Kama kwa mfano walioitisha mkutano walitaka kuzingatia uwakilishi wa kidini na wakafanya hivyo kwa wakristo (mfano wakawaalika KKKT, RC, AGT, etc) na kusahahu kufanya vivyo hivyo kwa waislamu na dini nyingine nadhani upo uhalali kwa waislamu au dini hizo nyingine kulalamika.

      Serikali ni lazima wawe sensitive kwenye masuala haya ya dini. Kwa mfano si sahihi kudhani kuna waislamu na wakristo pekee....wapo wengine hata kama ni monority ambao pengine hawana mahala pengine pa kusemea.
      "Rather than love, than money, than fame, give me truth" ----Thoreau

    5. MJM is online now
      MJM
      #5
      MJM's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 30th March 2010
      Posts : 390
      Rep Power : 547
      Likes Received
      16
      Likes Given
      2

      Default Re: Bakwata yaishtukia serikali

      Hii nchi imekuwa hivi sababu ya viongozi wetu wa serikali kuendekeza matabaka. Mara ngapi wapinzani wamekuja na mawazo ya maana wakaishia kudhihakiwa kwa sababu tu si chama tawala? Suala la mjadala huu kuelekea uchaguzi mkuu mawazo yangetoka kwa wadau mchanganyiko kwa kuwajumuisha viongozi wa dini, NGOs, CBOs, nk. Kwa kuwabagua viongozi wa dini peke yao inamaana kuna agenda ya siri. Hapo ndipo uwakilishi wa sawa kwa sawa unapotakiwa kama walivyodai viongozi wa waislam.

      Mi naona sawa sawa tu hadi hapo viongozi wa serikali watakapoona umuhimu wa kuheshimu mawazo ya mtu regardless of political, religious or political background. Mimi ni Mkristo lakini kwa hili nasimama upande wa vikundi vya wakristo na waislam waliotoswa kwani nao ni muhimu kwa mustakabali wa Taifa hili


    6. #6
      Ngekewa's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 8th July 2008
      Posts : 4,659
      Rep Power : 1490
      Likes Received
      434
      Likes Given
      209

      Default Re: Bakwata yaishtukia serikali

      Huna hoja kazi yako kurukia conflicts tu! Usipoona ukweli uliopo basi umepumbaazwa na hisia!

    7. #7
      Ngekewa's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 8th July 2008
      Posts : 4,659
      Rep Power : 1490
      Likes Received
      434
      Likes Given
      209

      Default Re: Bakwata yaishtukia serikali

      No! Ni superior complex ya upande wa pili!

    8. #8
      Kabonde's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 12th August 2008
      Posts : 417
      Rep Power : 637
      Likes Received
      18
      Likes Given
      66

      Default Re: Bakwata yaishtukia serikali

      Hawana hoja kila siku wanalalamika bila sababu za msingi,wanataka serekali iwaalike wale wahuni shura ya maimu.hakuna haja serekali kusikiliza hoja za walioishiwa hoja ikibidi serekali iwatimua Bwakwata.

    9. #9
      Anyisile Obheli's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 13th December 2009
      Location : Rohoni
      Posts : 3,261
      Rep Power : 1129
      Likes Received
      69
      Likes Given
      82

      Default Re: Bakwata yaishtukia serikali

      Quote By MASOUD M.SAID View Post
      Mkutano ulioitishwa na ofisi ya waziri mkuu kati yake kwa niaba ya serikali na viongozi wa dini uliingia dosari hapo jana na kushindwa kuendelea baada ya ujumbe wa waislamu uliowashirikisha Bakwata tu kutilia shaka mwaliko huo.

      “Mheshimiwa mwenyekiti naomba uwakilishi wa Waislam katika mkutano huu uongezeke... tukitizama uhalisia, idadi ya Waislam na Wakristo haitofautiani sana, lakini ndani ya mkutano huu Waislam tupo 15 wakati wenzetu wapo zaidi ya 40! “...Nasema hivi kwa sababu na sisi Waislam tunayo Jumuiya ya Taasisi za Kiislamu ambazo hazipo BAKWATA nao wana waumini wao na ninyi mlivyotuletea mwaliko mmeweka idadi ya viongozi 15 tu, sasa kwa mantiki hii lengo lenu kwa upande wetu halitatimia,” alisema Sheikh Lolila.

      Huu ni upendeleo wa wazi ambao hata hao waliokuwa wakipendelewa ili kujenga tabaka wameshtuka.
      mi naona hapo hakuna sababu ya msingi sana, zaidi imekaa kiitikadi bila elimu, kwani uwingi ndiyo uchangiaji wa mawazo? wanaweza wakaambiwa waende waislamu wote kote nchini, lakini wakawa maamuma kwa hoja husika na kushindwa kuichangia, kuna haja ya kubadilika kimtazamo hasa kwa kipindi hiki cha sayansi na teknolojia, pale si mahari kutaka kuchagua nani awe mtume wa mambo ya dini, hvyo waweze kuhoji kuwa watashindwa kutokana na idadi ndogo ya wanachama wao,


      Mentally Change is needed for them to overcome the situation.
      ........................HAKUNA TIBA YA KIFO............
      HESHIMU WATU NA PIA JIHESHIMU, KISHA, MPENDE MUNGU

    10. #10
      Kigogo's Avatar
      Banned Array
      Join Date : 14th December 2007
      Location : Calabash
      Posts : 8,484
      Rep Power : 0
      Likes Received
      1302
      Likes Given
      318

      Default Re: Bakwata yaishtukia serikali

      kwanza aliyeitisha huu mkutano mwenyewe hana akili..mkutano kama huu ni wa nini? yaani nchi hii haina vipaumbele kabisa sijui kwa nini

    11. #11
      Abunwasi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 25th June 2009
      Location : Urbanite
      Posts : 712
      Rep Power : 650
      Likes Received
      48
      Likes Given
      66

      Default Re: Bakwata yaishtukia serikali

      Ninapata taabu sana iwapo wanajamii [baadhi] wanaona ni hoja kuzungumzia wingi wa waislamu katika NEC-CCM na wengine wakizunguzia wingi viongozi wa kiislam ndani ya serikali ya JK na zote hizi zikawa hoja nzito jamvini lakini wachangiaji hao hao wanaona hoja ya Bakwata ni Hovyo I just dont understand some of u guys and babes

    12. #12
      Kilembwe's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 19th August 2009
      Posts : 960
      Rep Power : 692
      Likes Received
      116
      Likes Given
      145

      Default Re: Bakwata yaishtukia serikali

      Suala hapa sio idadi ya watu ni uwiano wa uwakilishi! ukiangalia idadi ya wakristo walioalikwa ni wazi walizingalitia uwakilishi wa kila dhehebu, lakini kwa idadi hiyo ya ndugu zetu waislamu ni wazi kabisa walioitisha huo mkutano hawakuzingatia uwakilishi wa madhehebu, na hili ndio tatizo mara nyingi watu hufikiri kuwa uislam ni dhehebu moja tu!

    13. #13
      alles's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 14th October 2006
      Posts : 432
      Rep Power : 735
      Likes Received
      85
      Likes Given
      71

      Default Re: Bakwata yaishtukia serikali

      Wadau, sio BAKWATA peke yao walioishtukia serikali.Hata viongozi wengine wa dini wameshtuka.
      Pitieni iyo nakala chini. Muone watu walivyochoka kudanganywa.

      Padri: Viongozi wa dini msinunuliwe na serikali

      *Awataka kuwa mstali wa mbele kulikomboa taifa leo
      *Aonya miaka mitano ijayo hali ya nchi itakuwa mbaya

      Na Tumaini Makene

      WAKATI viongozi wa dini wanakutana na serikali jijini Dar es Salaam jana na leo, padri mmoja wa Kanisa Katoliki ameibuka na kuwatakja viongozi wasikubali kununuliwa wala kurubuni badala yake waweke msimamo wa kuleta mabadiliko nchini.

      Huku akihoji kuwa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kitaendelea kutawala mpaka lini wakati maendeleo ya nchi yanazorota, Padri Baptiste Mapunda ambaye amekuwa mmoja wa watu walio mstari wa mbele katika kutoa maoni na kuchambua mwenendo wa utawala na watawala nchini, amesema kuwa wakati umefika wa kukiambia ukweli CCM kuwa kimeshindwa kuendesha nchi, kuwakemea mafisadi na kuwaletea maendeleo wananchi.

      Padri Mapunda ambaye ni mmoja wa viongozi wa Kanisa Katoliki nchini ambao wamekuwa wakizungumzia hadharani masuala mbalimbali ndani ya nchi, amewaambia wananchi kuwa muda wa kutumia kura zao vyema kuleta mabadiliko umefika, huku akiwataka kuacha kuhongwa fulana, pilau, pombe, kofia na vitenge, akisema uongozi haununuliwi, bali hupewa mtu anayefaa.

      Katika taarifa yake aliyoituma kwa Majira juzi, Padri Mapunda ambaye kwa sasa yuko nchini Kenya kwa Masomo ya Uandishi wa Habari, alisema kuwa kura ni silaha kubwa ambayo haipaswi kuchezewa inayoweza kuleta mapinduzi ya siasa, kiuchumi, kijamii na kiutamaduni.

      Katika uchambuzi wake huo alioupatia kichwa cha habari kisemacho "Viongozi wa Dini msiweke Mkataba na CCM wala kuhongwa", Padri Mapunda alisisitiza kuwa viongozi wa dini zote nchini wanapaswa kuwa mstari wa mbele kuliokoa taifa, kwani hali itazidi kuwa mbaya kama Watanzania wataendelea kuongozwa kwa mtindo uliopo sasa.

      "Ninashangaa ujasiri wa CCM kuwaita viongozi wa madhehebu ya dini na kuwaandalia semina. Semina hii inatia shaka kwa muda kama huu. Kwanza lazima ijulikane miezi michache ya nyuma serikali ya CCM ilikuwa na 'madharau makubwa sana' kwa viongozi wa dini kufuatia matamshi na nyaraka mbalimbali walizotoa.

      "Serikali imekuja kugundua kwamba viongozi wa dini wanashika watu wengi sana kuliko wanavyofanya wao katika majukwaa ya kisiasa. Dini ni suala nyeti sana katika jamii, kama mtu hajui basi ni kipofu," alisema Padri Mapunda huku akitoa mfano wa jinsi viongozi wa dini nchini Kenya wanavyotishia kukwamisha Rasimu ya Katiba mpya.

      Pia alitoa mfano wa wa Uingereza ambako kilichokuwa chama tawala cha Labour kimeondolewa madarakani kwa kupigwa dafrao katika uchaguzi na kilichokuwa chama pinzani cha Conservative, huku akiwataka viongozi wa dini waache kukibeba CCM ili watu washuhudie kiyama chake na akahoji "CCM inataka itawale miaka 100?"

      Aliwataka viongozi wa dini watumie nafasi yao kikamilifu na wala wasiwe sehemu ya kuendeleza ufisadi nchini. Akiongeza kuwa nchi inanuka kila aina ya ufisadi, akisema kuendelea kuiacha CCM itawale ni kufuru kwa Watanzania na kwa Mungu.

      "Viongozi wa dini msikubali kuhongwa wala kuweka mikataba ya kurudi nyuma na kupoozwa. Mkumbuke kuwa miaka mingine mitano ijayo hali ya Tanzania itakuwa mbaya sana kama tutaendelea na serikali hii kwa mtindo huu uliopo sasa. Mimi yangu macho nataka kuona viongozi wa dini sasa waongoze mapambano ya kuleta mapinduzi katika nchi ya Tanzania.

      "Nafasi ya viongozi wa dini popote pale inajulikana, msiwe sehemu ya kuendeleza Ufisadi nchini, bila viongozi wa dini nchi leo hii ingekuwa wapi? Mmeona Uingereza wamefanya demokrasia ya kweli, Labour wameng'olewa madarakani. Na CCM inataka itawale miaka mingapi 100? Huku ni kutafuta kufuru kwa Mungu na Watanzania kwa ujumla. Semina inayoendelea sasa hivi kati ya CCM na viongozi wa dini iwe ya kuiambia ukweli CCM kwamba sasa ikubali kwamba imeshindwa kuendesha nchi na kuwaletea maendeleo wananchi.

      "Imeshindwa kabisa kuwakemea mafisadi. Kwangu, itakuwa ni aibu kubwa kama viongozi wa dini watakula njama na CCM ama kupoozwa makali yao, naamini mtasimama kidete katika uchaguzi ujao. Acheni kuibeba CCM halafu tuone kiama chake," alisema Padri Mapunda.

      Aliwataka Watanzania kutumia haki ya kura zao kuleta mabadiliko nchini na kuachana na zawadi za kupita wanazohongwa wakati wa uchaguzi na viongozi wanaosaka madaraka, "Dawa ni moja tu, kama ukipewa rushwa ya kura, chukua, lakini kamwe usimpe kura maana amejidhihirisha kuwa HAFAI kabisa kuwa kiongozi, uongozi haununuliwi bali unapewa na watu wakiona unafaa."

      Pia alizungumzia suala la viongozi wenye umri mkubwa kung'ang'ania madaraka akiwataka vijana kuacha kuwavusha wazee katika nafasi mbalimbali, kwani dunia ya leo inahitaji vijana katika uongozi.

      "CCM lazima ishikishwe adabu, kwa mara zote karibu na uchaguzi inajaribu kunyenyekea sana kwa viongozi wa dini. Mimi nasema ni wakati wa kufanya unabii, nchi inazaidi kudidimia...Na kwa upande wa vijana, nawaasa acheni kuwavusha wazee katika nafasi mbalimbali. Pitisheni vijana wenzenu katika nafasi mbalimbali.

      "Dunia ya leo inahitaji vijana Waziri Mkuu wa Uingereza David Cameroon aliyenyakua madaraka ana miaka 43 tu, mpo hapo vijana? Sasa hawa wazee wengi nchini Tanzania kwa nini wanang'ang'ania madaraka? Kuna nini ndani ya uongozi?" alihoji Padri Mapunda.
      Source:http://www.majira.co.tz/index.php?op...dini-msinunuli

    14. #14
      Fundi Mchundo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 9th November 2007
      Posts : 4,351
      Rep Power : 2682
      Likes Received
      194
      Likes Given
      137

      Default Re: Bakwata yaishtukia serikali

      Wangetaka kutenda haki basi kila Imam wa msikiti angealikwa maana katika dhehebu la wa-sunni kila msikiti unasimama wenyewe, hakuna mfumo kama walionao wamisheni wamashemasi, mapadiri, maskofu, makadinali n.k. Kwa vile tumetofautiana kiutawala basi hatuwezi kila kitu ikawa sawa kwa sawa. Wadai kuongezwa uwakilishi lakini si kwa sababu wamisheni wako wengi!

      Amandla....
      Fundi Utumbo

    15. #15
      Kitila Mkumbo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 25th February 2006
      Posts : 3,940
      Rep Power : 6971
      Likes Received
      1102
      Likes Given
      36

      Default Re: Bakwata yaishtukia serikali

      Hao watu wa serikali hawapo makini and they are not sensitive at all. Wamefanya a fatal mistake. Wana sababu zipi za msingi za kualika viongozi wa kikristo 40 na wa kiislamu 15? Ni kutafuta chochoko na mfarakano usio na lazima. Incompetence in this government seems to be widespread and unlimited, hata kwenye mialiko linawashinda kutumia mantiki? Yaani hawakujua kwamba hii lingelete shida??!
      A Struggle Without Casualties is No Struggle-Steve Biko

    16. #16
      Mzee Mwanakijiji's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 10th March 2006
      Location : Kijijini
      Posts : 29,614
      Rep Power : 46736
      Likes Received
      16716
      Likes Given
      8547

      Default Re: Bakwata yaishtukia serikali

      Katika hili Bakwata wana hoja; Tatizo ni kuwa serikali bado haikubali kuwa kuna waislamu nje ya Bakwata! Jambo la maana ni kutoa mwaliko kwa madhehebu yote ya kidini na kuwaacha waamue nani aje nani asije; ni kuweka idadi tu kuwa dhehebu linaweza kuleta wawakilishi say wasiozidi watano tena kwa njia nyepesi tu.

      a. Mnatangaza semina ya serikali na madhehebu ya dini (siyo viongozi wa dini) - kila dhehebu linaweza kutuma wajumbe wasiozidi wanne kwa mfano
      b. Madhehebu yanayotaka kushiriki yanajiandikisha kati muda uliowekwa
      c. Nafasi za semina ni watu sema 50 tu kwa hiyo wanaofika kwanza kutimiza idadi ndiyo hapo
      d. Kutoka hapo waliojiandikisha kwa muda na kufuata masharti wanapewa barua ya kuwathibitishia kushiriki kwao katika hizo semina.

      Sasa mkishafanya hivyo kama at end mtakuwa na Waislamu asilimia 70 na Wakristu asilimia 30 hakuna atakayelalamika; au kinyume chake. tatizo ni mmoja genius ambaye amekaa kwenye kiti chache enzi na kuanza kuamua "nani tumualike"! BAKWATA wamefanya vizuri kuamsha dhamira za serikali.
      [email protected]
      The Best of Tanzanian Socio-Political Blogging - http://www.mwanakijiji.com

    17. #17
      Hofstede's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 15th July 2007
      Posts : 3,604
      Rep Power : 21345
      Likes Received
      981
      Likes Given
      988

      Default Re: Bakwata yaishtukia serikali

      Quote By Mzee Mwanakijiji View Post
      Katika hili Bakwata wana hoja; Tatizo ni kuwa serikali bado haikubali kuwa kuna waislamu nje ya Bakwata! Jambo la maana ni kutoa mwaliko kwa madhehebu yote ya kidini na kuwaacha waamue nani aje nani asije; ni kuweka idadi tu kuwa dhehebu linaweza kuleta wawakilishi say wasiozidi watano tena kwa njia nyepesi tu.

      a. Mnatangaza semina ya serikali na madhehebu ya dini (siyo viongozi wa dini) - kila dhehebu linaweza kutuma wajumbe wasiozidi wanne kwa mfano
      b. Madhehebu yanayotaka kushiriki yanajiandikisha kati muda uliowekwa
      c. Nafasi za semina ni watu sema 50 tu kwa hiyo wanaofika kwanza kutimiza idadi ndiyo hapo
      d. Kutoka hapo waliojiandikisha kwa muda na kufuata masharti wanapewa barua ya kuwathibitishia kushiriki kwao katika hizo semina.

      Sasa mkishafanya hivyo kama at end mtakuwa na Waislamu asilimia 70 na Wakristu asilimia 30 hakuna atakayelalamika; au kinyume chake. tatizo ni mmoja genius ambaye amekaa kwenye kiti chache enzi na kuanza kuamua "nani tumualike"! BAKWATA wamefanya vizuri kuamsha dhamira za serikali.
      Mi mtazamo wangu ni kuwa semina ya nini katika muda huu wa kuelekea uchaguzi?. Semina ingekuwa na mantiki mwanzoni mwa awamu ya nne kuita viongozi wa dini na kuomba maoni yao na ushauri wa nini nchi ifanye katika miaka mitano ijayo ya uongozi. Sasa kama wao walikuwa wanajua watafanya nini na wameshindwa kufanya hivyo hii semina itasaidia nini wananchi? zaidi ya kupigia kampeni walewale walioshindwa kutekeleza waliyoyaahidi katika miaka mitano iliyopita. Yaani wanataka viongozi wa dini wadanganye waumini wao wakati wanajua kabisa maandishi kuwa yanawakataza kusema uongo?.

      CCM silaha yao kubwa ni kudumisha amani, lakini ukweli ni kwamba amani si sera ya chama bali ni attitude ya wananchi, na watanzania by nature ni watulivu japo sasa uvumilivu unaenda ukipungua kwa kufanywa mazuzu na watawala wanaowaogopea kila uchaguzi unapofika. "CCM ni chama pekee kinachotishia amani ya watanzania, mara nyingi wakiona wanashindwa kwenye chaguzi mbalimbali hutumia mbinu chafu ambazo ni vyanzo vya uvunjifu wa amani (bila haki amani ipo mashakani) kwa kuwa wao wanapolisi, jeshi, hivyo hulazimisha watakayo wao na si wananchi- hii ni hatari sana kwa afya ya amani na maendeleo ya nchi yetu". Siku wananchi wakisema basi tutashuhudia watu wanapelekwa The hague baada ya upatanishi.

    18. #18
      Mkandara's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd March 2006
      Location : T dot
      Posts : 13,768
      Rep Power : 7665
      Likes Received
      4930
      Likes Given
      4509

      Default Re: Bakwata yaishtukia serikali

      Hakuna cha hoja wala nini... Huu ni ujinga mkubwa wa serikali kutaka kuwagawa watu wake.. Ni lini serikali iwe inatoa mwaliko kwa viongozi wa dini kushiriki ktk mkutano ili iwe nini?..

      Sijawahi kuona Ofisi ya waziri mkuu wala rais wa nchi yeyote akifanya hivyo pasipo sababu maalum inayohusiana na dini hizo.
      Tatizo la tanzania viongozi wetu wote wanatumia kivuli cha dini kujipatia kura. wanawatumia viongozi wa dini kuwawezesha kushinda ktk chaguzi na hali kama hii inazidisha uhasama wa wazi baina ya waumini.

      Na kibaya zaidi sisi wenyewe kwa Ujinga na Ulimbukeni wetu tunaendekeza sana ujinga kama huu na kuupa sifa za kufikiria mapuingufu ya dini nyingine, tunapenda sana mialiko ya Ikulu au ofisi wa waziri mkuu pasipo sababu ya msingi ili mradi tuonekane tupo karibu zaidi na utawala..
      Exploration of reality

    19. #19
      Fundi Mchundo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 9th November 2007
      Posts : 4,351
      Rep Power : 2682
      Likes Received
      194
      Likes Given
      137

      Default Re: Bakwata yaishtukia serikali

      Quote By Mzee Mwanakijiji View Post
      Katika hili Bakwata wana hoja; Tatizo ni kuwa serikali bado haikubali kuwa kuna waislamu nje ya Bakwata! Jambo la maana ni kutoa mwaliko kwa madhehebu yote ya kidini na kuwaacha waamue nani aje nani asije; ni kuweka idadi tu kuwa dhehebu linaweza kuleta wawakilishi say wasiozidi watano tena kwa njia nyepesi tu.

      a. Mnatangaza semina ya serikali na madhehebu ya dini (siyo viongozi wa dini) - kila dhehebu linaweza kutuma wajumbe wasiozidi wanne kwa mfano
      b. Madhehebu yanayotaka kushiriki yanajiandikisha kati muda uliowekwa
      c. Nafasi za semina ni watu sema 50 tu kwa hiyo wanaofika kwanza kutimiza idadi ndiyo hapo
      d. Kutoka hapo waliojiandikisha kwa muda na kufuata masharti wanapewa barua ya kuwathibitishia kushiriki kwao katika hizo semina.

      Sasa mkishafanya hivyo kama at end mtakuwa na Waislamu asilimia 70 na Wakristu asilimia 30 hakuna atakayelalamika; au kinyume chake. tatizo ni mmoja genius ambaye amekaa kwenye kiti chache enzi na kuanza kuamua "nani tumualike"! BAKWATA wamefanya vizuri kuamsha dhamira za serikali.
      Mimi nadhani hapa hamuitendei haki serikali. Mnalinganisha machungwa na maembe. Kama serikali imealika viongozi wamadhehebu ya dini basi bila shaka tofaut ya waalikwa itajitokeza. Kwa wakristu wakatoliki, waangalikana, waluteri, assemblies, presbyterians, pentecosts, church of the latter day saints, kakobez,African Inland Church, Moravians n.k. wote watawakilishwa maana kila moja ni dhehebu na lina uongozi wake unaotambulika. Kwa waislamu kuna sunni na upande wa wama'shia kuna bohora, ismailia basi. Upande wa Sunni hawana uwakilishi unaokubalika na wote, Bakwata hawana mamlaka kidini kama vile walivyo hao wengine. Kwa Sunni kila msikiti na kila muislamu anajisimamia, hakuna mwakilishi au hierachy kama ilivyo kwa wamisheni. Washia ndiyo wanamfumo unaofanana na wamisheni, hierarchy inayoeleweka, tatizo ni kuwa wenzao wanawaona feki. Ndiyo maana nilisema awali kama tulitaka kweli haki ifanyike basi viongozi wote wa Misikiti Tanzania wangealikwa ili kuwawakilisha wa'sunni. Hii dhahiri isingewezekana, basi kilichobaki serikali ingejitahidi kupata wawakilishi kutokana na vikundi vinavyogombea kuwakilisha dhehebu la wa'sunni. Nakubaliana nanyi kuwa kuwakaribisha Bakwata kulikuwa misguided. Lakini vivyo hivyo kudai parity katika uwakilishi ni kuwa disingenious.

      Amandla......
      Last edited by Fundi Mchundo; 15th May 2010 at 09:59.
      Fundi Utumbo

    20. #20
      Mzee Mwanakijiji's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 10th March 2006
      Location : Kijijini
      Posts : 29,614
      Rep Power : 46736
      Likes Received
      16716
      Likes Given
      8547

      Default Re: Bakwata yaishtukia serikali

      Quote By Mkandara View Post
      Hakuna cha hoja wala nini... Huu ni ujinga mkubwa wa serikali kutaka kuwagawa watu wake.. Ni lini serikali iwe inatoa mwaliko kwa viongozi wa dini kushiriki ktk mkutano ili iwe nini?..

      Sijawahi kuona Ofisi ya waziri mkuu wala rais wa nchi yeyote akifanya hivyo pasipo sababu maalum inayohusiana na dini hizo.
      Tatizo la tanzania viongozi wetu wote wanatumia kivuli cha dini kujipatia kura. wanawatumia viongozi wa dini kuwawezesha kushinda ktk chaguzi na hali kama hii inazidisha uhasama wa wazi baina ya waumini.

      Na kibaya zaidi sisi wenyewe kwa Ujinga na Ulimbukeni wetu tunaendekeza sana ujinga kama huu na kuupa sifa za kufikiria mapuingufu ya dini nyingine, tunapenda sana mialiko ya Ikulu au ofisi wa waziri mkuu pasipo sababu ya msingi ili mradi tuonekane tupo karibu zaidi na utawala..
      Ni kweli ni ujinga! Lakini naamini katika utendaji wa kazi mbalimbali serikali itakuwa inakutana na viongozi au watendaji wa dini mbalimbali haijalishi mada ni nini. La maana kwangu ni kuwa wakati inafanya hivyo (iwe ni kuzungumzia masuala ya elimu, afya, siasa, uchumi n.k) serikali inatoa mialiko. Hili ni jambo la kawaida mahali pote huwezi tu kusema "njooni" bila utaratibu maalumu. Lakini unapotoa mwaliko pia ni lazima uwe mwaliko ambao hautasababisha mgawanyiko kama walivyofanya sasa. Lakini nakubaliana kabisa kuwa ni ujinga kufanya mikutano ya namna hii bila ya kutumia akili! au kutoifanya kwa sababu ya kutotataka kuwashirikisha viongozi wa dini.
      [email protected]
      The Best of Tanzanian Socio-Political Blogging - http://www.mwanakijiji.com

    Page 1 of 3 123 LastLast

    Similar Topics

    1. Replies: 30
      Last Post: 3rd October 2011, 15:30
    2. CUF yaishtukia Serikali ya Muungano suala la mafuta
      By mlaizer in forum Jukwaa la Siasa
      Replies: 17
      Last Post: 18th March 2011, 08:00
    3. Serikali na BAKWATA
      By Samvulachole in forum Jukwaa la Siasa
      Replies: 13
      Last Post: 5th August 2007, 03:04

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...