Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Askofu Malasusa msemaji wa familia ya Lowasa

    Report Post
    Page 2 of 2 FirstFirst 12
    Results 21 to 36 of 36
    1. #1
      mfianchi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 1st July 2009
      Location : Likulufusi
      Posts : 3,651
      Rep Power : 1242
      Likes Received
      612
      Likes Given
      1266

      Default Askofu Malasusa msemaji wa familia ya Lowasa

      Imebidi nijiulize baada ya kusoma kwenye gazeti kuwa Askofu Malasusa alikuwa msemaji wa familia ya Lowasa kwenye harusi ya binti yake,sijui huu urafiki umeanza baada ya Malasusa kuwa Askofu wa Dayosisi ya Mashariki pwani,kwa kiongozi wa dini ambaye anaelewa tuhuma za Lowasa kujifanya anamfagilia kwa kumsifia mambo amabyo wala Lowasa hanayo ni unafiki mkubwa si ntashangaa hapo baadaye tukimsikia Askofu Malsusa akisema Lowasa ni chaguo la Mungu,Si elewi uhusiano uliopo kati ya Lowasa na hawa maaskofu wetu kwanza Askofu Laizer wa Arusha naye akajitoma kumpokea Lowasa pale Arusha baada ya kupima hoja za Richmond hata akajiuzulu,kabla hatujakaa sawa mkewe Lowasa akazindua kitabu kama kawaida Maaskofu akiwemo Kardinali Pengo wakajitoma kwenye hiyo hafla jamani maaskofu kama hamjijui Lowasa anawatumia kwa malengo yake na sisi waumini wenu mnatutia kinyaa kwa hizo tabia zenu !!


    2. #21
      muhanga's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 16th April 2009
      Posts : 852
      Rep Power : 688
      Likes Received
      260
      Likes Given
      348

      Default Re: Askofu Malasusa msemaji wa familia ya Lowasa

      wapendwa naomba niwakumbushe tu kuwa maaskofu wachungaji n.k. ni binadamu kama mimi na wewe, na taasisi za dini ni taasisi kama ilivyo taasisi zingine mf. benki, viwanda vya bia n.k. kwenye dini pia huhitajika fedha, msisahau hata yuda alimkana YESU kwa vipande vya fedha, kwa hiyo bado hat hawa viongozi wa dini wa leo wanaendeleza hayo yaliyopita. Kwanza ukiliangalia kanisa au taasisi ya dini kwa nje ndio unaweza ukawa muumini mzuri, ukiingia kwa undani wallah lazima utaikana dini yako, kuna mambo meeeeengi sana ya uchafu mkubwa yanafanywa kwa mgongo wa dini, dini dini. so tujue kuwa kanisa/maaskofu ni wakosefu kama wengine na yaliyo mengi wanayafanya kwa manufaa yao na si kwa mujibu wa neno la Mungu

    3. #22
      Msanii's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 4th July 2007
      Posts : 6,216
      Rep Power : 1933
      Likes Received
      218
      Likes Given
      278

      Default Re: Askofu Malasusa msemaji wa familia ya Lowasa

      nimetapika kabisa.

      siamini kama kweli malasusa ameamua kukumbatia jambazi leo.
      alipaswa kumhubiria kwanza aache uovu, arudishe alichoiba na riba juu kisha afunguliwe milango ya mbingu. Ukwasi wa matajiri hauwapi uhalali wa kumiliki mbingu, labda wataimiliki dunia na kuzimu pekee.
      " If you hear a voice within you say "you cannot paint", then by all means paint, and that voice will be silenced"
      [email protected]

    4. #23
      Marigwe's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 28th November 2009
      Posts : 222
      Rep Power : 530
      Likes Received
      3
      Likes Given
      0

      Default Re: Askofu Malasusa msemaji wa familia ya Lowasa

      Hivi siyo huyu Malasusa aliyemkemea yule mchungaji wa KKKT Kijito nyama aliemwalika Rostam Azizi kwenye harambee ya kwaya? Wakatangaza kuwa fedha ya kifisadi hawatachukua? Na mchungaji yule akahamishwa/fukuzwa? Sasa inaelekea wanaliona suala la EL kama vile mwana kilutheri anapigwa vita. Jamani viongozi wetu acheni hizo!!!

    5. #24
      Kinombo's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 24th February 2007
      Posts : 219
      Rep Power : 673
      Likes Received
      5
      Likes Given
      23

      Default Re: Askofu Malasusa msemaji wa familia ya Lowasa

      Baada ya Harusi------ Viongozi wengi hawakuuzulia kwenye TISA DISEMBA--- SIKU YA UHURU.
      so, wapi priority-- Lowasa and Family walipopanga Harusi walijua kabisa 9/12 hipo na ni siku mhimu kwa taifa la Watanganyika..........ndo maana kama Waziri mkuu wa zamani walitakiwa angalau watie jicho...lakini wapi.......

      WHERE BOYZ 2 MEN...... WAMEJITENGA.

    6. #25
      Gold Digger's Avatar
      Member Array
      Join Date : 21st May 2009
      Location : Nyumbani
      Posts : 86
      Rep Power : 530
      Likes Received
      8
      Likes Given
      8

      Default Re: Askofu Malasusa msemaji wa familia ya Lowasa

      Mtenganishe siasa na dini. Padre, Mchungaji, Askofu na wanaroho hawaruhusiwi kubagua binadamu kutokana na dhambi au tuhuma, kwani mwenyezi mungu alimtuma mwanae kuwaokoa watenda dhambi. Baba wa kiroho yupo hapa kukusaidia wewe mtenda dhambi, they are not here tu judge...only god does that!
      Every moment of every day is another chance to CHANGE things


    7. #26
      samvande2002's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 6th March 2009
      Location : pretoria, R.S.A
      Posts : 286
      Rep Power : 581
      Likes Received
      9
      Likes Given
      89

      Default Re: Askofu Malasusa msemaji wa familia ya Lowasa

      malasusa kapozwa na cha juu,ndio maana anakuwa mstari wa mbele kusifia mambo ya kipumbavu katika jamii...tulitegemea awe wa kwanza kukemea mambo ya kishenzi aliyoyafanya lowasa kwa manufaa ya taifa lake(malasusa). badala yake anasifia ujinga mtupu..ndio maana mimi sio muumini wa dini yoyote ile kwani ni upumbavu mtupu unaoendelea kwenye hizi dini
      "siongei na mbwa, naongea na mwenye mbwa"--Juma Nkamia (MB)

    8. #27
      Ndahani's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 3rd June 2008
      Location : Somewhere
      Posts : 9,660
      Rep Power : 4023
      Likes Received
      2944
      Likes Given
      5072

      Default Re: Askofu Malasusa msemaji wa familia ya Lowasa

      Quote By Pasco View Post
      Wajemeni, Maaskofu ni Wachungaji, kazi ya wachungaji ni kuwachunga kondoo wa Bwana wasipotee, Masiya alikuja kwa waliopotea na wale walio elemewa na mizigo ili wapumzishwe.

      EL amepotea na ameelemewa na mizigo ya tuhuma, shutuma na kila aina ya bezo, dhihaka, kejeli, matukano, ya kila aina mpaka chuki binafsi mumo humo, kwa watu wa Mungu, huu ndio wakati wa kukaa karibu kabisa na EL na sio kumtenga, bali kumkumbatia mpaka aguswe na roho wa Bwana, atakuja mbele ya kadamnasi ya watu, atatubu, atasamehewa, atatakaswa na atangara kama mbalamwezi tayari kwa 2015!.

      Amini nawaambieni, 'jiwe walikolikataa waashi, litafanywa kuwa jiwe kuu la pembeni'. Kwake Yeye, wa kwanza atakuwa wa mwisho, na wamwisho atakuwa wa kwanza.

      Acha Maaskofu watimize mapenzi ya Bwana, ya kuwarudisha kundini kondoo waliopotea.
      Mbona huo mchakato ameshaunza mara baada ya kugundua kosa. EL siyo mchezo! Hajapoteza vision yake. Anailinda kama mboni ya jicho. Kwaufundi mkubwa anarekebisha yaliyopita na kuweka sawa pale palipo pinda. Sijui issues za integrity yake zitakuwaje ili 2015 ndoto yake itimie ila namuona ameamua kupigana kufa na kupona!!
      We are all inventors, each sailing out on a voyage of discovery, guided each by a private chart, of which there is no duplicate. The world is all gates, all opportunities.
      Ralph Waldo Emerson

    9. #28
      Geza Ulole's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 31st October 2009
      Posts : 3,804
      Rep Power : 1341
      Likes Received
      773
      Likes Given
      140

      Default Re: Askofu Malasusa msemaji wa familia ya Lowasa

      Quote By M-bongo View Post
      Ishu sio maaskofu tu, mchangia hoja aseme hata Dk Salim, warioba,Mbatia walikuwepo pia lakini tatizo isiwe kuwepo kwa hao prominent figures, je Watanzania tumefikia zama ambazo hatuwezi kuhudhuria shughuli za kijamii za watanzania wenzetu eti kwa kuwa tu tuna tofauti nao kimitazamo? sioni hoja hapo
      kuwepo kwa hao viongozi si tatizo! tatizo ni kumsafisha!

    10. #29
      Kigogo's Avatar
      Banned Array
      Join Date : 14th December 2007
      Location : Calabash
      Posts : 8,484
      Rep Power : 0
      Likes Received
      1302
      Likes Given
      318

      Default Re: Askofu Malasusa msemaji wa familia ya Lowasa

      Quote By mfianchi View Post
      Imebidi nijiulize baada ya kusoma kwenye gazeti kuwa Askofu Malasusa alikuwa msemaji wa familia ya Lowasa kwenye harusi ya binti yake,sijui huu urafiki umeanza baada ya Malasusa kuwa Askofu wa Dayosisi ya Mashariki pwani,kwa kiongozi wa dini ambaye anaelewa tuhuma za Lowasa kujifanya anamfagilia kwa kumsifia mambo amabyo wala Lowasa hanayo ni unafiki mkubwa si ntashangaa hapo baadaye tukimsikia Askofu Malsusa akisema Lowasa ni chaguo la Mungu,Si elewi uhusiano uliopo kati ya Lowasa na hawa maaskofu wetu kwanza Askofu Laizer wa Arusha naye akajitoma kumpokea Lowasa pale Arusha baada ya kupima hoja za Richmond hata akajiuzulu,kabla hatujakaa sawa mkewe Lowasa akazindua kitabu kama kawaida Maaskofu akiwemo Kardinali Pengo wakajitoma kwenye hiyo hafla jamani maaskofu kama hamjijui Lowasa anawatumia kwa malengo yake na sisi waumini wenu mnatutia kinyaa kwa hizo tabia zenu !!
      kwani kuna ubaya gani askofu akiwa MC au msemaji wa familia???mbona kikwete mlikubali alipoitwa chaguo la mungu!!! umesahau maneno ya waungwana kuwa mwenye nguvu muache apite...he is powerful and he can do anything ..we hujaona sherehe za send off ya mtoto wake ilinoga kuliko sherehe zetu za uhuru pale shamba la bibi

    11. #30
      Kigogo's Avatar
      Banned Array
      Join Date : 14th December 2007
      Location : Calabash
      Posts : 8,484
      Rep Power : 0
      Likes Received
      1302
      Likes Given
      318

      Default Re: Askofu Malasusa msemaji wa familia ya Lowasa

      Quote By samvande2002 View Post
      malasusa kapozwa na cha juu,ndio maana anakuwa mstari wa mbele kusifia mambo ya kipumbavu katika jamii...tulitegemea awe wa kwanza kukemea mambo ya kishenzi aliyoyafanya lowasa kwa manufaa ya taifa lake(malasusa). badala yake anasifia ujinga mtupu..ndio maana mimi sio muumini wa dini yoyote ile kwani ni upumbavu mtupu unaoendelea kwenye hizi dini
      acha kutusi dini ..kwanza wewe umekimbia kwenu unakaa huko SA ya huku yanakuwashia nini...umasikini unawatia hasira sana..EL mnaye mpaka awe rais ndo mtafunga midomo....hahaaaaa

    12. #31
      Lekanjobe Kubinika's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 6th December 2006
      Location : Tanzania
      Posts : 2,415
      Rep Power : 1664
      Likes Received
      318
      Likes Given
      586

      Default Re: Askofu Malasusa msemaji wa familia ya Lowasa

      Quote By Ngongo View Post
      Askofu Malasusa ni Askofu wa dayosisi ya mashariki na pwani pia ni Askofu mkuu wa Kanisa la Kiinjili la kilutheri Tanzania [KKKT].Ushiriki wa Askofu Malasusa na Askofu Thomas Laiser kwenye sherehe za kumwaga mtoto wa E N Lowassa kwa mara nyingine umelizalilisha kanisa na viongozi wake jinsi walivyotayari kuwakumbatia matajiri bila kujali njia walizotumia kuupata utajiri.

      Mara kadha kanisa limejikuta linajitia doa kwasababu viongozi wake hawataki kufuata maandiko matakatifu.Sikuwepo kwenye sherehe lakini bila shaka kulikuwepo pombe nyingi zilizowafanya wageni kukaa kwenye sherehe hadi usiku wa manane.Fikiria kanisa la KKKT linavyokemea ulevi [unywaji wa pombe] lakini viongozi wake wa juu yaani maaskofu wawili na akili zao wanashiriki kwenye sherehe kwasababu tu Lowassa ana fedha.

      Sipendi viongozi wa kanisa kukubali kutumika na wanasiasa wasiokuwa na maadili kama E N Lowassa.
      Lakini mtuhumiwa sio mkosaji. Kujiuzuru ilibidi kwa sababu ya wadhifa wake. Amehukumiwa wapi kwamba ni mkosaji Lowasa? Hata kama anayo makosa, hakuna aliyempeleka mahakamani kuthibitisha uhalifu wake. Maneno ya wapinzani sio hukumu ya Lowasa.

      Lowasa pia alikuwa mzee wa kanisa pale Azania Front kwa muda mrefu, amefanya kazi kwa karibu sana na wachungaji wengi waliowahi kupitia pale. Kwa hiyo ikiwa mtaani watu wanakutuhumu wewe kuwa mchawi tuamini kwamba wewe umethibitika kuwa mchawi kweli na tukutenge? Jamani tusibebe dhambi za wengine. Ameshindwa nini mtu yeyote kupeleka ushahidi wake mahakamani kuanika ukweli wa tuhuma hizo. Kwa maoni yangu atabaki kuwa na tuhuma mpaka tuhuma hizo zithibitishwe.

      leka

    13. #32
      Bujibuji's Avatar
      Banned Array
      Join Date : 4th February 2009
      Location : NYUMBANI PANONO
      Posts : 14,415
      Rep Power : 0
      Likes Received
      7413
      Likes Given
      5746

      Default Re: Askofu Malasusa msemaji wa familia ya Lowasa

      kazi ya uaskofu ni kurudisha zizini kondoo waliopotea.

    14. #33
      Fidel80's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd May 2008
      Location : UVUNGUNI
      Posts : 19,136
      Rep Power : 9519
      Likes Received
      3234
      Likes Given
      1264

      Default Re: Askofu Malasusa msemaji wa familia ya Lowasa

      Mmesahau kuwa chuo cha Tumaini Dar na Iringa vimejitenga?
      Hawa wa Dar wanafanya michango kwa hali na mali na wao wajenge chuo kikubwa kama cha Iringa sasa wapi watapata pesa nyingi kama sio kwa mafisadi? Wanajidai wanawasafisha hapo hapo na wao wanatokea na kuponea njaa zao humo humo.
      **^^+..Ukiuza Utumbo usiogope nzi..+^^**
      Chuda Raha
      Email: [email protected]

    15. #34
      Omumura's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 20th August 2009
      Posts : 474
      Rep Power : 594
      Likes Received
      11
      Likes Given
      2

      Exclamation Re: Askofu Malasusa msemaji wa familia ya Lowasa

      Askofu malasusa ni rafiki mkubwa wa lowassa.Nakumbuka hata wakati wa mchakato wa kumtafuta mkuu wa kkkt, lowassa alitia mkono wake ili malasusa achaguliwe. Aidha, baada ya kuchaguliwa malasusa, lowassa alimwandalia sherehe ya kumpongeza pale oysterbay.Sioni jipya hapo, bado Eddo ataendelea kumtumia tu pamoja na viongozi wengine wa dini mufilisi.

    16. #35
      Bulesi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 14th May 2008
      Posts : 3,381
      Rep Power : 1252
      Likes Received
      349
      Likes Given
      74

      Default Re: Askofu Malasusa msemaji wa familia ya Lowasa

      Quote By Vangi View Post
      Ni kawaida kwa kanisa la Lutherani kuongozwa na viongozi wa siasa. Nafikiri Lowasa ana say sana ndani ya kanisa lile. Ndo maaana askofu Laizer alisafiri toka Arusha hadi Dar. Pia ninakumbuka vizuri namna ambavyo David Msuya alivyowahi kuwa na influence kubwa katika doyosisi mojawapo nchini na kusababisha migogoro mikubwa. I guess kanisa la kilutheri linajipendekeza sana kwa wenye pesa. Lichunge sana maana huyo Malasusa, ningemwalika aje abariki harusi yangu angesema nimwone mchungaji wa usharika wangu. lakini kwakuwa aliyemwomba anazo, mmmh hata kazi ya kuhudumia waumini wengine inasitishwa. Kuna haja ya kanisa hili kujiangalia upya, namna ambavyo linawahudumia waumini wake. Naamin waumini wote masikini kwa matajiri ni sawa.
      Siku hizi dini zote ni biashsra na ndio maana ukienda kwenye sala zao mambo ni ya sadaka,michango na minada ili kupata fedha na hapo ndipo wenye nazo wanapopata upenyo wa kuwa na influence kubwa!! Sio hivyo tu, siku hizi tofauti na zamani watu wenye fedha na vyeo wana hadhi tofauti katika makanisa na ndio maana ukienda pale Azania front kusali utakuta kuna sehemu za kukaa ambazo ni reserved kwa watu fulani; mfano ni Lowassa ingawa sio waziri mkuu tena lakini kanisa la Malasusa limemtengea sehemu yake maalum, sasa sijui ndio utaratibu wao na kama ni hivyo siku ambayo vigogo wengi wakija kusali sijui itakuwaje? Kanisa lisilete ubaguzi kwa waumini wake wakati wa ibada, kama kuna protocol iwe baada ya misa na sio wapambe kuongozana na Lowassa hata anapokwenda kupokea chakula cha BWANA hapo inakuwa dhihaka madhabahuni!! Anakotoka Malasusa watu hawatumiwi namna hii, haipendezi.

    17. #36
      Nyuki's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 7th July 2009
      Location : D'salaam
      Posts : 375
      Rep Power : 582
      Likes Received
      6
      Likes Given
      0

      Default Re: Askofu Malasusa msemaji wa familia ya Lowasa

      Quote By Yetu macho View Post
      Waswahili walisema "Penye njaa penyeza rupia" hii ndio kazi ya rupia za kifisadi. Wataitumia kujisafisha kwa kila gharama na kwakushibisha kila tumbo lenye njaa na lisiloshiba.
      Tusisahau pia Malasusa ni binadamu na ni baba wa familia. Pamoja na kuwajibika kwa kanisa anawajibika kwa familia pia hivyo anajaribu kuwajengea watoto wake mtandao maana si lazima wao wajewaelekee mrengo wake aliopo(Uchungaji/ Uaskofu).Na kanchi haka kamekua ka mtandao kila pahala.Naamini roho yake haitaki ajihusishe na hawa mafisadi lakini mwili wake ni dhaifu. Hii hali ya mwili na roho kutofautiana kimatakwa ilimtokea hata masiha pale alipokua anaelekea kusulubiwa, hivyo huu ni udhaifu wa kawaida kikubwa ni uwezo wa kuushinda ambao Malasusa ameshadhihirisha kushindwa kuuhimili udhaifu huu.

      Tutoe wito kwa watanzania wenye imani wawaombee viongozi waregevu hawa
      \


      nADHANI SI PENYE NJAA NI PENYE UDHIA PENYEZA RUPIA

    Page 2 of 2 FirstFirst 12

    Similar Topics

    1. JK na Malasusa wapelekewa malalamiko kuhusu askofu mdegela
      By Mzito Kabwela in forum Habari na Hoja mchanganyiko
      Replies: 29
      Last Post: 7th September 2011, 14:50
    2. Fedha zilimwagwa kumng'oa Askofu Malasusa KKKT...................
      By Rutashubanyuma in forum Habari na Hoja mchanganyiko
      Replies: 5
      Last Post: 9th December 2010, 11:53
    3. Askofu Malasusa aunga mkono ongezeko la ada vyuo vikuu
      By Pdidy in forum Jukwaa la Elimu (Education Forum)
      Replies: 21
      Last Post: 10th August 2009, 18:47
    4. Askofu Malasusa-tuachieni Kanisa Letu!
      By mwanaizaya in forum Habari na Hoja mchanganyiko
      Replies: 13
      Last Post: 15th July 2008, 10:53
    5. Ndugu Askofu Malasusa unataka kufanya kweli ama ni changa la macho hili ?
      By Lunyungu in forum Habari na Hoja mchanganyiko
      Replies: 2
      Last Post: 27th December 2007, 08:35

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...