Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Mganga wa Kienyeji ashikiliwa Kwa Kudhalilisha

    Report Post
    Results 1 to 3 of 3
    1. #1
      MziziMkavu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd February 2009
      Location : European Union
      Posts : 22,210
      Rep Power : 19215
      Likes Received
      8166
      Likes Given
      26659

      Default Mganga wa Kienyeji ashikiliwa Kwa Kudhalilisha

      MGANGA wa kienyeji mmoja mkazi wa wilayani Nkasi mkoani Rukwa, anashikiliwa na polisi mkoani humo kwa tuhuma za kuwadhalilisha wanawake wawili kwa kutaka kufanya nao mapenzi bila ridhaa yao nakudai hayo ndiyo masharti ya dawa yao. Ilidaiwa kuwa mganga huyo alikuwa akiwapeleka wanawake hao katika msitu mmoja mkali na kuwavua nguo zote na kisha kuwachanja chale mwili mzima na kuwanyoa vinyoleo vilivyopo sehemu za siri.


      Ilidaiwa kuwa hiyo ndiyo ilikuwa ni kawaida yake ndani ya wiki moja katika zoezi la kuwaahidi akina mama hao kuwa hayo ndiyo yalikuwa masharti ya dawa yao ili waweze kufanikiwa.


      Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Rukwa, Isunto Mantage alisema matukio hayo yalikuwa ni ya nyakati tofauti tofauti moja likiwa mwishoni mwa wiki iliyopita na lingine mwanzoni mwea juma hili.

      Kamanda Mantage alifafanua kuwa tukio la kwanza lilitokea saa 10 jioni wakati mwanamke mwenye umri wa miaka 40 ambaye jina lake linahifadhiwa , mkazi wa kijiji cha Isunta kilichopo katika wilaya hiyo ya Nkasi aliyekuwa akisumbuliwa na maumivu ya tumbo pamoja na kuhara damu kwa muda mrefu alikwenda kwa mganga huyo kwa lengo la kupatiwa matibabu.


      Alisema alifika kwa mganga huyo kwa lengo la kupata tiba na kisha mganga huyo alimpeleka hadi katika msitu wa kijiji cha Mkangale kilichopo nje kidogo ya mji huo wa Namanyere kwa lengo la kumtengenezea dawa.


      Kamanda Mantage alisema kuwa inadaiwa kuwa mara baada ya kufika katika msitu huo mtuhumiwa huyo alimwamuru mama huyo kuvua nguo zote na kisha kuanza kumchanja chale mwili mzima na kumnyoa vinyweleo katika sehemu zake za siri.

      Alisema mara baada ya kumvua mama huyo nguo zote alimpaka dawa za kienyeji mwili mzima na kumuamuru mama huyo wafanya nae mapenzi kitendo mama huyo aligoma.


      Kamanda Mantage alifafanua kuwa baada ya mama huyo kukataa kufanya naye mapenzi ndipo mtuhumiwa huyo alipoanza kumtisha mama huyo kuwa ana uwezo wa kumletea nyoka ili aweze kumdhuru na ndipo mama huyo aliposhikilia msimamo wake na kisha kuvaa nguo zake na kukimbia na kumwacha mganga huyo porini.

      Alisema tukio la pili lilitokea siku mbili baada ya lile la kwanza saa 11 jioni ambapo pale mama mwingine mwenye umri wa miaka 64 mkazi wa kijiji cha Kipundu Kalla aliyekuwa akisumbuliwa na maumivu ya mkono wake wa kulia.


      Alisema kuwa mama huyo alivuliwa shanga zake 24 na kupatiwa vitisho vingi kutoka kwa mganga huyo, lakini naye aling'ang'ania msimamo wake wa kutotaka kufanya nae mapenzi na mganga huyo.


      Alisema mara baada ya taarifa hizo kulifikia jeshi hilo, msako mkali ulifanywa mara moja na kufanikiwa kumkamata mganga huyo nyumbani kwake na katika hali ya kushangaza alikutwa akiwa amevaa shanga 139 kiunoni kwake na kuongeza kuwa uchunguzi wa awali umebaini kuwa mganga huyo hakuwa na kibali cha chochote cha kumruhusu kuendesha shughuli za uganga wa jadi .


      Hata hivyo ilibainika kuwa wanawake hao wawili waliodhalilishwa na mganga huyo walikuwa wameolewa na waume zao hawakuwa na taarifa zozote za kwenda kupata matibabu kwa mganga huyo wa jadi.

      http://www.nifahamishe.com/NewsDetai...3327730&&Cat=1

    2. RukaaJuu Final

    3. #2
      eRRy's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 12th June 2009
      Location : United States
      Posts : 1,014
      Rep Power : 709
      Likes Received
      65
      Likes Given
      162

      Default Re: Mganga wa Kienyeji ashikiliwa Kwa Kudhalilisha

      Waganga wa Aina hii, Sanaa Tupu!
      "Come to me, all you who are weary and burdened, and I will give you rest."-Jesus Christ
      Matthew 11:28

    4. #3
      Masanilo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd October 2007
      Location : Swat valley, Keta Keta
      Posts : 19,117
      Rep Power : 5479
      Likes Received
      3525
      Likes Given
      1949

      Default Re: Mganga wa Kienyeji ashikiliwa Kwa Kudhalilisha

      Mh Mzidakaya anatokea huko eeehhhh

      Kindness is the language which the deaf can hear and the blind can see - Mark Twain
      CCM is enemy of GOD

    5. Miaka 50

    Similar Topics

    1. bendera ya simba kama ya mganga wa kienyeji
      By dubu in forum Jokes/Utani + Udaku/Gossips
      Replies: 0
      Last Post: 30th October 2011, 16:31
    2. Ashughulikiwa na mganga wa kienyeji..............
      By Rutashubanyuma in forum Mahusiano, mapenzi, urafiki
      Replies: 21
      Last Post: 30th December 2010, 21:20
    3. Mganga wa kienyeji!
      By Mwalimu in forum Jamii Photos
      Replies: 4
      Last Post: 14th December 2010, 12:38
    4. Mganga wa kienyeji matatani kwa kubaka..........
      By Rutashubanyuma in forum Jukwaa la Sheria (The Law Forum)
      Replies: 1
      Last Post: 3rd December 2010, 21:21
    5. mganga wa kienyeji AKA Cleric
      By Koba in forum Habari na Hoja mchanganyiko
      Replies: 1
      Last Post: 11th November 2010, 16:12

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...