wa wakina Kaka pia mnaweza kuchangia mjadala huu kuhusiana na hii kauli ya Kikwete,"“Adui wa mwanamke ni mwanamke mwenyewe, msifikiri kuwa maadui ni wanaume, wapo wanawake wasiopenda wenzao wapate ambapo huwafanyia hiana kwa madai kuwa watawapita kimaendeleo,” alisisitiza.
Kwa maoni yangu adui wa mwanamke ni ujinga unaosababishwa na wanawake wengi kukosa elimu ama kwa sheria za nchi au familia zao kutoona umuhimu wa watoto wa kike kuendelea na elimu ya juu
wa wakina Kaka pia mnaweza kuchangia mjadala huu kuhusiana na hii kauli ya Kikwete,"“Adui wa mwanamke ni mwanamke mwenyewe, msifikiri kuwa maadui ni wanaume, wapo wanawake wasiopenda wenzao wapate ambapo huwafanyia hiana kwa madai kuwa watawapita kimaendeleo,” alisisitiza.
Kwa maoni yangu adui wa mwanamke ni ujinga unaosababishwa na wanawake wengi kukosa elimu ama kwa sheria za nchi au familia zao kutoona umuhimu wa watoto wa kike kuendelea na elimu ya juu
Kwa maoni yangu,
Adui wa mwanamke ni mwanaume.
Wanawake makazini wana uwezo sawa au hata kushinda
wanaume hasa kwa umakini wa kazi zao.
Ma-boss wengi ni wanaume, hupenda kuendeleza mfumo
dume ambao ni mbaya sana. Kati ya managers kumi
wa kampuni, mwanamke atakuwa mmoja au hakuna kabisa.
Katika idara za makampuni - mfano katika benki inayomsikiliza
mteja, idara nzima ina managers wanaume, hakuna hata mwanamke
mmoja anaefikiriwa kupewa umeneja. Hii sio sawa, haiwezekani
idara nzima wanaume tu ndiyo wenye uwezo, ni vizuri kuwapa
nafasi wanawake pia.
Kwa hali kama hizi- adui wa mwanamke ni mwanaume, hasa
wasioamini kuwapa nafasi wanawake wajiendeleze-kila mtu
anahitaji pesa-si wanaume tu.
A "friend" is what the "heart" needs all the time!
Du,
Kila tatizo- basi ni mfumo dume! Hata masengenyo, wivu, umbeya je ni matokeo ya mfumo dume?
Ila nakubali kuwa wanaume wamechangia zaidi kuharibu amani na kuleta vita duniani (angalia Iraq, Middle East N.K).
Viongozi wengi ni wanaume- pengine wanawake wakipewa nafasi dunia itakuwa na amani zaidi????
Du,
Kila tatizo- basi ni mfumo dume! Hata masengenyo, wivu, umbeya je ni matokeo ya mfumo dume?
Ila nakubali kuwa wanaume wamechangia zaidi kuharibu amani na kuleta vita duniani (angalia Iraq, Middle East N.K).
Viongozi wengi ni wanaume- pengine wanawake wakipewa nafasi dunia itakuwa na amani zaidi????
Hapana, si kila tatizo.
Wapewe nafasi tuone wakishindwa.
Mwanamke mwenzie asipopenda, haizuii
yeye kupewa uongozi, huwezi kuacha kumpa
kwa kudai mwanamke mwenzie hapendi.
Wapewe waongoze.
Kwa mambo mengi mabaya wafanyayo wanaume,
ladies are not daring, mostly they think
of their families esp. kids before doing
the worst things!! This is very true!
A "friend" is what the "heart" needs all the time!
Amazingfriend,
Yes- mimi sina neno kutoa nafasi dada/mama zetu waongoze! Ikiwa pia lakina akina mama wenzao watawapa kura!
Ila kweli mwananke akipata pesa hufikiria watoto, familia na maendeleo- sisi wanaume tukipata za ziada mara zingine tunasahau wake na familia- tunakuwa kwenye pombe zaidi, na mambo ya mabibi n.k
Ila kweli wanawake wakipewa nafasi- ni wazuri tu sana- mara nyingi kuliko wanaume. Sema pia wanawake wengine hupata hizo nafasi kwa njia za mkato kupitia wanaume- hii huwavunjia heshima!
Adui wa mwanamke ni mfumo DUME period! hayo mengine ni blah blah tu.Kuwe na haki sawa kwa wanawake na wanaume ktk nafasi za kazi na masomo ili tuprove hili!Nimependa wazo la viti maalum kutolewa bungeni I hope litapita ili wanawake waingine bungeni kwa nguvu zao na sio kubebwa au vinginevyo including 'technology know who'tunalingojea hilo kwa hamu sana na hiyo itapunguza kupasha viti bungeni badala yake kutakuwa na kuchangia mada kama JK alivyosema.
Nadhani pia UWT itapitisha hilo wazo la watoto wa kike kuendelea na masomo baada ya kujifungua, hii itawasaidia kuwa na future pamoja na mtoto atakayezaliwa kwasababu mkimkatisha masomo nini hatima yake? si umaskini uliokithiri?? Napinga wazo la JK kuwa hiyo itasababisha watoto wengi kubeba mimba.
Lets think progressive here...I wish U all the best.
100% true!!!
Kutokana na kutopewa hizo nafasi, huamua kuzipata
kwa style hiyo!! What a shame!!
AF.
Amazingfriend,
Je inabidi nafasi wazipiganie au wapewe? Hizo za kupewa ndo hapo wanajivunjia heshima! Ila tatizo la Bongo kazi nyingi na hata nafasi za juu ni mlango wa nyuma! Na rushwa zipo za aina nyinyi- zote ni rushwa tu! Hata kupanda cheo unakuta rushwa! sasa tufanyeje?
Adui wa mwanamke ni mfumo DUME period! hayo mengine ni blah blah tu.Kuwe na haki sawa kwa wanawake na wanaume ktk nafasi za kazi na masomo ili tuprove hili!Nimependa wazo la viti maalum kutolewa bungeni I hope litapita ili wanawake waingine bungeni kwa nguvu zao na sio kubebwa au vinginevyo including 'technology know who'tunalingojea hilo kwa hamu sana na hiyo itapunguza kupasha viti bungeni badala yake kutakuwa na kuchangia mada kama JK alivyosema.
Nadhani pia UWT itapitisha hilo wazo la watoto wa kike kuendelea na masomo baada ya kujifungua, hii itawasaidia kuwa na future pamoja na mtoto atakayezaliwa kwasababu mkimkatisha masomo nini hatima yake? si umaskini uliokithiri?? Napinga wazo la JK kuwa hiyo itasababisha watoto wengi kubeba mimba.
Lets think progressive here...I wish U all the best.
Mashoo,
Acha kutafuta mchawi- Mfumo dume kila kitu! Wanawake pia wana tamaa ya kushindana, ktk new fashion n.k sasa hii inawweka ktk vishawishi!
Amazingfriend,
Je inabidi nafasi wazipiganie au wapewe? Hizo za kupewa ndo hapo wanajivunjia heshima! Ila tatizo la Bongo kazi nyingi na hata nafasi za juu ni mlango wa nyuma! Na rushwa zipo za aina nyinyi- zote ni rushwa tu! Hata kupanda cheo unakuta rushwa! sasa tufanyeje?
Ni vizuri kuzipigania kwa qualifications na presentations,
ila kama wanavyoteuliwa wanaume, wanawake pia iwe hivyo.
Usawa kwa mambo yote. Kumbuka si kila nafasi wanaume
mmegombea! True? Guess that will be fair enough.
Ladies are capable.
A "friend" is what the "heart" needs all the time!
Sijakataa wanawake wanashindana, wanchukiana na wanaoneana wivu nk. lakini huwezi kusema hicho ndio kinawashinda kuendelea au kupata vyeo kazini.Namini kama m'mke amepata nafasi ya kupata elimu nzuri akapata proffessional yake nzuri, kama kuna nafasi ya kazi na ana right qualification ataipata, trust me hata kama kuna mwanamke around ambaye hampendi! upo hapo? that's my point! wanawake wapewe nafasi sawa kielimu na kijamii,na hii ianzie ktk malezi nyumbani mtreat mtoto wa kike sawa na wa kiume,na tuachane na mila potofu kuwa mwanaume ndio bora zaidi na mengine yataenda sambamba!
Mimi nina maoni tofauti kuhusiana na viti maalum vya wanawake. Hata katika nchi nyingi za magharibi sasa hivi wanatafuta namna ya kuongeza idadi ya wanawake katika mabunge yao baada ya kuona kwamba mabunge yao miaka nenda miaka rudi bado idadi ya wabunge wanawake ni ndogo sana. Sijui wataamua nini ili kuongeza idadi ya wanawake katika mabunge yao maana kuna upinzani mkubwa hasa kutoka kwa baadhi ya wanaume kwamba hakuna yeyote anayestahili kupata upendeleo wa aina fulani ili kuingia bungeni.
Kuhusu bunge letu mimi naona kuna haja ya kundeleza upendeleo maalum kwa wanawake ili mradi tu wanawake watakaochaguliwa ni wasomi na wapo makini katika mambo mengi yanayoendelea Tanzania na ulimwengu kwa ujumla. Nawafahamu wanawake mbali mbali kwenye makampuni au mawizara ambao kwa maoni yangu wanastahili kabisa kuwa wabunge, lakini wakisimama na wanaume wengi hawataambulia chochote hivyo wapewe upendeleo maalum, vinginevyo asilimia 99 ya Bunge itakuwa ni wanaume.
Kwa kumalizia matatizo ya wanawake kwa maoni yangu ni wengi wao kutokupata elimu ya juu ama kutokana na mfumo uliokuwepo au wazazi kutoona umuhimu wa watoto wa kike kuendelea na elimu ya juu na mfumo dume ambao unawanyima madaraka wanawake wasomi katika nyanja mbali mbali walizosomea. Hili la adui wa maendeleo ya mwanamke ni mwanamke mimi silioni.
Mimi nina maoni tofauti kuhusiana na viti maalum vya wanawake. Hata katika nchi nyingi za magharibi sasa hivi wanatafuta namna ya kuongeza idadi ya wanawake katika mabunge yao baada ya kuona kwamba mabunge yao miaka nenda miaka rudi bado idadi ya wabunge wanawake ni ndogo sana. Sijui wataamua nini ili kuongeza idadi ya wanawake katika mabunge yao maana kuna upinzani mkubwa hasa kutoka kwa baadhi ya wanaume kwamba hakuna yeyote anayestahili kupata upendeleo wa aina fulani ili kuingia bungeni.
Kuhusu bunge letu mimi naona kuna haja ya kundeleza upendeleo maalum kwa wanawake ili mradi tu wanawake watakaochaguliwa ni wasomi na wapo makini katika mambo mengi yanayoendelea Tanzania na ulimwengu kwa ujumla. Nawafahamu wanawake mbali mbali kwenye makampuni au mawizara ambao kwa maoni yangu wanastahili kabisa kuwa wabunge, lakini wakisimama na wanaume wengi hawataambulia chochote hivyo wapewe upendeleo maalum, vinginevyo asilimia 99 ya Bunge itakuwa ni wanaume.
Kwa kumalizia matatizo ya wanawake kwa maoni yangu ni wengi wao kutokupata elimu ya juu ama kutokana na mfumo uliokuwepo au wazazi kutoona umuhimu wa watoto wa kike kuendelea na elimu ya juu na mfumo dume ambao unawanyima madaraka wanawake wasomi katika nyanja mbali mbali walizosomea. Hili la adui wa maendeleo ya mwanamke ni mwanamke mimi silioni.
BAK,
Kuendelea kuwapa nafasi za upendeleo wanawake bungeni kwa mtizamo wangu kutaendelea kuwaweka daraja la chini. lazima ifike mahali wanawake wapate nafasi kwa kuzishindia (on merit) sio kwa favor. Ikiwa tutaendeleza mtindo wa nafasi za upendeleo tutasahau kuwa wanatakiwa wawe kwenye equal footing na wanaume
kama kweli wananwake wanataka kuwa na nafasi sawa na wanaume katika ngazi mbalimbali ni lazime wawe na courage ya kuzipigania, kuchagua wanawake wenzao, na kuacha kile kinachoitwa PHD(Pull Her Down) Ukweli ni kwamba anayemshusha mwanamke ni mwanamke mwenzie...stereotyping iko kwenye akili za mwanamke sio mwanaume..tukubali ukweli tuanzie hapo; wanaume wanachukulia pale wanawake walipoachia..yaani, mwanamke anajidharau, au anamdharau mwanamke mwenzie, ndipo mwanamume anapata courage ya kumkandamiza/kumdharau mwanamke husika
Vikao vya wanaume kumzungumzia mwanamke vinahusiana na mambo kadhaa ya tabia au mahusiano yake na wanaume; lakini vya wanawake dhidi ya wanawake wenzao ni vya mauaji (character assasination)ya hali ya juu ya sifa za mwanamke husika tena kwa sababu za kizushi/wivu/binafsi/ na mambo kama hayo
Ni mjadala mkali, lakini kama kuna mtu atakayetoa excuse ya mfumo dume, basi asiache kusema mwanamke nadiye anayetake part ya kuunda huo mfumo dume. Nadhani wanaume wengi vidume dunia hiyo walizaliwa na kina mama9 Mbali na waliozaliwa kwa chupa) na kulelewa zaidi na kina mama. Kwa kina mama wanapart kubwa ya lawama kuhusu huo mfumo.
Tunachotakiwa kinadada ni KUJIAMINI. Hizi special favours ndio zinatufanya tuonekane "wanyonge". What a man can do we can also do.
Shida ni pale tunapotaka kutumia "uanamke" ku win over men or over other females.
Msimamo wangu ni kwamba apart from getting education...take us to school. We do not need any favours!
Mama lao,
suala ni
-Kujiamini
-Kujiheshimu
-Elimu
-Exposure (nina maana huwezi kugombea uongozi ikiwa hujui A,B,C zake..na wala hujui pa kuanzia...)
-Support (from family/husband/fellow women
..mengine yafuate
Sasa najaribu kupiga picha najikuta ni flash tu zinatokea na picha zinaungua tu. You know why? Pingeni WAZIWAZI hii kitu ya viti vya upendeleo Bungeni. Hapo nitakupeni credit kuwa sasa wanawake wameamua!
Pingeni bila kuchoka! Pingeni pia suala la mahari kutolewa na mwanaume mkitoa mbadala wa hayo. Bado mna safari ndefu sana mama zanguni. Napenda kukuungeni mkono lakini elewa katika wanawake 100 ni 5 tu ambao wako imara karibia na wanaume katika mambo mengi.
Well, si wanaume wote wanawa-beat wanawake. Hilo liko wazi; Mwenyezi Mungu hakukosea kuwawekeni kuwa wasaidizi wetu ati... Ninyi ni kila kitu kwa mwanaume. Bila ninyi hatujiwezi; watapinga wengi hili lakini ukweli ndio huo! Mwanamke ni nuru ya mwanaume na mabavu ya mwanaume huisha kwa mwanamke... Labda awe nunda tu!
Lakini...
Haiba ya mwanamke si kuwa hajiwezi; utaiona kazi na uwezo wake kwa mwanaume aliyeoana nae au mwenzake wa ndoa. Never feel down; wale wanaowabeza au kuwafikiria vinginevyo wana mifumo dume vichwani mwao lakini ukweli wa mambo u ndani ya vichwa vyao.
BAK,
Kuendelea kuwapa nafasi za upendeleo wanawake bungeni kwa mtizamo wangu kutaendelea kuwaweka daraja la chini. lazima ifike mahali wanawake wapate nafasi kwa kuzishindia (on merit) sio kwa favor. Ikiwa tutaendeleza mtindo wa nafasi za upendeleo tutasahau kuwa wanatakiwa wawe kwenye equal footing na wanaume
kama kweli wananwake wanataka kuwa na nafasi sawa na wanaume katika ngazi mbalimbali ni lazime wawe na courage ya kuzipigania, kuchagua wanawake wenzao, na kuacha kile kinachoitwa PHD(Pull Her Down) Ukweli ni kwamba anayemshusha mwanamke ni mwanamke mwenzie...stereotyping iko kwenye akili za mwanamke sio mwanaume..tukubali ukweli tuanzie hapo; wanaume wanachukulia pale wanawake walipoachia..yaani, mwanamke anajidharau, au anamdharau mwanamke mwenzie, ndipo mwanamume anapata courage ya kumkandamiza/kumdharau mwanamke husika
Vikao vya wanaume kumzungumzia mwanamke vinahusiana na mambo kadhaa ya tabia au mahusiano yake na wanaume; lakini vya wanawake dhidi ya wanawake wenzao ni vya mauaji (character assasination)ya hali ya juu ya sifa za mwanamke husika tena kwa sababu za kizushi/wivu/binafsi/ na mambo kama hayo
sorry dadas, you gotta start with yourselves
Kama tunataka Bunge letu lionyeshe hali halisi ya nchi yetu kwamba ina wanawake na wanaume ili kufanikisha hili basi upendeleo wa viti maalum vya akina mama inabidi uendelee ili mradi tu watakaoteuliwa ni wasomi na wana uwezo sio tu wakuwa wabunge bali pia mawaziri.
Kutaka wanawake wagombee na wanaume basi bunge litajaa wanaume na kwa maoni yangu hili si jambo jema kwa maendeleo ya nchi yetu.
Kwanza wagombea wanaume ndio watoa takrima (RUSHWA)wazuri wakati wa kampeni kwa kuangusha mapilau dhidi ya wafuasi na hata wasio wafuasi, kuwapeleka bar wanywe mpaka wawe chakarii na hata kuwapa pesa pia.
Pili kuna wapiga kura ambao hata kama mwanamke ana qualifications zaidi ya mwanaume basi watakuwa radhi kumpigia kura mwanaume(mfumo dume) badala ya mwanamke.
Marekani ambayo imepata uhuru wake mwaka 1776, miaka 231 iliyopita mpaka leo kuna watu wanasema "America is not ready for a Woman president." hili mimi linanishangaza sana. Kwenye senate yao ya watu 100 wanawake hawafiki hata 20!! kwenye Congress ya watu 450 wanawake kama sikosei hawafiki hata 100.
Wanawake wameshaonyesha kama wanauwezo kama wanaume. Wanarusha ndege, wanafuzu Phd, Masters katika fields mbali mbali masters na wakipewa nafasi ya kuongoza pia wanafanya vizuri tu, lakini kizingiti chao kikubwa ni mifumo dume katika nchi mbali mbali duniani.
Kwa hiyo bado Tanzania tuna haja ya kuendeleza upendeleo maalum kwa viti vya wanawake, kama tunataka Bunge la wanaume watupu basi tuufute huu upendeleo na matokeo yake tutayaona.
Kama tunataka Bunge letu lionyeshe hali halisi ya nchi yetu kwamba ina wanawake na wanaume ili kufanikisha hili basi upendeleo wa viti maalum vya akina mama inabidi uendelee ili mradi tu watakaoteuliwa ni wasomi na wana uwezo sio tu wakuwa wabunge bali pia mawaziri.
Kutaka wanawake wagombee na wanaume basi bunge litajaa wanaume na kwa maoni yangu hili si jambo jema kwa maendeleo ya nchi yetu.
Kwanza wagombea wanaume ndio watoa takrima (RUSHWA)wazuri wakati wa kampeni kwa kuangusha mapilau dhidi ya wafuasi na hata wasio wafuasi, kuwapeleka bar wanywe mpaka wawe chakarii na hata kuwapa pesa pia.
Pili kuna wapiga kura ambao hata kama mwanamke ana qualifications zaidi ya mwanaume basi watakuwa radhi kumpigia kura mwanaume(mfumo dume) badala ya mwanamke.
Marekani ambayo imepata uhuru wake mwaka 1776, miaka 231 iliyopita mpaka leo kuna watu wanasema "America is not ready for a Woman president." hili mimi linanishangaza sana. Kwenye senate yao ya watu 100 wanawake hawafiki hata 20!! kwenye Congress ya watu 450 wanawake kama sikosei hawafiki hata 100.
Wanawake wameshaonyesha kama wanauwezo kama wanaume. Wanarusha ndege, wanafuzu Phd, Masters katika fields mbali mbali masters na wakipewa nafasi ya kuongoza pia wanafanya vizuri tu, lakini kizingiti chao kikubwa ni mifumo dume katika nchi mbali mbali duniani.
Kwa hiyo bado Tanzania tuna haja ya kuendeleza upendeleo maalum kwa viti vya wanawake, kama tunataka Bunge la wanaume watupu basi tuufute huu upendeleo na matokeo yake tutayaona.
Bubu,
Napenda your reaction- as a realist! Ni vema wanawake wapewe nafasi za upendeleo kwa sasa- hadi hapo wengi watakapokuwa na elimu na kuanza kupambana na mfumo dume kwa kura. Huu mfumo dome umekuwepo miaka maelfu- inashangaza leo eti JK anasema haungi mkono Viti maalumu! Tuna uhuru miaka 40 tu- hizi sababu za kihistoria zitachukua mda kusahihisha- sii leo au miaka 10 pengine miaka 50 ijayo!
Licha ya Marekani angalia hapa Afrika out of 53 states kuna raisi mmoja tu Mwanamke! Middle East Hakuna!
Kwa hiyo wakati wanawake ndo wanasoma kwa wingi sasa wanasoma viti maalumu muhimu. Otherwise basi CCM waamue baadhi ya majimbo wagombee akina mama tu (say 40% of majimbo)- ila hii itakuwa ni ukiukaji wa haki za wanaume who are capable! Angalia hata waliojitokeza kugombea CCM- 85% ni wanaume!
Rome was not built in one day!
Halafu Bubu angalia hata hapa JF wengi ya wanawake wanaongea tu- pamoja huwa ni wasomi wazuri- ukiwaambia wagombee- wapi?
Follow Us Here