Watanzania wakataa shirikisho Afrika Mashariki - JamiiForums |The Home of Great Thinkers

Go Back   JamiiForums |The Home of Great Thinkers > Public Forums > Habari na Hoja mchanganyiko


Habari na Hoja mchanganyiko Una jambo umeliona kutoka chanzo chochote cha habari? Usisite, liweke hapa uwahabarishe wenzako. Hoja binafsi pia ziwekwe hapa.


Reply
 
LinkBack Thread Tools Rate Thread Display Modes
Old 14th July 2007, 05:23 PM   #1
Watanzania wakataa shirikisho Afrika Mashariki
Bubu Ataka Kusema Bubu Ataka Kusema is offline 14th July 2007, 05:23 PM

Watanzania wakataa shirikisho Afrika Mashariki
*Asilimia 76 hawataki liwepo kabisa
*Kikwete asema maoni hayo yataheshimiwa

Na Ramadhan Semtawa

KAMATI ya kukusanya maoni kuhusu uharakishwaji (fast tracking) wa uanzishwaji wa Shirikisho la Kisiasa la Afrika Mashariki, imewasilisha ripoti yake kwa Rais Jakaya Kikwete, huku asilimia 75.9 ya Watanzania, wakipinga mpango huo.

Ripoti hiyo inaonyesha jinamizi la kero za muungano bado linaitafuna Tanzania, kwani idadi hiyo iliyopinga, imetaka kwanza kero hizo zitatuliwe kabla ya kukimbilia kwenye shirikisho.

Wakati hao wakipinga baada ya kuulizwa, wengine asilimia 3.3, bila ya kuulizwa, walituma maoni yao kukataa kabisa kuwepo kwa shirikisho hilo.

Akiwasilisha ripoti hiyo Ikulu jijini Dar es Salaam jana, Mwenyekiti wa kamati ya kukusanya maoni kuhusu mpango huo, Profesa Samwel Wangwe, alisema asilimia 20.8, waliunga mkono mpango huo kasi.

Katika ripoti hiyo, inaelezwa kuwa jumla ya Watanzania 65,000 walipata fursa ya kutoa maoni yao katika mikoa na wilaya zote, ambazo kamati ilifika.

Ripoti hiyo ambayo imegawanyika katika vitabu viwili pamoja na mkanda wa video, imegawanwa katika makundi mawili ambayo ni kisiasa na jamii.

Inaeleza kwamba Watanzania waliopinga shirikisho wamekuwa na sababu mbalimbali, ambazo moja ni ya kisiasa, kwamba hawalifahamu shirikisho hilo.

Sababu nyingine ni pamoja na demokrasi na utawala bora, ambapo Watanzania wana shaka kama vitu hivyo viwili vipo katika nchi nyingine.

Watanzania hao pia wameangalia suala la ulinzi, usalama na amani na tofauti za kiitikadi na pia walipinga kutokana na tofauti ya maendeleo ya kiuchumi kati ya nchi hizo na Tanzania hasa kulinganisha na Kenya.

Sababu nyingine ni kutaka kwanza, Tanzania itatue kero zake za muungano na Zanzibar kwani hadi sasa hazijamalizwa.

Akizungumza sababu za kuchelewa kuwasilisha ripoti hiyo, Profesa Wangwe, alisema kamati ilichukua maoni kwa njia mbalimbali ambazo ni pamoja na vyombo vya habari, kujaza dodoso na mtandao wa kompyuta kwa ajili ya kuwezesha hata Watanzania walio nje kupiga kura.

Rais Kikwete akizungumzia suala hilo, alisema maoni hayo ya Watanzania yataheshimiwa.

Alisema ingekuwa ni tatizo kama Watanzania hao wangesema hawataki shirikisho, lakini kwa kuwa hawataki liharakishwe, yeye haoni kama ni tatizo.

Rais Kikwete alisema ripoti hiyo itapelekwa katika ngazi ya Baraza la Mawaziri, ili ifanyiwe kazi na kisha kupelekwa katika wizara husika ya Afrika Mashariki kwa ajili ya kuendelea na mchakato.

Kama maoni hayo yatazingatiwa, mchakato wa kuundwa kwa shirikisho utakwenda kama ilivyoelezwa katika mkataba wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC).

Tayari hadi sasa nchi za EAC, zimeanza kutumia mfumo mmoja wa forodha (Customs Union), huku makubaliano mengine kama soko la pamoja (Common Market), sarafu ya pamoja (Monetary Union) na shirikisho la kisiasa (Political Federation) yakiwa bado hayajakamilika.

Tume hiyo ilianza kazi yake Oktoba 13 mwaka jana na imekabidhi ripoti yake Julai 13, ikiwa ni zaidi ya miezi sita imepita tangu ripoti hiyo ilipotakiwa kuwasilishwa.

 
Bubu Ataka Kusema's Avatar
Bubu Ataka Kusema
JF Premium Member
Points: 12,707,061, Level: 100 Points: 12,707,061, Level: 100 Points: 12,707,061, Level: 100
Activity: 50% Activity: 50% Activity: 50%
Join Date: Sun Feb 2007
Location: Mfaranyaki
Posts: 12,694
Thanks: 1,055
Thanked 1,211 Times in 704 Posts
Views: 327
Reply With Quote
  #2  
Old 14th July 2007, 06:47 PM
Koba Koba is offline
Koba has no status.
JF Senior Expert Member
Points: 279,454, Level: 100 Points: 279,454, Level: 100 Points: 279,454, Level: 100
Activity: 13% Activity: 13% Activity: 13%
 
Join Date: Tue Jul 2007
Location: Pasadena California
Posts: 3,262
Thanks: 87
Thanked 100 Times in 68 Posts
Rep Power: 29
Koba will become famous soon enoughKoba will become famous soon enoughKoba will become famous soon enoughKoba will become famous soon enoughKoba will become famous soon enoughKoba will become famous soon enoughKoba will become famous soon enoughKoba will become famous soon enough
Default

hata wakati wa kukusanya maoni ya vyama vingi 80% ya watanzania walikuwa hawataki vyama vingi..same thing here na FEDERATION itakuja tuu na kitu kizuri sana,dunia ya leo hatutaki kubanwabanwa acha tupanue nchi na uhuru wa kwenda popote na kufanya chochote as long as unaheshimu sheria na ujinga kama watu wa BOT na Richmond nakuhakikishia hautatokea
Reply With Quote
  #3  
Old 23rd October 2008, 08:14 PM
Bubu Ataka Kusema's Avatar
Bubu Ataka Kusema Bubu Ataka Kusema is offline
Bubu Ataka Kusema says life is GOOD!
JF Premium Member
Points: 12,707,061, Level: 100 Points: 12,707,061, Level: 100 Points: 12,707,061, Level: 100
Activity: 50% Activity: 50% Activity: 50%
 
Join Date: Sun Feb 2007
Location: Mfaranyaki
Posts: 12,694
Thanks: 1,055
Thanked 1,211 Times in 704 Posts
Rep Power: 2049
Bubu Ataka Kusema is one of most respected JF members!Bubu Ataka Kusema is one of most respected JF members!Bubu Ataka Kusema is one of most respected JF members!Bubu Ataka Kusema is one of most respected JF members!Bubu Ataka Kusema is one of most respected JF members!Bubu Ataka Kusema is one of most respected JF members!Bubu Ataka Kusema is one of most respected JF members!Bubu Ataka Kusema is one of most respected JF members!Bubu Ataka Kusema is one of most respected JF members!Bubu Ataka Kusema is one of most respected JF members!Bubu Ataka Kusema is one of most respected JF members!
Default Shirikisho A. Mashariki lapigwa mwereka

Date::10/23/2008
Shirikisho A. Mashariki lapigwa mwereka
Na Ramadhan Semtawa
Mwananchi

UAMUZI wa wakuu wa nchi 26 za Afrika kuunganisha soko la pamoja katika nchi hizo, umeondoa ndoto ya kuanzisha shirikisho la kisiasa la Jumuiya ya Afrika Mashariki.

Hatua hiyo inatokana na mpango wa wakuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) na Jumuiya ya Soko la Pamoja kwa Nchi za Kusini na Mashariki mwa Afrika (Comesa), kuanzisha mchakato huo ambao utameza mambo ya jumuiya hizo.

Shirikisho la Afrika Mashariki linahusisha nchi za Tanzania, Uganda, Kenya, Burundi na Rwanda na tayari nchi hizo zilishapiga hatua kubwa kuelekea kuwa kitu kimoja, huku mabilioni ya fedha yakiwa yametumika katika mchakato huo, ambao pia ulihusisha kutafuta maoni kwa wananchi.

Baadhi ya taasisi za Shirikisho la Afrika Mashariki zilishaanza kufanya kazi, ikiwemo sekretarieti inayoratibu shughuli zote za shirikisho hilo, bunge, mahakama huku mamilioni mengine yakitumika kujenga ofisi za makao makuu mjini Arusha, lakini uamuzi uliofanywa juzi unaweza kuwa mwanzo za kuzorota kwa harakati hizo.

Akijibu swali kutoka gazeti hili kuhusu uamuzi huo wakuu wa nchi 26 uliofanywa nchini Uganda, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernad Membe alisema ni dhahiri hapo baadaye kama mchakato utakwenda kama ulivyo, shirikisho hilo halitakuwepo.

"Dah..., ndiyo, halitakuwepo, kadri tunavyokwenda katika mpango huu wa kuunganisha soko la nchi zetu hizo za jumuiya tatu, ni dhahiri kuna mambo yatabidi yajiondoe," alisema.

Membe alifafanua kuwa mpango huo wa kuunganisha jumuiya tatu unalenga kuwezesha kuwepo soko kubwa la pamoja la watu 527 milioni na mfumo wa forodha.

Hata hivyo, alisema mchakato wa kuelekea soko la pamoja kwa EAC bado unaendelea na kwamba, kama ni kusitishwa, basi hiyo itakuja kufahamika baadaye baada ya mchakato wa jumuiya hizo tatu.

"Lakini mchakato ndani ya EAC ambao tumefikia sasa kuhusu Common Market (soko la pamoja), bado unaendelea, huku taratibu za soko jipya nazo zikiendelea,"alifafanua.

Membe alisema katika mchakato huo wa jumuiya tatu, wakuu hao wameunda timu ya kuangalia taratibu za kisheria kwa ajili ya kutafuta uhalali wa jambo hilo.

"Sasa, katika kufanikisha mpango huo wa kuanzisha soko kubwa kwa kuunganisha Comesa, Sadc na EAC, wakuu wameamua kuunda timu ya wataalamu ambayo itafuta uhalali kisheria," alisisitiza.

Kwa ufafanuzi, Membe alisema timu hiyo itafanya kazi kwa kipindi cha miezi sita kuona njia bora za kuweza kufanikisha ndoto hiyo.

Alisema kuanzishwa kwa soko kubwa la pamoja katika ukanda huo kwa kuunganisha ukanda wa Kusini, Kati na Mashariki ya Afrika hadi Misri, kutakuwa na faida kubwa kwa maendeleo ya ukanda huu.

"Kwa hiyo, kuanzisha Free Trade Area, kuna manufaa makubwa ikiwa ni pamoja na kuweza kukaribiana na matatizo mbalimbali kama misuko misuko ya kuanguka kwa taasisi za kifedha katika mataifa makubwa," alisisitiza.

Membe alisema eneo hilo lina wakazi hao 527 milioni kati ya idadi jumla ya wakazi wa Afrika ambao ni 940 milioni, ambao wanachukua sehemu kubwa ya bara hilo.

Waziri Membe alitetea kuwa China imekuwa ikipata maendeleo kutokana na kuwa na idadi kubwa ya watu hivyo biashara inayofanyika nayo pia huwa kubwa.

Katika Shirikisho la Afrika Mashariki inatarajiwa kuwapo maingiliano makubwa zaidi ya kiuchumi na biashara, pia kuondolewa vikwazo vya kufanya kazi baina ya mataifa hayo pamoja na masuala muhimu ya uwekezaji katika ardhi suala ambalo limezua utata miongoni mwa mataifa hayo, huku mengine yakipinga hatua hiyo.

Katika hatua nyingine, Membe alisema wakuu hao wamejadili kwa kina mambo yanayoendelea katika nchi za Somalia, Burundi na Mauritania.

Alisema kwa upande wa Burundi msuluhishi wa mgogoro huo ambaye ni Waziri wa Usalama wa Afrika Kusini, Charles Nqakula, alitoa utekelezaji wa mpango wa amani nchini humo.

Hata hivyo, alisema hadi sasa mpango huo umekwama kutokana na kundi la FNL Palipehutu lilanalongozwa na Agathon Rwasa, kukaata kubadili jina la kundi hilo ili kuondoa dhana ya ukabila ambayo inapingana na katiba.

Kuhusu kuingizwa katika serikali, alisema kundi hilo linadai kuwa na jeshi kubwa msituni ambalo ni takriban askari 21,000 lakini linashindwa kuthibitisha huku likidai fedha nyingi kwa ajili ya kuwalipa.
__________________
~*~Life is Good~*~
Reply With Quote
Reply

Bookmarks

Tags
afrika, mashariki, shirikisho, wakataa, watanzania


Currently Active Users Viewing This Thread: 1 (0 members and 1 guests)
 
Thread Tools
Display Modes Rate This Thread
Rate This Thread:

Posting Rules
You may not post new threads
You may not post replies
You may not post attachments
You may not edit your posts

BB code is On
Smilies are On
[IMG] code is On
HTML code is Off
Trackbacks are Off
Pingbacks are Off
Refbacks are On


Similar Threads
Thread Thread Starter Forum Replies Last Post
Kazi ya kuubomoa upinzani ndiyo imeanza ama inatekelezwa? Mugishagwe Jukwaa la Siasa 12 2nd February 2010 10:21 AM
East African Federation (EAF) Views nmkenda International Forum 1186 19th November 2009 05:38 AM
Watanzania bado wamelewa Ujamaa! Rev. Kishoka Jukwaa la Siasa 196 12th November 2009 05:32 PM
Profesa Wangwe anapotosha ukweli Lunyungu Habari na Hoja mchanganyiko 0 13th May 2007 09:46 AM
Lowassa ahudhuria mkutano wa Afrika na Ufaransa MwanaCCM Habari na Hoja mchanganyiko 0 16th February 2007 05:21 AM

Tuma Ukurasa huu kwa rafiki yako!


All times are GMT +3. The time now is 06:33 AM.

Powered by JamiiForums.com
Copyrights reserved to JamiiForums.com