Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Zanzibar: Padre apigwa Risasi na watu wasiojulikana

    Report Post
    Page 11 of 23 FirstFirst ... 91011121321 ... LastLast
    Results 201 to 220 of 441
    1. DSN
      #1
      DSN's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 1st April 2011
      Location : Home Tanzania
      Posts : 1,443
      Rep Power : 4453
      Likes Received
      690
      Likes Given
      576

      Default Zanzibar: Padre apigwa Risasi na watu wasiojulikana

      Kwa mujibu wa Breaking News Sasa hivi toka Radio One, Padre anayejulikana kwa jina la Ambrose Mkenda amepigwa Risasi na Watu wasiofahamika kwenye gate la nyumbani kwake wakati akifunguliwa gate aingie nyumbani kwake maeneo Kitomondo Mjini Zanzibar, ambako ndiko makazi yake yalipo akiwa ndani ya gari aliyokuwa akiendesha pekee yake.

      Hali yake sio nzuri kwani Risasi aliyopigwa imemdhuru maeneo ya mdomoni.

      Waliompiga Risasi Padre huyo inasemekana ni watu waliokuwa kwenye pikipiki, ambao walimvamia akisubilia afunguliwe gate kuingia nyumbani kwake.

      Kuna nini? Katika siku muhimu kwa waumini wa Kikristo kufanyika kwa tendo kama ilo kwa kiongozi wa madhehebu makubwa kama Roman Catholic.

      Wanaojua kinachojili huko Zanzibar watujuze Tafadhari kulikoni, katika siku njema kama hii ya Christmas.

      NOTE:
      Ujumbe Mkuu wa Kanisa La Roman Catholic katika Christmas ya mwaka huu 2012:
      "UPENDO NA AMANI NDIO UJUMBE MKUMBWA WA SIKUKUU HIYO"


      Picha kwa niaba ya Mwanajamii forum kwa ID ya Mchami


      TAARIFA YA LEO TAREHE 26/12/2012 KWENYE VYOMBO VYA HABARI KUHUSU TUKIO:
      Father Ambros Mkenda wa Parokia ya Mpendae katika Kanisa Katoliki Mjini Zanzibar amepigwa risasi na watu wasiojulikana nje ya nyumba yake majira ya saa 12 jioni wakati akitokea kanisani

      Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Mjini Magharibi Aziz Juma Mohammed amethibitisha kutokea kwa tukio hilo ambalo alisema Father amepigwa risasi na ameumizwa sehemu ya kichwa na amekuwa akitoka damu nyingi kichwani na tayari anapatiwa matibabu katika hospitali kuu ya Mnazi Mmoja.

      Alisema jeshi la polisi linaendelea na uchunguzi wa tukio hilo ili kubaini wahusika walifanya uhalifu huo kwa madhumuni gani kabla ya kuchukuliwa hatua za kisheria.

      “Sisi tunahesabu kuwa kitendo hiki ni kitendo cha kihalifu na tunawatafuta wahalifu waliofanya kitendo hiki kwa hivyo bado ni mapema kusema kwamba kitendo hiki kimefanywa na nani kwa kuwa bado uchunguzi wetu unaendelea na hadi sasa hakuna mtu tuliyemshika kuhusikana na tukio hili” alisema Kamanda.

      Kamanda Aziz akisimulia tukio hilo alisema walipata taarifa majira ya saa 2 na kwenda katika eneo la tukio ambapo Father alikuwa akitokea kanisani na kutaka kuelekea nyumbani kwake wakati akiwa ndani ya gari ndipo aliposhambuliwa na watu wasiojulikana na kuanguka.

      “Tumekuta mabaki ya risasi ndani ya gari yake na katika vioo vyake vya gari vimevunjika na tumekuta damu chini pale” alisema Kamanda.

      Aidha Kamanda Azizi alisema Father Ambros yeye ni mhasibu pale kanisani na hivyo mara nyingi watu wananaamini kwamba katika siku za krismass mara nyingi sadaka hukusanywa fedha nyingi na hivyo wanamini kwamba alikuwa fedha mikononi na ndipo inawezekana waliamua kumpiga risasi wakitaka kuchukua fedha hizo.

      Hata hivyo alisema uchunguzi wa awali ndio utakaoeleza ni suala gani lililopelekea kupigwa risasi lakini wanaendelea na uchunguzi huo ambapo uchunguzi ndio utakaojulikana sababu kamili ya tukio hilo.

      Akizungumzia tukio hilo, Askofu Michael Hafidh wa Kanisa la Anglikan la Mkunazini amesema wamesikitishwa na wamepokea kwa mshituko mkubwa tukio hilo hasa kwa kuzingatia matukio kama hayo hayajawahi kutokea ya kuwahujumu viongozi wa dini.

      Alisema tukio hilo ni miongoni mwa matukio ya kushtusha na yanaashiria hali mbaya ya kiusalama na kuwaomba viongozi wa serikali kuchukua hatua za tahadhari kubwa kwani matukio kama hayo yameanza kutokea kwa viongozi wa dini ambapo mwanzo ilianzia kwa Sheikh Soraga na baadae kutokea kwa Father Ambros.

      “ Hii ni hali ya hatari katika nchi yetu na haipendezi lakini serikali lazima ijue sisi hatuwezi kujua wala hatuwezi kujilinda lakini serikali inapaswa kutulinda sisi ndio wananchi wake” alisema Askofu Hafidh.

      Askofu Hafidh alisema hivi karibuni kumekuwepo vipeperushi vilivyosambazwa na watu vikiwatisha watu wenye imani ya kikristo ambapo alisema miongoni mwao walikuwa na khofu juu ya kusambazwa kwa vipeperushi hivyo na kuiomba serikali iongeze ulinzi.

      “Tumeona hivi vipeperushi na kwa kweli tulikuwa na khofu juu ya vipeperushi hivi lakini ndio tunasema tunaelekea wapi katika maisha haya” alisema Akofu Hafidh.

      “Sisi hatuamini kwamba kuna kisasi kwa viongozi wa dini lakini tunachukulia hilo ni tukio la kihalifu na pia hatuna vipeperushi vya aina yoyote vinavyoelezea kuwatisha viongozi wa dini kwa hivyo tunachukulia hayo ni matukio ya kihalifu na wala hatuamini kwamba matukio haya ni ya dini fulani” alisema Kamanda Azizi.

      Akielezea kuhusiana na hilo Kamanda Aziz alisema jeshi la polisi limejipanga na kuzidisha ulinzi katika maeneo yote ya makanisa ambapo kumesambazwa polisi wa kutosha kwa kuwa wanajua wakati wa sherehe mambo ya kihalifu hujitokeza.

      “Sisi kawaida huwa tunaweka ulinzi siku za sherehe zozote lakini kwanza makanisa yote yamewekwa ulinzi wa kutosha kabisa lakini wahalifu wanapotaka kufanya uhalifu huwezi kujua watatumia mbinu gani na saa ngapi na watafanya uhalifu huo wapi, lakini ulinzi upo wa kutosha” alisisitiza Kamanda Aziz.
      Last edited by DSN; 26th December 2012 at 09:08.
      Invisible, Elli, Pasco and 5 others like this.

    2. Miaka 50

    3. #201
      hodogo's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 11th March 2012
      Posts : 235
      Rep Power : 410
      Likes Received
      90
      Likes Given
      59

      Default Re: Zanzibar: Padre adaiwa kupigwa Risasi

      Quote By Mdondoaji
      Kim ,

      Shida watu wanaumwa bado na propaganda za udini. Ila wakristo ndugu zanguni ni vema mtafakari hili swala la mfumo kristo nchini. Ubaguzi unaondelea unajenga chuki na matabaka na mwishoe kila jambo linatfsiriwa kwa udini na chuki.

      Nilikuwapo

      Falsafa ya mfumo kristo ni falsafa mufilisi inayobebwa na watu waliofilisika kifikra, ambao wanajitahidi "kuibaka" historia kwa kutoa hata takwim bila tathmini ya kitaalamu.

      Kwa mtazamo wako Mdonoaji, kujaribu kuturejesha kwenye mada hii wakati tukitafakari vitendo vinavyoashiria uvunjifu wa amani nchini, inatia shaka, inawezekana wewe ni msemaji wa hiki kikundi na unajaribu kupima joto la jamvi!

    4. #202
      kelao's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 24th September 2012
      Posts : 960
      Rep Power : 923
      Likes Received
      141
      Likes Given
      8

      Default Re: Zanzibar: Padre adaiwa kupigwa Risasi

      So sad!lakini kama ni uchokozi dhidi ya kanisa Catholic wajue watapata matatizo makubwa.tunamwombea huyo padre apone haraka.hao watu wanaosukuma hayo mambo ya kidini Mungu atawashushia mkono wake wenye nguvu.
      DSN likes this.

    5. #203
      dkirenga's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 21st December 2012
      Posts : 148
      Rep Power : 352
      Likes Received
      21
      Likes Given
      0

      Default Re: Zanzibar: Padre adaiwa kupigwa Risasi

      Asalaa wana JF kweli inaumiza sana kuwadhuru viongozi wa dini tupate wapi Amani ndugu zangu

    6. #204
      kwamwewe's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 15th July 2010
      Posts : 856
      Rep Power : 5406
      Likes Received
      99
      Likes Given
      125

      Default Re: Zanzibar: Padre adaiwa kupigwa Risasi

      Quote By Buntungwa
      Tumechoshwa na kauli za kijinga namna hii.
      kauli nyengine za kijinga ni kama hizi, hasa watu wanapokuwa hawataki kuoa na kupenda kuchukua vya watu

      yaweza kutokea hata haya

      KARIBU MLIMA SAYUNI...UWANJA WA UWAZI NA UKWELI KUHUSU MASUALA YOTE YA KIBIBLIA NA UKRISTO: Mchungaji Auwawa kwa baada ya kufumaniwa


      kauli nyengine za kijinga ni hizi http://www.bongo5.com/padri-atiwa-mb...-kifo-05-2007/

    7. #205
      kelao's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 24th September 2012
      Posts : 960
      Rep Power : 923
      Likes Received
      141
      Likes Given
      8

      Default

      Quote By Bilal Yussuf
      please msikimbilie kujenga hoja au kuhusisha jambo hili na udini mana inawezekana padri ana visasi na kundi ama mtu fulani nje au ndani ya kanisa.
      naomba tuliachie jeshi la polisi lifanye kazi yake kisha tusubiri ripoti yao itakavyo sema.
      jeshi la police lipi ndugu yangu? Hili hili la CCM au lingine!

    8. RukaaJuu Final

    9. #206
      hodogo's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 11th March 2012
      Posts : 235
      Rep Power : 410
      Likes Received
      90
      Likes Given
      59

      Default Re: Zanzibar: Padre adaiwa kupigwa Risasi

      Quote By abdul 28
      uthaifu wa watanganyika jamii forums
      1) kushindwa kufikiria nini chanzo matatizo ni nini
      kulisukuma au kulihusisha tatizo hili na uamsho
      kushabikia udini
      vipi mtu haija thibitishwa hata na serekali ukurupuke na kusema uamsho hao
      jiulize kwa nini uamsho haijafutwa kisheria


      CHANZO CHA MATATIZO CCM NA SEREKALI YAKE KUTUMIA SERA YA DINI KUFICHA UHALISIA HILI HALITA WASAIDIA
      utamsikia kesho kutwa Benard Member atawambia umoja wa EU na jumuiya za kimataifa ya kuwa uwamsho wameuwa Padri zanzibar waisilamu wanawaonea waikristo zanzibar
      hii ni kuificha dhana ya wazanzibar kudai nchi yao juu ya jumuiya za kimataiofa

      zanzibar matokeo ya kuuliwa viongozi wa dini sio mageni askari wa FFU walimpiga shekhe wa msikiti wa mtendeni risasi ndani ya msikiti na ziko kesi nyingi ila hawa askari ubaya ubaya huzizima kutiwa tindi kwa shekhe suraga

      sasa wana jamii fikirieni kwa makini hasa watanganyika
      ccm na serekali yake wasipindishe mnadai ya uamsho uamsho wanataka nchi yao sio chengine huu ni udhaifu wa ccm na raisi wao usalama wa taifa na polisi
      Wewe ni msemaji wa uamsho? Hujashuhudia serikali ikionekana kama inafumbia macho baadhi ya matukio katika jamii kutokana na mgongano wa masilahi kwa watendaji hao serikalini?

      Ndio maaana marehemu Baba wa Taifa alipokua anasisitiza dhamira Za kauli za kisiasa kuendana na matendo katika maisha halisi ya wanasiasa, alitumia kauli kama "KUIMBA KIJAMAA NA KUCHEZA KIBEPARI!" Ishi unachokihubiri na kukiamini! Ndo maana siku hizi wanasiasa wanadai kupiga vita ufisadi ili hali wenyewe ni mafisadi wakubwa!!

    10. #207
      tedo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 17th August 2011
      Location : uchochoroni
      Posts : 5,500
      Rep Power : 4640
      Likes Received
      1260
      Likes Given
      880

      Default Re: Zanzibar: Padre adaiwa kupigwa Risasi

      Ohhh my God....nini tena jamani..sasa nakumbuka ule uzi wa Mzee Mwanakijiji.

    11. #208
      Zuwely salufu's Avatar
      Member Array
      Join Date : 7th October 2012
      Posts : 85
      Rep Power : 350
      Likes Received
      15
      Likes Given
      0

      Default Re: Zanzibar: Padre apigwa Risasi na watu wasiojulikana

      Amani itawale znz kwa nini znz?

    12. #209
      Elizabeth Dominic's Avatar
      JF Premium Member Array
      Join Date : 7th December 2007
      Posts : 2,733
      Rep Power : 5463
      Likes Received
      1962
      Likes Given
      2652

      Default Re: Zanzibar: Padre apigwa Risasi na watu wasiojulikana

      Nakuombea upone Pd. Sad indeed.........Kikwete and co mmeifanyia nini nchi yetu sasa?
      Enyi mnaoumiza binadamu wenzenu kwa udini na unafiki mwengine SHAME be upon you, hakika mtalipwa stahiki zenu
      K.Msese likes this.

    13. #210
      Jabulani's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 26th March 2009
      Location : Kituo cha Polisi Jamii
      Posts : 2,977
      Rep Power : 1371
      Likes Received
      823
      Likes Given
      254

      Default Re: Zanzibar: Padre adaiwa kupigwa Risasi

      Quote By abdul 28
      utamsikia kesho kutwa Benard Member atawambia umoja wa EU na jumuiya za kimataifa ya kuwa uwamsho wameuwa Padri zanzibar waisilamu wanawaonea waikristo zanzibar
      hii ni kuificha dhana ya wazanzibar kudai nchi yao juu ya jumuiya za kimataiofa
      Sasa kudai nchi ya Zanzibar ndio Padri apigwe risasi? Wazanzibari waisilamu hawana akili kabisa
      Kamanda wa Polisi Jamii - Kanda Maalumu

    14. #211
      Jabulani's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 26th March 2009
      Location : Kituo cha Polisi Jamii
      Posts : 2,977
      Rep Power : 1371
      Likes Received
      823
      Likes Given
      254

      Default Re: Zanzibar: Padre apigwa Risasi na watu wasiojulikana

      Quote By Mdondoaji
      ... Ila wakristo ndugu zanguni ni vema mtafakari hili swala la mfumo kristo nchini.
      Zanzibar nako mnadai kuna mfumo Kristo? Huu wimbo wajinga wachache wamewakaririsha wajinga wengi, kila kitu mfumo Kristo!
      Kamanda wa Polisi Jamii - Kanda Maalumu

    15. #212
      Mponjori's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st February 2011
      Posts : 1,181
      Rep Power : 654
      Likes Received
      257
      Likes Given
      4

      Default

      Quote By Kitimoto
      Leo alikuja kijana amevaa kanzu nyumbani kwangu akiomba msaada wa fedha kwa ajili ya kituo cha kulelea watoto yatima, kwa kifupi nilimwambia sina pesa. Ni mara ya nne kuja, siku za nyuma walikuwa wawili, walishakuja wakiomba mchango kwa ajili ya ujenzi wa icho kituo nikawapatia. Wakaja tena wakiomba kwa ajili ya ujenzi wa Madrasa nikawapatia, wakaja kwa ajili ya watoto yatima nikawapatia.

      Baada ya haya majanga wanayoyafanya kwa sisi Wakristo nimesitisha michango na najuta kuwapa michango siku za nyuma. Kwa hii habari ya leo akija/wakija nitamwambia/nitawaambia wazi aende/waende kutafuta michamgo kwa waislamu wenzao.
      mkuu nakushauri uendelee mungu atakulipa. Onyesha tofauti

    16. #213
      MUNDALI WA ILEJE's Avatar
      Member Array
      Join Date : 27th September 2012
      Posts : 32
      Rep Power : 341
      Likes Received
      9
      Likes Given
      0

      Default Re: Zanzibar: Padre apigwa Risasi na watu wasiojulikana

      Da sasa wanatupeleka kubaya ndugu zangu wameanza na viongoz wa dini

    17. #214
      mchemsho's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 8th June 2011
      Posts : 2,016
      Rep Power : 810
      Likes Received
      271
      Likes Given
      22

      Default Re: Zanzibar: Padre apigwa Risasi na watu wasiojulikana

      get well soon catholic Father....aliyepigwa risasi ni binadamu mwenye nyama anaumia pia, hayo ya utumishi polisi ndio watatithibitishia kwamba alipigwa risasi sababu ya utumishi wake au la! again , get well soon!

    18. #215
      mpemba mbishi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th November 2011
      Posts : 916
      Rep Power : 0
      Likes Received
      101
      Likes Given
      0

      Default Re: Zanzibar: Padre apigwa Risasi na watu wasiojulikana

      Sheikh Farid= Alijiteka mwenyewe

      Sheikh Soraga= Alijimwagia mwenyewe

      Padri Mkenda= Kajipiga mwenyewe.

      Hapo sioni kama kuna tatizo tusikuze Mada au vyenginevyo tuwalaumu wenyewe na au tuwaulize kwanini hua wanafanya hivi?

    19. #216
      Mmwaminifu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 15th October 2010
      Posts : 885
      Rep Power : 721
      Likes Received
      134
      Likes Given
      19

      Default

      Quote By mpemba mbishi
      Huyo Padri kajipiga mwenyewe ili achafue mazingira! Kuna tabia ya VIONGOZI WA DINI wa Zanzibar kujifanyia matukio wenyewe au mumeshaanza kusahau wajameni!!
      mh! Hapa unamaanisha ana akili sawa na yule aliyejiteka.

    20. #217
      Tewe's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th January 2008
      Posts : 453
      Rep Power : 671
      Likes Received
      64
      Likes Given
      12

      Default

      Vita vyetu si juu ya damu na nyama ila ni juu ya falme na mamlaka

    21. #218
      Mmwaminifu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 15th October 2010
      Posts : 885
      Rep Power : 721
      Likes Received
      134
      Likes Given
      19

      Default

      Quote By mpemba mbishi
      Sheikh Farid= Alijiteka mwenyewe

      Sheikh Soraga= Alijimwagia mwenyewe

      Padri Mkenda= Kajipiga mwenyewe.

      Hapo sioni kama kuna tatizo tusikuze Mada au vyenginevyo tuwalaumu wenyewe na au tuwaulize kwanini hua wanafanya hivi?
      Mkuu. Hii analysis yako unataka kumaanisha nini?

    22. #219
      Jabulani's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 26th March 2009
      Location : Kituo cha Polisi Jamii
      Posts : 2,977
      Rep Power : 1371
      Likes Received
      823
      Likes Given
      254

      Default Re: Zanzibar: Padre adaiwa kupigwa Risasi

      Quote By dudus
      Naona hatuelewani, labda niulize kivingine: Nitajie nyumba za ibada, viongozi, na waumini wa dini ambao ni walengwa "maalumu" wa Kony kwenye mashambulizi yake. Huko Zanzibar tumeshuhudia dini fulani tu ikilengwa kwenye mashambulizi; kwa ufananisho huo, nitajie upande wa Kony.
      Huyo KIM KARDASH hawezi kukuelewa mkuu, si unajua elimu zao!
      Kamanda wa Polisi Jamii - Kanda Maalumu

    23. #220
      Queen Kyusa's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 25th April 2011
      Posts : 518
      Rep Power : 512
      Likes Received
      98
      Likes Given
      127

      Default

      Quote By abdul 28
      uthaifu wa watanganyika jamii forums
      1) kushindwa kufikiria nini chanzo matatizo ni nini
      kulisukuma au kulihusisha tatizo hili na uamsho
      kushabikia udini
      vipi mtu haija thibitishwa hata na serekali ukurupuke na kusema uamsho hao
      jiulize kwa nini uamsho haijafutwa kisheria


      CHANZO CHA MATATIZO CCM NA SEREKALI YAKE KUTUMIA SERA YA DINI KUFICHA UHALISIA HILI HALITA WASAIDIA
      utamsikia kesho kutwa Benard Member atawambia umoja wa EU na jumuiya za kimataifa ya kuwa uwamsho wameuwa Padri zanzibar waisilamu wanawaonea waikristo zanzibar
      hii ni kuificha dhana ya wazanzibar kudai nchi yao juu ya jumuiya za kimataiofa

      zanzibar matokeo ya kuuliwa viongozi wa dini sio mageni askari wa FFU walimpiga shekhe wa msikiti wa mtendeni risasi ndani ya msikiti na ziko kesi nyingi ila hawa askari ubaya ubaya huzizima kutiwa tindi kwa shekhe suraga

      sasa wana jamii fikirieni kwa makini hasa watanganyika
      ccm na serekali yake wasipindishe mnadai ya uamsho uamsho wanataka nchi yao sio chengine huu ni udhaifu wa ccm na raisi wao usalama wa taifa na polisi
      Sasa mkuu kama wanadai nchi yao ndo washambulie wakristo hao ndo wameshika nchi yao! Hata kama mnasema tz ina mfumo kristo mbona znz imejaa waislamu huo mfumo kristo upo wapi

    Page 11 of 23 FirstFirst ... 91011121321 ... LastLast

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...