Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Hivi ni nini kazi ya Waziri Mkuu Tanzania?

    Report Post
    Results 1 to 9 of 9
    1. #1
      KadaMpinzani's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 31st January 2007
      Location : Chadema Restaurant
      Posts : 5,011
      Rep Power : 1629
      Likes Received
      1
      Likes Given
      0

      Default Hivi ni nini kazi ya Waziri Mkuu Tanzania?

      Jamani jamani tusitake kutibuana akili hapa, mie kila leo napata kizunguzungu juu ya kazi halisi ya mheshimiwa PM wetu na hadi bado kwa kweli sijajua. Ebu oneni hapa sasa, amekuwa kama kiranja wa chekechea.

      Lowassa kuwauliza wakuu watatu wa mikoa kwanini timu za mikao yao hazikuhudhuria mashindao ya raidha.
      By Saidi Nguba | Published 06/29/2007 | Habari Mpya | Unrated
      WAZIRI Mkuu Edward Lowassa amesema atawauliza Wakuu wa Mikoa ya Kigoma, Lindi na Mtwara kwa nini timu za mikoa yao hazikufika kwenye mashindano ya kitaifa ya riadha aliyoyafungua mjini Dodoma leo (Ijumaa Juni 29, 2007).

      “Nakutana nao Jumatatu saa 7.30 mchana na nitawauliza kwa nini timu za mikoa yao hazikuja Dodoma,” alisema Lowassa alipokuwa akiyafungua mashindano hayo ya 46 ya siku mbili, kwenye uwanja wa Jamhuri.

      Aliongeza: “Nimeamua kuja hapa kwa sababu michezo ya riadha imekuwa ikiendelea vizuri sana miaka ya nyuma, lakini sasa imezorota…nataka tusaidiane tuifufue.”

      Wakuu wa mikoa 21 ya Tanzania Bara wako Dodoma kusikiliza kikao cha Bunge, hasa wakati huu wa makadirio ya Ofisi ya Waziri Mkuu ambayo inajumuisha Tawala za Mikoa na Serikalia za Mitaa.

      Jumatatu mchana watakutana na Waziri Mkuu kujadili namna ya utekelezaji wa bajeti ya mwaka 2007/2008.

      Waziri Mkuu Lowassa alisema kuwa Tanzania ina vipaji vingi vya riadha na akawataja wanariadha mashuhuri duniani waliotokea hapa nchini ambao ni pamoja na Philbert Bayi, Suleiman Nyambui, Juma Ikangaa, Francis Naali na John Yuda.

      Wengine ambao ni wanawake aliowataja kuwa walifanya vizuri ni pamoja na Mwinga Mwanjala, Nzael Kyomo na Restituta John.

      “Wote hawa ni uthibitisho kuwa tuna vipaji vya kuosha kutupatia sifa katika nchi yetu…ni jukumu la vyama vya michezo kushirikiana na Serikali kukuza vipaji mbalimbali vilivyoko nchini,” aliongeza.

      Katika ufunguzi huo, wanariadha walishindana mbio za mita 400 wanawake na mita 5000 wanaume na mita 200 kwa walemavu ambazo Waziri Mkuu alizishuhudia.

      Alitoa medali kwa Luiza John aliyeshinda mita 400 wanawake; Dickson Marwa, mita 5000 na Wilbrod Constantine, mita 200 walemavu.

      Waziri Mkuu pia alimwelekeza Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Margareth Sitta ambaye alikuwepo uwanjani, kueleza, ifikapo mwishoni mwa mwaka huu, lini mashindano ya michezo ya shule za msingi, sekondari na vyuo vya ualimu yatarejeshwa baada ya kusitishwa mwaka 2003.

      Mapema risala ya Shirikisho la Riadha Tanzania ilieleza kuwa ushiriki wa mikoa katika Mashindano ya Riadha ya Taifa haujawa mzuri tangu kusitishwa kwa mashindano ya shule.

      suala la msingi, je nini outcome ya hayo aliyosema ? jibu, NOTHING.

    2. FemaTV & Radio

    3. BAK
      #2
      BAK's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th February 2007
      Location : Mfaranyaki
      Posts : 26,591
      Rep Power : 44963
      Likes Received
      8327
      Likes Given
      8324

      Default

      Kuhakikisha wabunge wa CCM hawakemei maovu mbali mbali yanayowakera wananchi, na kuwapa wabunge watakaokiuka hilo karipio kali na hata kuwafukuza ubunge na kuwanyang'anya kadi ya chama.

    4. #3
      MegaPyne's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 4th May 2006
      Posts : 589
      Rep Power : 100000
      Likes Received
      2
      Likes Given
      0

      Default

      Quote By Bubu ataka kusema
      Kuhakikisha wabunge wa CCM hawakemei maovu mbali mbali yanayowakera wananchi, na kuwapa wabunge watakaokiuka hilo karipio kali na hata kuwafukuza ubunge na kuwanyang'anya kadi ya chama.
      I wanted to say the same thing. Umeniwahi.

    5. #4
      MzalendoHalisi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 24th June 2007
      Posts : 3,942
      Rep Power : 1397
      Likes Received
      72
      Likes Given
      120

      Default

      Taratibu!
      EL ni PM ila pia ni mwanadam- wakati mwingine tumchukulie kama mwandam- tuna mapungufu. Ila tumeshamwandama sana tayari. Simtetei ila naona tuwe a bit balanced! Sasa kama alialikwa kufungua hizo mbio za riadha- Lindi na Mtwara wakakosekana akae kimya? Au amwambie Pinda au Khatib au Chama cha Riadha? "Piga nyundo- wakatu chuma kina moto". Wakati mwingine ni vyema kuwapasha hapo hapo

    6. BAK
      #5
      BAK's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th February 2007
      Location : Mfaranyaki
      Posts : 26,591
      Rep Power : 44963
      Likes Received
      8327
      Likes Given
      8324

      Default

      Anayaona ya Kigoma, Mtwara na Lindi kukosekana katika michezo ambayo haimuongezei tija Mtanzania yeyote, lakini la kuifanya mikataba ya uchimbaji madini kuwa siri hadi leo halioni pamoja na kelele kila kukicha toka kwa wananchi!!! Ama kweli kipaumbele cha nchi yetu kimekaa kinyume nyume au kimgongo mgongo!!!

    7. Miaka 50

    8. #6
      Kichuguu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th October 2006
      Location : Popote Porini
      Posts : 6,836
      Rep Power : 3271
      Likes Received
      1314
      Likes Given
      916

      Default

      Waziri Mkuu ni mteule wa Rais kama waziri mwingine yeyote; anaweza kuvuliwa madaraka hayo na Rais wakati wowte. Lakini cha ajabu ni kuwa anakuwa na madaraka juu ya bunge lote. Huweza kunyamazisha wabunge wasiongelee jambo na spika akafyata mkia. Ni kama vile kwenye mfumo wa utawala wetu executive branch iko juu ya legislative branch.

      Ndiyo maana niliwahi kusema kuwa sioni umuhimu wa madaraka ya Waziri Mkuu wakati tuna rais na makamu wake wawili. Katiba mpya ndiyo solution.
      Kichuguuu: Nyumba inayohifadhi mchwa na nguchiro kwa pamoja bila mkwaruzo

    9. #7
      MzalendoHalisi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 24th June 2007
      Posts : 3,942
      Rep Power : 1397
      Likes Received
      72
      Likes Given
      120

      Default

      Du,
      Pengine Mtwara na Lindi hawajaonekana kwani ndugu zangu Chingani ni mahiri kwa Soka na pengine siyo riadha! Mbona Kombe la Taifa Soka Mt na Lindi walishiriki?
      Kichuguu- hilo la separation of powers nakubalina kiasi!

    10. #8
      Samvulachole's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 22nd October 2006
      Posts : 744
      Rep Power : 792
      Likes Received
      6
      Likes Given
      4

      Default

      NA WAZIRI kiongozi zanzibaR KAZI YAKE NI NINI?

    11. #9
      KadaMpinzani's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 31st January 2007
      Location : Chadema Restaurant
      Posts : 5,011
      Rep Power : 1629
      Likes Received
      1
      Likes Given
      0

      Default

      huyu waziri mkuu kazi yake ni kuongea tu bila ya kutekeleza, na nani asiyejua ! mbaya zaidi hajui kuwa ahadi ni deni, yeye anatoa tu mihadi ooh hivi mara vile, mwishowe kichwa chake kizima kimejaa ahadi mpaka anashindwa aanze wapi aishie wapi !poleni sana viongozi wetu !

    Similar Topics

    1. Mashaka: Kazi na Mamlaka ya Waziri Mkuu ya Kikatiba
      By Kasheshe in forum Jukwaa la Siasa
      Replies: 12
      Last Post: 14th June 2012, 08:39
    2. Hivi hii ya Waziri Mkuu imekaaje?
      By Sizinga in forum Jukwaa la Siasa
      Replies: 21
      Last Post: 2nd July 2011, 23:24
    3. Hivi ukitaka kufanya kazi Tanzania hizo TGS na PUTS zinamaanisha nini???
      By eliesikia in forum Business & Economic Forum
      Replies: 2
      Last Post: 28th December 2010, 15:28
    4. Replies: 0
      Last Post: 27th December 2010, 17:58
    5. Mawaziri kufutwa kazi,asema Waziri Mkuu!
      By Ab-Titchaz in forum International Forum
      Replies: 16
      Last Post: 2nd April 2009, 11:10

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...