Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: EWURA yabariki mafuta yaliyokataliwa Rwanda, sasa kuuzwa nchini

    Report Post
    Results 1 to 9 of 9
    1. #1
      Kimbori's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st February 2012
      Posts : 1,188
      Rep Power : 603
      Likes Received
      161
      Likes Given
      11

      Default EWURA yabariki mafuta yaliyokataliwa Rwanda, sasa kuuzwa nchini

      SHEHENA ya mafuta iliyopelekwa nchini Rwanda, Burundi na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), imekataliwa katika nchi hizo kwa kukosa ubora na kurudishwa Tanzania ambapo sasa yameanza kuuzwa, Mwananchi Jumapili limebaini.

      Licha ya maelfu ya lita za mafuta hayo ya dizeli na petroli kukataliwa katika nchi hizo, Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (Ewura), Julai 31 mwaka huu ilitoa kibali cha kuruhusu mafuta hayo kuuzwa nchini ikieleza kuwa ilipima na kubaini yanafaa kutumika nchini.

      Mafuta hayo yalinunuliwa na kampuni tano za mafuta nchini na kusafirishwa kwenda katika nchi hizo, lakini yalirudishwa baada ya kubainika kuwa hayafai.

      Juni 4 mwaka huu, Kamishna wa Huduma kwa wateja wa Mamlaka ya Mapato ya Rwanda (RRA), Richard Tusabe, alimwandikia barua Naibu Kamishna wa Wateja na Bidhaa wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), kumweleza kuwa Rwanda imeyarudisha mafuta hayo kwa kuwa hayana kiwango kinachokubalika nchini humo.

      Barua hiyo yenye kumbukumbu namba 0654/RRA/CCS/FOD-PMU/12, imeeleza kuwa mafuta hayo yaliyopelekwa Rwanda na malori manne, baada ya kupimwa na kupakuliwa hatimaye yalionekana hayafai, hivyo iliamriwa yarejeshwe nchini.

      Kutoka Rwanda malori hayo yalisindikizwa chini ya uangalizi wa RRA hadi katika mpaka wa Tanzania na Rwanda eneo la Rusumo, ili hatua za kuyarudisha kwa kampuni zilizoagiza ifanywe na Tanzania.

      Barua nyingine iliyoandikwa Mei 30 mwaka huu na Naibu Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Viwango la Rwanda (RBS), Injinia Ntiyamira Patrice ilieleza kuwa, mafuta hayo hayana viwango na kwamba hata DRC pia waliyakataa, baada ya kuyapima na kubaini kuwa hayakuwa na ubora.

      Hata hivyo, katika barua yake ya Julai 31, 2012, Mkurugenzi wa Ewura, Haruna Masebu alitoa idhini ya kuuzwa kwa lita 171,730 za petroli nchini kutoka Rwanda, ikiwa ni sehemu tu ya mafuta hayo yaliyorejeshwa nchini.

      Akizungumza na Mwananchi Jumapili kuhusu suala hilo jana, Masebu alisema mafuta yote yanayopita nchini kwenda nchi jirani hayapimwi na Ewura.

      “Sheria za Afrika Mashariki ndiyo zinaeleza hivyo, kama yalikubalika huko yalikokwenda au yalikataliwa sisi haituhusu,” alisema Masebu.

      Alifafanua kwamba hakuna mafuta machafu yanayotumika nchini na kwamba, ili mafuta yaweze kuingia sokoni ni lazima yawe na ubora unaokubalika nchini.

      Chanzo:
      Mwananchi Jumapili

    2. Miaka 50

    3. #2
      Kingo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 12th May 2009
      Posts : 371
      Rep Power : 585
      Likes Received
      54
      Likes Given
      106

      Default re: EWURA yabariki mafuta yaliyokataliwa Rwanda, sasa kuuzwa nchini

      Kwa sentensi ya mwisho ya Masebu inamaanisha Tz ni kiwango duni. Wengine wakikataa sisi tunasema kwetu ni kiwango, lete! Hivi ni lini tutakua makini na nchi yetu na wananchi wake?

    4. #3
      Ubungo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 7th April 2012
      Posts : 1,151
      Rep Power : 589
      Likes Received
      204
      Likes Given
      185

      Default re: EWURA yabariki mafuta yaliyokataliwa Rwanda, sasa kuuzwa nchini

      Ulaji kila mahali

    5. #4
      Shark's Avatar
      Banned Array
      Join Date : 25th January 2010
      Posts : 4,573
      Rep Power : 0
      Likes Received
      1305
      Likes Given
      245

      Default

      Quote By Kingo
      Kwa sentensi ya mwisho ya Masebu inamaanisha Tz ni kiwango duni. Wengine wakikataa sisi tunasema kwetu ni kiwango, lete! Hivi ni lini tutakua makini na nchi yetu na wananchi wake?
      Tunao TBS kazi yao ni kupima mafuta na kutoa certificates,
      wapo pia jamaa wa vipimo kama Intertek na SGS.
      Ni UONGO kudai kua hawapimi TRANSIT FUEL, waliyapima na wakatoa vibali. Wanaona aibu kukubali maana kua walilipua upipimaji. Pia itasababisha watumiaji wa mafuta kutokuyaamini!!

    6. #5
      sesy nzenga's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 16th June 2012
      Posts : 118
      Rep Power : 372
      Likes Received
      11
      Likes Given
      94

      Default re: EWURA yabariki mafuta yaliyokataliwa Rwanda, sasa kuuzwa nchini

      kweli hii ndio tanzania dampo la kila kitu

    7. RukaaJuu Final

    8. #6
      King Kong III's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 15th October 2010
      Location : Enaboishu-Umenyeni
      Posts : 11,920
      Rep Power : 5062
      Likes Received
      3199
      Likes Given
      2653

      Default re: EWURA yabariki mafuta yaliyokataliwa Rwanda, sasa kuuzwa nchini

      Tanzania shamba la bibi,Tanzania Jalala! TBS,TFDA,EWURA wamelala usingizi mzito!

    9. #7
      Nyalotsi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 20th July 2011
      Posts : 2,653
      Rep Power : 927
      Likes Received
      587
      Likes Given
      83

      Default

      Quote By King Kong III
      Tanzania shamba la bibi,Tanzania Jalala! TBS,TFDA,EWURA wamelala usingizi mzito!
      hizi mamlaka mkapa alizianzisha kwa malengo mazuri lakini kazi waliyoivamia ya kutafuta mianya ya rushwa na kuitumia kushibisha matumbo yao ndo imetufikisha hapa. Ukiongeza na uamuzi wa kile kichwa cha nazi ndo kabisaa tumeliwa. Hukawii kuona tfda wana ukaribu mkubwa na waingizaji wa vipodozi, madawa feki, mchele mbovu gmo kutoka nje. Bila kubadilika hatusongi mbele! Lazima kila mtu awe anafanyiwa evaluation kwa kazi aliyoifanya in field, siyo kwenye makaratasi na computer.
      rodrick alexander likes this.

    10. #8
      kupe's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 26th July 2012
      Posts : 628
      Rep Power : 0
      Likes Received
      103
      Likes Given
      5

      Default

      Quote By Shark
      Tunao TBS kazi yao ni kupima mafuta na kutoa certificates,
      wapo pia jamaa wa vipimo kama Intertek na SGS.
      Ni UONGO kudai kua hawapimi TRANSIT FUEL, waliyapima na wakatoa vibali. Wanaona aibu kukubali maana kua walilipua upipimaji. Pia itasababisha watumiaji wa mafuta kutokuyaamini!!

      something is better than nothing . acha yaje tu tutayatumia

    11. #9
      amkawewe's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 8th December 2011
      Posts : 748
      Rep Power : 525
      Likes Received
      120
      Likes Given
      535

      Default re: EWURA yabariki mafuta yaliyokataliwa Rwanda, sasa kuuzwa nchini

      Jamani ni petrol station gani inaaminika niwe naweka mafuta bajaji yangu full tank?

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...