Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Ajali tena-wanakwaya 11 rai wa kenya wafa katika ajali ya basi

    Report Post
    Results 1 to 3 of 3
    1. #1
      bemg's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 25th April 2010
      Posts : 1,613
      Rep Power : 783
      Likes Received
      218
      Likes Given
      344

      Post Ajali tena-wanakwaya 11 rai wa kenya wafa katika ajali ya basi

      WATU 11 wanaoaminika kuwa raia wa Kenya wamefariki dunia papo hapo, huku wengine saba wakiwa mahututi baada ya mabasi waliyokuwa wakisafiria kutoka Nairobi kwenda Dar es Salaam kupata ajali katika Mto Wami mkoani Pwani.Mbali na vifo hivyo, ajali hiyo pia ilisababisha majeruhi 25 na saba kati yao waliripotiwa kuwa mahututi na walipelekwa katika Hospitali ya Tumbi, Kibaha kwa matibabu.Ajali hiyo ilitokea katika Kijiji cha Makole, wilayani Bagamoyo wakati abiria hao ambao ni wanakwaya walipokuwa wakisafiri kutoka Kenya kwenda Dar es Salaam kushiriki katika tamasha la uimbaji.

      Ajali hiyo ilitokea jana saa 11 alfajiri ikihusisha magari manne, mawili kati yake yakiwa ni mabasi hayo yakitokea Kenya na malori mawili ya hapa nchini.Tukio hilo pia lilifunga Barabara Kuu ya Chalinze - Segera kwa zaidi ya saa nane hivyo abiria waliokuwa wakisafiri kuelekea na kutoka mikoa ya Kaskazini ikiwamo nchi ya Kenya kwenda na kutoka Dar es Salaam kukwama.

      Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani, Ernest Mangu alisema raia hao wa Kenya ni waumini wa Kikristo na walikuwa wakielekea Dar es Salaam kwenye tamasha la kwaya.

      Source Mwananchi

      Wakti huo huo nipashe linahabari za basi la kampuni ya Allys Sport Bus linalosafirisha abiria kutoka Dar es Salaam na Mwanza liliacha njia na kupinduka baada ya kutokea ajali inayodaiwa kusababishwa na basi la Shabiby lililokuwa likitokea mkoani Dodoma kwenda Dar es Salaam na kusababisha mabasi matatu kuacha njia eneo la Mkundi Makunganya barabara kuu Dodoma-Morogoro ambapo katika ajali hizo zaidi ya abiria 40 walijeruhiwa mkoani hapa.
      Ni jambo zuri na la kupendeza sana ndugu kuishi pamoja kwa umoja

    2. Miaka 50

    3. #2
      bemg's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 25th April 2010
      Posts : 1,613
      Rep Power : 783
      Likes Received
      218
      Likes Given
      344

      Default Re: Ajali tena-wanakwaya 11 rai wa kenya wafa katika ajali ya basi

      Poleni wafiwa na wale waliopata majeraha Mungu awaponyeshe.
      Ni jambo zuri na la kupendeza sana ndugu kuishi pamoja kwa umoja

    4. #3
      Kassim Awadh's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 12th March 2012
      Posts : 587
      Rep Power : 480
      Likes Received
      108
      Likes Given
      785

      Default Re: Ajali tena-wanakwaya 11 rai wa kenya wafa katika ajali ya basi

      Inshu iko toka jana hii,nilidhani we leo umeambatanisha na picha za tukio
      Lokissa likes this.

    5. FemaTV & Radio

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...