Serikali inahusika 100% kwenye Miss Tanzania, Wasanii waichana live
Katika nyimbo ya Solo Thang inayokwenda kwa jina la Miss Tanzania ni wazi kuwa aliyezungumziwa hapo Si Miss Tanzania bali ni nchi ya Tanzania. Katika wimbo huo ambao upo kwenye link hii hapa chini kuna mistari ifuatayo kwenye mashairi hayo
http://www.hulkshare.com/dl/o7mepz38l1s4/?d=1
Ubeti wa Kwanza
Baba yake alikuwa mkoloni kipindi huyu Miss mwali
Mchonga alikata utepe lakini hakuvinjari
Sababu alikua busy kumlinda na geti kali
Kumbe wenzake wanabinjuka, kushtuka akakaa mbali
Demu alikua na heshima kabla haijatangazwa Rukhsa
Chukua Chako Mapema ukimkonyeza tu umegusa
Ana kifua kimebetuka sio maziwa ni madini
Kayaacha wazi, watu wanashika hapo ndio anaponiudhi mimi
Watu wanagonga tu Ikulu tena kwa mitindo huru
Kavu kavu bila kinga hajali vinavyodhuru
Kawa shangingi na amedata hana uwoga wa kunguru
Anapenda sana chapaa haimtoshi kodi na ushuru
Ana kijungu matata laini kama nyanya masalo
Anatingisha Afrika nzima na mzigo Kilimanjaro
Usimchezee kwa vidani sio pete sio hereni
Anamiliki tanzanite kama ardhi ya Mererani
Sura dhahabu inaita kama amezaliwa Geita
Tatizo ndio kicheche kila mwanaume ndio amepita
Hata Benja hakutoka Kapa huyu demu hajatulia
Kama rushwa ndio kikwapa ananuka na kunukia
Kiitikio
Miss Tanzania
Nakupenda ila hujatuliaa
Vitendo vyako sitojivunia
Sifa yako kubwa umefulia
Miss Tanzania
Ubeti wa Pili
Bora angebaki kuwa modo kama Flavian Matata
Ila demu amejiachia kisa anaendekeza bata
Sitachoka kuwakilisha jinsi anavyoniacha hoi
Juzi juzi kaopolewa na Handsome Boy
Kabla hapo shoga zake wote kashawaona mabwege
Sababu hawana dira na yeye ameshahongwa ndege
Anafaa kuwa Miss Dunia maandalizi longolongo
Tatizo anakula sana akijamba ni Songosongo
Mara ghafla kanenepa kumbe mimba B.O.T.
Kumbe demu aligawa EPA watu wamepiga hafu jii
Alizugwa na akaunti hewa kuwadi Bwana Bilal
Mara mdomo naye kazimwa bila hata picha ya kaburi
Kinachomponza huyu shawty utulivu sifuri
Ila hakuna anayepinga kwamba huyu demu ni mzuri
Mixer siasa na biashara demu ameshakuwa chotara
Mishe za Dar akimaliza Mjengoni anakwenda lala
Kadri miaka inavyokwenda demu anazidi fulia
Kumbe weupe ni mkorogo ona mwili sasa umefifia
Demu kazidi umalaya wacha mabwana wamteme
Haogopi kuliwa mtungo kisa anagawa umeme
Ubeti wa Tatu
Wadaku walishamfuma anakula denda na Richmond
Dowans akazidi kete akamvisha pete ya diamond
Binti masikini akanasa bwana mshenga ndio Lowasa
Shemeji hataki hata picha ndio tabia gani sasa
Ndoa ilifungwa kwa vifijo vigogo wakala pizza
Keki nzima wale wao share yetu si ni giza
Sio hayo demu ana mengi ya kuchukiza
Malighafi ashazinadi for sale anajiuza
Mtaani ilivuma rumor demu kawa mama huruma
Uchumi umefungwa drip maendeleo ndio kali homa
Mali asili ndio kitasa kila ufunguo ndio unapita
Toka alipovunja ungo nusu karne imeshapita
Mapenzi kafanya mradi anamegwa na mafisadi
Amani kwa time bomb binti amekumbatia radi
Vitendo vyake vibaya vinafanya adharaulike
Tabia Katiba sio Msahafu ndio useme isibadilike
Mikosi inayomkuta ndio kwanza anatabasamu
Hajali waliomzunguka kama nao binaadamu
Mbagala walimbaka mpaka akamwaga damu
Na juzi Gongo la Mboto kaanza kujamba mabomu
Apelekewe rais Wimbo huu jamani akausikiepia Mwinyi, na Mkapa
Last edited by Godfrey Electronics; 4th August 2012 at 08:04.
Angetulia katika utunzi wake/mashairi yaliyoenda shule huu wimbo ungekuwa na maana lakini kama kawaida ya watunzi wa bongo fleva kajichanganya na utunzi wake kitu ambacho kinaonesha dhahiri kuwa hajuwi kutunga nyimbo za muziki ila ngonjera. Ushauri wangu, solo ukitunga ngonjera wape wanamuziki waliobobea wasahihishe, usikurupukie kuimba tu na kuchanganya vitu.
Re: Serikali inahusika 100% kwenye Miss Tanzania, Wasanii waichana live
Song limetulia sana, tunaomba tulipate haraka tupo Songea coz huu utafungiwa soon, coz umemponda m;kulu moja kwa moja wala hujiulizi kwa kweli mshikaji kafulia hana ishu tena.
Re: Serikali inahusika 100% kwenye Miss Tanzania, Wasanii waichana live
By Apta Kayla
Anamzungumzia Mwl Nyerere hapa. Aliikomboa nchi, hakuifaidi, ukiunganisha ni huo mstari wa ruksa unapata jibu.
Na kweli! nilipata kuiona video ya vita vya kagera,kuna mahala benjamin w m! alikuwa yupo na nyerere baada ya vita kwisha! aisee, ukiambiwa makapa huyu ndo yule niliemuona pale, siamini machoyangu mpaka leo!
MZUNGU AKIJICHUBUA HUJUE MOYONI ANA UAFRICA!.by stamina
Re: Serikali inahusika 100% kwenye Miss Tanzania, Wasanii waichana live
anakifua kimebetuka! sio maziwa hadi madini! kayaacha wazi watu wanashika tu! HAPO NDO ANANIUZI MIMI.
kama rushwa ndo kikwapa,ananuka na kunukia!
kuadi bwana bilali nae kazimwa tu bila hata picha ya kaburi!(HIKI KIPANDE JIBU LIKO MABWEPANDE)
bwana mshenga ndo lowassa! wao wanakula keki tu,shea yetu sisi ni giza(?)
hivi uyu jamaa hayupo humu kwa magreat thinker? mkali sana! ivi huko nje aliko hamna mapori kama ya mabwepande kweli! mana yule jamaa asije akatumwa kwenda kule!
MZUNGU AKIJICHUBUA HUJUE MOYONI ANA UAFRICA!.by stamina
Re: Serikali inahusika 100% kwenye Miss Tanzania, Wasanii waichana live
By Dauphine
Katika nyimbo ya Solo Thang inayokwenda kwa jina la Miss Tanzania ni wazi kuwa aliyezungumziwa hapo Si Miss Tanzania bali ni nchi ya Tanzania. Katika wimbo huo ambao upo kwenye link hii hapa chini kuna mistari ifuatayo kwenye mashairi hayo
http://www.hulkshare.com/dl/o7mepz38l1s4/?d=1
Ubeti wa Kwanza
Baba yake alikuwa mkoloni kipindi huyu Miss mwali Mchonga alikata utepe lakini hakuvinjari
Sababu alikua busy kumlinda na geti kali
Kumbe wenzake wanabinjuka, kushtuka akakaa mbali
Demu alikua na heshima kabla haijatangazwa Rukhsa Chukua Chako Mapema ukimkonyeza tu umegusa
Ana kifua kimebetuka sio maziwa ni madini
Kayaacha wazi, watu wanashika hapo ndio anaponiudhi mimi
Watu wanagonga tu Ikulu tena kwa mitindo huru
Kavu kavu bila kinga hajali vinavyodhuru
Kawa shangingi na amedata hana uwoga wa kunguru
Anapenda sana chapaa haimtoshi kodi na ushuru
Ana kijungu matata laini kama nyanya masalo
Anatingisha Afrika nzima na mzigo Kilimanjaro
Usimchezee kwa vidani sio pete sio hereni
Anamiliki tanzanite kama ardhi ya Mererani
Sura dhahabu inaita kama amezaliwa Geita
Tatizo ndio kicheche kila mwanaume ndio amepita
Hata Benja hakutoka Kapa huyu demu hajatulia
Kama rushwa ndio kikwapa ananuka na kunukia
Kiitikio
Miss Tanzania
Nakupenda ila hujatuliaa
Vitendo vyako sitojivunia
Sifa yako kubwa umefulia
Miss Tanzania
Ubeti wa Pili
Bora angebaki kuwa modo kama Flavian Matata
Ila demu amejiachia kisa anaendekeza bata
Sitachoka kuwakilisha jinsi anavyoniacha hoi
Juzi juzi kaopolewa na Handsome Boy
Kabla hapo shoga zake wote kashawaona mabwege
Sababu hawana dira na yeye ameshahongwa ndege
Anafaa kuwa Miss Dunia maandalizi longolongo
Tatizo anakula sana akijamba ni Songosongo
Mara ghafla kanenepa kumbe mimba B.O.T.
Kumbe demu aligawa EPA watu wamepiga hafu jii
Alizugwa na akaunti hewa kuwadi Bwana Bilal
Mara mdomo naye kazimwa bila hata picha ya kaburi
Kinachomponza huyu shawty utulivu sifuri
Ila hakuna anayepinga kwamba huyu demu ni mzuri
Mixer siasa na biashara demu ameshakuwa chotara
Mishe za Dar akimaliza Mjengoni anakwenda lala
Kadri miaka inavyokwenda demu anazidi fulia
Kumbe weupe ni mkorogo ona mwili sasa umefifia
Demu kazidi umalaya wacha mabwana wamteme
Haogopi kuliwa mtungo kisa anagawa umeme
Ubeti wa Tatu
Wadaku walishamfuma anakula denda na Richmond
Dowans akazidi kete akamvisha pete ya diamond
Binti masikini akanasa bwana mshenga ndio Lowasa Shemeji hataki hata picha ndio tabia gani sasa
Ndoa ilifungwa kwa vifijo vigogo wakala pizza
Keki nzima wale wao share yetu si ni giza
Sio hayo demu ana mengi ya kuchukiza
Malighafi ashazinadi for sale anajiuza
Mtaani ilivuma rumor demu kawa mama huruma
Uchumi umefungwa drip maendeleo ndio kali homa
Mali asili ndio kitasa kila ufunguo ndio unapita
Toka alipovunja ungo nusu karne imeshapita
Mapenzi kafanya mradi anamegwa na mafisadi
Amani kwa time bomb binti amekumbatia radi
Vitendo vyake vibaya vinafanya adharaulike
Tabia Katiba sio Msahafu ndio useme isibadilike
Mikosi inayomkuta ndio kwanza anatabasamu
Hajali waliomzunguka kama nao binaadamu
Mbagala walimbaka mpaka akamwaga damu
Na juzi Gongo la Mboto kaanza kujamba mabomu
Apelekewe rais Wimbo huu jamani akausikiepia Mwinyi, na Mkapa
... Its great Song
... Awamu zote wamo MCHONGA, RUKHSA, BENJA mKAPA, HANDSOME BOY
Jitihada zifanywe kwa wahusika kupata ... Huu mziki wausikilize wacheze na zaidi wauchukulie hatua ili uwe maarufu zaidi na zaidi ... Na ujumbe uende mabali zaidi na zaidi!!
Never Get Angry; Never Make Threat; Reason With People;
"Napenda the logic of the words because in some ways it says about individual-not to use emotions-when scrutinizing something, whether it involves you or not" ...-by AshaDiii @ Jamiiforums 26th July 2011.
Re: Serikali inahusika 100% kwenye Miss Tanzania, Wasanii waichana live
huu wimbo napendekeza uwe wa tatu baada ya zile mbili za taifa (Mungu ibariki...na TanzaniaTanzania...). utawasaidia sana hata hawa vijana wa kizazi cha bongo flava kujua umuhimu wa siasa safi kwenye nchi yao hasa kina Bushoke, Dokii, Hafsa Kazinja wanaokesha kuinadi ccm magamba.
Halafu haya mashairi apewe cpt John Komba ayatengenezee kwaya moja nzuri hivi ili ujumbe uwafikie pia wapenda kwaya.
Wabunge hasa hawa wa ccm ni bora waupate huu wimbo halafu watafakari na hizo kelele zao NDIYOOOOOO!! kwa kila kitu.
Ningeweza ningependekeza upigwe kenye radio stations mfululizo japo wiki mbili labda hii inaweza ikasaidia kidogo watanzania kutafakari mustakabari wa nchi yetu na rasilimali zake. BIG UP SOLOOOOO!
Follow Us Here