Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Jogoo mwenye shanga na hirizi azua kizazaa

    Report Post
    Results 1 to 12 of 12
    1. #1
      Young Master's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 22nd December 2008
      Location : Arusha, Tanzania.
      Posts : 6,101
      Rep Power : 7416
      Likes Received
      2062
      Likes Given
      1476

      Default Jogoo mwenye shanga na hirizi azua kizazaa

      WAKAZI wa Mtaa wa Nyanchenche Road mjini Sengerema juzi walifurika kushuhudia tukio la kuonekana jogoo asiye na manyoya akitembea huku akiwa amefungwa shanga na hirizi mbili shingoni na mabawa yake yakiwa yamechanjwa chale na kupakwa dawa nyeusi.

      Tukio hilo lililovuta umati wa watu lilitokea juzi saa 7:00 mchana kwenye moja ya familia ya mtaa huo ambaye alidai kwamba kuku huyo alijitokeza nyumbani kwake bila kufahamu alikotokea.

      Kuku huyo wa ajabu alikutwa na wananchi katika mji huo ulioko kando kando ya barabara, jambo lililowashtua wakazi wa Sengerema waliofika kulishuhudia huku wakilihusisha na imani za kishirikina.

      Katika tukio hilo hakuna mwananchi aliyejitokeza kumshika kuku huyo, huku wenyeji wa mji husika wakiendelea na shughuli zao licha ya kuonyesha mshituko.

      Akizungumza na waandishi wa habari,Mwenyekiti wa kitongoji hicho Leah James alieleza kushangazwa na tukio hilo aliloliita la ajabu, na kwamba halijawahi kutokea katika kitongoji hicho kwani limeibua hisia tofauti miongoni mwa wanajamii.

      Nimepata taarifa za tukio hili ilikuwa mchana muda wa saa saba na tumefika mpaka eneo la tukio, kwa kweli inashangaza na kusikitisha, huyo kuku wa ajabu hana nyoya hata moja wala alama ya kidonda na amechanjwa chale kwenye mbawa zake,kavishwa hirizi mbili shingoni na amefungwa shanga kwenye mbawa zake alisema mwenyekiti.

      Baada ya tukio hilo uongozi wa eneo hilo na sungusungu uliamua kuitisha mkutano siku iliyofuata ambapo walifuatilia na kumbaini mmiliki wa kuku huyo kuwa ni Leticia Makoye ambaye alidai kuku huyo ni wake na humtumia katika shughuli za uganga wa kienyeji .

      Kikao hicho kiliamua kumrudishia kuku huyo ingawa alikuwa tayari amekufa kutokana na kupigwa baridi usiku kucha,maamuzi yaliyopingwa na wananchi na hivyo kulazimika kumshambulia kwa mawe hadi nyumbani kwake huku viongozi wa mtaa huo wakimpatia ulinzi hadi alipoingia ndani ya nyumba.
      Mr Rocky, MziziMkavu, paty and 1 others like this.
      Advertise your products, business & services with us 100% free |www.globaladverts.biz

    2. Study Abroad

    3. #2
      MziziMkavu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd February 2009
      Location : European Union
      Posts : 22,113
      Rep Power : 19194
      Likes Received
      8048
      Likes Given
      26489

      Default Re: Jogoo mwenye shanga na hirizi azua kizazaa

      Ningelikuwa ni mimi ningemkamata huyo kuku na kumchinja na kumla ina siwe kitu chochote kile imani za kishirikina hizo. Mkuu Young_Master
      SIMBA mtoto likes this.
      Only Do What Your Heart Tells You




      Allah
      Has Not Revealed A Disease without Treatment....
      (Prevention is Better Than Cure) Email Address yangu hii [email protected]

    4. #3
      paty's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 19th October 2010
      Location : never never land
      Posts : 1,024
      Rep Power : 973
      Likes Received
      270
      Likes Given
      62

      Default Re: Jogoo mwenye shanga na hirizi azua kizazaa

      sisi ndo maana hatuendelei , tunaishi karne 15,
      MziziMkavu likes this.
      CHADEMA mwendo mdundo - T 2015 CDM

    5. #4
      Remmy's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 9th June 2009
      Location : home
      Posts : 4,339
      Rep Power : 7766
      Likes Received
      1543
      Likes Given
      1792

      Default Re: Jogoo mwenye shanga na hirizi azua kizazaa

      Ukistaajabu ya Musa, utaona ya Firauni.
      MziziMkavu and Young Master like this.

    6. #5
      Remmy's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 9th June 2009
      Location : home
      Posts : 4,339
      Rep Power : 7766
      Likes Received
      1543
      Likes Given
      1792

      Default Re: Jogoo mwenye shanga na hirizi azua kizazaa

      Quote By MziziMkavu
      Ningelikuwa ni mimi ningemkamata huyo kuku na kumchinja na kumla ina siwe kitu chochote kile imani za kishirikina hizo. Mkuu Young_Master
      Unamlaje kuku wa hivo? Hana manyoya....
      Akiwa sio kuku je?
      Usije kula mtu.
      MziziMkavu likes this.

    7. Miaka 50

    8. #6
      Caroline Danzi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 19th December 2008
      Location : Dar es Salaam
      Posts : 2,708
      Rep Power : 1072
      Likes Received
      647
      Likes Given
      214

      Default Re: Jogoo mwenye shanga na hirizi azua kizazaa

      Duniani kuna mambo! lol
      MziziMkavu likes this.

    9. #7
      Mr Rocky's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 10th October 2007
      Location : Hungumalwa
      Posts : 9,145
      Rep Power : 46180
      Likes Received
      6454
      Likes Given
      5321

      Default Re: Jogoo mwenye shanga na hirizi azua kizazaa

      Mkuu Young_Master hapo hakuna kitu cha chale wala nini
      Unamkamata na kumla tuone kama kuna chochote tena unaweka na sala kabisa wakati unamla
      Bado watu wana imani za ajabu sana
      MziziMkavu likes this.
      When you are in Love you can't fall asleep because reality is better than your dreams

    10. #8
      Young Master's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 22nd December 2008
      Location : Arusha, Tanzania.
      Posts : 6,101
      Rep Power : 7416
      Likes Received
      2062
      Likes Given
      1476

      Default Re: Jogoo mwenye shanga na hirizi azua kizazaa

      Quote By Remmy
      Unamlaje kuku wa hivo? Hana manyoya....
      Akiwa sio kuku je?
      Usije kula mtu.
      Ndio hapo sasa.. MziziMkavu angalia usije kula visivyoliwa.
      MziziMkavu likes this.
      Advertise your products, business & services with us 100% free |www.globaladverts.biz

    11. #9
      Young Master's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 22nd December 2008
      Location : Arusha, Tanzania.
      Posts : 6,101
      Rep Power : 7416
      Likes Received
      2062
      Likes Given
      1476

      Default Re: Jogoo mwenye shanga na hirizi azua kizazaa

      Quote By Mr Rocky
      Mkuu Young_Master hapo hakuna kitu cha chale wala nini
      Unamkamata na kumla tuone kama kuna chochote tena unaweka na sala kabisa wakati unamla
      Bado watu wana imani za ajabu sana
      Mkuu Mr Rocky embu kajaribu kwanza wewe...ukifanikiwa kumla bila kudhurika basi na mimi ndio nitaenda kujaribu.
      Advertise your products, business & services with us 100% free |www.globaladverts.biz

    12. #10
      Vinci's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 6th July 2009
      Location : Piyaya
      Posts : 2,002
      Rep Power : 902
      Likes Received
      307
      Likes Given
      394

      Default Re: Jogoo mwenye shanga na hirizi azua kizazaa

      Huyo angekamatwa tuu achinjwe....hakuna kitu cha kalumanzira wala nini...nadhan ni jiran anampima mwenzake imani.anamtishia nyau. baadae atamtumia paka aliemvalisha shanga
      MziziMkavu and Young Master like this.
      "If I have seen further it is by standing on the shoulders of Giants" (Newton, 1675)





    13. #11
      Young Master's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 22nd December 2008
      Location : Arusha, Tanzania.
      Posts : 6,101
      Rep Power : 7416
      Likes Received
      2062
      Likes Given
      1476

      Default Re: Jogoo mwenye shanga na hirizi azua kizazaa

      Quote By Vinci
      Huyo angekamatwa tuu achinjwe....hakuna kitu cha kalumanzira wala nini...nadhan ni jiran anampima mwenzake imani.anamtishia nyau. baadae atamtumia paka aliemvalisha shanga
      Teh teh teh!!! Haya bwana.
      Advertise your products, business & services with us 100% free |www.globaladverts.biz

    14. #12
      Katavi's Avatar
      JF Bronze Member Array
      Join Date : 31st August 2009
      Location : Lyamba Lya Mfipa
      Posts : 19,551
      Rep Power : 16758
      Likes Received
      2474
      Likes Given
      1841

      Default Re: Jogoo mwenye shanga na hirizi azua kizazaa

      Haya mambo bwana ndio maana hatuendelei.
      MziziMkavu and Young Master like this.

    15. FemaTV & Radio

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...