
By
Choi
mafisadi sio serikalini tu, hata kwenye sekta binafsi. nilikuwa na kiduka changu cha dawa baridi nimemuweka mdada aniuzie nikienda kazini anaenda kkoo anachukua dawa zake ndio anauza hapo dukani zangu haziuziki mpaka nikafunga duka ndio jirani akaja kunipa hiyo siri. ukienda posta kwenye maduka ya wahindi wauzaji wanakwambia hii bidhaa inauzwa 300000,lakini nenda pale mlangoni umpe mlinzi 150000 na bidhaa utaikuta hapohapo! ukikaa ofisini unaletewa saa ya 300000 unaambiwa lete 150000, ukiuliza imetoka wapi unaambiwa imeibiwa airport! usiache mafundi wakutengenezee matofali wakati haupo watabadilisha ratio bila kujali ubora utajijua mwenyewe na nyumba yako
hayo ni machache niliyokutana nayo, sasa niambieni tunaanzia wapi kurekebisha hii hali!!
Follow Us Here