Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Tanzania usipofisadi serikalini - adhabu ni hii

    Report Post
    Page 2 of 2 FirstFirst 12
    Results 21 to 27 of 27
    1. #1
      salosalo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 7th June 2012
      Location : Arusha
      Posts : 529
      Rep Power : 541
      Likes Received
      133
      Likes Given
      36

      Default Tanzania usipofisadi serikalini - adhabu ni hii

      Kwa muda mrefu watanzania tumekuwa na tabia ya kusifu uovu unapofanyika.... sasa imekwenda hadi makazini. mtu akiajiriwa serikalini kwenye nafasi yoyote yenye mianya ya kuiba au kufisadi bila kufanya hivyo anatukanwa kila aina ya tusi na watz wenzake wanao mzunguka. Zaidi wale waliowahi kushika nafasi za namna hiyo serikalini bila utajiri mpaka kustaafu,wamekuwa wakinyooshewa vidole na kuambiwa Ugoigoi wao ndo uliowaponza.

      Lakini kwa wale waliopata kuliibia taifa(kufisadi) kwa namna yoyote wanaitwa wajaja, kwamba huyo sio boya kama maboya wengine. Maneno haya yanazungumzwa mbele ya watoto wanaokua. Wanajegwa kwa kuamini kuwa kuibia serikali ndio ujanja, kinyume na hapo ni uboya. Kumbe naomba jamii tubadilike, tuanye kusifu uchafu huku tukidhani tunajenga kumbe tunabomoa. Tena watu wakiwa kazini ukawazuia kuiba mali ya umma basi watakuundia mikasa ili ufukuzwe kazini kwa madai kuwa unaweka jam. Kwa serikalini kama wanamamlaka kubwa basi maramoja utahamishwa kituo cha kazi.

      Nashauri vita dhidi ya ufisadi ianzie nyumbani kwetu. Wazee wa busara semeni kitu hapa....
      katoto, fige and Ndukidi like this.


    2. #21
      KISHOKA_ZUMBU's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 4th April 2012
      Location : DAR ES SALAAM
      Posts : 124
      Rep Power : 387
      Likes Received
      41
      Likes Given
      14

      Default Re: Tanzania usipofisadi serikalini - adhabu ni hii

      Kama tutakubali kubaki maskini tunaweza kuwa Ethical, nina maana 2kikubali mfumo wa ujamaa 2naweza kuwa ethical.
      Katka mfumo wa uchumi wa kibepari haiwezekani kuwa Ethical.
      Ufisadi is there 2 stay!
      Ukiona m2 anapiga kelele ni kwasababu hajauona mfereji wa kuchota, akishauona kimyaa.

    3. #22
      Nov11's Avatar
      Junior Member Array
      Join Date : 16th July 2012
      Posts : 4
      Rep Power : 0
      Likes Received
      0
      Likes Given
      6

      Default Re: Tanzania usipofisadi serikalini - adhabu ni hii

      wafundishwe na sisi wenyewe wazazi wa sasa wenye watoto wadogo,tukianzia hapo nafikiri labda itasaidia kuwa na kizazi chenye maadili.

    4. #23
      salosalo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 7th June 2012
      Location : Arusha
      Posts : 529
      Rep Power : 541
      Likes Received
      133
      Likes Given
      36

      Default Re: Tanzania usipofisadi serikalini - adhabu ni hii

      Quote By Borat69 View Post
      Mkuu,
      Hii nadhani itakuwa ngumu kidogo. Mimi nakumbuka nilipokuwa mdogo(6-7yrs) huko kipindi cha nyuma nilikuwa nikipita jikoni nyumbani na kukuta nyama inachemshwa nilikuwa nanyakua Kama paka jizi na kukimbilia uwani kula..bila kujali nilikuwa naihujumu familia yetu,huku lawama zote zikienda kwa dada (house girl) kwamba ndiye aliyekuwa akifanya ufisadi wa mboga. Arobaini zangu zilifika nikakamatwa na mfupa uwani,nikatandikwa na fimbo ya mpera na tabia ya uhujumu mboga ikakomea hapo.

      Kwa hiyo kuna uwezekano kabisa hivi vitabia tunavyo tokea utoto. Inahuzunisha lakini ndio ukweli.
      Kwa hiyo unashauri tuwatafutie fimbo za mpera hawa mafissad ili waache kama wewe? Nimefurahishwa sana na comment yako

    5. #24
      salosalo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 7th June 2012
      Location : Arusha
      Posts : 529
      Rep Power : 541
      Likes Received
      133
      Likes Given
      36

      Default Re: Tanzania usipofisadi serikalini - adhabu ni hii

      Quote By Choi View Post
      mafisadi sio serikalini tu, hata kwenye sekta binafsi. nilikuwa na kiduka changu cha dawa baridi nimemuweka mdada aniuzie nikienda kazini anaenda kkoo anachukua dawa zake ndio anauza hapo dukani zangu haziuziki mpaka nikafunga duka ndio jirani akaja kunipa hiyo siri. ukienda posta kwenye maduka ya wahindi wauzaji wanakwambia hii bidhaa inauzwa 300000,lakini nenda pale mlangoni umpe mlinzi 150000 na bidhaa utaikuta hapohapo! ukikaa ofisini unaletewa saa ya 300000 unaambiwa lete 150000, ukiuliza imetoka wapi unaambiwa imeibiwa airport! usiache mafundi wakutengenezee matofali wakati haupo watabadilisha ratio bila kujali ubora utajijua mwenyewe na nyumba yako
      hayo ni machache niliyokutana nayo, sasa niambieni tunaanzia wapi kurekebisha hii hali!!
      Nimechoka mwili mzima. Ila mimi naona jukumu hilo wakipewa wanahabari yaani magazeti, Radio na Tv ili wapandikize mbegu ya uzalendo kwa watoto wanaokua bila kuwasahau walimu has wale wa primary na secondary.
      Matangazo yanayofaa kwenye Tv ni yale yanayotangaza biashara huku yakihimiza Maadili mema kama lile la safari larger. yeyote atakaye liangalia atahamasika kufanya kazi kwa kujituma sana ili kufikia malengo yake. Tangazo kama la Godoro la commfy linahamasisha rushwa, eti mtu kakamatwa anauza godoro feki la comfy anamwambia mnunuaji asimshitaki polisi ili ampe godoro halisi la comfy bure. Kama sio kufundisha na kuhamasisha rushwa ni nini hii?

    6. #25
      salosalo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 7th June 2012
      Location : Arusha
      Posts : 529
      Rep Power : 541
      Likes Received
      133
      Likes Given
      36

      Default Re: Tanzania usipofisadi serikalini - adhabu ni hii

      Quote By KISHOKA_ZUMBU View Post
      Kama tutakubali kubaki maskini tunaweza kuwa Ethical, nina maana 2kikubali mfumo wa ujamaa 2naweza kuwa ethical.
      Katka mfumo wa uchumi wa kibepari haiwezekani kuwa Ethical.
      Ufisadi is there 2 stay!
      Ukiona m2 anapiga kelele ni kwasababu hajauona mfereji wa kuchota, akishauona kimyaa.
      Si bora hata kama wanachota wazielekeze kwenye uwekezaji hapa nchini ili waTz wafaidike na ongezeko la ajira. Walivyowajinga wanapeleka benki za nje ama wanawekeza nchi za nje bula kujua kuwa wanaendeleza nchi za wenzao na kuacha ya kwao ikisuasua. Lakini Maisha Bila ufisadi yanawezekana hata katika mfumo wa kibepari


    7. #26
      salosalo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 7th June 2012
      Location : Arusha
      Posts : 529
      Rep Power : 541
      Likes Received
      133
      Likes Given
      36

      Default Re: Tanzania usipofisadi serikalini - adhabu ni hii

      Quote By kerusa View Post
      wafundishwe na sisi wenyewe wazazi wa sasa wenye watoto wadogo,tukianzia hapo nafikiri labda itasaidia kuwa na kizazi chenye maadili.
      Mkuu hao unaowaita wazazi ndio ambao mtoto wake akiokota bunda la pesa na kumpelekea aliyedondosha, nyumbani hapakaliki. Atamtandika mtoto na kumwita kila jina baya, mara kenge we! mjinga mkubwa.. ua unataka usile leo.. nisikilize vizuri we litoto lipuuzi, sikunyingine ukiokota pesa ficha na kimbia nyumbani uniletee.sawasawa?(kwa ukali na kitisho)

    8. #27
      salosalo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 7th June 2012
      Location : Arusha
      Posts : 529
      Rep Power : 541
      Likes Received
      133
      Likes Given
      36

      Default Re: Tanzania usipofisadi serikalini - adhabu ni hii

      Quote By Choi View Post
      mafisadi sio serikalini tu, hata kwenye sekta binafsi. nilikuwa na kiduka changu cha dawa baridi nimemuweka mdada aniuzie nikienda kazini anaenda kkoo anachukua dawa zake ndio anauza hapo dukani zangu haziuziki mpaka nikafunga duka ndio jirani akaja kunipa hiyo siri. ukienda posta kwenye maduka ya wahindi wauzaji wanakwambia hii bidhaa inauzwa 300000,lakini nenda pale mlangoni umpe mlinzi 150000 na bidhaa utaikuta hapohapo! ukikaa ofisini unaletewa saa ya 300000 unaambiwa lete 150000, ukiuliza imetoka wapi unaambiwa imeibiwa airport! usiache mafundi wakutengenezee matofali wakati haupo watabadilisha ratio bila kujali ubora utajijua mwenyewe na nyumba yako
      hayo ni machache niliyokutana nayo, sasa niambieni tunaanzia wapi kurekebisha hii hali!!
      Ukweli mtupu huo mkubwa tena kama kuna bidhaa zinakaa ndani ya mabox usisite kufungua ili kujiridhisha kama bado zimo. Unaweza ukawa unaonyeshwa mabox tupu huku mali ilishauzwa kitambo

    Page 2 of 2 FirstFirst 12

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...