muwamba ngoma, ngozi huvutia kwake? Chadema tunapenda sana Dr. Slaa kiasi cha kusahau mapungufu yake kama binadamu mwingine. Kitendo cha kuzaa watoto wawili na kama kweli walikuwa wanakaa pamoja zaidi ya miezi 6 chini ya paa moja na majirani wa kuprove hilo wapo Rose anakuwa mke wa Dr. Slaa by default so she is a legal wife. Hatuingilii mahakama ni maoni tu
Mkuu kuna mambo kadhaa kwenye post yako:-
(i) Hapo kwenye green: kuzaa hata watoto mia nje ya ndoa haku-justify ndoa na yule uliyezaa naye. So, that is pointless.
(ii) Hapo kwenye red: Inawezekana lakini umeangalia upande mmoja tu in favor of Rose. Hebu angalia upande wa pili wa coin, suppose Rose ndiye aliyemtelekeza Dr. Slaa? Au kwa kuwa ni yeye (Rose) ndiye anayelalamika unadhani hawezi akawa ndiye chanzo cha mgogoro?
(iii) Hapo kwenye red: Umezingatia dhana iitwayo "UTORO KWENYE NDOA"? Umezingatia pia kwamba mume n mke wasipokuwa pamoja kwa muda fulani ndoa inakuwa VOID? Katika shauri hili inawezekana Rose au Dr. Slaa au wote wamekuwa watoro kwenye "ndoa" yao kwa muda unaotambulika kisheria hivyo dhana ya ndoa haipo. Usiangalie upande mmoja tu wa kuungana hata kutengana pia kunatambulikana kisheria.
(iv) Huyu Rose kama si kutumiwa, angeibuka mapema kabla muda unaotambuliwa kisheria wa UTORO KWENYE NDOA haujakamilika. Mtu hawako pamoja kwa zaidi ya miaka sijui mingapi halafu leo unaibuka eti ni mume wangu hana hata aibu? Anachopaswa kudai ni MALI WALIYOCHUMA PAMOJA (kama ipo) na sio HAKI YA MUME.
(v) Ndoa tarajiwa ya Dr. Slaa na Josephine: Sijui ndoa ya Dr. Slaa inatarajiwa kufungwa kwa madhehebu gani ila kama ni madhehebu ya kikristo; ndoa huwa ndoa halali pale inapofungwa kiimani. Hivyo, dhana yako uliyoitaja hapo kwenye red haitambuliki na kanisa hivyo Dr. Slaa hakuwahi kuwa na ndoa hapo kabla.
Otherwise, binafsi nampongeza sana Dr. W. Slaa na Mkewe Mtarajiwa, Josephine Mushumbusi, kwa kuachana na maisha ya ukapera na kuanza maisha mapya ya ndoa. Hongereni sana Maharusi wetu. Mwenyezi Mungu awajalie maisha marefu yenye baraka na fanaka kwa familia yenu.
Follow Us Here