Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Ukombombozi wa wanywaji pombe umeribia.

    Report Post
    Results 1 to 17 of 17
    1. #1
      Kurunzi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 31st July 2009
      Location : DAR ES SALAAM
      Posts : 2,012
      Rep Power : 905
      Likes Received
      392
      Likes Given
      171

      Default Ukombombozi wa wanywaji pombe umeribia.

      KILA mwaka Serikali
      imekuwa ikiongeza kodi
      kwenye vinywaji, hususan
      pombe ili kukidhi bajeti
      ya mapato na matumizi
      yake. Hali hiyo
      husababisha bei ya
      pombe kupanda karibu kila mwaka na
      kuwaongezea mzigo wanywaji kwa kulazimika
      kuzama zaidi kwenye mifuko yao ili kugharimia
      kinywaji hicho.Kwa miaka yote hiyo wanywaji
      wamekuwa wakilia kimoyomoyo bila ya kuwa na
      mahali pa kupaza sauti zao, hali inayoifanya
      Serikali ione kinywaji ni mahali kukimbilia
      kupata fedha.
      Kulingana na taarifa za viwanda vya bia, bei ya
      kinywaji hicho huenda ikapanda kwa karibu
      asilimia 25, kuanzia mwezi huu, jambo ambalo
      limewafanya wanywaji kusema; “Hapana!
      Haiwezekani.”
      Kwa sababu hiyo, wanywaji tayari wameunda
      jukwaa lao la kupaza sauti zao na tayari
      wameweka mikakakati ya kudai haki
      zao.Chombo hicho wamekipa jina “Chama cha
      Wanywa Pombe kwa Staha Tanzania (TRBDA)”
      na tayari kimesajiliwa na sasa kipo katika
      harakati za mikakati ya kukabiliana na Serikali.
      “Sisi tunachotaka ni bei ya bia kushuka au
      kubakia palepale (Sh1,700). Hili ni suala nyeti
      na hatari kuliko watu wanavyolifikiria sasa,”
      anasema Rais wa TRBDA, Gasisi Mahuti.
      Anaongeza; “Chama kimesajiliwa Mei 22
      mwaka huu, hivyo tuna nguvu ya kisheria
      kufanya kazi na kutetea maslahi ya wanachama
      wetu.
      “Tunaona kero kila mwaka, kila Bajeti ya Serikali
      wanakuja na mikakati ya kuongeza kodi kwenye
      pombe.”
      Mahuti anasema kwa miaka mingi mzigo huo
      wa ongezoko la bei ya bia ambayo ndiyo
      inayotumiwa na watu wengi, imekuwa
      ikiongezeka, lakini safari hii, hali ni mbaya
      zaidi.
      Mzigo huo kwa wanywaji anasema
      umechangiwa na mambo mawili makubwa
      ambayo ni kuongezeka kwa gharama za maisha
      na kiwango kikubwa cha kodi kwa mwaka huu
      wa fedha 2012/13 ulioanza leo.
      “Hiyo bei itasababisha wanywaji wengi kuhama
      kwenye kinywaji salama na kwenda kwenye
      kinywaji hatarishi na haramu,” analalamika
      Mahuti.
      Anavitaja vinywaji hatarishi kuwa ni baadhi ya
      pombe za kienyeji ambazo ni hatari kwa afya
      kwa sababu nyingi zinaandaliwa kwenye
      mazingira machafu na hakuna udhibiti. Pombe
      haramu anaitaja kuwa ni gongo.
      Madhara ya kupandishwa bei ya pombe,
      anasema siyo hayo tu bali yapo ya kuathiri
      uchumi na maenedeleo ya watu.
      “Nenda baa utaona. Siku hizi wanywaji wengi
      hawakai pamoja kila mmoja akiingia baa
      anaagiza bia yake tofauti na hapo awali mtu
      anazungusha ‘raundi’.
      “Hili ni tatizo maana watu wengi sasa ‘hawa-
      socialize’. Hawakai pamoja baa kubadilishana
      mawazo, kupeana mbinu za maisha. Hii ni
      hatari,” analalamika Mahuti.
      Vita na Serikali
      Mahuta anasema athari za kupanda kwa bei ya
      bia ni nyingi na wanatarajia kuziwasilisha
      serikalini kutaka zipunguzwe.
      Kuhusu namna watakavyowasilisha taarifa hizo,
      Mahuti anasema kwa kuanza watawasiliana na
      ofisi ya Waziri wa Fedha na Uchumi na hata
      likishindikana watabisha hodi ofisi ya Waziri
      Mkuu, Mizengo Pinda.
      Pamoja na malalamiko hayo, anasema
      wamekusudia kuishawishi Serikali kubuni
      vyanzo vingine vya fedha ambavyo imekuwa
      ikishindwa kuvitumia kutokana na uzembe wa
      watendaji wake.
      Baadhi ya sekta nchini zinapopeleka madai
      yake serikalini hugoma ili kutoa shinikizo.
      Kuhusu wana mpango wa kugoma endapo
      serikali itakaidi kushusha kodi.
      Kiiongozi huyo anakiri kuwa wanywaji wakigoma
      Serikali inaweza ikatikisika kwa sababu
      wanachangia pato kubwa serikalini.“Lakini sisi
      hatutaki kufikia huko (kugoma) au kuandamana.
      Sisi tunaenda kuzungumza tu hatuna haja ya
      kufanya fujo.
      “Sisi wanywa pombe kwa staha tunatazamia
      busara zaidi zitatumika kuliko kulazimishana na
      kusababisha madhara,” anasema.Nimemuuliza,
      iwapo busara zitashindikana watachukua hatua
      gani, anasema: “Kama nilivyokuambia awali
      wanywa pombe walikuwa hawana jukwaa la
      kusemea. Sasa wanalo.
      “Tunaamini kwamba Serikali ilikuwa inaongeza
      kodi kwa kutofahamu madhara yake ama kwa
      kutokuwa na vyanzo vingine. Sisi tunaenda
      kuwaambia madhara yake na tunaenda
      kuwaeleza njia nyingine za mapato. Suala la
      kugoma, kuandamana; halipo.”
      Anasema kwa miaka mingi wanywaji ndio
      wamekuwa wakichangia pato la Serikali na
      kufanikisha utaji wa huduma mbalimbali kwa
      jamii kama vile elimu, afya na maji.
      Ingawa wanywaji wamekuwa wakichangia hayo
      yote, anasema wao si wote wenye fedha sana
      bali wengi wao ni watu wa kipato cha kawaida.
      “Mtu haindi kunywa pombe kwa sababu ana
      pesa nyingi. La, hasha! Ni sehemu tu ya
      kubadilishana mawazo na kupata maarifa. Hii ni
      njia ya kupashana habari,” anasema.
      Majuku mengine TRBDA
      Mahuti anasema jukumu la kuanzishwa kwa
      TRBDA siyo tu kutetea maslahi ya wateja katika
      suala la bei tu bali mikakati mingene ya kiafya,
      kijamii na kielimu.
      Anasema Septemba Mosi mwaka huu kwa mara
      ya kwanza hapa nchini chama hicho
      kitaadhimisha tamasha kubwa la maadhimisho
      ya siku ya wanywa pombe duniani.
      Anasema siku hiyo imekuwa ikisheherekewa
      duniani, lakini hapa nchini imekuwa haijulikani
      kwa sababu hakuna chombo cha uhamasishaji
      wa maadhimsiho.
      Mzee Wa Rubisi likes this.


    2. #2
      Gwangambo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 30th June 2012
      Location : Mabwepande
      Posts : 1,125
      Rep Power : 576
      Likes Received
      267
      Likes Given
      87

      Default Re: Ukombombozi wa wanyaji pombe umeribia.

      Duuuh, inaelekea habari uliiandaa vizuri ukiwa hujawa keroro, baada ya kupiga ulabu ukatafuta title na ku-post.
      " ukombombozi" "wanyaji" "umeribia"
      Pombe nouma!
      Sigma likes this.

    3. #3
      Mshuza2's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th December 2010
      Posts : 1,309
      Rep Power : 691
      Likes Received
      201
      Likes Given
      17

      Default

      Makubwaa!

    4. #4
      Sigma's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 26th February 2011
      Location : The 2nd House on the Left
      Posts : 4,456
      Rep Power : 1376
      Likes Received
      989
      Likes Given
      662

      Default Re: Ukombombozi wa wanyaji pombe umeribia.

      hii habari nzuri.
      ...------------------------------------------------.---------------------------------------------------------------------..Rather Kill a FRIEND than Risk Missing an ENEMY

    5. #5
      hamidshaban's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 4th January 2011
      Posts : 137
      Rep Power : 521
      Likes Received
      18
      Likes Given
      0

      Default

      kutegemea kodi ya pombe! Nchi haiwezi kupiga hatua. Maana siyo mpango wa Mungu.achane kunywa pombe muone kama mtakufa.


    6. #6
      Sigma's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 26th February 2011
      Location : The 2nd House on the Left
      Posts : 4,456
      Rep Power : 1376
      Likes Received
      989
      Likes Given
      662

      Default Re: Ukombombozi wa wanyaji pombe umeribia.

      Kesho baada ya kuamka naheng'ova kapige supu,
      usizimue,
      ukishakuwa sober,
      njoo rekebisha title,
      au omba mods wakurekebishie title fresh.
      ...------------------------------------------------.---------------------------------------------------------------------..Rather Kill a FRIEND than Risk Missing an ENEMY

    7. #7
      Sigma's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 26th February 2011
      Location : The 2nd House on the Left
      Posts : 4,456
      Rep Power : 1376
      Likes Received
      989
      Likes Given
      662

      Default Re: Ukombombozi wa wanyaji pombe umeribia.

      TRBDA'
      nimependa.
      kirefu chake nini vile?
      hiki ndo chama.
      ...------------------------------------------------.---------------------------------------------------------------------..Rather Kill a FRIEND than Risk Missing an ENEMY

    8. #8
      hamidshaban's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 4th January 2011
      Posts : 137
      Rep Power : 521
      Likes Received
      18
      Likes Given
      0

      Default Re: Ukombombozi wa wanyaji pombe umeribia.

      &then kupeana mawazo bar! You must be kidding. Let us be a bit more serious. Iv wajapan au wachina mawazo ya maendeleo wanayapata bar

    9. #9
      hamidshaban's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 4th January 2011
      Posts : 137
      Rep Power : 521
      Likes Received
      18
      Likes Given
      0

      Default Re: Ukombombozi wa wanywaji pombe umeribia.

      &kuungana itakuwa ngumu maana kwa wengine ndo zaman ikiitwa mtama kwa watoto! Si ndo imekuwa ya wachache?achana uchafu huo. Havakupeleka popote

    10. #10
      simplemind's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 10th April 2009
      Posts : 2,951
      Rep Power : 1180
      Likes Received
      531
      Likes Given
      0

      Default Re: Ukombombozi wa wanywaji pombe umeribia.

      Salushan ni homemade beer. Piga beer zako nyumbani tax free halafu unamalizia bar na hizo over taxed beer.

    11. #11
      asigwa's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st September 2011
      Location : Tandhaniya
      Posts : 4,497
      Rep Power : 1291
      Likes Received
      1242
      Likes Given
      1267

      Default Re: Ukombombozi wa wanywaji pombe umeribia.

      kweli mkuu suala la kugoma kunywa haliwezekani kwani wengine tusipostua kidogo tunahisi matumbo yanatetemeka... dawa ni kupanga siku ya maandamano tunaanzia pale sinza kijiweni mpaka magogoni tukiwa tushatupia kama 6 hivi kila kichwa halafu moja mononi tunaomba tukutane na mkuu wa kaya

    12. #12
      meningitis's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 17th November 2010
      Location : sewahaji
      Posts : 3,032
      Rep Power : 3234
      Likes Received
      1063
      Likes Given
      155

      Default Re: Ukombombozi wa wanywaji pombe umeribia.

      siku hizi ni bia mbili tu mapeema nyumbani.CUT SPENDING!!! TRA itakula kwenu.

    13. #13
      Mzee Wa Rubisi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 6th November 2010
      Location : Chini ya mgomba
      Posts : 1,299
      Rep Power : 696
      Likes Received
      210
      Likes Given
      272

      Default Re: Ukombombozi wa wanywaji pombe umeribia.

      wazo zuri

    14. #14
      dizo's Avatar
      Member Array
      Join Date : 2nd April 2012
      Posts : 30
      Rep Power : 370
      Likes Received
      0
      Likes Given
      0

      Default

      Quote By hamidshaban View Post
      &then kupeana mawazo bar! You must be kidding. Let us be a bit more serious. Iv wajapan au wachina mawazo ya maendeleo wanayapata bar
      Acha kutuzingu wachina wanatuhusu nini? hapa tunazungumzia Tz.

    15. #15
      St. Paka Mweusi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd September 2010
      Location : Ukune,
      Posts : 5,632
      Rep Power : 13946
      Likes Received
      1785
      Likes Given
      3653

      Default Re: Ukombombozi wa wanywaji pombe umeribia.

      Quote By simplemind View Post
      Salushan ni homemade beer. Piga beer zako nyumbani tax free halafu unamalizia bar na hizo over taxed beer.
      Quote By asigwa View Post
      kweli mkuu suala la kugoma kunywa haliwezekani kwani wengine tusipostua kidogo tunahisi matumbo yanatetemeka... dawa ni kupanga siku ya maandamano tunaanzia pale sinza kijiweni mpaka magogoni tukiwa tushatupia kama 6 hivi kila kichwa halafu moja mononi tunaomba tukutane na mkuu wa kaya
      Quote By meningitis View Post
      siku hizi ni bia mbili tu mapeema nyumbani.CUT SPENDING!!! TRA itakula kwenu.
      Quote By Mzee Wa Rubisi View Post
      wazo zuri
      Quote By dizo View Post
      Acha kutuzingu wachina wanatuhusu nini? hapa tunazungumzia Tz.




      Yeees Hommies, nawaona hapo na ninatoa big up kwa aliyekuja na wazo hilo maana tumeonewa kiasi cha kutosha,na pamoja na mchango wetu kwa Taifa bado tumepuuzwa kiasi cha kutosha kwa kuitwa walevi na wakati mwingine hata kunyanyaswa makazini kisa nini huwa muhudhuriaji mzuri pale chini ya muti,sasa tunasema basi na ikibidi hata kugoma tugome tu tuone wahudumu wote na wachoma kitimoto wataajiriwa na nani..
      UKICHOKA KUFANYA SIRI,FUMANIWA TU YAISHE . By Simon Kitururu.

    16. #16
      Mkirua's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 9th September 2010
      Posts : 3,555
      Rep Power : 1066
      Likes Received
      1288
      Likes Given
      621

      Default Re: Ukombombozi wa wanywaji pombe umeribia.

      Karibu Calabash.....
      The world suffers a lot. Not because of the violence of bad people, but because of the silence of good people!

    17. #17
      Mphamvu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 28th January 2011
      Location : Pale pale kwa JANA!
      Posts : 7,340
      Rep Power : 18686
      Likes Received
      1117
      Likes Given
      1064

      Default Re: Ukombombozi wa wanywaji pombe umeribia.

      Naomba mwongozo wa kufungua ofisi ndogo ya chama huku niliko... Halafu mi nacheza game zote, taifa mpaka ndondo, ila kwa staha.

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...