Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Taarifa ya BLW Znz kuhusu Meli za Iran

    Report Post
    Results 1 to 16 of 16
    1. #1
      Barubaru's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 6th April 2009
      Location : Doha, Qatar
      Posts : 5,732
      Rep Power : 1916
      Likes Received
      1163
      Likes Given
      941

      Default Taarifa ya BLW Znz kuhusu Meli za Iran

      TAARIFA KWA BARAZA LA WAWAKILISHI JUU YA USAJILI WA MELI ZA NJE ULIOFANYWA NA SMZ KUPITIA MAMLAKA YA USAFIRI BAHARINI ZANZIBAR MARITIME AUTHORITY – ZMA

      Mhe. Spika,

      Tarehe 27/06/2012 Vyombo vya Habari hapa Tanzania (The Citizen) na nchi za nje (International news Agency – Bloomberg) viliandika makala kuhusu usajili wa meli 10 za mafuta (Tankers). Ilidaiwa katika makala hayo kuwa Meli hizo zilisajiliwa Zanzibar na zinapeperusha Bendera ya Tanzania na kwamba zinafanya biashara na Kampuni ya Serikali ya IRAN. Gazeti la “The Citizen la tarehe 27 Juni, 2012 lilikuwa na kichwa cha habari “Iran Tankers adopt TZ Flag to avoid embargo” (meli za mafuta za Iran zinatumia bendera ya Tz kukwepa vikwazo.

      TAARIFA YA ZMA

      Mamlaka ya Usafiri Baharini Zanzibar Maritime Authority – ZMA ni Mamlaka iliyoundwa kwa sheria No. 3 ya mwaka 2009 ambayo pamoja na kazi nyengine inasimamia utekelezaji wa Sheria ya usafiri wa Bahari Zanzibar ya mwaka 2006 (Zanzibar Maritime Transport Act 2006).

      Sheria ya Zanzibar Maritime Transport Act 2006, kifungu no. 8 cha sheria hii, kinasomeka kama ifuatavyo:

      Section 8 (1). There shall be established the registers of Tanzania Zanzibar ships to be Known as:-
      (a). Tanzania Zanzibar International Register of Shipping for ocean going ships; and
      (b) Tanzania Zanzibar Register of Shipping for coastal Ships.
      (2). A ship shall be a Tanzania Zanzibar ship for the purpose of this Act if that ship is registered under this part.
      Katika kutekeleza jukumu la usajili wa meli kama ilivyoelekezwa katika kifungu 8(1)(a) hapo juu, Serikali ya Mapinduzi Zanzibar imetiliana mkataba na kampuni ya PHILTEX ya Dubai kufanya usajili wa meli za kimataifa. (Open Registry). Usajili huu umekuwa ukifanyika tangu mwaka 2009 na mpaka sasa ZMA kupitia Wakala wake imesajili meli 399 ikiwa ni pamoja na meli za mafuta, makontena, General cargo na meli za Abiria.

      Kama nilivyoeleza hapo awali, vyombo vya habari vimechapisha makala ya usajili wa meli 10 ambazo zinadaiwa ni meli za IRAN kulingana na makala zao hizo.

      SMZ inatoa taarifa rasmi juu ya meli za mafuta ilizosajiliwa wiki mbili zilizopita pamoja na majina ya meli, ukubwa wake, majina ya makampuni inayomiliki meli hizo na nchi zilizotoka kabla ya kupata usajili kwa ZMA, kama ifuatavyo:

      Jina la meli GRT (Ukubwa) Company name Ilikotoka

      1. Daisy 81479 Daisy Shipping Co. Ltd Malta
      2. Justice 164241 Justice Shipping Co. Ltd Cyprus
      3. Magnolia 81479 Magnolia Shipping Co. Ltd Malta
      4. Lantana 81479 Lantana Shipping Co. Ltd Malta
      5. Leadership 164241 Leadership Shipping Co. Ltd Cyprus
      6. Companion 164241 Companion Shipping Co. Ltd Malta
      7. Camellia 81479 Camellia Shipping Co. Ltd Malta
      8. Clove 81479 Clove shipping Co. Ltd Malta
      9. Courage 163660 Courage Shipping Co. ltd Cyprus
      10. Freedom 163660 Freedom shipping Co. Ltd Cyprus
      11. valor 160930 valor Shipping Co. Ltd. Cyprus

      Jumla ya GRT ni 1,388,368 tons

      Meli hizi ni 11 kama zinavyoonekana katika orodha hapo juu ni miongoni mwa meli nyingi zinazobadilisha usajili wao (De registration). Meli zilizosajiliwa na ZMA zinatoka nchini Cyprus na Malta. Sambamaba na meli hizi 11 zilizosajiliwa na ZMA, meli za mafuta nyengine 20 ambazo zinasemekana zilikuwa kwenye usajili wa nchi za Ulaya zimebadilisha usajili wao na kwenda usajili wa “TUVALU Islands”.

      ZMA ilimtaka Wakala wake Philtex Corporation kuwaita wenye meli hizi na kuwataka kujieleza kuhusu uhusuiano wao na Serikali ya au makampuni ya mafuta ya IRAN. Philtex ilikutana na Wamiliki hao siku ya Alkhamis tarehe 28/06/2012 katika afisi za Philtex Corporation na Wamiliki hao wameeleza kwamba hawana uhusianao na Serikali au mamlaka yoyote nchini Iran na wameamua kuja kusajili meli ZMA kwa ridhaa yao na kwa kufata matangazo ya usajili wetu wa nje (Open Registry).

      Pamoja na maelezo hayo, wamiliki hao wametangaza kwamba ikiwa ZMA haiko tayari kuendelea na usajili wa meli zao, wanaweza kufuta usajili wao na tayari wanafikiria kufanya mazungumzo na open Registry nyengine (PANAMA) lakini hawana nia ya kurudi walikotoka, yaani Cyprus na Malta.

      Kinyume na maelezo yaliyotolewa na vyombo vya habari juu ya uraia wa wamiliki wa meli hizi, Wamiliki wa meli hizi kama walivyojieleza katika usajili wa meli zao wana uraia wa British Vergin Islands na Sychelles.

      Kulingana na “United Nations Convention Law of the Sea”, Article 91, na za “Geneva convection of Registration” articles 6, 7 na 8, na kulingana na Zanzibar Maritime Transport Act of 2006, section 8, Zanzibar ikiwa ni nchi moja kati ya nchi mbili zinazounda Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inayo haki ya kusajili meli yeyote kulingana na taratibu na Sheria za Zanzibar, na sheria za Kimataifa zinazoongoza usajili huo.

      Maelezo haya yanatolewa ili kutoa usahihi wa uvumi kuwa Zanzibar imesajili meli za IRAN ambazo zimewekewa vikwazo na Marekani na nchi za Umoja wa Ulaya (European Union) juu ya usafirishaji na uuzaji wa mafuta kutoka Iran.

      Mhe. Spika, taarifa hizi za vyombo vya habari hazina madhumuni yeyote zaidi ya kuwavunja moyo wenye Makampuni ya meli wanaotaka kusajili meli zao kwetu.

      Hivyo basi Serikali inatamka wazi kwamba Usajili uliofanywa kwa meli hizi umefuata taratibu zote zilizowekwa kisheria na kwamba Serikali imekuwa ikifanya na itaendelea kufanya mazungumzo na wenye meli mbalimbali ili kuongeza idadi na ukubwa wa meli inazosajili nje ya nchi. Biashara hii ya ukubwa wa GRT 1,388,368 Tons katika kipindi cha wiki mbili na maombi mapya matano kwa meli zitakazokuwa na ukubwa wa zaidi ya GRT 500,000 imeshtua Makamuni mengine na hata nchi nyengine zisizoitakia mema Zanzibar katika juhudi zake za kukuza mapato na uchumi wake.

      Hata hivyo mamlaka itafata sheria zote zilizowekwa kitaifa na kimataifa katika biashara ya usafiri baharini na itahakikisha meli zinasajiliwa chini ya mamlaka hii zinafata taratibu ilizoweka.

      Mhe. Spika, kabla ya taarifa hizi za vyombo vya habari (The Citizen), Waziri wa Uchukuzi wa SMT Mhe. Harisson Mwakyembe) alipokuwa akijibu suala Bungeni hivi juzi hakuonyesha kurishika kwake katika usajili wa meli (Open Registry) inayofanywa na Zanzibar na kuahidi kufanya ziara ya kuja Zanzibar kuonana na Waziri anaehusika kuzungumzia suala hili. Taarifa za “The Citizen” zaweza kuwa ni muendelezo wa Mhe. Mwakyembe kutoridhika kwake katika usajili unaofanywa na Serikali kupitia uwakala wake huko Dubai.

      Mhe. Spika, Zanzibar haifungiki kusajili meli za nchi yeyote.
      Hili ni suala la kibiashara na kwamba kwa Serikali yetu ni njia moja ya kuongeza mapato yanayoendesha Serikali, alimradi tu usajili huo hauvunji sheria za Kimataifa.

      Mhe. Spika,

      Zanzibar ina uhusiano mkubwa na wa muda mrefu na nchi nyingi ikiwemo IRAN na hivi karibuni Zanzibar ilipata ugeni (Makamo wa Rais wa Iran) na viongozi wetu walifanya mazungumzo ya namna gani IRAN itaendelea kusaidia Zanzibar katika miradi ya Maendeleo. Zanzibar haingependa kuingizwa kwa visingizio vyovyote na kwa njama zozote katika migogoro isiyowahusu.

      Hivyo, kwa taarifa hii, Serikali inakanusha rasmi uvumi wa vyombo vya habari kuhusiana na suala hili kama taarifa hii ilivyofafanua hapo juu.

      Mhe. Spika, naomba kuwasilisha.

      Hamad Masoud Hamad
      WAZIRI WA MIUNDOMBINU NA MAWASILIANO
      Pukudu likes this.
      Ukiwa mchoyo, usiwe mroho.

      Man Sharaf naf'sahu, fahuwa rasul

    2. FemaTV & Radio

    3. #2
      Hute's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 25th November 2010
      Posts : 1,402
      Rep Power : 710
      Likes Received
      354
      Likes Given
      23

      Default Re: Taarifa ya BLW Znz kuhusu Meli za Iran

      hawa midebwedo waongelea puani, dawa yao ni kujitenga nao tu, ili waendelee na zenji yao, hapo ndipo watakapoona kumbe walikuwa wanaponea kwenye muungano....kwanza wanatuchafulia hata jina, kwano wao ndo vinara wa ugaidi tz....
      Kama huna meno,usile bisi, kula Bwimbwi yaani kimbugi. Uongozi ukikushinda waachie wanaoweza!

    4. #3
      Pukudu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 6th January 2011
      Location : Maskani.
      Posts : 1,171
      Rep Power : 1385
      Likes Received
      334
      Likes Given
      81

      Default Re: Taarifa ya BLW Znz kuhusu Meli za Iran

      Imedadavuliwa vizuri na inaeleweka, naombeni kuuliza je? Hii taarifa Kwenye gazeti la Citzen,na ile BARUA toka congress Kama sikosei kipi kilitangulia? Je Wamarekani siku hizi wanafanyia "kazi" habari za magazeti ya kibongo.
      Anyway Mbona kila kitu kiko wazi kutokana na maelezo ya Huyo waziri! Sasa hizi tuhuma za wamarekani kwa watanzania zinatokea wapi? Au mishemishe za MASLAHI binafsi zimeanza? I'm confused a bit nipeni mwanga.

      Snitch likes this.
      If I agree with you both we'll be wrong...(Kama nikikubaliana na wewe wote tutakuwa tumepotoka)

    5. #4
      simplemind's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 10th April 2009
      Posts : 2,842
      Rep Power : 1154
      Likes Received
      505
      Likes Given
      0

      Default

      Quote By Hute
      hawa midebwedo waongelea puani, dawa yao ni kujitenga nao tu, ili waendelee na zenji yao, hapo ndipo watakapoona kumbe walikuwa wanaponea kwenye muungano....kwanza wanatuchafulia hata jina, kwano wao ndo vinara wa ugaidi tz....
      Home keeping youth have ever homely wits.

    6. #5
      BINARY NO's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th December 2011
      Posts : 549
      Rep Power : 482
      Likes Received
      136
      Likes Given
      63

      Default Re: Taarifa ya BLW Znz kuhusu Meli za Iran

      Zanzibar do what you want na sio sisi wa BARA tunataka mfanye...As long as you dont break international laws...Kusajiri MELI za IRAN hakuna kosa lolote kwani MAREKANI na ULAYA wamewawekea makampuni ya nchi zao kutofanya biashara ya mafuta na IRAN na kuondoa insurance kwenye MELI za ULAYA kwenda IRAN...So lazima mfahamu TANZANIA,ZANZBAR kufanya biashara na IRAN hakuna kosa kwani we all benefit na sio kutegemea misaada ya US/EU...Huo ugomvi wa US na IRAN hauwezi kutufanya sisi tu side na US by the way vikwazo sio vya UMOJA WA MATAIFA ila ni vya US/EU sasa kwanini watutishie kisa wanatupa misaada? Hakuna aja ya kuogapa eti tutawekewa vikwazo ata km wakiweka sio vikwazo vya UN bali ni vya nchi moja na huo ndo utakua mwanzo wa kupata akili na ndo chachu ya kujitegemea na sio kufikiria misaada ambayo inadharirisha utu wetu na isitoshe imekuepo tokea uhuru na still bado tupo maskini...nini tunaweza kufanya incase tumewekewa vikwazo na sisi ndo mwanzo wa kuwafukuza ktk mariasili zetu mf dhahabu,gas,mafuta urine nadhani apo watapata picha kua uhuru wa nchi moja hauwezi kuingiliwa na ka sanetor kamoja ka US

    7. Miaka 50

    8. #6
      Lambardi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 7th February 2008
      Location : KITAANI ZAIDI
      Posts : 4,507
      Rep Power : 1793
      Likes Received
      653
      Likes Given
      0

      Default Re: Taarifa ya BLW Znz kuhusu Meli za Iran

      Hamad wewe Hamad unatamba tu na usiyoyajua subiri watakavyokugeuka na kuombwa kujiuzulu baada ya tishio la kupigwa na vikwazo vya uchumi!!tulia tu utayakana maneno yako hayo!!yangu macho na masikio

    9. #7
      Bangoo's Avatar
      Banned Array
      Join Date : 3rd November 2011
      Posts : 2,269
      Rep Power : 0
      Likes Received
      370
      Likes Given
      0

      Default Re: Taarifa ya BLW Znz kuhusu Meli za Iran

      Kama tanganyika wakijitenga na znz basi znz itakuwa sehemu ya ugaidi duniani.

    10. #8
      Elli's Avatar
      Banned Array
      Join Date : 17th March 2008
      Location : Kijito-Upele
      Posts : 8,513
      Rep Power : 0
      Likes Received
      2102
      Likes Given
      1839

      Default Re: Taarifa ya BLW Znz kuhusu Meli za Iran

      Aaaahhhh hii ni ya zamani mkuu ila si MBAYA tukaicheki tena maana hata meli zilizotajwa sizo zilizoripotiwa

    11. #9
      Kassim Awadh's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 12th March 2012
      Posts : 584
      Rep Power : 478
      Likes Received
      108
      Likes Given
      769

      Default Re: Taarifa ya BLW Znz kuhusu Meli za Iran

      Quote By Skills4Ever
      Hamad wewe Hamad unatamba tu na usiyoyajua subiri watakavyokugeuka na kuombwa kujiuzulu baada ya tishio la kupigwa na vikwazo vya uchumi!!tulia tu utayakana maneno yako hayo!!yangu macho na masikio
      Kwani inshu kabisa ikoje mkuu?

    12. #10
      Albimany's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 11th April 2011
      Posts : 187
      Rep Power : 447
      Likes Received
      59
      Likes Given
      0

      Default Re: Taarifa ya BLW Znz kuhusu Meli za Iran

      Quote By Bangoo
      Kama tanganyika wakijitenga na znz basi znz itakuwa sehemu ya ugaidi duniani.

      Labda nikweli uyasemayo ila na zanzibar kutapungua ujambazi, ukimwi na umalaya!

    13. #11
      sanga malua's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 17th December 2011
      Posts : 226
      Rep Power : 420
      Likes Received
      46
      Likes Given
      54

      Default Re: Taarifa ya BLW Znz kuhusu Meli za Iran

      Hawa wazanzibar hawana focus. wamepania kufanya mambo mengi kwa wakati mmoja na yote yanautata katika mtazamo wa kidunia. UAMSHO inamwelekeo wa kigaidigaidi hivi na watu duniani wanawaangalia!hizi meli nazo mmh zina utata wake.kuna baadhi ya viongozi wanajitafutia shida duniani!ntie hata vikwazo wazungu hawata viweka watakuja mchana kweupeee watawakamata hao wanao wadanganya eti ZANZIBAR NI NCHI HURU haihitaji kuchaguliwa marafiki sawa lakini kufanya biashara na IRANI ni kujipalia mkaa wa moto angalieni mnakoekea siyo kuzuri,

    14. #12
      Candid Scope's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 8th November 2010
      Posts : 7,602
      Rep Power : 15259
      Likes Received
      3727
      Likes Given
      2861

      Default Re: Taarifa ya BLW Znz kuhusu Meli za Iran

      Zanzibar soon kitageuka kituo maarufu cha magaidi kama wakiamua **** huhu na kule. Pesa ina madhara yake.

    15. #13
      Mkirua's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 9th September 2010
      Posts : 3,384
      Rep Power : 1027
      Likes Received
      1160
      Likes Given
      595

      Lightbulb Re: Taarifa ya BLW Znz kuhusu Meli za Iran

      Quote By BINARY NO
      Zanzibar do what you want na sio sisi wa BARA tunataka mfanye...As long as you dont break international laws...Kusajiri MELI za IRAN hakuna kosa lolote kwani MAREKANI na ULAYA wamewawekea makampuni ya nchi zao kutofanya biashara ya mafuta na IRAN na kuondoa insurance kwenye MELI za ULAYA kwenda IRAN...So lazima mfahamu TANZANIA,ZANZBAR kufanya biashara na IRAN hakuna kosa kwani we all benefit na sio kutegemea misaada ya US/EU...Huo ugomvi wa US na IRAN hauwezi kutufanya sisi tu side na US by the way vikwazo sio vya UMOJA WA MATAIFA ila ni vya US/EU sasa kwanini watutishie kisa wanatupa misaada? Hakuna aja ya kuogapa eti tutawekewa vikwazo ata km wakiweka sio vikwazo vya UN bali ni vya nchi moja na huo ndo utakua mwanzo wa kupata akili na ndo chachu ya kujitegemea na sio kufikiria misaada ambayo inadharirisha utu wetu na isitoshe imekuepo tokea uhuru na still bado tupo maskini...nini tunaweza kufanya incase tumewekewa vikwazo na sisi ndo mwanzo wa kuwafukuza ktk mariasili zetu mf dhahabu,gas,mafuta urine nadhani apo watapata picha kua uhuru wa nchi moja hauwezi kuingiliwa na ka sanetor kamoja ka US
      umenichekesha sana.,...wewe mbara sio?? umeamua kujifanya mbara ili uongeze ***** humu?? Can you stand stand on you own withouth them and Tanganyika?? Probably mnataka kuwaua wananchi wenu kwa kwashiokor...
      The world suffers a lot. Not because of the violence of bad people, but because of the silence of good people!

    16. #14
      Mkirua's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 9th September 2010
      Posts : 3,384
      Rep Power : 1027
      Likes Received
      1160
      Likes Given
      595

      Default Re: Taarifa ya BLW Znz kuhusu Meli za Iran

      Quote By Albimany
      Labda nikweli uyasemayo ila na zanzibar kutapungua ujambazi, ukimwi na umalaya!
      Na huku bara pia tutaepuka ushoga....bora uvunjike kabisa....
      The world suffers a lot. Not because of the violence of bad people, but because of the silence of good people!

    17. #15
      andishile's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 1st April 2012
      Posts : 592
      Rep Power : 477
      Likes Received
      144
      Likes Given
      278

      Default Re: Taarifa ya BLW Znz kuhusu Meli za Iran

      kumekucha!

    18. #16
      KengeWaKijani's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 28th June 2012
      Posts : 103
      Rep Power : 367
      Likes Received
      16
      Likes Given
      0

      Default Re: Taarifa ya BLW Znz kuhusu Meli za Iran

      Mi cjaelewa kabisa.

    19. Study Abroad

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...