Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: UTEUZI: Wakili wa LULU awa Jaji

    Report Post
    Results 1 to 7 of 7
    1. #1
      mizambwa's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 8th October 2008
      Posts : 1,436
      Rep Power : 974
      Likes Received
      367
      Likes Given
      1805

      Default UTEUZI: Wakili wa LULU awa Jaji

      Rais amteua wakili wa Lulu kuwa Jaji.
      June 20, 2012
      Posted in: Habari vyanzo mbalimbali

      Leon Bahati

      RAIS Jakaya Kikwete amemwapisha kuwa Jaji wakili wa kujitegemea, Joaquine De-Mello ambaye alikuwa akimtetea msanii wa filamu Elizabeth Michael (Lulu) anayetuhumiwa kwa mauaji ya msanii mwenzake, Steven Kanumba.

      Wakili huyo, ambaye ni mshindi wa tuzo ya Mwanamke Jasiri Tanzania ya Martin Luther King ya mwaka 2012 na ambaye alikuwa pia alikuwa mmoja wa makamishna wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (CHRAGG) ni miongoni mwa majaji 10 walioapishwa jana na Rais Kikwete, Ikulu Jijini Dar es Salaam.
      De-Mello ni miongoni mwa mawakili wanne waliojitokeza Aprili mwaka huu kumtetea Lulu katika kesi hiyo ya mauaji inayomtuhumu kumuua usiku wa kuamkia Aprili 7, mwaka huu.

      Mawakili wengine wanaomtetea Lulu ambaye umri wake umekuwa na utata ni Kennedy Fungamtama, Peter Kibatala na Fulgence Massawe.

      Akizungumza kwenye viwanja vya Ikulu, De-Mello alisema baada ya kuteuliwa kuwa Jaji, sasa atafanya kazi hiyo na moja ya mikakati yake ni kukabiliana na changamoto za wingi wa kesi katika Mahakama Kuu ya Tanzania.

      Majaji wengine walioapishwa jana na Rais Kikwete ni Francis Mutungi, John Mgeta, Patricia Fikirini, Sam Rumanyika, Salvatory Bongole, Jerald Alex, Mathew Mwaim, Jacob Mwambegele na Latifa Mansook.
      Jaji Mkuu, Mohamed Chande Othman alisema amefurahi kuteuliwa kwa majaji hao na anawafahamu kuwa wote ni wazoefu na watatekeleza kazi zao kikamilifu.

      “Wote ni wazoefu. Ukiangalia utaona kuwa sita walikuwa wakifanya kazi mahakamani (Mahakama Kuu na Rufani), wawili mawakili wa kujitegemea na wawili pia mawakili wa Serikali,” alisema Jaji Othman.
      Alisema majaji hao wote kabla ya kupangiwa kazi rasmi itabidi waanze kufanya kazi ya kukabiliana na kesi zaidi ya 2,200 zilizopo katika Mahakama Kuu kitengo cha Ardhi.

      Uteuzi wa majaji hao 10, alisema unaifanya Mahakama Kuu sasa kuwa nao 69 tofauti na wale 16 wanaounda Mahakama ya Rufani.
      Othman alisema pamoja na uteuzi huo wanakabiliwa na changamoto nyingi zikiwemo za kulundikana kwa kesi nyingi kuliko uwezo wao.
      “Walioteuliwa watasaidia lakini ukweli ni kwamba bado tunakabiliwa na upungufu wa majaji. Kesi ni nyingi,” alisema Othman.

      Hakuweza kueleza mara moja idadi kamili ya majaji inayotakiwa ili kukidhi mahitaji lakini akasema kuwa Serikali imeliona hilo na imekuwa ikilifanyia kazi hatua kwa hatua.

      Licha ya upungufu wa majaji, Jaji Othman alisema wanakabiliwa na tatizo la kutumia teknolojia ya zamani ya kusikiliza na kuandika tofauti na maendeleo ya sasa ambayo yanahitaji kurekodi.
      “Mfumo huu wa kutumia teknolojia ya kisasa pia ungeweza kuharakisha kesi,” alisema Jaji Othman lakini akasema Kitengo cha Biashara tayari kimeanza kuifanyia kazi teknolojia ya kisasa.

      Kwa kutumia teknolojia hiyo, alisema mtu anaweza kutumia simu yake ya mkononi kujua siku ya kesi yake na hata kuperuzi kwenye mtandao kupata hukumu pamoja na mwenendo wa kesi yake.
      Alisema wanatarajia kwenda hatua kwa hatua ili kuhakikisha teknolojia hiyo ya kurahisisha kazi za mahakama inaenea idara zote za Mahakama Kuu na Mahakama ya Rufani.

      Majaji wengine wapya nao walisema kwenye mahojiano na waandishi wa habari kwamba moja ya changamoto ni kufanya kazi katika mazingira magumu na wingi wa kesi zilizolundikana katika mahakama hiyo.
      Jaji Mutungi alisema yeye anaamini kiu kubwa ya Watanzania ni kupatiwa haki na kwamba haki hiyo inapocheleweshwa pia ni tatizo jingine.

      Ili kuhakikisha anawatekelezea Watanzania haki zao, Mutungi alisema atajitahidi kufanya kazi kwa bidii na kumaliza kesi nyingi kwa haraka.

      Kwa upande wake, Jaji Mgeta alisema pamoja na wingi wa kesi kazi kubwa wanayopaswa kuifanya ni kuwa waadilifu na watenda haki.

      Alikiri kwamba Tanzania wako nyuma katika teknolojia ya kuendesha kesi lakini akasema hilo halipaswi kuwa ni jambo ambalo litawafanya warudi nyuma na kutotekeleza wajibu wao kikamilifu.

      Source: Mwananchi
      ============================== ============================== ============================== ==========

      MYTAKE: Huyu ni Wakili wa kujitegemea aliyejitolea kumsaidia LULU.
      Je, LULU anaandaliwa hukumu kama ya babu SEYA??



      MIZAMBWA
      INANIUMA SANA!!!
      SASA NIMEAMINI KUWA TANZANIA BILA CCM INAWEZEKANA!!!!, TUANDAE KABURI LA KUIZIKA MWAKA 2015

    2. Miaka 50

    3. #2
      Lokissa's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 20th November 2010
      Location : Goba
      Posts : 4,091
      Rep Power : 5807
      Likes Received
      1024
      Likes Given
      2876

      Default Re: UTEUZI: Wakili wa LULU awa Jaji

      haina uhusiano wowote.
      mbona wapo mawakili wengi tu wanakuwa majaji?
      hataweza kupewa hiyo kesi na pia haruhusiwi kijuhusisha na kesi zilizo ktk chamber yake alipotoka
      na hata hivo atapangiwa mikoani na wala sio dar, akibaki dar ni coincidence tu/
      You may know me but you have no Idea who I am !
      Reply With Quote

    4. #3
      Ulimakafu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 18th March 2011
      Location : Itabanya Balasi
      Posts : 10,922
      Rep Power : 2598
      Likes Received
      690
      Likes Given
      1614

      Default Re: UTEUZI: Wakili wa LULU awa Jaji

      Hongera zake.

    5. #4
      mkomatembo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 17th December 2011
      Location : Bweleo
      Posts : 1,019
      Rep Power : 637
      Likes Received
      228
      Likes Given
      1269

      Default Re: UTEUZI: Wakili wa LULU awa Jaji

      Quote By mizambwa
      Rais amteua wakili wa Lulu kuwa Jaji.
      June 20, 2012
      Posted in: Habari vyanzo mbalimbali

      Leon Bahati

      RAIS Jakaya Kikwete amemwapisha kuwa Jaji wakili wa kujitegemea, Joaquine De-Mello ambaye alikuwa akimtetea msanii wa filamu Elizabeth Michael (Lulu) anayetuhumiwa kwa mauaji ya msanii mwenzake, Steven Kanumba.



      Majaji wengine walioapishwa jana na Rais Kikwete ni Francis Mutungi, John Mgeta, Patricia Fikirini, Sam Rumanyika, Salvatory Bongole, Jerald Alex, Mathew Mwaim, Jacob Mwambegele na Latifa Mansook.


      Source: Mwananchi
      ============================== ============================== ============================== ==========

      MYTAKE: Huyu ni Wakili wa kujitegemea aliyejitolea kumsaidia LULU.
      Je, LULU anaandaliwa hukumu kama ya babu SEYA??



      MIZAMBWA
      INANIUMA SANA!!!
      Hapa ingekuwa majina ya mashariki mengi Edwin Mtei tungemsikia na wengine humu jamvini pia tungewasikia lakini sasa hivi shaaaari kabisa !

      Hongereni majaji na muwe waadilifu katika kazi zenu! na msubiri MOTO mkali unaowaka KWA KUDHULUMU HAKI NA NAFSI ZA WATU KABLA HAMJARUDI KWA MUUMBA WENU! NA KAMA HAMTAKI HAYA BASI UADILIFU NA HAKI YA BINADAMU WENZENU MUIWEKE KWANZA ...
      "If the Virgin Mary appears wearing a Veil on all her pictures, how can you ask me to sign on a HIJAB BAN law ?" -Roberto Maroni, Italian Minister.

    6. #5
      mkomatembo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 17th December 2011
      Location : Bweleo
      Posts : 1,019
      Rep Power : 637
      Likes Received
      228
      Likes Given
      1269

      Default Re: UTEUZI: Wakili wa LULU awa Jaji

      Quote By mizambwa

      MYTAKE: Huyu ni Wakili wa kujitegemea aliyejitolea kumsaidia LULU.
      Je, LULU anaandaliwa hukumu kama ya
      babu SEYA??


      MIZAMBWA
      INANIUMA SANA!!!
      Unashangaza sana na kupotoka kama wengine, hivi unaujua ukweli wa babu seya au unajisemea tu? Yule mzee alitenda kweli lile kosa na kama hukumbuki jaji aliewekwa kwanza alijitoa kwa kuwa alishindwa kuendesha kesi ile kwa kuwa ilikuwa inamuuma sana kuona watoto wadogo waloambukizwa ukimwi na babu seya kwanini mnapenda kuzusha uongo mara zote, imagine mtoto wako alawitiwe na kuambukizwa ukimwi je wewe utakaa ufurahi na kuona mtuhumiwa wako anaonewa? hebu peleleza kwanza yule jaji wa kwanza mwanamke aliekuwa akiskiliza kesi ya babu seya hakujitowa? babu seya alaaniwe mpaka kifo chake! kwa kutenda udhalimu ule ! tunashukuru kwa dawa za kupunguza makali ya virusi watoto angalau wataishi japo kwa shida !
      "If the Virgin Mary appears wearing a Veil on all her pictures, how can you ask me to sign on a HIJAB BAN law ?" -Roberto Maroni, Italian Minister.

    7. FemaTV & Radio

    8. #6
      Remmy's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 9th June 2009
      Location : home
      Posts : 4,342
      Rep Power : 7767
      Likes Received
      1545
      Likes Given
      1793

      Default Re: UTEUZI: Wakili wa LULU awa Jaji

      Hongera zake!

    9. #7
      MKANKULE's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 8th December 2011
      Posts : 140
      Rep Power : 704
      Likes Received
      20
      Likes Given
      19

      Default Re: UTEUZI: Wakili wa LULU awa Jaji

      CCM TUTAWAZIKA NA KUWAAGA KWA NYIMBO NYINGI ZINAZOTUMIKA MSIBANI.

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...