Hawa jamaa ni hatari, wamenijaribu mara kadhaa bila mafanikio..Huwa natumia principle yangu moja tu "I dont mess with anyone I dont know". Kuna siku jamaa alinisimamisha maeneo ya ubungo stand ya mkoa kwenye kituo cha basi kwenda mjini majira ya saa mbili kasoro usiku na kuanza mazungumzo nami
Jamaa: Samahani za leo
Mimi:Nzuri
Jamaa: Hapa naweza pata gari za masaki?
Mimi:Hapana,labda upande gari za msasani halafu ukapande gari nyingine mbele kwa mbele ,kondakta atakueleza zaidi
Tukiwa tunaendelea na mazungumzo akajitokeza mshikaji aliyeonekana kufuatilia maongezi yetu na kudakia mazungumzo nitamwita rafiki
Rafiki: ebwana vipi, anataka kwenda Masaki?
Mimi: Ndio
Rafiki: Sasa hapa unapanda gari za Msasani ukishuka unapanda bajaji,kwani unaelekea Masaki sehemu gani?
Jamaa:Barrick
Rafiki: Barrick saa mbili usiku huu? au una appointment na mtu pale?
Jamaa:Ndio,nina madini nauza kuna mtu pale naenda kuonana nae anisaidie kunielekeza wapi nitauza kirahisi
Rafiki: Ebwana angalia mjini hapa mzee,kuwa makini! Sasa hakuna shida mimi najua masoko tutakusaidia na mshikaji hapa utauza hayo madini ila na sisi itabidi ututoe.
Jamaa: Sawa haina shida,nitashukuru sana
Mimi: Sasa kwa sababu rafiki anajua mahali pa wewe kuuza madini yako atakusaidia mimi nina mambo yangu mengi nikasepa
Nikaondoka kisha nikasimama mbele kidogo kuna jamaa anauza pweza nikanza gonga kipande moja baada ya nyingine huku nawacheki kwa kuibia,walikuwa wakiniangalia kwa makini na hasira hivi,kama watu wanaotafuta namna ya kuni attack.baada ya dakika chache nilipotupa jicho sikuwaona tena..
Kuwa makini na matapeli na usisahau hawana alama usoni!!
Follow Us Here