Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Watoto wafanyiwa unyama gerezani

    Report Post
    Results 1 to 14 of 14
    1. #1
      MziziMkavu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd February 2009
      Location : European Union
      Posts : 22,181
      Rep Power : 19209
      Likes Received
      8137
      Likes Given
      26606

      Default Watoto wafanyiwa unyama gerezani

      Fidelis Butahe
      WATOTO wenye umri chini ya miaka 18 wanaotuhumiwa kwa makosa mbalimbali au waliohukumiwa huwekwa sehemu moja na watu wazima katika Gereza la Segerea, Dar es Salaam na baadhi yao kuingiliwa kinyume na maumbile na kuharibiwa vibaya.


      Tuhuma hizo nzito dhidi ya magereza zilibainika wakati Kamati ndogo ya Bunge ya Masuala ya Ukimwi, ilipokuwa ikiwasilisha kwa Kamati ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama inayoongozwa na Waziri Mkuu aliyejiuzulu, Edward Lowassa kile ilichokiona katika gereza hilo baada ya kufanya ziara.


      Kamati hiyo ilitoa taarifa yake katika kikao kilichofanyika Ofisi Ndogo za Bunge, Dar es Salaam wiki iliyopita ambacho pia kilihudhuriwa na maofisa mbalimbali wa Jeshi la Magereza akiwemo Kamishna wake Mkuu, Augustino Nanyaro.


      Habari kutoka ndani ya kikao hicho zinasema kuwa Kamati hiyo ya Ukimwi ilieleza kwamba watoto chini ya miaka 18 wanaofika katika gereza hilo kwa makosa mbalimbali, utambulisho wao huonyesha kuwa wana miaka 19 hadi 20.


      Taarifa hizo zilidai kwamba watoto hao ambao hukaa na wakubwa mchana, usiku huhamishiwa sehemu nyingine na kuingiliwa kinyume na maumbile kutokana na mazingira yalivyo ya kukosa pa kukimbilia.


      “Waligundua mengi sana, walisema kuwa watoto hao wengi wameharibika sehemu zao za siri. Kutokana na hali hiyo wanaowafanyia vitendo hivyo huwatumia pia kuingiza simu, sigara, bangi na dawa za kulevya gerezani. Wanaingiza vitu hivyo kwa kutumia sehemu zao za siri zilizoharibiwa,” kilisema chanzo cha habari kutoka kamati hiyo na kuongeza:


      “Unajua huwa wameharibika kwa hiyo sehemu zao huwa wazi na kubwa kiasi kwamba ni rahisi kuficha simu, bangi, sigara na dawa za kulevya bila kujulikana.”


      Makamu Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Rosweeter Kasikila alipoulizwa jana kuhusu tuhuma hizo alisema katika kikao hicho walipendekeza wakubwa kutengwa na watoto na kushauri upelelezi wa kesi kufanywa mapema ili kupunguza msongamano wa watuhumiwa.


      “Hali siyo nzuri yaani sehemu ya kuwekwa watu 40 wanawekwa watu 180. Jambo ambalo hatukulipenda ni jinsi watoto walivyokuwa wakiwekwa sehemu moja na watu wazima kwa sababu hujifunza mambo mengi ambayo si mazuri kwa umri wao” alisema Kasikila.


      Alisema kitendo cha watoto kukaa sehemu moja na watu wazima ndicho kinachosababisha hata kufanyiwa vitendo vichafu ikiwa ni pamoja na kuingiliwa kinyume na maumbile.“Tulieleza wazi kwamba watoto wanatakiwa kutengewa sehemu yao kwa sababu wakiwa wao wenyewe si rahisi kufanyiwa vitendo hivyo,” alisema Kasikila.


      Kwa mujibu wa chanzo chetu, katika kikao hicho maofisa wa magereza walipoulizwa kuhusu umri wa watoto hao walisema jambo hilo lipo ila hushindwa kufanya lolote kwa kuwa vielelezo vinavyoletwa huonyesha kuwa umri wao umezidi miaka 18.


      Habari zaidi zilieleza kwamba maofisa hao walisema hali hiyo inatokana na mfumo uliopo na kwamba unatakiwa kufanyiwa kazi.


      Naibu Kamishna wa Magereza, Fidelis Mboya alipoulizwa kuhusu hali hiyo, licha ya kukiri, alisema asingependa kueleza kwa undani mpaka apelekewe maswali kwa maandishi.


      “Nitumie maswali kwa maandishi ili na mimi nijibu kwa maandishi, hili jambo ni ‘very sensitive’ (nyeti sana), lete maswali nitakujibu kwa maslahi ya taifa,” alisema Mboya.


      Matukio ya utata wa umri
      Suala la umri wa watuhumiwa na hata wafungwa limekuwa gumzo katika siku za hivi karibuni baada ya mawakili wa mwigizaji wa filamu, Elizabeth Michael maarufu kama Lulu anayekabiliwa na kesi ya mauaji ya msanii mwenzake Steven Kanumba, kuwasilisha ombi lao Mahakama Kuu ikitaka iamuru kesi ya msanii huyo isikilizwe katika mahakama za watoto kwa madai kuwa mteja wao bado ni mtoto.


      Uamuzi huo ulikuja baada ya awali, kugonga mwamba katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu.
      Lakini, tayari katika Bkutano wa Bunge la Aprili 14, 2010 aliyekuwa Mbunge wa Viti Maalumu (CUF), Mgeni Jadi Kadika wakati akiuliza swali alitaka kujua Serikali haioni kuwa kuna ulazima watoto kujengewa magereza yao au kuwekwa sehemu maalumu.


      Alisema hilo linatakiwa kufanyika kwa kuwa watoto hao wanapokuwa gerezani hukutana na wafungwa wenye tabia mbalimbali kama wizi, ubakaji, ujambazi na kwamba watoto hao wanaweza kuiga tabia hizo.


      Akijibu swali hilo aliyekuwa Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani, Balozi Khamis Kagasheki alisema kwa mujibu wa Sheria zinazoratibu, kuongoza na kusimamia masuala ya mahabusu, wafungwa watoto wanapopelekwa magerezani wanapaswa kutenganishwa na wakubwa.


      Kagasheki alinukuu Kanuni za Uendeshaji wa Jeshi la Magereza (The Prisons Standing Orders) ya 2003, Kifungu Namba 502, vifungu vidogo vya (ii) na (iii), wafungwa watoto wanapopelekwa magerezani wanatenganishwa na wafungwa wakubwa.

      Watoto wafanyiwa unyama gerezani
      sweke34 likes this.
      Only Do What Your Heart Tells You




      Allah
      Has Not Revealed A Disease without Treatment....
      (Prevention is Better Than Cure) Email Address yangu hii [email protected]

    2. FemaTV & Radio

    3. #2
      LEGE's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 14th October 2011
      Location : Mwenge dar es salaam
      Posts : 1,057
      Rep Power : 595
      Likes Received
      208
      Likes Given
      145

      Default Re: Watoto wafanyiwa unyama gerezani

      Hivi yale magereza ya watoto watukutu kazi yake ni nini?

      Kama lile lililoko kule mbeya.
      MziziMkavu likes this.

    4. #3
      sweke34's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 28th September 2010
      Posts : 2,493
      Rep Power : 1255
      Likes Received
      734
      Likes Given
      1240

      Default Re: Watoto wafanyiwa unyama gerezani

      Inasikitisha sana...
      MziziMkavu likes this.

    5. #4
      MziziMkavu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd February 2009
      Location : European Union
      Posts : 22,181
      Rep Power : 19209
      Likes Received
      8137
      Likes Given
      26606

      Default Re: Watoto wafanyiwa unyama gerezani

      Quote By LEGE
      Hivi yale magereza ya watoto watukutu kazi yake ni nini?

      Kama lile lililoko kule mbeya.
      Magerza hayo ya watoto watukutu yamewkwa kaa show hayatumiki labda tuwaulize Viongozi Wahusika wapate kutujibu Serikali hatuna Viongozi wetu ni majina matupu utendaji wa kazi haupo mkuu.. LEGE

      Quote By sweke34
      Inasikitisha sana...
      Hatuna Viongozi wenye huruma na wanachi wao ndio maana Seriakali inaendeshwa hivyo hivyo ujuavyo mwenye nguvu mpishe apite mkuu.. sweke34
      LEGE likes this.
      Only Do What Your Heart Tells You




      Allah
      Has Not Revealed A Disease without Treatment....
      (Prevention is Better Than Cure) Email Address yangu hii [email protected]

    6. #5
      The Boss's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 18th August 2009
      Location : DARESALAAM
      Posts : 18,162
      Rep Power : 21615
      Likes Received
      13488
      Likes Given
      17790

      Default Re: Watoto wafanyiwa unyama gerezani

      hii nchi ndo maana ina laana
      MziziMkavu likes this.
      Watch your thoughts,They become words, Watch your words, They become deeds, Watch your deeds, They become habits, Watch your habits, They become character, Watch your character, It becomes your destiny!

    7. Miaka 50

    8. #6
      Rebel volcano's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 1st June 2012
      Posts : 404
      Rep Power : 431
      Likes Received
      84
      Likes Given
      0

      Default Re: Watoto wafanyiwa unyama gerezani

      inasikitisha sana!
      MziziMkavu likes this.

    9. #7
      August's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 18th June 2007
      Posts : 2,744
      Rep Power : 1162
      Likes Received
      251
      Likes Given
      2511

      Default Re: Watoto wafanyiwa unyama gerezani

      Quote By LEGE
      Hivi yale magereza ya watoto watukutu kazi yake ni nini?

      Kama lile lililoko kule mbeya.
      hii inaweza kuwa ni suluhisho la muda tu kwani kwenye watoto watukutu na sio watukutu kuna matatizo pia ya wale waliokubuhu na wale wasio kubuhu, sasa waliokubuhu watahamishia ubabe wao kwa hao wengine, jingine kuharibiwa kwa watoto kuna anzia na hawa watoto wa barabarani, waliotelekezwa na wazazi au na hali maisha ambapo wengi huanza kufanyiwa hivyo vitendo humo mabarabarani. sasa kutatua hili tatizo serikali inatakiwa ichukue hatu za muda mfupi na za muda mrefu, kwa mfano kwa sasa kambi nyingi za jeshi zipo tupu, kwanini serikali isiwapeleke watoto wa mitaani huko wakapata makazi na kuzalisha japo chakula chao cha kula, mabweni yapo ya kulala. hata watakapotoka huko wamekuwa na kujua kuzalisha. kuna wengine utasikia ametoroka nyumbani au amefukuzwa na ndugu asijue pa kwenda , akiishia mtaani ndio huko anajifunza tabia mbovu au anafanyiwa vitendo viovu.
      watu wengi tanzania watoto kwa vijana wanapotea njia kwa sababu hatuwapi njia mbadala au matumaini ya kwenda mbele zaidi ya wao kuhangaika wenyewe.

    10. Kbd
      #8
      Kbd's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 9th October 2009
      Posts : 942
      Rep Power : 677
      Likes Received
      294
      Likes Given
      135

      Default Re: Watoto wafanyiwa unyama gerezani

      Nimesikitika sana!!
      Hakika wema na fadhili zitanifuata siku zote za maisha yangu.....Zab 23:6

    11. #9
      TaiJike's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 14th December 2011
      Posts : 1,156
      Rep Power : 607
      Likes Received
      387
      Likes Given
      347

      Default Re: Watoto wafanyiwa unyama gerezani

      Tumelaaniwa na tunazidi kujiongezea laana.
      MziziMkavu likes this.
      * Nitashangaa kama hawa Watanzania watakataa kuasi. Kwanini wasiasi? * - Julius Kambarage Nyerere


    12. #10
      Mukalunyoisa's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 16th March 2012
      Posts : 139
      Rep Power : 389
      Likes Received
      19
      Likes Given
      2

      Default Re: Watoto wafanyiwa unyama gerezani

      Tanzania kila kitu ni hobelahobela
      MziziMkavu likes this.

    13. #11
      cicy's Avatar
      Member Array
      Join Date : 5th March 2011
      Posts : 15
      Rep Power : 419
      Likes Received
      6
      Likes Given
      42

      Default Re: Watoto wafanyiwa unyama gerezani

      mhhh mungu atuhurumie kwa kweli
      MziziMkavu likes this.

    14. #12
      mizambwa's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 8th October 2008
      Posts : 1,438
      Rep Power : 975
      Likes Received
      367
      Likes Given
      1808

      Default Re: Watoto wafanyiwa unyama gerezani

      MIZAMBWA
      INANIUMA Sana!!!
      MziziMkavu likes this.
      SASA NIMEAMINI KUWA TANZANIA BILA CCM INAWEZEKANA!!!!, TUANDAE KABURI LA KUIZIKA MWAKA 2015

    15. #13
      Comi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd October 2011
      Posts : 962
      Rep Power : 578
      Likes Received
      156
      Likes Given
      2

      Default Re: Watoto wafanyiwa unyama gerezani

      Ni kuomba mwenyezi mungu kubadili mioyo ya wana wa adam

    16. #14
      mizambwa's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 8th October 2008
      Posts : 1,438
      Rep Power : 975
      Likes Received
      367
      Likes Given
      1808

      Default Re: Watoto wafanyiwa unyama gerezani

      Quote By MziziMkavu
      Fidelis Butahe

      “Waligundua mengi sana, walisema kuwa watoto hao wengi wameharibika sehemu zao za siri. Kutokana na hali hiyo wanaowafanyia vitendo hivyo huwatumia pia kuingiza simu, sigara, bangi na dawa za kulevya gerezani. Wanaingiza vitu hivyo kwa kutumia sehemu zao za siri zilizoharibiwa,” kilisema chanzo cha habari kutoka kamati hiyo na kuongeza:


      “Unajua huwa wameharibika kwa hiyo sehemu zao huwa wazi na kubwa kiasi kwamba ni rahisi kuficha simu, bangi, sigara na dawa za kulevya bila kujulikana.Watoto wafanyiwa unyama gerezani
      Huu ni unyama wa hali ya juu sana.

      Hivi huko Gerezani hakuna watu au Askari ambao wanalinda. Sasa wanalinda nini au nao wanashiriki katika kufanikisha vitendo hivi.

      Na hao wanaofanya hivi vitendo huo majumbani kwao hawana watotot au wadogo zao wa umri huo???



      MIZAMBWA
      INANIUMA SANA!!!
      SASA NIMEAMINI KUWA TANZANIA BILA CCM INAWEZEKANA!!!!, TUANDAE KABURI LA KUIZIKA MWAKA 2015

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...