Habari wakuu,
leo nimeshuhidia tukio la kutisha na kusikitisha ambapo mtoto mwenye umri upatao miaka sita hivi amedakwa na simba wakati akiwa zoo.
inaonekana mtoto huyo alipenya kwenye fensi ndogo na kujikuta akiwa karibu kabisa na fensi kubwa yenye matundu makubwa na hatimaye kudakwa. kilichofuata hapo ni sisi kuanza kuwashambulia simba hao kwa mawe na hatimaye walimuachia mtoto huyo huku uso ukiwa umejaa damu na nyama za mapaja zikiwa zinaning'inia.
SOURCE: mimi mwenyewe, ninaishi karibu kabisa na eneo hilo.
Simba hao hapo pichani ndio waliotaka kukatisha maisha ya kiumbe huyo, sikuweza kupata picha ya tukio hilo kutokana na mshituko niliokuwa nao (lakini picha hii imepigwa mara baada ya tukio). Mama mtoto alizimia kwa muda, mtoto amechukuliwa kupelekwa hospitali.

Reply With Quote

Follow Us Here