Mtoto anusulika kuliwa na Simba bahari zoo Dar es Salaam
Habari wakuu,
leo nimeshuhidia tukio la kutisha na kusikitisha ambapo mtoto mwenye umri upatao miaka sita hivi amedakwa na simba wakati akiwa zoo.
inaonekana mtoto huyo alipenya kwenye fensi ndogo na kujikuta akiwa karibu kabisa na fensi kubwa yenye matundu makubwa na hatimaye kudakwa. kilichofuata hapo ni sisi kuanza kuwashambulia simba hao kwa mawe na hatimaye walimuachia mtoto huyo huku uso ukiwa umejaa damu na nyama za mapaja zikiwa zinaning'inia.
SOURCE: mimi mwenyewe, ninaishi karibu kabisa na eneo hilo.
Simba hao hapo pichani ndio waliotaka kukatisha maisha ya kiumbe huyo, sikuweza kupata picha ya tukio hilo kutokana na mshituko niliokuwa nao (lakini picha hii imepigwa mara baada ya tukio). Mama mtoto alizimia kwa muda, mtoto amechukuliwa kupelekwa hospitali.
Jamani! Picha ya mtoto aliyeraruliwa na simba ina raha gani kuwekwa hapa? Hata hivyo mleta thread kajieleza vya kutosha kwamba muda aliokuwa nao aliutumia kumwokoa mtoto na si kupiga picha. Hongera Lukansola kwa kumwokoa mtoto badala ya kupiga picha.
Re: mtoto anusulika kuliwa na simba bahari zoo dar es salaam
By Edson
mkuu hayo matundu yanatosha kupita mtoto
Inaweza kuwa matundu hayo hayatoshi kupita mtoto lakini simba walidhania kuwa mtoto huyo anaweza kupenya katika matundu hayo au walitaka kumla hivyo hivyo (vipande vya nyama yake vinaweza kupenya katika tundu hilo).
Re: mtoto anusulika kuliwa na simba bahari zoo dar es salaam
By HYGEIA
Jamani! Picha ya mtoto aliyeraruliwa na simba ina raha gani kuwekwa hapa? Hata hivyo mleta thread kajieleza vya kutosha kwamba muda aliokuwa nao aliutumia kumwokoa mtoto na si kupiga picha. Hongera Lukansola kwa kumwokoa mtoto badala ya kupiga picha.
Kuna mpiga picha mmoja alipiga picha ya mtoto huko Ethiopia akitaka kuliwa na tai kwa alishindwa kukimbia shauri ya njaa.
Dunia ilimlaumu sana huyo mpiga picha mpaka mpiga picha akajiua kwa stress.
Ulifanya kilichobora under the circumstances. Hongera Lukansola.
Injustice anywhere is a threat to justice everywhere.
Inaweza kuwa matundu hayo hayatoshi kupita mtoto lakini simba walidhania kuwa mtoto huyo anaweza kupenya katika matundu hayo au walitaka kumla hivyo hivyo (vipande vya nyama yake vinaweza kupenya katika tundu hilo).
thats correct great thinker, wengine ni wavivu wa kufikiri, au kila kitu wanachukulia mzaha.
King Kong hata ningefanya promo isingekuwa kwa mtindo huu, muda ambao ningetumia kupiga picha ndio niliotumia kumuokoa mtoto huyo nikiwa na watu wengine kama wawili au watatu.
Re: mtoto anusulika kuliwa na simba bahari zoo dar es salaam
hii habari ni kweli jana nimeona kwenye TV wamemuonyesha mtoto .ila kilicho niuzi ni mwenye zoo kutoa lawama kwa mzazi wa mtoto wakati wao wanajukumu la kutoa ulinzi inamana angetokea kichaa na kufungua mlango simba au chui watoke na kukimbilie mtaani lawama ni za nani.
inabidi hio zoo ingaramie gharama zote za mtoto mpaka apone na waombe radhi kwa wateja wao . mtoto amekamatwa na simba amesaidiwa na watazamaji wengine wala sio asikari wao walio pale. au mtaalamu wa wanyama pori.
pamoja na mzazi kuwa responsible na mtoto wake ila ile zoo inatakiwa kuwa responsible na wanyama wake wasiwadhuru wateja
hii habari ni kweli jana nimeona kwenye TV wamemuonyesha mtoto .ila kilicho niuzi ni mwenye zoo kutoa lawama kwa mzazi wa mtoto wakati wao wanajukumu la kutoa ulinzi inamana angetokea kichaa na kufungua mlango simba au chui watoke na kukimbilie mtaani lawama ni za nani.
inabidi hio zoo ingaramie gharama zote za mtoto mpaka apone na waombe radhi kwa wateja wao . mtoto amekamatwa na simba amesaidiwa na watazamaji wengine wala sio asikari wao walio pale. au mtaalamu wa wanyama pori.
pamoja na mzazi kuwa responsible na mtoto wake ila ile zoo inatakiwa kuwa responsible na wanyama wake wasiwadhuru wateja
pale zoo kuna msichana mmoja ambaye ndie kama mwangalizi, siku hiyo kazi yake ilikuwa ni kupiga mayowe na kukimbia ovyo kama mwehu.
Re: mtoto anusulika kuliwa na simba bahari zoo dar es salaam
niliiona hii itv kweli katoto kalikuwa na majereha usoni tumboni na miguuni kwene majapa inasikitisha
mama wa mtoto alijieleza kwamba alienda chooni na kumuacha mtoto reception baada ya kulipia matokeo yake katoto kakaanza survey alone na maza kutoka maliwatoni anakutana na simba wanajisevia mishkaki ya mwanae akazimahapohapo kuamka wote wako hosp na mtoto anaendelea fresh tuu. Ufoo saro aliripoti hii
Re: mtoto anusulika kuliwa na simba bahari zoo dar es salaam
Hili tukio limeshathibitishwa. Kwa waliokuwa wanadai picha, kweli ni maadili? Mtu analiwa na mnyama na wewe unapiga picha? Majuzi nilishuhudia ajali mbele yangu na jamaa kamwagwa ubongo wote. Nilitaka kuchukua picha nikasita
Re: mtoto anusulika kuliwa na simba bahari zoo dar es salaam
By Mfuatiliaji
hii habari ni kweli jana nimeona kwenye TV wamemuonyesha mtoto .ila kilicho niuzi ni mwenye zoo kutoa lawama kwa mzazi wa mtoto wakati wao wanajukumu la kutoa ulinzi inamana angetokea kichaa na kufungua mlango simba au chui watoke na kukimbilie mtaani lawama ni za nani.
inabidi hio zoo ingaramie gharama zote za mtoto mpaka apone na waombe radhi kwa wateja wao . mtoto amekamatwa na simba amesaidiwa na watazamaji wengine wala sio asikari wao walio pale. au mtaalamu wa wanyama pori.
pamoja na mzazi kuwa responsible na mtoto wake ila ile zoo inatakiwa kuwa responsible na wanyama wake wasiwadhuru wateja
Sawa kabisa Bro. Mwenye Zoo inabidi achukuliwe hatua (kama anashindwa kuwaangalia wanyama hao bora awaachie huru).
Follow Us Here