Zubedayo acha uongo. Huyu Mama ni jirani yangu na hajaua mtu yeyote. Ni kweli tukio la kifo lilitokea nyumbani kwake. Mimi mwenyewe binafsi nilisikitishwa sana na kifo cha kijana Onesmo, kwa kuwa yeye ni binadamu na alistahili kuishi kama wengine. Ni kweli pia kuwa huyu kijana alikuwa mfanyakazi wa huyu mama kabla ya kuacha kazi. Kama alikuwa anamdai huyu mama mshahara, wao wenyewe ndio wanaojua ukweli wa jambo hili mimi siwezi kubisha. Lakini, ukweli ni kwamba siku ya tukio kijana Onesmo alikwenda nyumbani kwa huyu mama kwa nia mbaya ndiyo maana alikuwa amebeba silaha (kisu). Alipofanikiwa kuingia ndani, alianza kumshambulia huyu mama na katika kujihami baada ya kuzidiwa, Mama wa watu alipiga kelele za mwizi. Kama mnavyojua Tanzania sheria ziko mikononi mwa Raia, hivyo walijitokeza na kumpiga kijana wa watu mpaka akafa. Ieleweke kuwa, kama huyu mama hakupata msaada wa raia basi angeuwawa yeye na huyo kijana.
Mungu ailaze Roho ya marehemu mahali pema peponi.
Follow Us Here