Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Nimehuzunishwa: Msome Mwandishi Athuman Hamis kisha Chukua Hatua Kumsaidia

    Report Post
    Page 1 of 2 12 LastLast
    Results 1 to 20 of 34
    1. #1
      mwaJ's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th September 2007
      Location : Nowhere
      Posts : 3,442
      Rep Power : 14606
      Likes Received
      2277
      Likes Given
      1497

      Default Nimehuzunishwa: Msome Mwandishi Athuman Hamis kisha Chukua Hatua Kumsaidia

      Habari ni ndefu lakini naomba msome mpaka mwisho. Si maneno yangu bali nimeileta kama ilivyo. Ninatumaini watakaoguswa watamsaidia.

      ATHUMANI HAMIS AONGELEA MUSTAKABALIWA MAISHA YAKE NA AOMBA MSAADA



      ATHUMAN HAMIS alikuwa ni mpiga picha katika vyombo vya habari tofauti na alipata ajaliya gari iliyopelekea kushindwa kufanya kufanya kazi na bado anaugua anaishi kwakulala na kukaa kwenye kiti chake maalum sababu anasumbuliwa na Uti wa mgongo(Spinal Cord).

      Mimi Athumani Hamisi Awali yayote, napenda kuwasalimia wote, wakubwa na vijana wenzangu Hii itakuwa mara yapili kuongea nanyi waandishi wenzangu, ndani ya miaka minne tokea nipate ajaliSeptemba 12, 2008 eneo la Kibiti Mkoani Pwani nikiwa na wenzangu Herry Makangeambaye kwa sasa ni marehemu na Anthony Siyame, tukiwa njiani kwenda Kilwamkoani Lindi kikazi. Mara ya kwanza niliongea nanyi 2010 baada ya kurejeakutoka Afrika kusini nilikopelekwa na Serikali kwa matibabu.

      Shukranizangu za awali, zimwendee Mhe Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Jakaya Kikwete aliyenitembelea katika Hospitali ya Muhimbili nilikolazwa na kuagizanilipelekwe nje kwa matibabu zaidi. Katika ajali ile, nilivunjika shingo naku-damage spinal cord iliyopelekea kupooza mwili wote kuanzia shingoni. Katikaoperesheni iliyofanywa na madaktari wa hospitali ya Mil Park, Afrika Kusiniwalilazimika kuunganisha shingo kwa nyuma. Shukraniza pili ni kwa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, kampuni ninayofanyia kazi yamagazeti ya serikali, wachapishaji wa Daily News, Sunday news, Habari LeoJumapili na Spoti leo, familia yangu iliyokuwa katika wakati mgumu wakati huohadi sasa watanzania wote wuamini wa dini zote waliokuwa wakiombea Pamoja namarafiki zangu waliokuwa wakihangaika huku na kule kwa namna moja ama nyingine.

      Niko mbeleyenu leo kuwaomba mnifikishie ujumbe kwa jamii kwa maelezo yafuatayo:- Ofisiyangu ya TSN ilinipangia nyumba ninayokaa Sinza Vatican, Wilaya ya Kinondonijijini Dar es salaam Mei 2010-2011 na mkataba ulikukwa kati ya mwenye nyumba naTSN ambao mimi sikuwahi kuuona hadi ninavyoongea na nyie leo. Mkataba uliishatena Mei 2011, mwenye nyumba alikwenda TSN kuomba kusaini mkataba mpya. Badalayake aliandikiwa mkataba mpya wenye jina langu na kupewa aniletee mimi nisaini.Nilipomuuliza mkataba wa kwanza uliingia na nani na ni nani alisaini. Alisemani TSN walisaini wakamwambia wana mgonjwa ambaye ni Staff wake atakuja kuishipale akitokea Afrika Kusini alikokwenda kwa matibabu.

      Mwenye nyumba akasema walimwambia gharama za nyumba ni za TSN, sasa nashangaa leo wameandika jinalako na mkataba ni kati yangu na wewe. Nikamwambia kaka, mimi sikutarajia kufikia hapa kwani mwaka 1999 ilipangwa mimi nifikie katika nyumba ya kampuni Upanga kuepusha gharama na ukaribu wa huduma za kitabibu, mpaka masuala yanguyatakapothibitishwa na Daktrari kama hali yangu itaruhusu mimi kuwezakufanyakazi ama vinginevyo. Rudi ofisini mkasaini kama mlivyofanya awali. Naumwambie kwa hali ya Athumani hawezi kusaini mkataba na mimi kulingana na haliyake. Isitoshe mi nilitiliana saini mkataba wa awali na TSN.
      Ukweli nilikataa kusaini zaidi ya mara tatu, mpaka Meneja Mwajiri siyo huyo wa sasa alipoingilia kati na kunithibitishia kuwa kampuni italipa nyumba mpaka uamuziwa madaktari utakapotoka, saini mimi nitakulinda.

      Niliporejea nyumbani nikawe kwa wino katika dole gumba wakaweka saini. Mpaka yalipojitokeza ya sasa.Ndugu waandishi wa habari, hali yangu japo imeimarika zaidi kuliko awali, leonimekuja na jambo ambalo litahusisha jamii na nyie ndiye wahusika Wakuu katikasuala hili.


      KIKUBWA ZAIDI LEO NI SHUKRANI NAOMBI
      Ukweli ulio wazi, nashukuru kwa Mungu na kujivunia kuwa TSN. Nimelelewa na TSN kwa miaka sita sasa. Imenilea nikiwa mgonjwa kwa miaka mine, nikiwa bado niko ndaniya ajira jambo ambalo ni gumu sana sehemu nyingine. Imelipa nyumba kwa miaka miwili na imesitisha kulipa kodi ya 2012-2013 kwa barua ya Februari 3, 2012 nakutoa maelezo kwenye barua kuwa imefikia hatua hiyo kutokana na kuwapawafanyakazi wake asilimia 15 ya mishahara yao kulipa nyumba. Nyumba walionipangia ni ya vyumba viwili na kodi iliyolipwa kwenye mkataba wa mwaka jana ni Milioni 4.8 Nilipatwa na mshutuko kidogo, nafsi ikanishauri niite menejiment nyumbani tushauriane katika hili.

      Walikuja Machi 28, na wakanipa pole ya kampuni tokea nirudi 2010 Shs 50,000. Lakini mazungumzo hayakuisha kutokana na muda na kuahidi kurudi wiki inayofuata kwa mazungumzo zaidi. Nimepewa notisi na mwenye nyumba April 23, 2010.
      Nadhani kutokana na kubanwa na kazi, hawakupata nafasi ya kurudi tena kumalizia mazungumzo. Kwa mtazamo wa kifikira ni wazi msimamo ulibaki palepale. Barua yakusitisha kulipa kodi haikuja kwangu tu bali pia mwenye nyumba alipata.

      UFAFANUZIKabla ya kuruhusiwa kurejea nyumbani Tanzania, Netcare Rehabilitation Hospital,wanautaratibu mzuri sana. Kabla ya kuwa – discharged wanakuruhusu ukae nje ya hospital kwa miezi mitatu, kama una mke au mume na kama huna utatafutiwa nurse awe wa kike ama wa kiume mimi nilipata nurse. Baada ya hapo una hudhuria mazoezi na vipimo kadhaa kwa miezi mitatu. Ukifaulu kumaliza miezi mitatu wewe na mwangalizi wako hasa wewe mgonjwa bila kupata matatizo, hapo wanaku-discharge.

      Nilipiga simu kwa Katibu Kiongozi Ikulu wakati huo, Philemon Luhanjo na kwaKatibu Mkuu wa Wizara ya Afya na Ustawi wa jamii anahitajika nurse kuja kukaanami nje ya hospital kwa miezi mitatu, je mtanisaidiaje? Kwa kweli jibu laolilikuwa moja tu hatutatuma nurse kutoka huku, tafuta huko huko, fedha zakumlipa, nyumba ya kulala, chakula na usafiri, andika budget itume harakatutalipa na wasiliana na ubalozi waje kujua unakaa wapi na fedha zitatumwaubalozini watakuwa wanakuletea. Nilipata nurse na miezi mitatu ilipokaribiakwisha nilifanya mawasiliano kujua kama kutatumwa mtu wa kunifuata, wakanijibu njoo naye huyo huyo watanzania waliofanikiwa kuangalia vyombo vya habari wengiwalimuona kwani nilirudi Mei 28, 2010.

      Baada ya mwezi alimaliza mkataba namekutakiwa kutafuta nurse wa kukaa naye kwa saa 24. Akapatikana na akafundishwana M-South Africa jinsi ya kukaa na mgonjwa wa Spinal Cord.
      TSN,wakamlipa nurse wa South Africa Rand 12,500 alizokuwa anadai na palepale nikauliza vipi kuhusu malipo ya nurse mpya ambaye ataachwa na mimi? Kwa sababuserikali imemaliza jukumu lake na waliniambia kwa kuwa wewe bado ni mwajiriwawa TSN, jukumu lote sasa utakuwa chini yao na ndiyo mmepewa pia jukumu lakumlipa kama mlivyofanya leo. TSN walinijibu palepale kuwa suala la kumlipa nurse ni lako na familia yako ila nyumba tutalipa.

      Vodacom walijitokeza kubeba gharama za tiketi nilipopata ajali kwenda Afrika Kusini nawasindikiaji wote, tiketi ya nurse niliyekuja naye. Pia wakalipa tiketi yangu na nurse Desemba 8, 2010 kwenda na kurudi Afrika Kusini kwa ajili ya check up.Baada ya TSN kulipa nurse yule msouth afrika, nikawapigia Vodacom Foundation kuwa nurse amemaliza mkataba na ameshalipwa fedha naomba mumkatie tiketi. Hivyo ilikuwa Juni 25 na kesho yake Juni 26 2010 jioni wakaja watu wawili kutoka Vodacom Foundation na mmoja kutoka TSN waliniambia wamekuja na vitu vitatu. Wakamshukuru nurse kwa kazi nzuri, lakini wakamwambia, sisi ni kutoka Vodacom. Vodacom Foundation inakuomba uendelee kumhudumia Athumani. Na Vodacom watakulipa mshahara lakina tunaomba upunguze kiwango.

      Yule nurse akakubali akapunguza nusu ya mshahara aliokuwa akilipwa na serikali.Wakamwambia sasa Vodacom Foundation inakata tiketi ya kwenda nyumbani Afrikakusini kuaga. Akaomba siku 15, mkataba wa mdomo ukakubaliwa na yule nurse namshahara wa kwanza ukawa Julai 2010 kuendelea na kazi chini ya Vodacom. Julai 2010 wakamlipa. Kilichoendela naomba nisiseme.

      Muda wacheckup ulifika Desemba 2010, nikaitaarifu Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii.Wakakubali wakaandika barua kwa kugawa majukumu. Afya wakasema watalipa gharamaza matibabu, Vodacom tiketi za kwenda na kurudi na TSN waliagizwa kulipa allowance kwa mgonjwa na nurse. Tukasafiri Desemba 8,2010 na tukarudi Februari28,2011. Malipo yaliyofanywa na TSN kidogo ni aibu naomba nisiseme. Hali hiyo ilinionyesha kuwa Vodacom Foundation walikuwa wanatambua uwepo wa yule nurse. Lakini hadi nurse anaondoka alilipwa mshahara mmoja tu na hata tiketi ya nurse kurudi Afrika Kusini Vodacom hawakulipa.

      Nililipa tiketi ya Business Class.Nikampa Rand 4,500 akakataa akachukua Rand 2,500 tu, akaniambia, Athumani nakuacha katika hali mbaya sana. Fuatilia haki zangu na zako, ukifanikiwa utaniambia na Account ya benki, First bank nakuachia utaniwekea.
      Vodacom Foundation hawajawahi kupokea simu yangu na Mkurugenzi wake hajawahi kupokea simu yangu wala kuongea na mimi tokea nipate ajali.

      Suala lingine waliniuliza nichague kitu kimoja, kujengewa nyumba au kusomeshewa watoto. Mimi nilichaguakujengewa nyumba. Walichukua chaguo langu. Tukamaliza mazungumzo. Baada yamwezi waliniambia suala lako limekubaliwa ila tumepata Mkurugenzi mpya, lakini usijali. Mpaka hapa ninavyoongea danadana ziliendelea mpaka ninavyoendelea kwenye nyumba, sijawahi tena kupata jibu kutoka Vodacom.
      La mwisho nilijibiwa na mmoja wa watu wa Vodacom Foundation aliniambia wewe uliingia mkataba na kampuni ya One Plass na si Vodacom Foundation.

      SIKU YA LEO Nimekujaleo kuutangazia umma hali ilivyo. Ukweli kwa sasa Account ya CRDB ilikuwamaalumu kwa ajili ya kusomeshea watoto, imekauka ya Postal bank ambayo yamshahara haina kitu. Pesa ya mshahara inayoingia benki ni 450,000 Nawalipanurse, msaidizi wake na mfanyakazi 370,000.
      Maisha yaulemavu ni ghali sikutarajia. Nina wanangu watatu, wa kwanza anamaliza darasala saba mwaka huu, wa pili yuko la nne na wa mwisho yuko la pili. Hawa wanasomaprimary za kulipia wote hawa nawalipia 200,000 kila mmoja kwa term jumla400,000 hizo shule zina term nne kwa mwaka. Gharama chakula, vifaa vyawanafunzi, gharama zao ndogondogo na za kifamilia Pamoja na chakula kwa mwezi,inakwenda kati ya 750,000 mpaka 900,000 kwa mwezi.

      Nimekuwa ombaomba mpaka watu kadhaa siwalaumu, wamechoka hawapokei simu wala kujibu sms.siyo siri ndugu wote wamekimbia waliobaki ni marafiki wa kweli wameniingiza katika familia zao. Hali yangu ni mbaya sana kiuchumi. Sina uwezo wa kulipa nyumba kwa gharama zozote zile. Mimi Athumani Hamisi, naomba watanzania watakaoguswa wanisaidie. Kubwa nyumba na ushauri wa madaktari walinishauri nisiishi mbali na mazingira ya hospitali kulingana na hali yangu. Makampuni, mashirika, wizara yoyote, shirikala nyumba la Taifa NHC, watu binafsi, serikali na Taasisi yoyote watakaoguswa na kilio changu nawaomba wanisaidie kwa njia yoyote. kwa waliotayari naomba misaada ipitie katika account No 01J2027048800 ya CRDB na Account No 010-00090488 ya Postal Bank Kwa wanaotumia mitandao ya simu, wanaweza kutumia M-pesa 0757 825 737, Tigopesa 0655 531 188 na Airtel Money 0784 531118; M-Pesa 0767 298 888 ya Chris Mahundi na Airtel Money 0686 710 977 ya Ephraim Mafuru.

      Habari kwahisani ya http://www.8020fashions.blogspot.com/
      Last edited by mwaJ; 6th June 2012 at 13:20.
      Azimio Jipya likes this.
      “Anyone who has never made a mistake has never tried anything new” -
      Albert Einstein

    2. Miaka 50

    3. #2
      Tangawizi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 25th June 2009
      Posts : 943
      Rep Power : 692
      Likes Received
      188
      Likes Given
      184

      Default Re: Nimehuzunishwa: Msome Mwandishi Athuman Hamis kisha Chukua Hatua Kumsaidia

      Pole sana Athumani. Hivi nini kilitokea mpaka baadhi ya watu wa jf kutiwa kwenye msukosuko?

    4. #3
      Wingu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 14th January 2011
      Posts : 3,966
      Rep Power : 1216
      Likes Received
      247
      Likes Given
      41

      Default Re: Nimehuzunishwa: Msome Mwandishi Athuman Hamis kisha Chukua Hatua Kumsaidia

      Pole sana Athumani ndo maana watu wanaamua kuwa mafisadi kwa sababu kama hizo.Asiye kuwepo na lake halipo ndo wanachokifanya hao watu manake wamekusahau kabisa ina uuma kwa kweli

    5. #4
      Mvaa Tai's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th August 2009
      Location : Ngudu, Mwanza
      Posts : 3,394
      Rep Power : 1175
      Likes Received
      1388
      Likes Given
      905

      Default Re: Nimehuzunishwa: Msome Mwandishi Athuman Hamis kisha Chukua Hatua Kumsaidia

      Nimeharibu siku yangu, any way I'll do what is possible
      Mnang'oa meno ya Tembo ili mukayauze, mnang'oa meno na Kucha za Watanzania wasio na hatia ili iweje?

    6. #5
      mwaJ's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th September 2007
      Location : Nowhere
      Posts : 3,442
      Rep Power : 14606
      Likes Received
      2277
      Likes Given
      1497

      Default Re: Nimehuzunishwa: Msome Mwandishi Athuman Hamis kisha Chukua Hatua Kumsaidia

      Quote By Ezan
      Nimeharibu siku yangu, any way I'll do what is possible
      Pole Ezan hicho ndicho kilichonipata mie lakini nikaona nisiishie kuhuzunika tu nikaamua kuileta huku nanyi muisome na kusaidia panapowezekana.
      Azimio Jipya likes this.
      “Anyone who has never made a mistake has never tried anything new” -
      Albert Einstein

    7. FemaTV & Radio

    8. #6
      Mwitongo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 30th January 2009
      Posts : 295
      Rep Power : 584
      Likes Received
      210
      Likes Given
      5

      Default Re: Nimehuzunishwa: Msome Mwandishi Athuman Hamis kisha Chukua Hatua Kumsaidia

      Jambo moja najifunza hapa. Kama kuna mambo muhimu katika maisha, nadhani ni kujiandaa mapema kabisa kimaisha. Matatizo yanayompata Athuman sote tunapaswa kuyatambua na kuajiandaa. Kama kijana una uwezo, jenga nyumba sasa. Usisubiri kesho. Kama athumani angekuwa kajenga, hakika leo angekuwa anahangaikia suala la ada, chakula na matibabu. Hapa kinachotatiza zaidi ni namna ya kulipia kodi ya pango. Vijana amkeni sasa!! Angalizo: Msijiandalie maisha kwa kuwa mafisadi. Tafuteni maisha kwa haki.

    9. #7
      mwaJ's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th September 2007
      Location : Nowhere
      Posts : 3,442
      Rep Power : 14606
      Likes Received
      2277
      Likes Given
      1497

      Default Re: Nimehuzunishwa: Msome Mwandishi Athuman Hamis kisha Chukua Hatua Kumsaidia

      Quote By Mwitongo
      Jambo moja najifunza hapa. Kama kuna mambo muhimu katika maisha, nadhani ni kujiandaa mapema kabisa kimaisha. Matatizo yanayompata Athuman sote tunapaswa kuyatambua na kuajiandaa. Kama kijana una uwezo, jenga nyumba sasa. Usisubiri kesho. Kama athumani angekuwa kajenga, hakika leo angekuwa anahangaikia suala la ada, chakula na matibabu. Hapa kinachotatiza zaidi ni namna ya kulipia kodi ya pango. Vijana amkeni sasa!! Angalizo: Msijiandalie maisha kwa kuwa mafisadi. Tafuteni maisha kwa haki.
      Mwitongo ushauri wako ni mzuri lakini ni muhimu kufahamu kuwa ajali inaweza kumpata mtu wakati wowote. Athuman alipata ajali kabla hajajenga na wala hilo si kosa lake maana kujenga mtu anajenga akiwa na uwezo wa kufanya hivyo. Tuyaache hayo, je Athuman anasaidiwaje? Hilo ndio suala la msingi kwa sasa. Jaribu kujiweka katika viatu vyake.
      Jasusi and BabaDesi like this.
      “Anyone who has never made a mistake has never tried anything new” -
      Albert Einstein

    10. #8
      NATA's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 10th May 2007
      Posts : 4,255
      Rep Power : 8416
      Likes Received
      1133
      Likes Given
      390

      Default Re: Nimehuzunishwa: Msome Mwandishi Athuman Hamis kisha Chukua Hatua Kumsaidia

      Quote By Tangawizi
      Pole sana Athumani. Hivi nini kilitokea mpaka baadhi ya watu wa jf kutiwa kwenye msukosuko?
      Juu ya ajari au?

    11. #9
      Mwitongo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 30th January 2009
      Posts : 295
      Rep Power : 584
      Likes Received
      210
      Likes Given
      5

      Default Re: Nimehuzunishwa: Msome Mwandishi Athuman Hamis kisha Chukua Hatua Kumsaidia

      Quote By mwaJ
      Mwitongo ushauri wako ni mzuri lakini ni muhimu kufahamu kuwa ajali inaweza kumpata mtu wakati wowote. Athuman alipata ajali kabla hajajenga na wala hilo si kosa lake maana kujenga mtu anajenga akiwa na uwezo wa kufanya hivyo. Tuyaache hayo, je Athuman anasaidiwaje? Hilo ndio suala la msingi kwa sasa. Jaribu kujiweka katika viatu vyake.
      Ni kweli, ajali ni ajali, lakini ndugu zangu kuna mipango katika maisha. Bahati mbaya wengi wetu tunadhani kwamba maisha ni kesho, na si leo. Kifo kipo, ajali ipo. Ukilitambua hilo, huwezi kubaki hivi hivi bila kufanya maandalizi. Angalia Kanumba, alikuwa na fedha na jina nene sana, lakini pengine alidhani kuwa angeishi miaka 70. Mungu hakutaka iwe hivyo. Muhimu hapa ni kuanza kujenga palepale unapokutana na fedha. usisubiri kuwa na milioni 200, la hasha! Anza na hizo hizo za kudunduliza. Maisha ni sasa (hapo ulipo sasa), na si kesho!

    12. #10
      asrams's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 4th September 2011
      Posts : 600
      Rep Power : 510
      Likes Received
      106
      Likes Given
      64

      Default

      Quote By Mwitongo
      Ni kweli, ajali ni ajali, lakini ndugu zangu kuna mipango katika maisha. Bahati mbaya wengi wetu tunadhani kwamba maisha ni kesho, na si leo. Kifo kipo, ajali ipo. Ukilitambua hilo, huwezi kubaki hivi hivi bila kufanya maandalizi. Angalia Kanumba, alikuwa na fedha na jina nene sana, lakini pengine alidhani kuwa angeishi miaka 70. Mungu hakutaka iwe hivyo. Muhimu hapa ni kuanza kujenga palepale unapokutana na fedha. usisubiri kuwa na milioni 200, la hasha! Anza na hizo hizo za kudunduliza. Maisha ni sasa (hapo ulipo sasa), na si kesho!
      Ni kweli unayosema kaka lakini kumbuka ajali haina kinga na kujenga ni majaaliwa pia.


      Sent from my NOKIA 3310 using Tapatalk HD
      BabaDesi likes this.

    13. #11
      Azimio Jipya's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th November 2007
      Location : Universal Space Station
      Posts : 3,281
      Rep Power : 5414
      Likes Received
      1006
      Likes Given
      1731

      Default Re: Nimehuzunishwa: Msome Mwandishi Athuman Hamis kisha Chukua Hatua Kumsaidia

      mwaJ honestly nimehuzunishwa pia!

      Seems like complicated issue ... ! I will do something!

      Mtu yeyote anaweza kujikuta kwneye situation close realated na hizo and the rest ...!
      Roulette likes this.
      Never Get Angry; Never Make Threat; Reason With People;
      "Napenda the logic of the words because in some ways it says about individual-not to use emotions-when scrutinizing something, whether it involves you or not" ...-by AshaDiii @ Jamiiforums 26th July 2011.


    14. #12
      Moony's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 16th April 2011
      Location : Oshakati, Namibia
      Posts : 1,104
      Rep Power : 630
      Likes Received
      260
      Likes Given
      279

      Default Re: Nimehuzunishwa: Msome Mwandishi Athuman Hamis kisha Chukua Hatua Kumsaidia

      Quote By Mwitongo
      Jambo moja najifunza hapa. Kama kuna mambo muhimu katika maisha, nadhani ni kujiandaa mapema kabisa kimaisha. Matatizo yanayompata Athuman sote tunapaswa kuyatambua na kuajiandaa. Kama kijana una uwezo, jenga nyumba sasa. Usisubiri kesho. Kama athumani angekuwa kajenga, hakika leo angekuwa anahangaikia suala la ada, chakula na matibabu. Hapa kinachotatiza zaidi ni namna ya kulipia kodi ya pango. Vijana amkeni sasa!! Angalizo: Msijiandalie maisha kwa kuwa mafisadi. Tafuteni maisha kwa haki.
      Kama si fisadi, ajenge kwa mshahara upi?

    15. #13
      KALYOVATIPI's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th August 2011
      Posts : 1,184
      Rep Power : 590
      Likes Received
      136
      Likes Given
      0

      Default

      Quote By Moony
      Kama si fisadi, ajenge kwa mshahara upi?
      450000 mshahara ada ya watoto laki 2 bado ajala labda ajenge banda la kuku

    16. #14
      Zamaulid's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 25th May 2009
      Location : PANDAGI CHIZA
      Posts : 3,641
      Rep Power : 1296
      Likes Received
      942
      Likes Given
      401

      Default Re: Nimehuzunishwa: Msome Mwandishi Athuman Hamis kisha Chukua Hatua Kumsaidia

      Quote By KALYOVATIPI
      450000 mshahara ada ya watoto laki 2 bado ajala labda ajenge banda la kuku
      mmmh!ngoja niishie kuguna tu!!maana naona unanikatisha tamaa!

    17. #15
      Lambardi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 7th February 2008
      Location : KITAANI ZAIDI
      Posts : 4,512
      Rep Power : 1794
      Likes Received
      654
      Likes Given
      0

      Default Re: Nimehuzunishwa: Msome Mwandishi Athuman Hamis kisha Chukua Hatua Kumsaidia

      Pole sana mpiganaji,nina hakika TSN wamesikia na watajadili kupata muafaka wa kukusaidia zaidi ama la wakuite mshauriane nini hatma yako!!
      Na sheria inasemaje!

    18. #16
      Azimio Jipya's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th November 2007
      Location : Universal Space Station
      Posts : 3,281
      Rep Power : 5414
      Likes Received
      1006
      Likes Given
      1731

      Default Re: Nimehuzunishwa: Msome Mwandishi Athuman Hamis kisha Chukua Hatua Kumsaidia

      Quote By Skills4Ever
      Pole sana mpiganaji,nina hakika TSN wamesikia na watajadili kupata muafaka wa kukusaidia zaidi ama la wakuite mshauriane nini hatma yako!! Na sheria inasemaje!
      Pia nimewaza kuhusu swla la sheria!Pili! Hivi in real sense mtu kama huyo anasaidiwaje ili ilete maana? kumchangia kila siku kwa kumrushia kwenye simu? AU ipi ni njia concrete ya kumsaaidia kwa hali ilivyo sasa?
      Never Get Angry; Never Make Threat; Reason With People;
      "Napenda the logic of the words because in some ways it says about individual-not to use emotions-when scrutinizing something, whether it involves you or not" ...-by AshaDiii @ Jamiiforums 26th July 2011.


    19. #17
      mwaJ's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th September 2007
      Location : Nowhere
      Posts : 3,442
      Rep Power : 14606
      Likes Received
      2277
      Likes Given
      1497

      Default Re: Nimehuzunishwa: Msome Mwandishi Athuman Hamis kisha Chukua Hatua Kumsaidia

      Quote By Azimio Jipya
      Pia nimewaza kuhusu swla la sheria!Pili! Hivi in real sense mtu kama huyo anasaidiwaje ili ilete maana? kumchangia kila siku kwa kumrushia kwenye simu? AU ipi ni njia concrete ya kumsaaidia kwa hali ilivyo sasa?
      Azimio Jipya ukiliangalia hili suala kisheria utajiuliza maswali mengi sana kuanzia kwenye malipo ya bima - ajali iliyosababisha kupoteza uwezo wa kufanya kazi, suala la kuumia kazini, je? bado yupo kwenye ajira ya TSN? Kama jibu ni ndio je, mwajiri wake anajukumu gani katika kumhudumia mfanyakazi wa aina yake in terms of accommodation (kumbuka amezungumzia nyumba za staff) n.k.

      Njia za kumsaidia zaweza kuwa pamoja na hiyo aliyoomba mwenyewe yaani kumchangia pesa. Lakini hii kwa maoni yangu haitakuwa endelevu maana watu hawataweza kuchangia kila mara anapopungukiwa na ndio maana amesema baadhi ya watu aliowategemea wamechoka na hawapokei hata simu zake.

      Lengo la kuileta hii habari JF ni kupata michango ya wana JF ya hali, mali na mawazo pia namna huyu ndugu atakavyoweza kutoka katika hali aliyomo. Watu wanaweza kuchangia pesa na hizo pesa badala ya kuzitumia zote ashauriwe namna ya kuzifanyia mradi ambapo pia atashauriwa namna ya kupata wasimamizi wa huo mradi maana yeye katika hali yake hataweza kusimamia na mawazo mengine ya kumsaidia ili mradi aondokane na huu utegemezi mkubwa aliyotumbukia baada ya ajali.

      Najaribu tu kufikiria wako wapi wadada na akina kaka wa JF akina Bishanga Saint Ivuga Bujibuji Mtambuzi Pasco Senetor Mwali Preta sweetlady Kipipi kisukari Smile Michelle charminglady BADILI TABIA na wengineo waje wasaidie mawazo yao katika hili.
      Last edited by mwaJ; 7th June 2012 at 23:41.
      “Anyone who has never made a mistake has never tried anything new” -
      Albert Einstein

    20. #18
      Bujibuji's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 4th February 2009
      Location : NYUMBANI PANONO
      Posts : 13,800
      Rep Power : 11185
      Likes Received
      6989
      Likes Given
      5168

      Default Re: Nimehuzunishwa: Msome Mwandishi Athuman Hamis kisha Chukua Hatua Kumsaidia

      Huyu amekuwa ni mpiga picha wa muda mrefu wa magazeti ya chama na serikali.
      Iweje leo wale waliokuwa wana pozi mbele ya kamera yake wamemtupa?
      Ndani ya CCM hakuna urafiki ila kuna unafiki.
      Wito kwa Wazalendo wenzangu wote, tusiangalie nyuma, kama tulivyo fanya kwa Sajuki, tufanye leo tena, Tumchangie huyu mwenzetu
      Quote By mwaJ
      <BR><BR>@Azimio Jipya ukiliangalia hili suala kisheria kutajiuliza maswali mengi sana kuanzia kwenye malipo ya bima - ajali iliyosababisha kupoteza uwezo wa kufanya kazi, suala la kuumia kazini, je? bado yupo kwenye ajira ya TSN? Kama jibu ni ndio je, mwajiri wake anajukumu gani katika kumhudumia mfanyakazi wa aina yake in terms of accommodation (kumbuka amezungumzia&nbsp;nyumba za staff) n.k.&nbsp;<BR><BR>Njia za kumsaidia&nbsp;zaweza kuwa&nbsp;pamoja na hiyo aliyoomba mwenyewe yaani kumchangia pesa.&nbsp;Lakini hii&nbsp;kwa maoni yangu haitakuwa endelevu maana watu hawataweza kuchangia kila mara anapopungukiwa na ndio&nbsp;maana amesema&nbsp;baadhi ya watu aliowategemea wamechoka na hawapokei hata simu zake. <BR><BR>Lengo la kuileta hii habari&nbsp;JF ni kupata michango ya wana JF ya hali, mali&nbsp;na&nbsp;mawazo pia namna huyu ndugu atakavyoweza kutoka katika hali aliyomo. Watu wanaweza kuchangia pesa na hizo pesa badala ya kuzitumia zote&nbsp;ashauriwe namna ya kuzifanyia mradi&nbsp;ambapo pia atashauriwa namna ya kupata wasimamizi wa huo mradi maana yeye katika hali yake hataweza kusimamia na mawazo mengine ya kumsaidia ili mradi aondokane na huu utegemezi mkubwa aliyotumbukia baada ya ajali.<BR><BR>Najaribu tu kufikiria wako wapi wadada na&nbsp;akina kaka&nbsp;wa JF&nbsp;akina Bishanga Saint Ivuga Bujibuji @Yo&nbsp;Yo Mtambuzi Pasco Senetor p Mwali Preta sweetlady Kipipi kisukari Smile&nbsp;@Ashadii Michelle charminglady BADILI TABIA na wengineo waje&nbsp;wasaidie mawazo yao katika hili.<BR>&nbsp;<BR><BR>
      mwaJ likes this.
      KAZI NDIO MSINGI WA MAENDELEO. NCHI MASIKINI HAIWEZI KUENDELEA KWA MSINGI WA FEDHA. NCHI MASIKINI HAIWEZI KUJITAWALA KAMA INATEGEMEA MSAADA KUTOKA NCHI ZA NJE- J. K. NYERERE

    21. #19
      Mwali's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 9th November 2011
      Location : Ushongo Mabaoni
      Posts : 5,764
      Rep Power : 26860
      Likes Received
      4283
      Likes Given
      4588

      Default Re: Nimehuzunishwa: Msome Mwandishi Athuman Hamis kisha Chukua Hatua Kumsaidia

      Quote By mwaJ
      Najaribu tu kufikiria wako wapi wadada na akina kaka wa JF akina Bishanga Saint Ivuga Bujibuji Mtambuzi Pasco Senetor Mwali Preta sweetlady Kipipi kisukari Smile Michelle charminglady BADILI TABIA na wengineo waje wasaidie mawazo yao katika hili.
      Sorry mpenzi, mi nipo ila naona mada imekaa ndefu sana
      Mi sipendi kusoma, hua nasinzia katikati, kabla sijamaliza
      Tafadhali nipe summary kwanza, kwa kifupi what is the issue?
      sweetlady likes this.
      Great spirits have always encountered violent opposition from mediocre minds
      Albert Einstein


    22. #20
      Mtambuzi's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 29th October 2008
      Location : Dar Es Salaam
      Posts : 6,089
      Rep Power : 27012
      Likes Received
      8208
      Likes Given
      17307

      Default Re: Nimehuzunishwa: Msome Mwandishi Athuman Hamis kisha Chukua Hatua Kumsaidia

      Quote By mwaJ
      Najaribu tu kufikiria wako wapi wadada na akina kaka wa JF akina Bishanga Saint Ivuga Bujibuji Mtambuzi Pasco Senetor Mwali Preta sweetlady Kipipi kisukari Smile Michelle charminglady BADILI TABIA na wengineo waje wasaidie mawazo yao katika hili.
      Ndio nimeiona hii habari, naninakumbuka kwa usahihi kabisa juu ya ajali hiyo iliyompata mwenzetu.
      Mimi sipendi unafiki, ninachoweza kumshauri ndugu yangu huyu ni kujaribu kupunguza bajeti yake......... ingawa wazo hili limechelewa, lakini hata hivyo anaweza kuangalia bajeti yake na kuipunguza.
      Kitu cha kwanza ilitakiwa atafute nyumba za bei rahisi kidogo, Kukaa sinza kuna gharama kubwa sana, kwa mfano angeweza kuhamia Mwananyamala karibu na hospitali kwani pale anaweza kupata nyumba nzuri kwa bei nafuu kidogo, pili gharama za shule za watoto nazo zinamkamua sana, najua alikuwa na lengo la kuwasomesha wanae shule nzuri za English Medium, lakini kwa hali yake kwa sasa inabidi ageukie shule za akina Kayumba...... (najua utakuwa ni uamuzi mgumu),
      tatu, ajishughulishe na shughuli za kiuchumi, kuna namna nyingi za kujiongezea kipato, kwa mfano kwa kuwa taaluma yake ni mpiga pisha wa magazeti, basi angejifunza uandishi wa makala hata kwa njia ya mtandao na angekuwa anafanya kazi akiwa nyumbani....
      kingine labda angetafuta ujuzi wowote wa kazi za mikono, sidhani kama angetangaza kupitia vyombo vya habari kwamba anatafuta mwalimu wa kumfundisha kazi za mikono angekosa.... Naamini angepata na hata gharama za kumlipa wangejitokeza wafadhili....... Kutegemea wafadhili kwa misaada ya kila siku huku ukiwa na maisha ghali ni shida kidogo.....
      Naamini kamaatafuata ushauri wangu anaweza kuvuka mtihani huu mgumu.....
      Nakumbuka wakati fualni niliwahi kuandika makala kuhusu tajiri mmoja wa kule Colorado nchini Marekani, yeye alimudu kusimama na kuwa tajiri mkubwa nchini humo pamoja na misukosuko ajali alizowahi kupana na kuwa mlemavu kama alivyo Athumani.

      Ukitaka kusoma habari hiyo unaweza kubofya hapa:

      http://www.jamiiforums.com/jf-chit-c...ya-maisha.html
      RR, BabaDesi and mwaJ like this.

    23. Study Abroad
    Page 1 of 2 12 LastLast

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...