Habari ni ndefu lakini naomba msome mpaka mwisho. Si maneno yangu bali nimeileta kama ilivyo. Ninatumaini watakaoguswa watamsaidia.
ATHUMANI HAMIS AONGELEA MUSTAKABALIWA MAISHA YAKE NA AOMBA MSAADA
ATHUMAN HAMIS alikuwa ni mpiga picha katika vyombo vya habari tofauti na alipata ajaliya gari iliyopelekea kushindwa kufanya kufanya kazi na bado anaugua anaishi kwakulala na kukaa kwenye kiti chake maalum sababu anasumbuliwa na Uti wa mgongo(Spinal Cord).
Attachment 55614
Mimi Athumani Hamisi Awali yayote, napenda kuwasalimia wote, wakubwa na vijana wenzangu Hii itakuwa mara yapili kuongea nanyi waandishi wenzangu, ndani ya miaka minne tokea nipate ajaliSeptemba 12, 2008 eneo la Kibiti Mkoani Pwani nikiwa na wenzangu Herry Makangeambaye kwa sasa ni marehemu na Anthony Siyame, tukiwa njiani kwenda Kilwamkoani Lindi kikazi. Mara ya kwanza niliongea nanyi 2010 baada ya kurejeakutoka Afrika kusini nilikopelekwa na Serikali kwa matibabu.
Shukranizangu za awali, zimwendee Mhe Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Jakaya Kikwete aliyenitembelea katika Hospitali ya Muhimbili nilikolazwa na kuagizanilipelekwe nje kwa matibabu zaidi. Katika ajali ile, nilivunjika shingo naku-damage spinal cord iliyopelekea kupooza mwili wote kuanzia shingoni. Katikaoperesheni iliyofanywa na madaktari wa hospitali ya Mil Park, Afrika Kusiniwalilazimika kuunganisha shingo kwa nyuma. Shukraniza pili ni kwa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, kampuni ninayofanyia kazi yamagazeti ya serikali, wachapishaji wa Daily News, Sunday news, Habari LeoJumapili na Spoti leo, familia yangu iliyokuwa katika wakati mgumu wakati huohadi sasa watanzania wote wuamini wa dini zote waliokuwa wakiombea Pamoja namarafiki zangu waliokuwa wakihangaika huku na kule kwa namna moja ama nyingine.
Niko mbeleyenu leo kuwaomba mnifikishie ujumbe kwa jamii kwa maelezo yafuatayo:- Ofisiyangu ya TSN ilinipangia nyumba ninayokaa Sinza Vatican, Wilaya ya Kinondonijijini Dar es salaam Mei 2010-2011 na mkataba ulikukwa kati ya mwenye nyumba naTSN ambao mimi sikuwahi kuuona hadi ninavyoongea na nyie leo. Mkataba uliishatena Mei 2011, mwenye nyumba alikwenda TSN kuomba kusaini mkataba mpya. Badalayake aliandikiwa mkataba mpya wenye jina langu na kupewa aniletee mimi nisaini.Nilipomuuliza mkataba wa kwanza uliingia na nani na ni nani alisaini. Alisemani TSN walisaini wakamwambia wana mgonjwa ambaye ni Staff wake atakuja kuishipale akitokea Afrika Kusini alikokwenda kwa matibabu.
Mwenye nyumba akasema walimwambia gharama za nyumba ni za TSN, sasa nashangaa leo wameandika jinalako na mkataba ni kati yangu na wewe. Nikamwambia kaka, mimi sikutarajia kufikia hapa kwani mwaka 1999 ilipangwa mimi nifikie katika nyumba ya kampuni Upanga kuepusha gharama na ukaribu wa huduma za kitabibu, mpaka masuala yanguyatakapothibitishwa na Daktrari kama hali yangu itaruhusu mimi kuwezakufanyakazi ama vinginevyo. Rudi ofisini mkasaini kama mlivyofanya awali. Naumwambie kwa hali ya Athumani hawezi kusaini mkataba na mimi kulingana na haliyake. Isitoshe mi nilitiliana saini mkataba wa awali na TSN. Ukweli nilikataa kusaini zaidi ya mara tatu, mpaka Meneja Mwajiri siyo huyo wa sasa alipoingilia kati na kunithibitishia kuwa kampuni italipa nyumba mpaka uamuziwa madaktari utakapotoka, saini mimi nitakulinda.
Niliporejea nyumbani nikawe kwa wino katika dole gumba wakaweka saini. Mpaka yalipojitokeza ya sasa.Ndugu waandishi wa habari, hali yangu japo imeimarika zaidi kuliko awali, leonimekuja na jambo ambalo litahusisha jamii na nyie ndiye wahusika Wakuu katikasuala hili.
KIKUBWA ZAIDI LEO NI SHUKRANI NAOMBI
Ukweli ulio wazi, nashukuru kwa Mungu na kujivunia kuwa TSN. Nimelelewa na TSN kwa miaka sita sasa. Imenilea nikiwa mgonjwa kwa miaka mine, nikiwa bado niko ndaniya ajira jambo ambalo ni gumu sana sehemu nyingine. Imelipa nyumba kwa miaka miwili na imesitisha kulipa kodi ya 2012-2013 kwa barua ya Februari 3, 2012 nakutoa maelezo kwenye barua kuwa imefikia hatua hiyo kutokana na kuwapawafanyakazi wake asilimia 15 ya mishahara yao kulipa nyumba. Nyumba walionipangia ni ya vyumba viwili na kodi iliyolipwa kwenye mkataba wa mwaka jana ni Milioni 4.8 Nilipatwa na mshutuko kidogo, nafsi ikanishauri niite menejiment nyumbani tushauriane katika hili.
Walikuja Machi 28, na wakanipa pole ya kampuni tokea nirudi 2010 Shs 50,000. Lakini mazungumzo hayakuisha kutokana na muda na kuahidi kurudi wiki inayofuata kwa mazungumzo zaidi. Nimepewa notisi na mwenye nyumba April 23, 2010. Nadhani kutokana na kubanwa na kazi, hawakupata nafasi ya kurudi tena kumalizia mazungumzo. Kwa mtazamo wa kifikira ni wazi msimamo ulibaki palepale. Barua yakusitisha kulipa kodi haikuja kwangu tu bali pia mwenye nyumba alipata.
UFAFANUZIKabla ya kuruhusiwa kurejea nyumbani Tanzania, Netcare Rehabilitation Hospital,wanautaratibu mzuri sana. Kabla ya kuwa – discharged wanakuruhusu ukae nje ya hospital kwa miezi mitatu, kama una mke au mume na kama huna utatafutiwa nurse awe wa kike ama wa kiume mimi nilipata nurse. Baada ya hapo una hudhuria mazoezi na vipimo kadhaa kwa miezi mitatu. Ukifaulu kumaliza miezi mitatu wewe na mwangalizi wako hasa wewe mgonjwa bila kupata matatizo, hapo wanaku-discharge.
Nilipiga simu kwa Katibu Kiongozi Ikulu wakati huo, Philemon Luhanjo na kwaKatibu Mkuu wa Wizara ya Afya na Ustawi wa jamii anahitajika nurse kuja kukaanami nje ya hospital kwa miezi mitatu, je mtanisaidiaje? Kwa kweli jibu laolilikuwa moja tu hatutatuma nurse kutoka huku, tafuta huko huko, fedha zakumlipa, nyumba ya kulala, chakula na usafiri, andika budget itume harakatutalipa na wasiliana na ubalozi waje kujua unakaa wapi na fedha zitatumwaubalozini watakuwa wanakuletea. Nilipata nurse na miezi mitatu ilipokaribiakwisha nilifanya mawasiliano kujua kama kutatumwa mtu wa kunifuata, wakanijibu njoo naye huyo huyo watanzania waliofanikiwa kuangalia vyombo vya habari wengiwalimuona kwani nilirudi Mei 28, 2010.
Baada ya mwezi alimaliza mkataba namekutakiwa kutafuta nurse wa kukaa naye kwa saa 24. Akapatikana na akafundishwana M-South Africa jinsi ya kukaa na mgonjwa wa Spinal Cord. TSN,wakamlipa nurse wa South Africa Rand 12,500 alizokuwa anadai na palepale nikauliza vipi kuhusu malipo ya nurse mpya ambaye ataachwa na mimi? Kwa sababuserikali imemaliza jukumu lake na waliniambia kwa kuwa wewe bado ni mwajiriwawa TSN, jukumu lote sasa utakuwa chini yao na ndiyo mmepewa pia jukumu lakumlipa kama mlivyofanya leo. TSN walinijibu palepale kuwa suala la kumlipa nurse ni lako na familia yako ila nyumba tutalipa.
Vodacom walijitokeza kubeba gharama za tiketi nilipopata ajali kwenda Afrika Kusini nawasindikiaji wote, tiketi ya nurse niliyekuja naye. Pia wakalipa tiketi yangu na nurse Desemba 8, 2010 kwenda na kurudi Afrika Kusini kwa ajili ya check up.Baada ya TSN kulipa nurse yule msouth afrika, nikawapigia Vodacom Foundation kuwa nurse amemaliza mkataba na ameshalipwa fedha naomba mumkatie tiketi. Hivyo ilikuwa Juni 25 na kesho yake Juni 26 2010 jioni wakaja watu wawili kutoka Vodacom Foundation na mmoja kutoka TSN waliniambia wamekuja na vitu vitatu. Wakamshukuru nurse kwa kazi nzuri, lakini wakamwambia, sisi ni kutoka Vodacom. Vodacom Foundation inakuomba uendelee kumhudumia Athumani. Na Vodacom watakulipa mshahara lakina tunaomba upunguze kiwango.
Yule nurse akakubali akapunguza nusu ya mshahara aliokuwa akilipwa na serikali.Wakamwambia sasa Vodacom Foundation inakata tiketi ya kwenda nyumbani Afrikakusini kuaga. Akaomba siku 15, mkataba wa mdomo ukakubaliwa na yule nurse namshahara wa kwanza ukawa Julai 2010 kuendelea na kazi chini ya Vodacom. Julai 2010 wakamlipa. Kilichoendela naomba nisiseme.
Muda wacheckup ulifika Desemba 2010, nikaitaarifu Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii.Wakakubali wakaandika barua kwa kugawa majukumu. Afya wakasema watalipa gharamaza matibabu, Vodacom tiketi za kwenda na kurudi na TSN waliagizwa kulipa allowance kwa mgonjwa na nurse. Tukasafiri Desemba 8,2010 na tukarudi Februari28,2011. Malipo yaliyofanywa na TSN kidogo ni aibu naomba nisiseme. Hali hiyo ilinionyesha kuwa Vodacom Foundation walikuwa wanatambua uwepo wa yule nurse. Lakini hadi nurse anaondoka alilipwa mshahara mmoja tu na hata tiketi ya nurse kurudi Afrika Kusini Vodacom hawakulipa.
Nililipa tiketi ya Business Class.Nikampa Rand 4,500 akakataa akachukua Rand 2,500 tu, akaniambia, Athumani nakuacha katika hali mbaya sana. Fuatilia haki zangu na zako, ukifanikiwa utaniambia na Account ya benki, First bank nakuachia utaniwekea. Vodacom Foundation hawajawahi kupokea simu yangu na Mkurugenzi wake hajawahi kupokea simu yangu wala kuongea na mimi tokea nipate ajali.
Suala lingine waliniuliza nichague kitu kimoja, kujengewa nyumba au kusomeshewa watoto. Mimi nilichaguakujengewa nyumba. Walichukua chaguo langu. Tukamaliza mazungumzo. Baada yamwezi waliniambia suala lako limekubaliwa ila tumepata Mkurugenzi mpya, lakini usijali. Mpaka hapa ninavyoongea danadana ziliendelea mpaka ninavyoendelea kwenye nyumba, sijawahi tena kupata jibu kutoka Vodacom.La mwisho nilijibiwa na mmoja wa watu wa Vodacom Foundation aliniambia wewe uliingia mkataba na kampuni ya One Plass na si Vodacom Foundation.
SIKU YA LEO Nimekujaleo kuutangazia umma hali ilivyo. Ukweli kwa sasa Account ya CRDB ilikuwamaalumu kwa ajili ya kusomeshea watoto, imekauka ya Postal bank ambayo yamshahara haina kitu. Pesa ya mshahara inayoingia benki ni 450,000 Nawalipanurse, msaidizi wake na mfanyakazi 370,000. Maisha yaulemavu ni ghali sikutarajia. Nina wanangu watatu, wa kwanza anamaliza darasala saba mwaka huu, wa pili yuko la nne na wa mwisho yuko la pili. Hawa wanasomaprimary za kulipia wote hawa nawalipia 200,000 kila mmoja kwa term jumla400,000 hizo shule zina term nne kwa mwaka. Gharama chakula, vifaa vyawanafunzi, gharama zao ndogondogo na za kifamilia Pamoja na chakula kwa mwezi,inakwenda kati ya 750,000 mpaka 900,000 kwa mwezi.
Nimekuwa ombaomba mpaka watu kadhaa siwalaumu, wamechoka hawapokei simu wala kujibu sms.siyo siri ndugu wote wamekimbia waliobaki ni marafiki wa kweli wameniingiza katika familia zao. Hali yangu ni mbaya sana kiuchumi. Sina uwezo wa kulipa nyumba kwa gharama zozote zile. Mimi Athumani Hamisi, naomba watanzania watakaoguswa wanisaidie. Kubwa nyumba na ushauri wa madaktari walinishauri nisiishi mbali na mazingira ya hospitali kulingana na hali yangu. Makampuni, mashirika, wizara yoyote, shirikala nyumba la Taifa NHC, watu binafsi, serikali na Taasisi yoyote watakaoguswa na kilio changu nawaomba wanisaidie kwa njia yoyote. kwa waliotayari naomba misaada ipitie katika account No 01J2027048800 ya CRDB na Account No 010-00090488 ya Postal Bank Kwa wanaotumia mitandao ya simu, wanaweza kutumia M-pesa 0757 825 737, Tigopesa 0655 531 188 na Airtel Money 0784 531118; M-Pesa 0767 298 888 ya Chris Mahundi na Airtel Money 0686 710 977 ya Ephraim Mafuru.
Habari kwahisani ya http://www.8020fashions.blogspot.com/

Reply With Quote



Follow Us Here