Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Mgeja aibua tuhuma nzito Barrick

    Report Post
    Page 1 of 2 12 LastLast
    Results 1 to 20 of 31
    1. #1
      engmtolera's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st October 2010
      Posts : 3,605
      Rep Power : 1330
      Likes Received
      780
      Likes Given
      655

      Default Mgeja aibua tuhuma nzito Barrick

      na Mwandishi wetu, Shinyanga

      MWENYEKITI wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Shinyanga, Hamis Mgeja ameituhumu kampuni ya uchimbaji madini ya Barrick kwa kuchimba madini ya fedha na shaba kinyemela.Mgeja ambaye pia ni mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM, Taifa, amedai kuwa kampuni hiyo pia imekiuka mkataba wake, na sasa inachimba dhahabu nje ya maeneo iliyopewa rasmi.Mwenyekiti huyo ametoa tuhuma hizo juzi katika kikao cha ushauri cha mkoa, akisema zipo taarifa za uhakika kuwa mwekezaji ameingia katika eneo kubwa mno, nje ya lile alilopewa kisheria, na kwamba amekuwa akichimba chini kwa chini umbali mrefu.“Kuna taarifa za vijana wetu zinaonesha kuwa Barrick sasa amekwenda umbali mrefu sana wa zaidi ya kilometa nne na karibu ataingia Mkoa wa Geita.“Hakuna ubishi kwamba huu ni wizi, lazima ufanyike uchunguzi wa haraka, tukiacha wizi huu uendelee, ipo hatari ya vizazi vijavyo vikatusuta,” alisema Mgeja.Alikiri kuwa maisha ya Watanzania wanaoishi jirani na maeneo ya migodi ni magumu kiuchumi, wakati mwekezaji anajipatia kipato kikubwa kutoka katika madini ya shaba na fedha ambayo halipii chochote serikalini.Aliishauri serikali kupitia upya mkataba wa mwekezaji huyo wa Bulyanhulu ili aweze kulipa mrabaha mwingine kutokana na madini ya shaba na fedha anayoyapata kutoka katika mgodi huo wa dhahabu anaoumiliki hivi sasa.Taarifa hiyo iliwashitua baadhi ya wajumbe wa kamati hiyo ya ushauri ya mkoa, na kutaka hatua za kisheria zichukuliwe dhidi ya mwekezaji huyo.
      M2S likes this.
      "The person who says it cannot be done should not interrupt the person doing it."

    2. FemaTV & Radio

    3. #2
      WA-UKENYENGE's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 1st October 2011
      Location : Inside a Smart Grid
      Posts : 2,417
      Rep Power : 5038
      Likes Received
      782
      Likes Given
      1788

      Default Re: Mgeja aibua tuhuma nzito Barrick

      Hilo mbona lipo siku nyingi, au ndiyo inataka kugeuzwa turufu ya kisiasa? Haiwezekani inshu kama hii niliisikia miaka 4 - 5 iliyopita leo mgeja ndiyo anaanza kubwabwaja tena akiwa mkazi wa mkoa husika! Ukimuuliza kafanya nini kwa ajili ya mkoa wa shinyanga, utasikia aaaa! mara Ooooo.
      "The usual conclusion is that you can't put a price on a human life. But you can if you must".

    4. #3
      Elli's Avatar
      Banned Array
      Join Date : 17th March 2008
      Location : Kijito-Upele
      Posts : 8,513
      Rep Power : 0
      Likes Received
      2102
      Likes Given
      1839

      Default Re: Mgeja aibua tuhuma nzito Barrick

      Alikua wapi siku zote? au alisubiri wafike kilimeta nne? pambaf

    5. #4
      KASHOROBANA's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 30th July 2011
      Posts : 1,462
      Rep Power : 687
      Likes Received
      233
      Likes Given
      86

      Default Re: Mgeja aibua tuhuma nzito Barrick

      Huyu mzee ni mnafiki pia fisadi mkubwa, kwani hizo si ndio sera zenu za chukua chako mapema (ccm), na zaidi ya yote alikuwa wapi?
      Mnafiki sana uyu mzee wala hatudanganyiki wewe mzee mgeja ni mshirika mzuri tu wa mafisadi pia magamba

    6. #5
      Liz Senior's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 19th April 2007
      Posts : 463
      Rep Power : 710
      Likes Received
      33
      Likes Given
      24

      Default Re: Mgeja aibua tuhuma nzito Barrick

      Wameshindwa kuelewana nini tena? Kuna mtu karushwa hapo
      Ndahani likes this.
      Knowledge does not lead to change—understanding does

    7. Miaka 50

    8. #6
      Josephine03's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 7th February 2012
      Posts : 733
      Rep Power : 514
      Likes Received
      285
      Likes Given
      373

      Default

      Atakuwa kanyimwa mgawo huyo hana lolote, mbona tunaijua toka kitambo

      Sent from my BlackBerry 9910 using JamiiForums

    9. #7
      Elungata's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 28th January 2011
      Posts : 3,711
      Rep Power : 1249
      Likes Received
      416
      Likes Given
      0

      Default Re: Mgeja aibua tuhuma nzito Barrick

      Huo mgodi utaifishwe haraka sana.

    10. #8
      Mnama's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 13th October 2010
      Posts : 737
      Rep Power : 1162
      Likes Received
      174
      Likes Given
      108

      Default Re: Mgeja aibua tuhuma nzito Barrick

      Mhusika ambaye angeweza kushughulikia hilo swala kesha chukua chake mapema , huyo mzee analeta poroja za barazani kufurahisha umati hana lolote.

    11. #9
      Bajabiri's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 31st December 2010
      Posts : 9,741
      Rep Power : 2884
      Likes Received
      1115
      Likes Given
      52

      Default

      Quote By engmtolera
      na Mwandishi wetu, Shinyanga

      MWENYEKITI wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Shinyanga, Hamis Mgeja ameituhumu kampuni ya uchimbaji madini ya Barrick kwa kuchimba madini ya fedha na shaba kinyemela.Mgeja ambaye pia ni mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM, Taifa, amedai kuwa kampuni hiyo pia imekiuka mkataba wake, na sasa inachimba dhahabu nje ya maeneo iliyopewa rasmi.Mwenyekiti huyo ametoa tuhuma hizo juzi katika kikao cha ushauri cha mkoa, akisema zipo taarifa za uhakika kuwa mwekezaji ameingia katika eneo kubwa mno, nje ya lile alilopewa kisheria, na kwamba amekuwa akichimba chini kwa chini umbali mrefu.“Kuna taarifa za vijana wetu zinaonesha kuwa Barrick sasa amekwenda umbali mrefu sana wa zaidi ya kilometa nne na karibu ataingia Mkoa wa Geita.“Hakuna ubishi kwamba huu ni wizi, lazima ufanyike uchunguzi wa haraka, tukiacha wizi huu uendelee, ipo hatari ya vizazi vijavyo vikatusuta,” alisema Mgeja.Alikiri kuwa maisha ya Watanzania wanaoishi jirani na maeneo ya migodi ni magumu kiuchumi, wakati mwekezaji anajipatia kipato kikubwa kutoka katika madini ya shaba na fedha ambayo halipii chochote serikalini.Aliishauri serikali kupitia upya mkataba wa mwekezaji huyo wa Bulyanhulu ili aweze kulipa mrabaha mwingine kutokana na madini ya shaba na fedha anayoyapata kutoka katika mgodi huo wa dhahabu anaoumiliki hivi sasa.Taarifa hiyo iliwashitua baadhi ya wajumbe wa kamati hiyo ya ushauri ya mkoa, na kutaka hatua za kisheria zichukuliwe dhidi ya mwekezaji huyo.
      aaaaa,,,,,,jamani yaan leo ndo bwana hamis amejua ni wizi????,,,anataka tusutwe na nani tena???mimi binafsi nawasuta wao kwa kugawa madini,,,,,,sasa anamwambia nani????,sheria ya madini ni mbovu,na watu washasema sana tu,na tume lukuki zimeundwa,hakua jipya hapo

    12. #10
      Bajabiri's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 31st December 2010
      Posts : 9,741
      Rep Power : 2884
      Likes Received
      1115
      Likes Given
      52

      Default

      Quote By Mnama
      Mhusika ambaye angeweza kushughulikia hilo swala kesha chukua chake mapema , huyo mzee analeta poroja za barazani kufurahisha umati hana lolote.
      tena na gahawa mkononi,,,,kwani kuna jipya hapo????si kweli kwamba kamishna wa madini hajui hii dili

    13. #11
      Bajabiri's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 31st December 2010
      Posts : 9,741
      Rep Power : 2884
      Likes Received
      1115
      Likes Given
      52

      Default

      Quote By Josephine03
      Atakuwa kanyimwa mgawo huyo hana lolote, mbona tunaijua toka kitambo

      Sent from my BlackBerry 9910 using JamiiForums
      binafsi nimewaza kitu kama hiki,kwa sasa atapewa MGAO,WASHAMSIKIA

    14. #12
      engmtolera's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st October 2010
      Posts : 3,605
      Rep Power : 1330
      Likes Received
      780
      Likes Given
      655

      Default Re: Mgeja aibua tuhuma nzito Barrick

      Quote By Josephine03
      Atakuwa kanyimwa mgawo huyo hana lolote, mbona tunaijua toka kitambo

      Sent from my BlackBerry 9910 using JamiiForums
      Tukiachana na mambo ya mgao,lakini jamani inakuwaje wawekezaji wanaionea sana tanzania? inakuwaje kuchimba madini ambayo hawaruhusiwi kuchimba

      waziri husika,madudu mengine hayo

      jamani tuvunje mkataba,kuanza upya si ujinga
      "The person who says it cannot be done should not interrupt the person doing it."

    15. #13
      zomba's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th November 2007
      Posts : 15,822
      Rep Power : 14621
      Likes Received
      2842
      Likes Given
      1961

      Default Re: Mgeja aibua tuhuma nzito Barrick

      Huyu Mgeja kachemsha, utachimbaje dhahabu itoke dhahabu pekee? migodi mingi duniani (kama si yote) ya dhahabu huwa inatoa na fedha na shaba kwa kiwango fulani.
      System At Work

      "nimetembea angani na ardhini Tanzania nzima sijaona Rais na serikali iliyotukuka kiutendaji kama hii ya KIKWETE." - Freeman Aikaeli Mbowe

    16. #14
      BADILI TABIA's Avatar
      JF Bronze Member Array
      Join Date : 13th June 2011
      Location : DUNIANI
      Posts : 14,564
      Rep Power : 5615
      Likes Received
      6211
      Likes Given
      2281

      Default Re: Mgeja aibua tuhuma nzito Barrick

      si walishapokea 10%? watulie....
      umeona wapi mtu anasafirisha mchanga nje?

      aaah hivi wale waliopiga wananchi na kuwaua kwa kutumia polisi na kusingizia chama fulani cha siasa walikuwa mgodi upi?
      "Behind every great fortune there is a crime."
      - Honore de Balzac (1799-1850)

    17. #15
      TaiJike's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 14th December 2011
      Posts : 1,156
      Rep Power : 606
      Likes Received
      387
      Likes Given
      347

      Default Re: Mgeja aibua tuhuma nzito Barrick

      Quote By engmtolera
      Tukiachana na mambo ya mgao,lakini jamani inakuwaje wawekezaji wanaionea sana tanzania? inakuwaje kuchimba madini ambayo hawaruhusiwi kuchimba

      waziri husika,madudu mengine hayo

      jamani tuvunje mkataba,kuanza upya si ujinga
      engmtolera hii kitu si yaleo alikuwa wapi na ni mkazi wa shy?

      Wawekezaji hawaineni tza ni ujinga wetu watz wa kushindwa kuwawajibisha walafi wachache wanaotumikia matumbo yao na famili zao na kuisahau tz na watu wake.
      * Nitashangaa kama hawa Watanzania watakataa kuasi. Kwanini wasiasi? * - Julius Kambarage Nyerere


    18. #16
      engmtolera's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st October 2010
      Posts : 3,605
      Rep Power : 1330
      Likes Received
      780
      Likes Given
      655

      Default Re: Mgeja aibua tuhuma nzito Barrick

      Quote By TaiJike
      engmtolera hii kitu si yaleo alikuwa wapi na ni mkazi wa shy?

      Wawekezaji hawaineni tza ni ujinga wetu watz wa kushindwa kuwawajibisha walafi wachache wanaotumikia matumbo yao na famili zao na kuisahau tz na watu wake.
      Taijike
      ni kweli kuna jamaa kanitonya hapa anadai tangu 1998 jamaa wamekuwa wakipeleka mchanga wa madini hayo nje,lakini pia mwaka huo tayari walikuwa wamevuka 5km nje ya mkataba,ila viongozi wetu wapo na wanakura raha tu
      "The person who says it cannot be done should not interrupt the person doing it."

    19. #17
      TaiJike's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 14th December 2011
      Posts : 1,156
      Rep Power : 606
      Likes Received
      387
      Likes Given
      347

      Default Re: Mgeja aibua tuhuma nzito Barrick

      engmtolera
      Ni ujinga/umbumbu wetu wa kuangalia na kuridhika na hali yoyote ile inayojitokeza hata kama siya kawaida. Mkataba wao ni dhahabu hiyo shaba na fedha iko ktk mrahaba na mkataba upi? na ilipogundulika kuwa barrick imevuka mpaka wa uvunaji wake wa dhahabu na kuingia mpaka Mkoa mpya wa geita ni hatua zipi zilichukuliwa kwa mali ilikwisha ondoka, kwa upande wa serikali na wakazi wa maeneo husika?
      * Nitashangaa kama hawa Watanzania watakataa kuasi. Kwanini wasiasi? * - Julius Kambarage Nyerere


    20. #18
      watu8's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 19th February 2010
      Location : Juu ya Tukutuku
      Posts : 15,074
      Rep Power : 31287
      Likes Received
      7471
      Likes Given
      7485

      Default Re: Mgeja aibua tuhuma nzito Barrick

      haya ndio malipo ya kuchagua kitu kinaitwa CCM, wanaingia madarakani kwa nguvu za giza na kufunga akili za wananchi kwa nguvu za kichawi ili hata wasihoji maslahi ya Taifa lao....

    21. #19
      Bajabiri's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 31st December 2010
      Posts : 9,741
      Rep Power : 2884
      Likes Received
      1115
      Likes Given
      52

      Default

      Quote By engmtolera
      Tukiachana na mambo ya mgao,lakini jamani inakuwaje wawekezaji wanaionea sana tanzania? inakuwaje kuchimba madini ambayo hawaruhusiwi kuchimba

      waziri husika,dudu mengine hayo

      jamani tuvunje mkataba,kuanza upya si ujinga
      mdau yaan unahisi serikali HAIJUI??????HAKUNA LINALOFANYIKA BILA WAO KUJUA,,,,KAMA KAJUA MGEJA BASI WANAJUA WEEEENGI MNO

    22. #20
      wantuzu's Avatar
      Member Array
      Join Date : 24th November 2011
      Posts : 41
      Rep Power : 386
      Likes Received
      13
      Likes Given
      11

      Default Re: Mgeja aibua tuhuma nzito Barrick

      nimefanya kazi kwenye huo mgodi husika kwa miaka si chini ya saba nnachoweza kuwashauri wabongo , ni kwenda ofisini kwao pale hamza azizi rd masaki , watawapa kibari cha kwenda kutembea mgodini kwa gharama zao...
      tusishuhudie habari ambazo hatuna uhakika nazo na watu wasitumie udhaifu wa watanzania wa kutafuta usahihi wa habari kujinufaisha kisiasa , acheni !

    Page 1 of 2 12 LastLast

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...