Wadau kama mnavyojua leo ndio maadhimsho ya miaka 60 tangu Elizabeth II atawazwe kua malkia wa Uingereza.
Sasa kuna kitu kimoja nimekikumbuka leo na naomba kwa mwenye kumbukumbu atujuze.
Nilipokua mdogo nilikua nasikia eti yule Ex Rais wa malawi hayati Hasting Kamuzu Banda alikua ni daktari binafsi wa Malkia. Na kazi yake kubwa ilikua ni kutibu sehemu ya uzazi (nyeti) ya huyo Queen.
Sasa Waingereza kwa kuhofia Dk Banda asije kula tunda, ikabidi wampe sharti la kuhasiwa. Na yeye akatoa sharti kwamba sawa ila apewe Urais wa Malawi. Wakakubaliana and the rest is history.
Jee wenzangu habari hii ni ya kweli?

Reply With Quote



Follow Us Here