Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Mapokezi ya Rais wa Bank ya Afrika ni zaidi ya Rais wa Nchi

    Report Post
    Page 1 of 3 123 LastLast
    Results 1 to 20 of 47
    1. #1
      Thanda's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 6th April 2012
      Location : Multiple Destination
      Posts : 1,891
      Rep Power : 1607
      Likes Received
      566
      Likes Given
      1523

      Default Mapokezi ya Rais wa Bank ya Afrika ni zaidi ya Rais wa Nchi

      Haya ..niko Arusha,Mkutano wa Bank ya Maendeleo ya Afrika (African Development Bank) kwa hapa umekuwa hosted na Wizara ya Mkulo(nakumbuka tulikaa vikao vingi sana kuhakikisha mkutano huu unafanyika Afrika Mashariki, Mkulo akapiga debe kwamba "Tanzania Tunaweza Bila Kuwezeshwa"kweli ukaja Arusha... lugha tunayoitumia ni Kiingereza na Kifaransa....wafaransa wa kizungu na wa kiafrika...kiswahili NO, mimi naongea kiswahili,. nakutana na mmoja wa waandaaji wa mkutano huu wa kimataifa wa wachumi."votre nom siil vous plait?=Your name please? najitambulisha,naye pia anajitambulisha kwangu, ana uraia wa nchi mbili Ghana na Ufaransa, ni dada mcheshi, mzungu, na ni mara yake ya kwanza kuja Tanzania, tunasalimiana, lakini ghafla Magavana wanaanza kuingia, mnisamehe sijapiga picha..waandishi wa habari usiseme.

      Msafara wa rais wa bank ya maendeleo ya Afrika anakaribia kuingia hapa...maafisa usalama kama kawaida.Askari wamejipanga kwa ajili ya kutoa heshima kwa Rais, wote wana silaha...wanapokea maelekezo. mkutano haufanyiki hapa hotelini, ni eneo la AICC(Arusha International Conference Center) hapa ni kula na kulala tu...na vikao vingine vidogovidogo(billateral meetings, working conferences na Launching of AGF, Mabenki yote yana uwakilishi hapa.Wawakilishi wa bank mbalimbali wako hapa, makampuni ya simu pia, TANAPA wanaongoza kwa kuutangaza utalii.

      Naiona red carpet kutoka mlangoni hadi kwenye kambarau (lift)ya hotel....

      Pikipiki za polisi ziko nne, zinaingia kwa mbwembwe, askari wa usalama barabarani wako hadi ndani ya hotel wanaelekeza magari kila mahali..haya zinaingia gari za polisi kama nne, Field Force Unit, Ambulance ya polisi, Magari aina ya PRADO hayana idadi...yote yana nembo ya kampuni ya ANGONI. Magari madogo madogo na yale ya kukodi hayana idadi. La mheshimiwa silioni,..huyu hapa anashuka, ni mtu wa makamu kidogo, amevaa shati la rangi ya kijivu, suruali nyeusi, na miwani ya jua,. tunampokea anatupa mikono mmoja baada ya mwingine..anasema jambo karibu Tanzania, no anaongea kiswahili, jamani anaongea kiswahili safi...(nimerudi nyumbani,,,,anasema) ni mwafrika kutoka Africa ya...aaaaaaaaaaaaahh, kumbe ni Mheshimiwa Donald Kaberuka, Mnyarwanda anayeitumikia Bank hiyo kwa kipindi cha pili(Miaka Mitano).Anaelekezwa kwenda katika kambarau (lift)..anaingia...end of story. tuliobaki nje, raia na maafande wa usalama wote tunaelekea maeneo yetu muhimu.

      Amesoma hapahapa Tanzania na Uingereza na Mwaka 1997 alikuwa waziri wa fedha wa Rwanda...Si tu anapewa salamu za ki-protokali, bali pia nimeangalia wingi wa askari eneo hili na aina ya ulinzi kwa mtu ambaye kwangu naona bora angepokewa kawaida kama viongozi wengine na sio mapokezi zaidi ya yale ya rais wa nchi...haya ngoja tuone mapokezi ya Kikwete kesho hapahapa katika hotel ya Mount Meru, Arusha
      Last edited by Thanda; 27th May 2012 at 21:08.

    2. Miaka 50

    3. #2
      nngu007's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 2nd August 2010
      Posts : 11,235
      Rep Power : 3562
      Likes Received
      3062
      Likes Given
      462

      Default Re: Mapokezi ya Rais wa Bank ya Afrika ni zaidi ya Rais wa Nchi

      So, What? Is this really supposed to be here? a Tanzanian Critical Political Issue?

      HELP !!!! where is our MODS??? Sometimes we do fail to deliver a political news

    4. #3
      Kimbunga's Avatar
      JF Platinum Member Array
      Join Date : 4th October 2007
      Location : Kisiwani Juma
      Posts : 7,484
      Rep Power : 6170
      Likes Received
      3058
      Likes Given
      1020

      Default Re: Mapokezi ya Rais wa Bank ya Afrika ni zaidi ya Rais wa Nchi

      Jana imebidi nikimbie toka Arusha niende kuishi Babati manake Arusha hakuna Hotel zote ziko full booked kwa ajili ya mkutano wa AfDB! Hii si ndio tuliambiwa kwamba zimenunuliwa laptops kwa kila mshiriki kama sikosei? Isije ikawa hasara nyingine kama ya Sulvan.
      Thanda likes this.

    5. #4
      Mama Mdogo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st November 2007
      Posts : 1,356
      Rep Power : 859
      Likes Received
      677
      Likes Given
      73

      Default Re: Mapokezi ya Rais wa Bank ya Afrika ni zaidi ya Rais wa Nchi

      Quote By Kimbunga
      Jana imebidi nikimbie toka Arusha niende kuishi Babati manake Arusha hakuna Hotel zote ziko full booked kwa ajili ya mkutano wa AfDB! Hii si ndio tuliambiwa kwamba zimenunuliwa laptops kwa kila mshiriki kama sikosei? Isije ikawa hasara nyingine kama ya Sulvan.

      Una mmana mkutano wa Sulvan uliitia hasara nchi yetu? Kiasi gani (US $ ngapi)?
      Anyone who has never made a mistake has never tried anything new - Albert Einstein
      No problem can be solved from the same level of consciousness that created it
      - Albert Einstein


    6. #5
      Mrdash1's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st September 2010
      Posts : 1,379
      Rep Power : 1460
      Likes Received
      305
      Likes Given
      201

      Default Re: Mapokezi ya Rais wa Bank ya Afrika ni zaidi ya Rais wa Nchi

      Herald hunter, umenifurahisha sana na umahili wa uandishi wako ni burudani tosha
      Thanda likes this.

    7. RukaaJuu Final

    8. #6
      Thanda's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 6th April 2012
      Location : Multiple Destination
      Posts : 1,891
      Rep Power : 1607
      Likes Received
      566
      Likes Given
      1523

      Default Re: Mapokezi ya Rais wa Bank ya Afrika ni zaidi ya Rais wa Nchi

      Habari ni habari, nini maana ya forum?...ni kujuzana yanayojiri, unataka kusema kuwa hoja hii haipaswi kufahamika kwa wadau? Au huwa hausafiri na kujifunza mambo?, USHAURI WA BURE: Tembea na ujifunze kwa watu, ili kujua wenzako wanafanya nini, kwanini, wapi na lini..hiyo itakusaidia sana.

      Karibu Arusha, Mkutano ni wa delegates zaidi ya 3000, hakuna pa kulala kama sio mwenyeji wa Arusha labda uwe ulifanya booking mwezi uliopita( Mwezi April)
      Last edited by Thanda; 27th May 2012 at 21:23.

    9. #7
      Thanda's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 6th April 2012
      Location : Multiple Destination
      Posts : 1,891
      Rep Power : 1607
      Likes Received
      566
      Likes Given
      1523

      Default Re: Mapokezi ya Rais wa Bank ya Afrika ni zaidi ya Rais wa Nchi

      Ni kweli, nafasi hakuna...zote zenye majina haya zimejaa pia ( INNS, RESORTS, GUEST HOUSES, MOTELS, DELUXES)nakwambia zote zimejaa. mkutano unaanza kesho, AICC, Simba Hall. Pia Kumbi za Mbayuwayu,Tausi,Mbuni na Manyara ziko booked hadi mkutano uishe.

    10. #8
      Thanda's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 6th April 2012
      Location : Multiple Destination
      Posts : 1,891
      Rep Power : 1607
      Likes Received
      566
      Likes Given
      1523

      Default Re: Mapokezi ya Rais wa Bank ya Afrika ni zaidi ya Rais wa Nchi

      Asante sana Mr Dash, Ila naomba nisikukaribishe Arusha kama uko mkoa mwingine, hadi Mkutano huu uishe kwani nina uhakika unaweza kosa pa kulala.Kama huamini muulize Kimbunga kwanini ameamua kwenda kulala Babati.

    11. #9
      Thanda's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 6th April 2012
      Location : Multiple Destination
      Posts : 1,891
      Rep Power : 1607
      Likes Received
      566
      Likes Given
      1523

      Default Re: Mapokezi ya Rais wa Bank ya Afrika ni zaidi ya Rais wa Nchi

      Mimi hapa sina comment kuhusu hasara, ila Mama Mdogo, C.E.O wa Sullivan, Ambassador Carl Masters, ambaye ndiye mume wa Hope Sullivan na mmiliki wa mlolongo wa makampuni kwa ajili ya kuwawezesha waafrika,aliingia jana jioni toka Marekani, akaonana na Mh. Rais, na leo hii yuko Arusha. Sasa kama unaweza mtafuta ili kumuuliza hilo, fine! Mimi sina haki ya kutoa namba zake za simu ingawa ninazo. Ila yuko, na hivi ninavyoongea na wewe amevaa shati jeupe na suruali ya light blue, viatu vyeusi. Leo anaonekana smart bila suti, amekaa upande wa mwisho kwenye kona anakunywa ginger beer (soda aina ya tangawizi ya kopo) kinywaji maarufu kwao Jamaica.

      Anaweza akatusaidia kama mkutano aliouleta Arusha Mwaka 2008 ulikuwa na faida zipi ( Mimi nilikuwa mshiriki namba 2115 katika Mkutano huo)na hadi leo vile vitambulisho ninavyo.

    12. #10
      JingalaFalsafa's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 13th April 2012
      Location : Africa.
      Posts : 342
      Rep Power : 426
      Likes Received
      213
      Likes Given
      80

      Default

      Quote By Herald Hunter
      Habari ni habari, nini maana ya forum?...ni kujuzana yanayojiri, unataka kusema kuwa hoja hii haipaswi kufahamika kwa wadau? Au huwa hausafiri na kujifunza mambo?, USHAURI WA BURE: Tembea na ujifunze kwa watu, ili kujua wenzako wanafanya nini, kwanini, wapi na lini..hiyo itakusaidia sana.

      Karibu Arusha, Mkutano ni wa delegates zaidi ya 3000, hakuna pa kulala kama sio mwenyeji wa Arusha labda uwe ulifanya booking mwezi uliopita( Mwezi April)
      Kwangu mimi, UAFRIKA ni zaidi ya mambo yote chini ya jua. Mwakilishi wa Afrika, huwezi kumfananisha na mtu wa kanchi kamoja, kasicho na hata dira. Alistahili zaidi ya aliyotendewa, labda tu awe mamluki. Ila African Bank ni bonge la hatua, kama tunaitakia mema Afrika yetu. AfrikaKwanza! AfrikaMoja! AfrikaSana!
      Mungu wetu yu tayari kutushindia, anaita sasa!
      Thanda likes this.

    13. #11
      Ndinani's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th August 2010
      Posts : 2,950
      Rep Power : 1532
      Likes Received
      745
      Likes Given
      237

      Default Re: Mapokezi ya Rais wa Bank ya Afrika ni zaidi ya Rais wa Nchi

      Tanzania / Africa tunaweza kuendelea tukitokomeza uongozi wa aina ya mkweree na chama chake cha magamba kwani hawana vision!!

    14. #12
      Saint Ivuga's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st August 2008
      Posts : 20,726
      Rep Power : 10177
      Likes Received
      5673
      Likes Given
      12666

      Default Re: Mapokezi ya Rais wa Bank ya Afrika ni zaidi ya Rais wa Nchi

      Quote By nngu007
      So, What? Is this really supposed to be here? a Tanzanian Critical Political Issue?

      HELP !!!! where is our MODS??? Sometimes we do fail to deliver a political news
      kiongozi unajua kuna aina ngapi za uandishi au za kufikisha habari?
      Thanda likes this.
      JF the best place to be. and the POWER of God be with us all the time.

    15. #13
      Bantugbro's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 22nd February 2009
      Posts : 2,410
      Rep Power : 1004
      Likes Received
      488
      Likes Given
      1499

      Default Re: Mapokezi ya Rais wa Bank ya Afrika ni zaidi ya Rais wa Nchi

      Acha jamaa atupe story, unajua hata bia zote ni bure kwa courtesy ya ndugu yetu Kaberuka....
      Just because presidents screws around, it doesn't make a president for screwing around..

    16. #14
      Lambardi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 7th February 2008
      Location : KITAANI ZAIDI
      Posts : 4,523
      Rep Power : 1797
      Likes Received
      654
      Likes Given
      0

      Default Re: Mapokezi ya Rais wa Bank ya Afrika ni zaidi ya Rais wa Nchi

      Ulinzi wote huo wanaogopa peoplezzzz powerr hakuna lingine

    17. #15
      MANI's Avatar
      JF Platinum Member Array
      Join Date : 22nd February 2010
      Location : CHINI YA MBUYU
      Posts : 1,915
      Rep Power : 954
      Likes Received
      569
      Likes Given
      632

      Default Re: Mapokezi ya Rais wa Bank ya Afrika ni zaidi ya Rais wa Nchi

      Quote By Kimbunga
      Jana imebidi nikimbie toka Arusha niende kuishi Babati manake Arusha hakuna Hotel zote ziko full booked kwa ajili ya mkutano wa AfDB! Hii si ndio tuliambiwa kwamba zimenunuliwa laptops kwa kila mshiriki kama sikosei? Isije ikawa hasara nyingine kama ya Sulvan.
      Mkuu unatazamiwa kutumia 12bn !
      Thanda likes this.
      " TANZANIA BILA CCM INAWEZEKANA"

    18. #16
      Ngongo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 20th September 2008
      Location : Mlima Meru
      Posts : 4,874
      Rep Power : 1977
      Likes Received
      2352
      Likes Given
      3038

      Default Re: Mapokezi ya Rais wa Bank ya Afrika ni zaidi ya Rais wa Nchi

      Tangu Lema apigwe chini mikutano Arusha imeongezeka sijui watawala wameamua wanatufundisha nini.Wamiliki wa mahotels wanacheka jinsi hotels zilivyojaaa.

    19. #17
      Songambele's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 20th November 2007
      Posts : 748
      Rep Power : 741
      Likes Received
      75
      Likes Given
      191

      Default Re: Mapokezi ya Rais wa Bank ya Afrika ni zaidi ya Rais wa Nchi

      Pamoja na mambo mengine theme Tanzania ni mwanachama na tunachangia pesa lukuki about 20bn USD lakini hatukopi uhsusani sector binafsi na mikopo yao si chini ya 10m USD, kidogo serikali imekopa kupitia kilimo kwanza lakini wabongo hatuna bankable business plan ya kuvuta mkwanja huko. Mkutano huu unaweza kuwashawishi restructuring ya mikopo yao nasi tuvute.
      Thanda likes this.
      You can't fight ignorance with knowledge!

    20. #18
      kanga's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 13th January 2011
      Posts : 729
      Rep Power : 569
      Likes Received
      288
      Likes Given
      409

      Default Re: Mapokezi ya Rais wa Bank ya Afrika ni zaidi ya Rais wa Nchi

      Kwa Taarifa yako ni kwamba Dr.Donald Kebaruka ni Mnyarwanda wa asili ya Tanzania.Amesoma shule ya Msingi Murongo ipo Wilayani Karagwe ,mkonia Kagera mpakani mwa Uganda na Tanzania na kumaliza shule ya msingi mwaka 1954.Shule hiyo ya msingi ndiyo pia amesoma mdada maarufu mjini Dar Madame Ritta Paulsen,shule hiyo iko kijijini kwao na Rita.Donald amekulia Tz na kufanya kazi hadi wakati wa uongozi wa Kagame ndio aliomba wanyarwanda waliopo nje ya nchi warudi Rwanda kujenga nchi yao na wengi hasa waliosoma na kukulia Tanzania walirudi na kupewa vyeo vya juu akiwemo Dr Donald.Hadi anapata kazi ya uraisi wa AfDB Rais Mkapa ndiye alikuwa champion wake kumpendekeza.
      Thanda likes this.

    21. #19
      Buswelu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 16th August 2007
      Location : Lake Victora Gold Field.
      Posts : 1,930
      Rep Power : 991
      Likes Received
      174
      Likes Given
      142

      Default Re: Mapokezi ya Rais wa Bank ya Afrika ni zaidi ya Rais wa Nchi

      Quote By kanga
      Kwa Taarifa yako ni kwamba Dr.Donald Kebaruka ni Mnyarwanda wa asili ya Tanzania.Amesoma shule ya Msingi Murongo ipo Wilayani Karagwe ,mkonia Kagera mpakani mwa Uganda na Tanzania na kumaliza shule ya msingi mwaka 1954.Shule hiyo ya msingi ndiyo pia amesoma mdada maarufu mjini Dar Madame Ritta Paulsen,shule hiyo iko kijijini kwao na Rita.Donald amekulia Tz na kufanya kazi hadi wakati wa uongozi wa Kagame ndio aliomba wanyarwanda waliopo nje ya nchi warudi Rwanda kujenga nchi yao na wengi hasa waliosoma na kukulia Tanzania walirudi na kupewa vyeo vya juu akiwemo Dr Donald.Hadi anapata kazi ya uraisi wa AfDB Rais Mkapa ndiye alikuwa champion wake kumpendekeza.
      Secondary kasomea Tabora boys....ni moja ya vichwa vya kinyarwanda wazazi wao walikimbia zamani wakati wa vurugu za kwanza kati ya wahutu na watusi. Kuna mwingine professor rwakabamba naye alisomea tanzania.

      Katika record zake bunge la budget la rwanda baada ya Genocide alipo present budget ya wizara ya fedha haikueleweka kabisa...kwa most of MP's wa wakati huo ambao walipewa vyeo tu kwa ajiri ya either kupambana na vita vinginevyo..ilibidi afungue darasa bungeni...na project na writting board kwa ajiri ya kueleza budget nzima...na maana yake....
      Thanda likes this.
      Live Life so Well That even Death Loves to see you Alive.

    22. #20
      Pinokyo Jujuman's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 5th February 2012
      Posts : 511
      Rep Power : 470
      Likes Received
      64
      Likes Given
      5

      Default

      Quote By Skills4Ever
      Ulinzi wote huo wanaogopa peoplezzzz powerr hakuna lingine
      Mie nadhani ni woga wa Al shabab; ujue Arusha na hapa Kenya si mbali na hawa jamaa ni tishio, sidhani kama wanaeza kuwa wanawaogopa CDM kwani CDM si chama cha magaidi wala wahuni na wapenda vurugu"
      Thanda likes this.

    Page 1 of 3 123 LastLast

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...