Tanzania sasa limeibuka limbi la makampuni yanayojiita Recruitment Agents eg Epic, Rada recruitment,Erolink,Infinity communication,etc...wamekamata nafasi zote za kazi kwa makampuni binafsi kiasi kwamba vijana wa kitanzania wanaomalizia vyuoni kupata ajira imekuwa kama ndoto...ni mpaka upitie kwa haya makampuni ndio upate kazi.
matatizo ya haya makampuni ni kama yafuatayo.
1. WEZI- wanaibia vijana especially wale fresh from school.wanawapa kazi ngumu kwa mshahara mdogo na wenye makato yasiyoeleweka .
2. WABABAISHAJI- Mishahara hiyo midogo isiyoendana na viwango vya elimu za hawa vijana haileweki siku ya kutoka, mara tarehe 28,30,2,5 hata 15 ya mwezi mwengine.
3. UNDUGU/URAFIKI- Wanapeana kazi,vyeo na madaraka kiundugu,kirafiki yaani hamna haki inafuuatwa. mfano,unakuta Financial manager anadiploma ama ndio kwanza yupo chuo analipwa 1.6M -2M Wakati kuna kijana ana masters, postgraduate diploma au hata bachelor degree wanampa kazi ya customer care na mshahara laki 3?
4. HAWAJUI SHERIA ZA KAZI- Wanaajiri vijana kwa mkataba wa customer care wa mwaka mmoja,katikati wanampeleka kwenye post nyengine yenye kazi nyingi zaidi kwa mkataba ule ule.Ni elimu ndogo walionao viongozi wa haya makampuni kama Rada,Brightday au Infinity communication.
NINA MENGE ILA UKWELI NI KWAMBA HAYA MAKAMPUNI HAYANA FAIDA YOYOTE KWA VIJANA, NI WEZI, WANAHARIBU SOKO LA AJIRA NA KUSHUSHA KIWANGO CHA MISHAHARA NA UTENDAJI WA KAZI PIA, KAMA MFANYAKAZI HARIDHIKI NA MSHAHARA, MAZINGIRA YA KAZI HATOFANYA KAZI KWA MOYO MMOJA.
YAFUNGWE IKIWEZEKANA, HATUYAHITAJI.
WEZI

Reply With Quote

Follow Us Here