Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Live kutoka Diamond Jubilee: Utoaji tuzo kwa waandishi bora 2011 - JK Mgeni rasmi

    Report Post
    Page 6 of 6 FirstFirst ... 456
    Results 101 to 120 of 120
    1. #1
      Mathias Byabato's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 24th November 2010
      Posts : 589
      Rep Power : 552
      Likes Received
      163
      Likes Given
      90

      Default Live kutoka Diamond Jubilee: Utoaji tuzo kwa waandishi bora 2011 - JK Mgeni rasmi

      nitawapatia live update kutoka hapa Diamond Jubilee ambako muda mfupi ujao waandishi kadhaa nchini watatuzwa kwa kutambua mchango wao katika kuhabarisha jamii kwa mwaka 2011.

      pia atakuwepo mwandishi bora wa jumla ,huyu atalamba takribani sh milioni 7


      wageni wanaingia kwa wingi

      nadokezwa kuwa TBC1 watakuwa live


      Updates
      Najulishwa hapa kuwa pia Rais atatumia muda huo kutoa hotuba.
      Mwandishi bora wa jumla ni kati ya hawa-David Azaria (Habari Leo, Mwanza); Neville Meena (Mwananchi ,Dar ) Joseph Bura(TBC Taifa ,Dar) na Polycarp Machira(The Citizen ,Dar).


      Mshindi wa jumla ni Nevile Meena wa Mwananchi


      Mteule wa tuzo ya Maisha na mafanikio katika Uandishi wa habari ni Fil Karashan


      1.mpiga picha bora
      ni Khamis Said kutoka uhuru

      2.mchoraji bora wa kibonzo
      ni Nathan Mpangala
      alichora katuni iliyoonesha wabunge wakijongeza posho huku wanananchi wakisota

      3.Utawala bora gazeti
      Nevile meena-Mwananchi

      4.utawala bora tv
      emmanuel buohera-itv

      5.utawala bora radio
      Noel Thomson

      6.Habari za Malaria-Gazeti
      Audax Mutiganzi-Rai

      7.Habari Malaria-Radio
      Gelvas Hubile-TBC

      8.Mwandishi bora Michezo-gazeti
      Iman man
      9.Habari za michezo -radio
      Abdala Majura
      10.Habari za michezo Tv
      Anuary Mkama mliman tv

      11.Habari za Watu wenye ulemavu-gazeti
      David Azaria

      12.Watu wenye ulemavu -tv
      Lekoko-Channel ten

      13.Mwandishi wenye ulemavu-radio
      Tuma Dandi

      14.Jinsia -Gazeti
      Nasra Abdalah-Tanzania daima

      15.Habari za Ukimwi-Gazeti
      Elias Msuya

      16.Habari za UKIMWI-Radio
      Beatrice Nangawe

      17.Habari za Afya-gazeti
      Sharifa Karokola

      18.Habari za afya-radio
      Secilia Ndabageze

      19.Habari za mazingira-Gazeti
      Lukas Liganga

      20.Uchumi na biashara-Gazeti
      Polycap machira-The Citizen

      21.Uchumi na biashara-tv
      Aneth Andrew-TBC

      22.Habari za elimu-gazeti
      Erick Kabendera

      22.Habari za elimu-TV
      Victoria Patrick-TBC Dodoma

      23.Habari za elimu-radio
      Grace kihondo

      24.Habari za watoto-Gazeti
      Nashon Kenedy

      25.Habari za watoto TV
      nanganile mwakanjala

      26.Habari za watoto-radio
      Mchome

      27.Ifadhi za taifa-Gazeti
      Paul Swaurts-raia mwema

      28.Ifadhi za Taifa-radio
      Alex Magwiza-TBC Taifa

      29.Utalii wa ndani-Gazeti
      Monica Luhondo

      30.Utalii wa ndani-TV
      Juma Lugazi

      31.Maafa na migogoro-gazeti
      Daniel Mbega

      32.Maafa na migogoro- radio
      Joseph bura

      33.Habari za sayansi na technlojia
      bernad lugongo

      34.Habari za sayansi na technlojia-radio
      Abel onesmo mwende

      35.Tuzo za telecomunication -gazeti
      Nevile Meena

      36.Habari zenye mvuto mkubwa kwa watu
      Polycap Machira

      Hotuba ya Waziri Nchimbi

      mswada wa sheria mpya ya habari nchini itashirkikisha wadau.
      uhuru wa vyombo vya habari uko juu sana tz
      vyombo vya habari vifanye kazi kwa weledi
      anamuomba rais awe akikutana na jukwaa la wahariri mara moja kwa mwaka
      anamkaribisha rais kutoa hotuba

      Hotuba ya Rais Kikwete
      Serikali itatazama namna ya kuunga mkono kuendeleza utoaji tuzo

      Tumieni siku hii kupima sekta ya habari nchini

      Tasnia ya habati tz imepata mafanikio makubwa-kwa uhuru wa habari

      vyombo vya habari vimeiongezeka nchini

      Serikali itaendelea kudumumisha uhuru wa habari nchini

      wanahitajika waandishi wazalendo kwa nchi yao

      je ni lazima kila picha mnazopiga zichapishwe?

      pamoja na uhuru mlionao waandishi je ni lazima kuandika habari za uchochezi?

      pawepo mfumo mzuri wa kusimamia ajira na maslahi ya waandishi nchini

      kuna waandishi wengi nchini hawana ajira na walioajiriwa hawajui hatima yao

      mtu yoyote atakayewalipa watamtumikia

      sijui kama wamiliki wana taratibu za kuajiri watu wenye sifa

      wanastahili kupata ujira mzuri,hawatakiwi kuajiri wasiosomea fani husika

      kuwepo mfumo mzuri katika kuanzisha vyombo vya habari na mfumo mzuri wa ajira

      waandishi watazame namna ya kutetea maslahi yao

      waandishi zingatieni maadili kwa kuandika habari za kweli na uhakika

      mpate machungu ya wale mnaowasingizia

      serikali itajikita katika kukuza sekta hii hasa katika mafunzo

      kupitia sheria mpya serikali itawekla utaratibu wa kusomesha waandishi nchini

      serikali inataka kuwepo uandishi wa kubobea katika jambo fulani

      kuna waandishi wanajitahidi kuonesha kuwa nchi ya tz ni ya hovyo,wakati wanaishi humo humo

      wakati mwingine mambo ya kufadhiliwa tabu tu,wengine hawataki tupige hatua

      nitaunda tume ya katiba siku chache zijazo,naomba waandishi mtusaidie kuelimisha jamii
      Rais Kikwete amemaliza hotuba

      Nawashukuru sana, ninakwenda kupumzika saa 11:47 usiku

      Wenu
      M.Byabato
      Last edited by Mathias Byabato; 30th March 2012 at 23:46. Reason: updates
      Kama Wewe ni Mwandishi kweli,unaamini ,una uhakika na uliandikalo basi Onesha Jina,Sura yako- Jeneral Ulimwengu


    2. #101
      Smartboy's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th November 2010
      Posts : 1,005
      Rep Power : 641
      Likes Received
      99
      Likes Given
      3

      Default Re: Tuzo za waandishi wa habari.

      Naona baba riz anawatolea uchovu kina Saed kubenea.

    3. #102
      kimboka one's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 23rd January 2010
      Posts : 623
      Rep Power : 602
      Likes Received
      62
      Likes Given
      2

      Default Re: Tuzo za waandishi wa habari.

      radio afya ya mwanza imefanya vizuri

    4. #103
      Dark City's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 18th October 2008
      Location : Roaming
      Posts : 11,781
      Rep Power : 23601
      Likes Received
      7154
      Likes Given
      11578

      Default Re: Live kutoka Diamond Jubilee: Utoaji tuzo kwa waandishi bora 2011 - JK Mgeni rasmi

      TBC1 wamejitahidi kurusha live ila floor management imekuwa ya hovyo sana!!
      "WE ALWAYS DON'T CHANGE UNTIL THE COST OF STAYING THE SAME EXCEEDS THE COST OF CHANGE....LOOKING BEYOND THE 31 OKTOBA 2010 LANDMARK"

      Retired Maj Gen DC (1947)...[email protected]

    5. #104
      Mizizi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 8th March 2008
      Location : MAKETE
      Posts : 1,089
      Rep Power : 759
      Likes Received
      309
      Likes Given
      20

      Default Re: Tuzo za waandishi wa habari.

      analaumu waandishi kuandika mambo mabaya! Sasa kama mabaya ndio yanafanywa, mazuri yataandikwa kutoka wapi?

    6. #105
      PakaJimmy's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th April 2009
      Posts : 14,910
      Rep Power : 22570
      Likes Received
      6525
      Likes Given
      2933

      Default Re: Live kutoka Diamond Jubilee: Utoaji tuzo kwa waandishi bora 2011 - JK Mgeni rasmi

      HATIMAYE jk amsifia Babu wa Loliondo!
      Anasema anatibu magonjwa yooote sugu!
      "The only thing that walks back from the tomb with the mourners and refuses to be buried is the character of a man.
      What a man is, survives him... it can never be buried"
      (GENEKAI-Jamiiforums, 4th November 2010 07:32PM).
      [email protected]


    7. #106
      JOHN MADIBA's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 30th January 2011
      Location : KwaZulu-Natal-SOUTH
      Posts : 233
      Rep Power : 471
      Likes Received
      150
      Likes Given
      18

      Default Re: Live kutoka Diamond Jubilee: Utoaji tuzo kwa waandishi bora 2011 - JK Mgeni rasmi

      Neville Meena mshindi wa jumla hii ni makala yake
      NIMEKUWAPO Arumeru Mashariki kwa zaidi ya wiki mbili sasa, nikifuatilia kampeni za uchaguzi mdogo wa ubunge ambao umepangwa kufanyika Jumapili ijayo, Aprili 1, 2012.

      Kwa ujumla kampeni hizi zimekuwa za kistaarabu zaidi ikilinganishwa na zile za mwishoni mwa mwaka jana wilayani Igunga ambako pia kulifanyika uchaguzi mdogo na CCM kuibuka washindi kupitia kwa mgombea wake, Dk Dalaly Kafumu.

      Waandishi wa habari tunaoandika matukio ya kampeni hizi ndiyo tunaotizamwa na Watanzania wote kuwapa kile kinachotokea kwani si wote wanaoweza kufika Arumeru Mashariki, lakini kinyume chake tunatia aibu kiasi cha kutisha.

      Vyombo vya habari vinawajibika kwa umma wa Watanzania walio wasomaji wa magazeti yetu, wasikilizaji wa radio zetu na hata watazamaji wa luninga zetu.

      Jambo moja ni dhahiri kwamba katika hadhira hii ambayo ni wateja wetu wapo wenye itikadi mbalimbali, ziwe za kisiasa, kidini na nyinginezo lakini pia wapo wasiokuwa na itikadi zozote zile, wao ni Watanzania, wala hawafungamani na upade wowote. Wote hawa tunapaswa kuwatumikia.

      Nijuavyo mimi sisi tunaoripoti habari za uchaguzi haimaanishi kwamba bora zaidi kuliko waandishi wa habari wengine la hasha, bali tumeaminiwa kutenda kwa niaba ya wenzetu wengi ambao pia wana uwezo kama wetu.

      Kwa kifupi naweza kusema tuko zamu na pengine kukiwa na uchaguzi mwingine tunaweza kupewa zamu nyingine, au wakapewa wenzetu.

      Ni kwa bahati mbaya kwamba sisi tulioaminiwa kufanya kazi ya kuripoti habari za kampeni za Arumeru Mashariki tumejisahau, kiasi cha kufanya kazi ambazo si zetu. Tumeacha maadili namisingi ya kazi zetu, tumeingia katika ushabiki wa vyama jambo ambalo si hatari tu kwa mustakabali wa demokrasia ya nchi yetu bali hata kwa maisha ya taaluma ya habari nchini.

      Waandishi wa habari katika kampeni hizi matendo yetu yanawatia kuchefuchefu hata makada wa vyama vya siasa vinavyoshiriki uchaguzi, kwani tumechukua kazi zao na tumegeuka kuwa makada na wakereketwa wa siasa kuliko wao. Hii si kazi yetu.

      Uswahiba huu na vyama vya siasa umetufanya kushindwa hata kuandika ukweli wa kile kinachotokea kwenye mikutano ya kampeni. Tunafikia mahali pa kuweka makubaliano ya kijinga ya kuua habari kwasababu tu ya ukereketwa wetu, sijui hili kwa maslahi ya nani!.

      Tumejengea baadhi ya waandishi wenzetu uhasama wa hali ya juu kwa kuwa watoa taarifa kwa viongozi wa kisaisa, tukibaguana kwamba huyu ni wa chama fulani, si mwenzetu na yule ni mwenzetu si kwa misingi ya taaluma ya habari bali kwa misingi ya vyama tunavyoviandikia habari.

      Badala ya kuwaandikia Watanzania, wenye uchu na shauku ya kufahamu mchakato wa demokrasia unavyokwenda Arumeru Mashariki, basi tunaviandikia vyama vya siasa vinavyoshiriki, hili si sawa kabisa na halikubaliki.

      Hali hii imetufikisha pabaya kwani katika kampeni hizi wapo waandishi wa habari hawawezi kufika katika kambi za vyama vingine kwani wao wamejibagua tayari kwamba wanautumikia mlengo wa kushoto au mlengo wa kulia.

      Nasema hivi kwa mifano hai kwani wengine ‘tumeshtakiwa’ na waandishi wenzetu kwa wanasiasa hawa, kwamba eti tupo kwa ajili ya kuhujumu vyama fulani, lakini kwa hulka ya wanasiasa walivyo mwishoni mwa siku wanatufikishia taarifa hizi, na kuwataja wale waliopeleka ‘mashtaka’.

      Katika haya tumeruhusu hata wanasiasa kutupangia aina ya habari tunazopaswa kuziandika na kuzituma kwenye vyombo vyatu vya habari, hii ni aibu na fedheha kubwa kwa taaluma yetu na waandishi ambao tuna tabia za aina hii.

      Hatuwezi kuacha tabia za aina hii kuendelea, lazima tuchukue hatua kama wanataaluma kwani kuziacha ni sawa na kuiweka taaluma ya habari rehani.

      Kama walivyo Watanzania wengine, waandishi wa habari nchini tuna uhuru wa kuwa wananchama wa vyama vya siasa, kushiriki uchaguzi na kuwachagua viongozi katika chaguzi mbalimbali.

      Lakini lazima tujitambue kwamba, kitaaluma tunapaswa kuwa juu ya ushabiki wa siasa za vyama, kwani kwa kufanya hivyo tu ndipo tunaweza kutekeleza wajibu wetu kwa Watanzania kwa haki.

      Tunapofanya kazi kwa ushabiki na upenzi wa kupitiliza tujue kwamba hatuwatendei haki walaji wa habari zetu ambao kwao habari ni zaidi ya vyama, siasa na wanasiasa.

      Wakati wadau na wanataaluma wa habari tukiendelea kutafakari jinsi ya kuikwamua taaluma hii hasa tunapokwama kwenye mitego ya kisiasa iwe kwa kupenda sisi wenyewe au kwa sababu nyinginenezo, ni wajibu wa kila mwandishi wa habari ajitambue kwamba ana wajibu upi kwa umma.

      Vinginevyo basi anayedhani kwamba taaluma hii inambana asitekeleze mapenzi yake ya kisiasa iwe ni kwa chama ama kwingineko, ajiengue mapema kwani kuondoka si dhambi, wapo wengi wamefanya hivyo na maisha yanaendelea.
      BRAVE HEART, REALLY EVERY MAN DIE

    8. #107
      kimboka one's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 23rd January 2010
      Posts : 623
      Rep Power : 602
      Likes Received
      62
      Likes Given
      2

      Default Hongera REDIO AFYA FM kwa Tunzo Nyingi

      Hii ni redio changa inayoibukia vizuri sana ndani ya asasi isiyo ya serikali Tandabu ya jijini mwanza.ina vipindi vizuri na hasa vya afya ya binadamu,kupitia kipindi cha daktari wa zamu na vingine vingi.hakika wanastahili tuzo walipewa waandishi wake na baraza la habari Tanzania.jitaidini mfike nchi nzima hongera sana

    9. #108
      Bangoo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd November 2011
      Posts : 2,775
      Rep Power : 5801
      Likes Received
      452
      Likes Given
      0

      Default Re: Live kutoka Diamond Jubilee: Utoaji tuzo kwa waandishi bora 2011 - JK Mgeni rasmi

      kujenga barabara
      serengeti siungi
      mkono hata kidogo
      jamani mbuga hii
      maarufu mno
      duniani mnaweka
      barabara?!!. NASEMA
      BILA KUSITA JK
      Ni JANGA!!! Kuu.

    10. #109
      Yericko Nyerere's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 22nd December 2010
      Location : Kigamboni, DSM
      Posts : 4,956
      Rep Power : 23052
      Likes Received
      3007
      Likes Given
      315

      Default Re: Live kutoka Diamond Jubilee: Utoaji tuzo kwa waandishi bora 2011 - JK Mgeni rasmi

      Kilichonifurahisha ni kauli ya mh rais juu ya UJENZI wa baraba waliyozuia wakenya kuwa itajengwa tu!

    11. #110
      Mwanajamii's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 5th March 2008
      Posts : 7,085
      Rep Power : 1814
      Likes Received
      24
      Likes Given
      13

      Default Re: Tuzo za waandishi wa habari.

      rais amezungumzia uhuru wa vyombo vya habari kwa kuzingatia wajibu,ukweli na weledi

    12. #111
      Bangoo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd November 2011
      Posts : 2,775
      Rep Power : 5801
      Likes Received
      452
      Likes Given
      0

      Default Re: Live kutoka Diamond Jubilee: Utoaji tuzo kwa waandishi bora 2011 - JK Mgeni rasmi

      Wanyama wengi
      watagongwa kweli

    13. #112
      Mwanajamii's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 5th March 2008
      Posts : 7,085
      Rep Power : 1814
      Likes Received
      24
      Likes Given
      13

      Default Re: Tuzo za waandishi wa habari.

      waandishi waepuke uchochezi,amezungumzia maslahi na ajira kwa waandishi wa habari ili kuepuka kutumiwa na watu wenye nia zao zingine/maslahi binafsi

    14. #113
      Stoudemire's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 24th March 2012
      Posts : 317
      Rep Power : 428
      Likes Received
      65
      Likes Given
      237

      Default Re: Tuzo za waandishi wa habari.

      Mlitaka tuzo apewe nani Dr Slaa hahaha acheni hizo.Pongezeni panapostahili. Wenzenu wanajitahidi wapo juani wanaandika habari nyie mnasema hamna weledi. Hebu kuweni na ustaarabu kidogo.

    15. #114
      Mwanajamii's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 5th March 2008
      Posts : 7,085
      Rep Power : 1814
      Likes Received
      24
      Likes Given
      13

      Default Re: Tuzo za waandishi wa habari.

      hotuba ya rais ilikuwa fupi lakini yenye maneno ya busara sana kwa future ya tanzania

    16. #115
      Mwanajamii's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 5th March 2008
      Posts : 7,085
      Rep Power : 1814
      Likes Received
      24
      Likes Given
      13

      Default Re: Tuzo za waandishi wa habari.

      kazungumzia katiba mpya na mchakato unaoendelea

    17. #116
      Bangoo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd November 2011
      Posts : 2,775
      Rep Power : 5801
      Likes Received
      452
      Likes Given
      0

      Default Re: Live kutoka Diamond Jubilee: Utoaji tuzo kwa waandishi bora 2011 - JK Mgeni rasmi

      Ukiwa na akili
      ya maiti bwana!
      slaa anainngiaje
      hapa!!!?

    18. #117
      Godyp's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 20th October 2011
      Posts : 125
      Rep Power : 412
      Likes Received
      18
      Likes Given
      0

      Default Re: Live kutoka Diamond Jubilee: Utoaji tuzo kwa waandishi bora 2011 - JK Mgeni rasmi

      Wapi Jerrry Muro jaman!
      Ktk tuzo au category yake haipo?

    19. #118
      Mwanajamii's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 5th March 2008
      Posts : 7,085
      Rep Power : 1814
      Likes Received
      24
      Likes Given
      13

      Default Re: Live kutoka Diamond Jubilee: Utoaji tuzo kwa waandishi bora 2011 - JK Mgeni rasmi

      JK Kukabidhi Tuzo Za Waandishi Nguli Leo

      RAIS Jakaya Kiwete leo usiku amekuwa mgeni rasmi katika utoaji wa Tuzo za Umahiri wa Uandishi wa Habari Tanzania (EJAT) 2011 jijini Dar es Salaam tukio lililomalizika hivi punde .Mchakato wa kuwapata waandishi bora kwa mwaka jana ulianza Februari 6 hadi 11 mwaka huu kwa jopo la majaji tisa wakiongozwa na Jaji Mkuu Wanceslaus Mushi kupitia kazi zilizowasilishwa na waandishi ili kumpata mshindi.

      Majaji walioshiliki ni AttilioTigalile, Edda Sanga, Yusuph Omar Chunda, Pili Mtambalike, Purdenciana Temba, Mwazo Millinga, Bernadina Chalali na Anaclet Rwegayura
      Kazi ziliziwasilishwa na waandishi wa habari zilikuwa 772 idadi ambayo ilikuwa zaidi ya ile ya Mwaka 2009 ambazo zilikuwa 304 na Mwaka 2010 zilikuwa 437.

      Tuzo ambazo zilikuwa zinashindaniwa ni pamoja na habari za Elimu, Watu wenye ulemavu, Utalii wa ndani, Hifadhi za taifa, Malaria, Mchora katuni na Mpiga picha bora.

      Tuzo nyingine ni za uandishi bora wa Biashara na uchumi, michezo na utamaduni, mazingira, afya, watoto, Virusi vya Ukimwi na Ukimwi, Utawala Bora, Jinsia, Mawasiliano pamoja na Sayansi na Teknolojia.


    20. #119
      Lambardi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 7th February 2008
      Location : KITAANI ZAIDI
      Posts : 4,588
      Rep Power : 1813
      Likes Received
      666
      Likes Given
      0

      Default Re: Live kutoka Diamond Jubilee: Utoaji tuzo kwa waandishi bora 2011 - JK Mgeni rasmi

      Jamani ina maana watangazaji Clouds Media hawana wanachojua ??mbona kama kipindi chao cha michezo kiko juu sana na wanachambua sana sana....vigezo gani vinatumika?Shafii Dauda,Luambano,Jeff Leah mbona wanajitahidi sana ???hata mmoja?duu kazi ipo!!

    21. #120
      PrN-kazi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 5th February 2011
      Posts : 2,248
      Rep Power : 5370
      Likes Received
      307
      Likes Given
      4

      Default Re: Live kutoka Diamond Jubilee: Utoaji tuzo kwa waandishi bora 2011 - JK Mgeni rasmi

      ...wana habari anzeni maandalizi mapema ya kihabari ili kwenye tuzo zijazo kila mtu atunukiwe kulingana na kazi yake maana wahenga wanasema ''MBUZI ANAKULA KULINGANA NA UREFU WA KAMBA YAKE''

    Page 6 of 6 FirstFirst ... 456

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...