TiGo Says
    Show/Hide This

    Topic: Kisa cha kusikitisha hivi kwa nini jeshi la polisi linafanya hivi?

    Report Post
    Results 1 to 10 of 10
    1. #1
      EasyFit's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 4th July 2011
      Posts : 816
      Rep Power : 510
      Likes Received
      561
      Likes Given
      191

      Default Kisa cha kusikitisha hivi kwa nini jeshi la polisi linafanya hivi?

      JESHI la Polisi nchini limeingia katika kashfa nyingine baada ya kijana Charles Patrick Paulo mkazi wa kijiji cha Mundemu wilayani Bahi mkoani Dodoma kulishushia tuhuma nzito za kupora fedha na kumbambikia kesi ya unyang’anyi.

      Kesi hiyo iliyoendeshwa kasi ilimtupa jela miaka 15 kabla ya kuachiwa huru miezi sita baadaye
      baada ya kushinda rufaa.

      Julai 20 mwaka jana, Paulo alitiwa hatiani na Hakimu wa Mahakama ya Mwanzo Mundemu
      F. Bulyota kwa shitaka la unyang’anyi kifungu namba 286 K/A Sura 16 na kutupwa jela kwa miaka 15.

      Hukumu hiyo ilianzisha safari mpya ya maisha kwa kijana Paulo ambaye aliachana na maisha ya uraiani akimuacha mchumba wake, Upendo Masila akiwa na ujauzito wa miezi miwili huku
      yeye akipelekwa katika Magereza ya Isanga kuanza kutumikia kifungo chake.

      Lakini kwa vile alijua kuwa hukumu yake imetokana na uonevu wa Polisi, wiki moja baadaye
      kijana Paulo aliwasilisha rufani yake kwa Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya ya Dodoma akipinga hukumu hiyo, rufani ambayo ilizaa matunda Januari 26 mwaka huu, pale Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Wilaya ya Dodoma, R.M Ngimilanga alipotoa hati ikiamuru
      kijana huyo kuachiwa huru mara moja.

      “Siku ya tarehe 20/07/2011 – Charles S/O Patrick Paulo Mshitakiwa katika jinai 52/2011 alifikishwa/ kutiwa hatiani mbele ya F.

      Bulyota Hakimu Mahakama ya Mwanzo – Mundemu kwa shitaka la unyang’anyi K/F 286 K/A
      Sura 16, jela miaka kumi na mitano (15)... “Hati hii inakuamuru wewe Ofisa wa Gereza kumwachia huru Charles S/O Patrick Paulo.

      Hati hii imetolewa kwa amri yangu na Mhuri wa Mahakama ya Wilaya leo tarehe 26/01/2012,” inasema hati hiyo ya kifungo baada ya rufaa ambayo inamfanya Paulo kurejea uraiani akimkuta mchumba wake Upendo akiwa tayari amejifungua mtoto Februari 2, mwaka huu, mtoto aliyebatizwa jina la Rogers.

      “Mchumba wangu amejifungua lakini sijawahi kumuona mtoto wangu naogopa kwenda
      kijijini Mundemu maana polisi wanasema wanataka kunipoteza kwa kuniua najua wataweza
      kwani walinibambikia kesi ya unyang’anyi nikahukumiwa miaka 15 jela lakini Mungu amenisaidia nimetoka….lazima sasa niwe makini,” anasema kijana Paulo ambaye sasa amegeuka kuwa mkimbizi ndani ya nchi yake mwenyewe akiishi kwa kujificha jijini Dar es Salaam.

      Mkasa wenyewe
      Akizungumza katika ofisi za gazeti hili jijini Dar es Salaam, wiki hii Paulo anasema kisa na mkasa wa sakata lake na Jeshi la Polisi vilianzia katika kijiji cha Kongogo wilayani Bahi alikokwenda kufanya biashara ya mnadani akiuza mitumba na nyama ya ng’ombe.

      Anasema baada ya kumalizika kwa mnada huo uliofanyika Desemba 12, 2010, alikwenda pembeni kidogo ya eneo la mnada kwenye kichaka na kujisaidia haja ndogo.

      Anasema baadaye alitoa fedha zake Sh 470,000 taslimu alizokuwa nazo awali na Sh 150,000
      za mauzo ya mitumba na kuzificha ndani ya bukta ili kuepusha kuibiwa.

      “Mara baada ya kuzificha fedha zangu ndani ya bukta walikuja polisi wawili. Kwanza walinihoji
      kwanini najisaidia vichakani, nikawajibu mara nyingi sehemu za minada huwa tunafanya hivyo
      kutokana na ukosefu wa vyoo.

      Hata hivyo walinipiga piga makofi mgongoni na kunitaka nipotee.

      “Kwanza nilianza kukimbia kwa kwenda vichakani lakini baadaye nikashituka kwamba kule
      hakukuwa na usalama nikaamua kurudi nilipotoka lakini polisi wale walikuwa wakinikimbiza na
      pikipiki. Baadaye niliamua kusimama… walipofika waliniuliza kwanini narudi kule mnadani
      tena, nilitaka kuwajibu walinipiga na kitako cha bunduki nikaanguka na kupoteza fahamu.

      “Nilipopata fahamu nilikuta wamenibeba kwenye pikipiki nikiwa katikati yao huku mkono
      wangu mmoja wakiwa wameufunga pingu ambayo ilikuwa pia imefungwa kwenye bomba la
      pikipiki. Niliwauliza walikuwa wananipeleka wapi…wakasema wanajua wao. Mwendo mfupi
      mbele waliniuliza kama waende na mimi au waniachie… niliomba waniachie, wakaniachia.”

      Alisema baada ya kufika nyumbani (Mundemu) aliamua kwenda hospitali lakini alishindwa
      kutibiwa akiagizwa kwanza kuwa na fomu ya matibabu (PF 3) kutoka Polisi. Anasema baadaye
      alipewa fomu hiyo na kutibiwa.

      “Baada ya matibabu nilianza kufuatilia suala hili. Nilianzia Polisi Mkoa kwa Kamanda wa
      Polisi wa Mkoa (RPC), Ofisa Malalamiko wa Mkoa na hata Polisi Wilaya ya Bahi. Nilifuatilia
      mara nyingi sana lakini nilikuwa napigwa danadana huku na kule… wale polisi baada ya
      kuona nawafuatilia sana walianza vitisho na kuniambia watanibambikia kesi nifungwe nipotee.

      “Baada ya kufuatilia sana baadaye Mkuu wa Polisi wa Wilaya ya Bahi (OCD) aliitisha gwaride la
      utambuzi kwa askari wake wote na nilifanikiwa kuwatambua askari walionipiga na kunipora
      fedha. OCD alianza kufuatilia suala hilo kwa kunitaka nilete mashahidi na nilifanya hivyo
      mara kadhaa bila kupewa haki yangu.”

      Alisema wakati akiendelea kufuatilia suala hilo, ghafla usiku wa Julai 18, kuamkia Julai 19, mwaka huu saa tisa usiku akiwa amelala nyumbani kwake walikuja watu kutoka ofisi ya Ofisa Mtendaji na kudai kuwa nimetajwa kuhusika katika tukio la uhalifu.

      “Asubuhi Julai 29, 2011 nilipandishwa kizimbani nikasomewa mashitaka na nilimuona huyo
      mama anayesema nilimvamia nyumbani kwake usiku huo nikiwa na wenzangu watatu na kupora mali zake na fedha. Cha ajabu sikuona hao wengine ninaoambiwa nilikuwa nao.

      Nilipohoji walisema walikuwa wamenitambua mimi ingawa walisema tulikuwa tumevaa soksi
      usoni.

      “Hakimu alinisomea mashitaka yangu na akamwambia mlalamikaji kuleta mashahidi
      wake. Mimi niliomba nipewe muda nilete mashahidi wangu kwa vile wengi walikuwa
      wamekwenda mnadani lakini kwa bahati mbaya kesho yake Julai 20, 2011 nilihukumiwa kifungo cha miaka 15 jela.

      “Hata hivyo pamoja na kuhukumiwa lakini nilisikitishwa na hatua ya polisi waliokuwa
      wakinipeleka gerezani kwa pikipiki wakiwa na mgambo kunifunga pingu na kunining’iniza
      mtini porini na kuanza kunichapa fimbo wakisema ni kutokana na kunikomesha kwa kujifanya
      mjanja,” alisema Paulo.

      Akizungumzia madai hayo, Ofisa Malalamiko wa Polisi Mkoa wa Dodoma SSP Pancras Mdimi
      alikiri kupokea jalada la Paulo na kusema kuwa limerudishwa Polisi Wilaya ya Bahi ambapo
      kesi yake ilipoanzia.

      Alisema kuwa, baada ya jalada hilo kuletwa likiwa halina hati ya mashtaka na nakala ya hukumu ambapo awali faili hilo liliitishwa baada ya mlalamikaji kuleta malalamiko yake.

      Mdimi alisema kuwa, hata mlalamikaji ambaye kwa sasa yuko Dar es Salaam alipotakiwa
      kuleta mashahidi kuhusiana na malalamiko yake alisema kuwa hawezi kumudu kuleta mashahidi hao kutokana na gharama.

      Hata hivyo alisema kuwa, watashughulikia madai ya mlalamikaji baada ya kupata faili
      kutoka Polisi Wilaya ya Bahi.

      "Mambo mengi yalikuwa hayajakamilika ndiyo maana faili lake halikushughulikiwa kabisa,"
      alisisitiza Mdimi.

      Kwa upande wake, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma Zelothe Stephen alipohojiwa na
      gazeti hili alimtaka Charles afuate utaratibu wakati shauri lake likishughulikiwa.

      "Afuate utaratibu aende pale kesi inapohusika kwa nini anatangatanga wakati shauri lake
      linashughulikiwa?" alihoji Kamanda Zelothe.

      Alisema kuwa, ni vizuri kama mtu huyo angefuata utaratibu kusubiri hatma ya madai yake.

      Hata hivyo kijana huyo ameliambia gazeti hili hawezi kutokana na watuhumiwa katika shauri hilo kuwapo huko na anaogopa safari hii haitakuwa kifungo bali kifo.
      Waberoya likes this.


    2. #2
      flora msoffe's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 28th October 2010
      Location : under a coconut tree
      Posts : 3,282
      Rep Power : 1038
      Likes Received
      300
      Likes Given
      133

      Default Re: Kisa cha kusikitisha hivi kwa nini jeshi la polisi linafanya hivi?

      Kwa unji hii yapo mengi sana kama haya lakini habari hatuzpati! ,afadhali na sku hizi vyombo vya habari vipo zamani..... Mmmh

    3. #3
      Pawaga's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 14th February 2011
      Posts : 255
      Rep Power : 418
      Likes Received
      24
      Likes Given
      0

      Default Re: Kisa cha kusikitisha hivi kwa nini jeshi la polisi linafanya hivi?

      makubwa,2taisha cjui

    4. #4
      Idimulwa's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th May 2011
      Posts : 1,063
      Rep Power : 568
      Likes Received
      294
      Likes Given
      140

      Default

      So sad...aiseeee!!

    5. #5
      Waberoya's Avatar
      JF Premium Member Array
      Join Date : 3rd August 2008
      Location : Busia-Uganda
      Posts : 5,773
      Rep Power : 1655
      Likes Received
      1372
      Likes Given
      2560

      Default Re: Kisa cha kusikitisha hivi kwa nini jeshi la polisi linafanya hivi?

      du so sad, sasa hao polisi wamechukuliwa hatua gani?? unajua kuua kwa uonevu kama huu kumbe kazi rahisi sana aisee!
      Hakuna msafi CCM, hakuna hata mmoja,..wote wamepotea hivyo wamepoteza utukufu wa uzalendo na upendo kwa taifa hili, na kupoteza sifa ya uraia

    6. #6
      Mkulima wa Kuku's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 13th January 2011
      Posts : 296
      Rep Power : 430
      Likes Received
      91
      Likes Given
      1

      Default

      Quote By Ng'wana Sweke View Post
      So sad...aiseeee!!
      Unaweza kuona wazi wale wanaodai afuate utaratibu ni kufunika ili jamaa ashindwe hizo taratibu waonekane hawana hatia. Nchi hii na jeshi la polisi ni rushwa tu hata wajitetee vipi

    7. #7
      Idimulwa's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th May 2011
      Posts : 1,063
      Rep Power : 568
      Likes Received
      294
      Likes Given
      140

      Default

      Quote By Mkulima wa Kuku View Post
      Unaweza kuona wazi wale wanaodai afuate utaratibu ni kufunika ili jamaa ashindwe hizo taratibu waonekane hawana hatia. Nchi hii na jeshi la polisi ni rushwa tu hata wajitetee vipi
      Mkuu Mkulima wa Kuku...inasikitisha sana...Yaani maisha ya mtu yanaharibiwa kisa shilingi laki 6!!Polisi walikuwa 2...kwa hiyo kila mmoja alikunja laki 3...sasa hii ni hela gani sasa...mpaka iwasukume kufanya unyama huu!!...Ama kweli hizi ni nyakati za mwisho.

    8. #8
      Inkoskaz's Avatar
      JF Premium Member Array
      Join Date : 6th November 2010
      Location : URT
      Posts : 3,482
      Rep Power : 1821
      Likes Received
      662
      Likes Given
      407

      Default Re: Kisa cha kusikitisha hivi kwa nini jeshi la polisi linafanya hivi?

      polisi wa tanzania wana matendo zaidi ya al shabab

    9. #9
      Inkoskaz's Avatar
      JF Premium Member Array
      Join Date : 6th November 2010
      Location : URT
      Posts : 3,482
      Rep Power : 1821
      Likes Received
      662
      Likes Given
      407

      Default

      Quote By Waberoya View Post
      du so sad, sasa hao polisi wamechukuliwa hatua gani?? unajua kuua kwa uonevu kama huu kumbe kazi rahisi sana aisee!
      Huyo jamaa aende kule LHRC kwa kina kiwanga wamsaidie.jeshi linafuga wahuni

    10. #10
      Daudi mchambuzi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 25th November 2010
      Posts : 2,685
      Rep Power : 1164
      Likes Received
      1379
      Likes Given
      9134

      Default Re: Kisa cha kusikitisha hivi kwa nini jeshi la polisi linafanya hivi?

      Hili ni moja kati ya matukio 1000 yanayofanywa na askari wa jeshi la polisi.
      Iko hivi, kuna jamaa nilipata kusoma naye kitambo na sasa ni polisi kitengo cha FFU.
      Juzi polisi huyu kaniambia kuwa, huwa anakodisha silaha yake kwa majambazi wakati wa lindo usiku (hasa akipangwa bank) na asubuhi hurejeshewa silaha yake na kitita cha laki mbili mpaka tatu kutoka kwa majambazi hayo.
      Hakuishia hapo, polisi huyo alizidi kunidokeza kuwa wanapoishiwa na pesa za matumizi huwa wanachukua silaha wakati wa lindo mida ya jioni na kuvaa makoti makubwa kama raia na kuvamia maduka makubwa ya biashara za jumla wakati wa kufunga na kutishia kwa silaha hizo za jamuhuri na kupora fedha kutoka ktk duka husika.
      Polisi wetu wakiwa huko mafunzoni hufundishwa utii wa uwoga na wanapewa treatment mbaya sana kiasi cha kuwafanya kuwa na roho mbaya na ya kikatili badala ya kuwa waaminifu na watii wa sheria.
      Mafunzo ya ukatili wanayofundishwa askari wetu yanawafanya walinzi hawa wa usalama wa raia na mali zao kugeuka na kuwa majambazi kwa kujaribu kujikwamua kwenye umaskini kwa kutumia ukatili uleule waliofunzwa huko CCP.
      Askari anayelipwa laki mbili unusu kwa kazi ya kulinda bank yenye billions of money lazima awe mwizi.
      Kwa kifupi polisi ndo wezi hapa tanzania.
      "Tupo ktk kipindi cha majaribu, tuweke jazba pembeni kisha tutafakari ili tufanye maamuzi sahihi na dunia itambue CHADEMA ni chama makini." BY Mh. Freeman MBOWE

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...