Ban Kimoon kaamua kuweka wazi matakwa ya taasisi yake kuwa ushoga utambuliwe katika nchi za Africa kwani wamechoka sasa na msimamo wa miaka mingi wa Africa kutotambua haki za mashoga.
African Union: Ban Ki-moon urges respect for gay rights
Sikubaliani na ushoga lakini nampa pongezi Ban Kimoon kutokuwa mnafiki kwa hilo ambalo ni dhahiri linalosimamiwa na taasisi yake.
Ban Kimoon amekuwa bosi wa Dr. Asha Rozi Migiro kwa miaka kadhaa katika hiyo taasisi yake. Tuliposhangilia Migiro kupata post ile basi haya anayotamka bosi wake ndiyo yaliyotakiwa yasisitizwe na taasisi nzima ambayo Migiro ni second in command.
Sijawahi kusikia waandishi wakimuuliza Dr. Asha Migiro kuhusu ushoga ambao bosi wake leo kaamua kutupasulia jipu. Mimi nadhani huu ni wakati wa waandishi wambane huyu mama tujue utekelezaji wake lilipokuja suala la ushoga kwenye kipindi chote alichokaa na Ban Kimoon na taasisi yake.
Ieleweka kuwa kumwuliza Dr. Asha Migiro si kumdhalilisha kwani hata Waziri Mkuu ameulizwa swali hilo bungeni akajibu kuwa "hata wanyama hawafanyi hivyo".
Hivyo thread yangu nategemea idumu.

Reply With Quote
Follow Us Here