Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Je vita ya wakuu wa mikoa na wananchi, wakuu wa mikoa wataiweza?

    Report Post
    Results 1 to 3 of 3
    1. #1
      Fasta fasta's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 15th February 2011
      Posts : 421
      Rep Power : 507
      Likes Received
      75
      Likes Given
      158

      Default Je vita ya wakuu wa mikoa na wananchi, wakuu wa mikoa wataiweza?

      Ndugu watanzania mliopo hapa Jf ninadhani kitendo cha wakuu wa mikoa naJeshi la Polisi na Mahakama kudhulumu haki za watanzania ni kitendo cha kulaani mpaka kufa. Huu ubaguzi wa aliye nacho na asiekuwa nacho utaendelea mpaka lini? Mababu na mabibi zetu, na baba na mama zetu walivumilia sana kwa kunyimwa elimu, na sisi tuseme basi na wao CCM sasa watuvumilie.

      Tunajitahidi kusomesha vijana wetu leo kufa na kupona ili wafanye nini, tujiulize,kama mashirika yamekufa na makampuni yote ya serikali na bado vijana wanahangaika kufungua maduka mikononi, kutembea na maduka mikononi serikali isiyokuwa na haya inakwenda kuwafetulia risasi, kuwapiga mabomu, na wasivyokuwa na utu, ubinadamu na akili zao zenye ndoto yakupenda madaraka wanawamwagia raia wenzao maji ambayo wanajua yanamadhara, yana sumu yakiingia mwilini. Sasa ni najiuliza vijana wetu wafanye nini ili wapate kipato kama watu wengine.

      Hii serikali inajivunia nini kwa taifa letu leo hii ndugu zangu. Tunajua ya kuwa Tanzania tuna vitu vingi tu ambavyo serikali ingetilia maanani tungekuwa mbali kuliko hata Kenya. Nikitoa mfano tulikuwa na mashirika ya umma ambayo serikali isingekuwa legelege kuyaongoza haya matatizo tunayoyaona leo yasigekuwepo vijana wengi wangekuwa na ajira.

      Leo hii hakuna hata shirika moja linalosifika hapa Tanzania, yote ni marehemu imebaki mifupa wamechukua ile minofu yote, halafu tukiuliza tunaambiwa tunavunja sheria. Pamoja na majonzi yote ya maisha magumu kwa watanzania, wakuu wa mikoa wanatutangazia ya kuwa ndio wamekabidhiwa nchi, kuliko hata yule aliyechaguliwa na wananchi, wakati haya mashirika yalifia mikononi mwao wakiwa wanaangalia,leo wanatuambia ni wakuu wa kamati ya maadili ya kupambana nawananchi wanapotafuta haki yao, ni kwa nini wasigepambana na serikaliya CCM kuuliza ajira za hawa vijana?


      Tunaombakila mkoa uliokuwa na shirika waaze kudai ili na sisi tuweze kupataajira kama wao na akina Rejea walivyopata ajira humu JF.
      Last edited by Fasta fasta; 12th November 2011 at 19:59.
      Kinyungu likes this.


    2. #2
      Laptani's Avatar
      Member Array
      Join Date : 30th September 2009
      Location : Arusha
      Posts : 83
      Rep Power : 511
      Likes Received
      12
      Likes Given
      2

      Default Re: Je vita ya wakuu wa mikoa na wananchi, wakuu wa mikoa wataiweza?

      Mi naona siasa zimewatawala badala ya ethics za administration.
      Kwa mfano mikoa ya Arusha na Mbeya, MaRC wamekosea kuanza kwa ubabe.
      Hii mikoa haitishiwi nyau bana, aende kule pwani kwa waswahili unamchimba mtu biti anagwaya, mikoa hii ni ya wagumu, unapiga mkwara wanakupa advertise namna watakavyo react na wewe saa ikifika.
      Kandoro muulize mzaliwa Mwakipesile hiyo ngoma inachezwaje na Bwana Magessa Arusha si mchezo uliza wenzio waliopita kama mzee Shirima, we hata manispaa inatosha kukunyima ucingizi, badilikeni, ongozeni. Kwa ubabe hamtoboi!!!??
      Fasta fasta likes this.

    3. #3
      Fasta fasta's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 15th February 2011
      Posts : 421
      Rep Power : 507
      Likes Received
      75
      Likes Given
      158

      Default Re: Je vita ya wakuu wa mikoa na wananchi, wakuu wa mikoa wataiweza?

      Quote By Laptani View Post
      Mi naona siasa zimewatawala badala ya ethics za administration.
      Kwa mfano mikoa ya Arusha na Mbeya, MaRC wamekosea kuanza kwa ubabe.
      Hii mikoa haitishiwi nyau bana, aende kule pwani kwa waswahili unamchimba mtu biti anagwaya, mikoa hii ni ya wagumu, unapiga mkwara wanakupa advertise namna watakavyo react na wewe saa ikifika.
      Kandoro muulize mzaliwa Mwakipesile hiyo ngoma inachezwaje na Bwana Magessa Arusha si mchezo uliza wenzio waliopita kama mzee Shirima, we hata manispaa inatosha kukunyima ucingizi, badilikeni, ongozeni. Kwa ubabe hamtoboi!!!??
      Mkuu,
      Hapa tulipofikia kwa hizi siasa uchwara za CCM hatuwezi kuvumilia. Wao wanajua ya kuwa wametufikisha hapa lakini bado wanazububu kutoa amri ili watu wafungwe mdomo. Kama walikuwa wakuu wa kamati ya maadili waliruhusu vipi hizi mali za watanzania zikaendeshwa kizembe.

      Bado niya yangu ipo palepale mikoa ishirikiane kudai haya mashirika waliyokuwa nayo. Nimefurahishwa sana na mbeya walivyokuwa wawazi bila kutafuna walivyotaka mkurugezi aridishe pesa zao za maji.

    Similar Topics

    1. Honoraria za wakuu wa mikoa na wilaya
      By Kiti in forum Habari na Hoja mchanganyiko
      Replies: 1
      Last Post: 20th September 2011, 19:28
    2. Wakuu wapya wa Mikoa waapishwa
      By Bongo Pix Blog in forum Habari na Hoja mchanganyiko
      Replies: 0
      Last Post: 16th September 2011, 18:51
    3. Wakuu wa MIKOA/WILAYA Wanajeshi
      By mwanamasala in forum Jukwaa la Siasa
      Replies: 1
      Last Post: 25th November 2009, 09:32
    4. Wakuu wa mikoa wapanguliwa
      By Nsaji Mpoki in forum Jukwaa la Siasa
      Replies: 68
      Last Post: 18th April 2009, 13:20

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...