Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Walemavu kupanda mlima kilimanjaro

    Report Post
    Results 1 to 3 of 3
    1. #1
      Steven Sambali's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 31st July 2008
      Location : Warsaw, Poland
      Posts : 198
      Rep Power : 590
      Likes Received
      32
      Likes Given
      193

      Default Walemavu kupanda mlima kilimanjaro

      WanaJamii,
      Kuna watalii wasio wa kawaida na kwa sasa niandikavyo ni kuwa wapo tayari Tanzania. Wapanda mlima hao walifikia Kenya na huko wakapokelewa na makamu wa rais wa Kenya. Leo jioni kutokana na News ni kuwa tayari wameshafika Tanzania na wamefikia Arusha. Wameshangazwa na baridi ya pale kwani wao wanafikiri Africa ni Sahara tu. Safari yao imeandaliwa na Mama mmoja ambaye ni Actor aitwaye Anna Dymna. Lengo la safari ni kuja Tanzania na kupanda mlima Kilimanjaro.
      Nisingeandika hii habari kama si kwamba, wapandaji wote ni vilema. Wengine hawana macho (Vipofu), wengine hawana mikono na wengine miguu. Katika hawa kuna bwana mdogo mmoja aitwaye Jan Mela ambaye na yeye ni kivutio kikubwa. Alikatwa mkono mmoja baada ya kuwa amenaswa na umeme. Pamoja na ulemavu huo, alijitahidi na kwenda na mwisho kufika kwenye POLE zote yaani North Pole na South Pole. Baridi la huko kwa kweli latisha.
      Naandika ili kama kuna wahusika basi wachangamkie hili tukio kwani ni tangazo kubwa sana la utalii kwa Tanzania. Waandishi wa habari na wizara husika fuatilieni na muone twaweza watumiaje hawa vilema wapandao Kilimanjaro yetu. Mungu Ibariki Tanzania.

      Kwa watao taka maelezo zaidi basi angalieni kurasa hizi. Ila zimeandikwa Kipolishi na itabidi mjaribu kutafasiri kwa kutumia Google.

      FOTO

      Wahusika wote wanaonekana hapa pamoja na maelezo yao kwa ufupi.

      Kilimandżaro 2008 – Mimo Wszystko - Uczestnicy

    2. Miaka 50

    3. #2
      Tonga's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 8th July 2008
      Posts : 175
      Rep Power : 590
      Likes Received
      0
      Likes Given
      0

      Default Re: Walemavu kupanda mlima kilimanjaro

      Its amazing what people can do regardless their dissabilities, we should always thank God for everything; including a nice day.
      ";)We all have 24 hrs each day, how we use them makes the difference btwn SUCCESS & FAILURE"

    4. #3
      Steven Sambali's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 31st July 2008
      Location : Warsaw, Poland
      Posts : 198
      Rep Power : 590
      Likes Received
      32
      Likes Given
      193

      Default Re: Walemavu kutoka Poland kupanda mlima kilimanjaro

      Quote By Tonga
      Its amazing what people can do regardless their dissabilities, we should always thank God for everything; including a nice day.
      Tonga,
      Ukiangalia katika hao, huyu bwana mdogo Jan Mela (John), hizi safari za kwenda North na South Pole zilimfanya awe maarufu sana na kumpa kujiamini katika maisha. Ulemavu wake sasa anaona ni kama faida. Ni sawa na wale wanaooenda kwenye michezo ya Olympic, wakirudi huwa wamebadilika sana ki-akili. Katika hao, yule kipofu watu walimuuliza kabla hajaondoka kuwa sasa na wewe kipofu kwa nini wataka kwenda kupanda mlima Kilimanjaro wakati huoni? Akasema kuwa tatizo siyo kuona ila kusikia sauti za huko, hali ya hela ya huko, kuvuta pumzi kwenye paa la Africa na kuisikia mwilini baridi ya huko. Naona ile kufika tu Africa kwake ilikuwa ni furaha kubwa sana. Huyo mama Anna Dymna anasema watakwenda wote na kurudi wote. Mmoja wao akikwama kwenda juu zaidi basi ndiyo utakuwa mwisho wa kupanda mlima.
      Katika maisha nimejifunza kitu kimoja. Huwa najitahidi nisilaani kwa nini tukio fulani limenikuta. Maana siku zinavyokwenda huwa ninaanza kumshuru Mungu kwa kunisababishia tukio hilo kwani aliniokoa kwa janga fulani. Yep, tumshukuru Mungu kwa kila jambo, liwe baya au zuri, Amen.

    5. RukaaJuu Final

    Similar Topics

    1. Ni muda gani mwanaume unatakiwa kumaliza kupanda mlima?
      By AZIMIO in forum Mahusiano, mapenzi, urafiki
      Replies: 34
      Last Post: 16th June 2011, 10:18
    2. Jamani nataka kupanda Mlima Kilimanjaro, naombeni msaada
      By sekulu in forum Business & Economic Forum
      Replies: 9
      Last Post: 6th June 2011, 10:17
    3. Celtel yamdhamini Mwinyi kupanda Mlima Kilimanjaro
      By MziziMkavu in forum Habari na Hoja mchanganyiko
      Replies: 2
      Last Post: 5th July 2009, 00:40
    4. Mlima Kilimanjaro wazua mzozo
      By X-PASTER in forum Habari na Hoja mchanganyiko
      Replies: 9
      Last Post: 27th September 2008, 03:22
    5. Replies: 5
      Last Post: 15th June 2008, 23:54

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...