
By
Jasusi
Hayo ndiyo maswali aliyokuwa anajiuliza Mwalimu Nyerere. Afrika bado ni chanzo cha mali ghafi rahisi za kuendesha Ulaya. Na hiyo hiyo Benki kuu ya dunia ndiyo iliyokuwa inamshauri Mwalimu asiwekeze kwenye elimu, ili tubaki duni, na asiwekeze kwenye afya, ili tuendelee kufa at the age of 40 na watoto wetu wakifa kabla ya kufikia umri wa miaka 5. Mwalimu alikataa. Mwinyi alipoingia akaanza kutekeleza maagizo ya World Bank, IMF matokeo yake tukatoka 85% literacy rate na kushuka kufikia 60%. Hivi leo nadhani tumeshafika asilimia 70% ya Watanzania hawajui kusoma na kuandika na Kikwete anajisifia kwa shule za kata ambazo kuna mwalimu mmoja kwa wanafunzi 120. Umeuliza maendeleo ni nini. Kwa maliasili tulizo nazo ningependa kuona Tanzania tuna shule nzuri, tuna huduma nzuri za afya, tunapunguza matumizi ya mkaa wa miti kwa nishati yetu na kutumia zaidi gesi tuliyo nayo na nishati ya jua, upepo etc. Ningependa kuona Watanzania tukivaa nguo nzuri, na siyo mitumba. Sisi tunazalisha pamba. Siyo lazima tuwe kama Marekani au Ulaya. Lakini tunaweza kuinua kiwango cha maisha ya raia wetu kwa kuwawezesha kuachana na nyumba za matope na makuti na kujenga nyumba za kisasa. Kwa nchi iliyo na dhahabu na madini mengineyo sioni sababu kwa nini katika miaka 20 ijayo hatuwezi kufikia living standards za Dubai au Saudi Arabia.
Asante sana Jaasusi kwa mchango wako, kwa kweli umejibu swali langu (ingawa bado kuna majibu mengi sahihi kwa swali hili). Nikikusoma vizuri, maendeleo yanatakiwa kuendeleza binadamu, na sio taasisi, Pia maendeleo ni utunzaji wa mazingira. Ila nataka kuelewa maendeleo hayo yatazalishwa na nini? sioni jibu la kuelekea upande wa nchi na uchumi...
Nataka pia kuongeza ufafanuzi wa Mwalimu kuhusu maendelo ili watakao kusoma na watakao changia wautumie kwa kuelewa/kuelewesha points:"Development is a process which enables human beings to realize their full potential, build self confidence and lead lives of dignity and fulfillment. It is a process which frees people from fear, of want and exploitation. It is a movement away from political, economic or social oppression. Through development, political Independence acquires its true significance" South Comission, headed by Julius K. Nyerere (collection of Nyerere speeches: 1966-1968)
Yeye pia anaweka msisitizo kwenye "uhuru" na "dignity, fulfillment" ila hajasema hivyo vitu vitapatikanaje bila uchumi kuhusishwa...
Follow Us Here