Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Profesa Wangari Maathai afariki dunia

    Report Post
    Results 1 to 7 of 7
    1. #1
      joseeY's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 4th November 2010
      Location : Small village
      Posts : 103
      Rep Power : 457
      Likes Received
      15
      Likes Given
      3

      Default Profesa Wangari Maathai afariki dunia

      MSHINDI wa Tuzo ya Amani ya Nobel kutoka Kenya, Profesa Wangari Maathai, amefariki dunia katika Hospitali ya Nairobi alikokuwa akitibiwa ugonjwa wa saratani. Maathai, aliyeshinda tuzo hiyo mwaka 2004, alikuwa mwasisi wa Shirika la Mazingira Kenya. Mkurugenzi wa Green Belt Movement, shirika ambalo Profesa Maathai alilianzisha, Profesa Karanja Njoroge alithibitisha kutokea kwa kifo hicho. Katika taarifa yake kwa vyombo vya habari jana, Profesa Njoroge alisema Maathai, aliaga dunia saa 10:00 alfajiri ya kuamkia jana katika hospitali hiyo alikokuwa akipatiwa matibabu. Alisema wakati wa kifo chake, Profesa Wangari alikuwa na wanafamilia na marafiki.

      Profesa Maathai ambaye amefariki akiwa na umri wa miaka 71, ameacha watoto watatu; wawili wa kiume na mmoja wa kike. Profesa Maathai alianzisha vuguvugu la Green Belt mwaka 1977 na alifanya kazi na wanawake kote nchini kuboresha maslahi yao na kuhifadhi mazingira.

      Alikuwa mtetezi mashuhuri wa matumizi bora ya maliasili na shughuli zake zilitambuliwa mara kwa mara kote duniani. Baada ya taarifa ya msiba kutangazwa, Rais wa Kenya Mwai Kibaki ambaye yupo New York, Marekani katika Mkutano wa Umoja wa Mataifa (UN), alituma salamu za rambirambi kwa Wakenya wote kutokana na msiba huo mkubwa.

      JK, Kofi Annan watuma rambi rambi Rais Jakaya Kikwete naye alituma salamu zake za rambirambi kupitia mtandao wa Twitter. Katika salamu hizo, Rais Kikwete alisema Afrika imepoteza mwanamke shupavu na Mwenyezi Mungu amlaze pema pemboni.

      Katibu Mkuu wa zamani wa Umoja wa Mataifa, Kofi Annan alisema Profesa Maathai, atakumbukwa milele na kuheshimiwa. Historia ya Profesa Maathai Wangari Muta Maathai alizaliwa Aprili Mosi, 1940 katika Kijiji cha Ihithe, Wilaya ya Nyeri, Kenya. Mwaka wa 2004 alikuwa mshindi wa Tuzo ya Nobel ya Amani iliyo mfanya awe mwanamke wa kwanza Mwafrika kuipata Januari 2003 - Novemba 2005, Alikuwa Mbunge na Waziri Msaidizi katika Serikali ya Mwai Kibaki. Mwaka 2007, katika maandalizi ya uchaguzi wa Kenya, Profesa Maathai alisimama upande wa Rais Kibaki lakini hakuteuliwa na Chama cha PNU kugombea ubunge kupitia Chama cha Mazingira Green Party.

      Elimu na tuzo Maathai alihudhuria shule ya msingi ya Ihithe, halafu shule ya upili ya Loreto Convent, Limuru. Baada ya kuhitimu sekondari, alienda ng’ambo kusoma Bayologia nchini Ujerumani na Marekani. Mwaka wa 1967, alipata shahada ya kwanza ya baiolojia kutoka Chuo Kikuu cha Benedictine, Marekani. Aliendelea na masomo yake katika Chuo Kikuu cha Pittsburg ambako alipata shahada ya uzamili.

      Alirejea Nairobi na kupata shahada ya uzamivu (PhD) kutoka Chuo Kikuu cha Nairobi katika somo la udaktari wa wanyama. Kuanzia mwaka wa 1977, Maathai alikuwa Profesa msaidizi wa anatomia ya wanyama huko Nairobi akiwa mwanamke wa kwanza kupata uprofesa katika Chuo Kikuu cha Nairobi.

      Tuzo alizopata
      Baadhi ya tuzo alizopata ni pamoja na ile ya Mwanamke wa Dunia (1983), Tuzo ya Goldman kwa Mazingira (1991), Elder of the Burning Spear (2003) kutoka Serikali ya Kenya, Tuzo ya Nobel ya Amani (2004) na Legion D’Honneur (2006) kutoka Serikali ya Ufaransa.

      Mwaka wa 1977, Maathai alianzisha shirika la Green Belt Movement ambalo linajihusisha hasa na mazingira, haki za raia na demokrasia. Ndoa na familia Mwaka wa 1969, Wangari Muta (jina lake la kuzaliwa) alifunga ndoa na Mwangi Maathai, mwanasiasa wa Kenya na kupata watoto watatu, Waweru, Wanjira na Muta, lakini walitengana baadaye.
      "Success is the sum of small efforts, repeated day in and day out."


    2. #2
      pmwasyoke's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th May 2010
      Location : Dar es Salaam
      Posts : 2,514
      Rep Power : 986
      Likes Received
      338
      Likes Given
      438

      Default Re: Profesa Wangari Maathai afariki dunia

      RIP Prof

    3. #3
      Ngongo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 20th September 2008
      Location : Mlima Meru
      Posts : 4,969
      Rep Power : 6858
      Likes Received
      2408
      Likes Given
      3171

      Default Re: Profesa Wangari Maathai afariki dunia

      RIP Prof Wangari.

    4. #4
      Pdidy's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 22nd November 2007
      Posts : 12,328
      Rep Power : 3455
      Likes Received
      1338
      Likes Given
      864

      Default Re: Profesa Wangari Maathai afariki dunia

      Masikini zile pesa sijui kama alizimaliza zote ama alitumiakwa furahaa loh
      mungu amuweke mahala pema peponi jamani
      KAMA NAONA NDUGU ZAKE WATAKAPOPAMBANA NA ZILE ZIFUTA JASHO HOPE WATOTO NI WAKUBWA

    5. #5
      Mwana wa Kitaa's Avatar
      Member Array
      Join Date : 20th July 2011
      Posts : 52
      Rep Power : 411
      Likes Received
      4
      Likes Given
      0

      Default Re: Profesa Wangari Maathai afariki dunia

      Mungu amlaze pema peponi.


    6. #6
      mikatabafeki's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th December 2010
      Posts : 4,873
      Rep Power : 1407
      Likes Received
      778
      Likes Given
      1463

      Default Re: Profesa Wangari Maathai afariki dunia

      R.i.p....................

    7. #7
      Mamndenyi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th April 2011
      Posts : 13,462
      Rep Power : 35821
      Likes Received
      6874
      Likes Given
      21098

      Default Re: Profesa Wangari Maathai afariki dunia

      R.I.P Profesa wetu.

    Similar Topics

    1. Profesa Maathai afariki dunia
      By MziziMkavu in forum Matangazo madogo
      Replies: 2
      Last Post: 1st October 2011, 18:40
    2. Life and Legacy of Wangari Maathai
      By dymosy in forum International Forum
      Replies: 0
      Last Post: 29th September 2011, 18:39
    3. Profesa Wangari Maathai afariki
      By Bajabiri in forum Habari na Hoja mchanganyiko
      Replies: 40
      Last Post: 26th September 2011, 16:37
    4. Wangari Maathai na mazingira.....
      By Dr. Chapa Kiuno in forum Habari na Hoja mchanganyiko
      Replies: 0
      Last Post: 30th September 2009, 12:00
    5. Profesa Haroub Othman afariki dunia
      By Mhache in forum Habari na Hoja mchanganyiko
      Replies: 3
      Last Post: 28th June 2009, 18:52

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...