Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Fizikia ya Ajali (The Physics of Accidents): Mabasi yetu yanaundwa au kuunganishwa wapi?

    Report Post
    Page 1 of 5 123 ... LastLast
    Results 1 to 20 of 94
    1. #1
      Mzee Mwanakijiji's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 10th March 2006
      Location : Kijijini
      Posts : 29,614
      Rep Power : 46736
      Likes Received
      16716
      Likes Given
      8547

      Default Fizikia ya Ajali (The Physics of Accidents): Mabasi yetu yanaundwa au kuunganishwa wapi?

      Nimejikuta na search google na yahoo kuhusu "ajali za basi" na kuangalia picha mbalimbali za ajali. Mara moja niliona pattern fulani hiyo ambayo imenifanya niulize swali kwa wenzetu wanaojua mambo ya engineering, physics and mechanics au hata metallurgy kuhusiana na mabasi yetu. Ukiondoa vijibasi vidogo vinavyoingizwa nchini mabasi mengi makubwa na malori yanaunganishwa nchini. Mengine yanatumia chasis za malori na kuwekwa body n.k Nakumbuka kulikuwepo hata na kampuni ya "Quality Bodies" or something like that. Lakini nimeangalia kidogo ajali hizi na madhara yake na nimeanza kujiuliza kama ukiiondoa tatizo la barabara yawezekana kuna matatizo ya msingi (structural problems) kwenye mabasi yetu? Na maswali mengine yakaanza:

      a. Ni chombo gani kinasimamia quality ya mabasi yanayounganishwa nchini?
      b. Viwango (standards) kinachotakiwa katika mabasi ni kwa kiasi gani kimeletwa katika uelewa wa sayansi na teknolojia ya karne hii mpya?
      c. Kabla mabasi hayajaingia kwenye huduma yanafanyiwa kwa kiasi gani majaribio ya kuhimili mikikimikiki (stress tests) ili kuhakikisha yatabehave vipi katika ajali maana baadhi ya mabasi ukiyaona unashindwa kuelwa kama ni impact peke yake inayosababisha madhara hivyo au hata structure ya basi haiko katika kuhimili mikikimikiki?
      d. Baada ya kulaumu "mwendo kasi" mara nyingi ajali zinapotokea au "kutokufuata sheria za usalama barabarani" yawezekana kuna maelezo ya kifizikia ya ajali hizi - kwa mfano uhusiano wa mwendo, uzito na impact au nguvu (force)? Yawezekana wasomi wetu kama walivyoshindwa kuukosoa ubepari (I couldn't resist that) wameshindwa kufanya utafiti wa kisayansi wa kuelewa chanzo cha ajali hizi (badala ya kukubali tu kuwa dunia ni flat) na kuja na mapendekezo ya nini kifanyike katika uungaji wa magari, maumbo yake n.k?
      e. Je muundo wetu wa barabara unachangia vipi kutokea kwa ajali hizi (kwa mfano eneo la Mikumi, Kibaha) ni kinara wa ajali kwanini?

      Ninaamini kabisa kuwa na sisi tuna uwezo na wapo watu wenye uwezo wa kuangalia mambo haya kisayansi na kuyaelewa na kuja na mapendekezo ya kisayansi badala ya "kudra" na kusema ni "mapenzi ya Mungu". Anybody?


      Angalia hizi picha na jiulize maswali yako na kama unamawazo ya majibu
      Attached Files
      [email protected]
      The Best of Tanzanian Socio-Political Blogging - http://www.mwanakijiji.com


    2. #2
      Kimbunga's Avatar
      JF Platinum Member Array
      Join Date : 4th October 2007
      Location : Kisiwani Juma
      Posts : 7,543
      Rep Power : 6185
      Likes Received
      3103
      Likes Given
      1025

      Default Re: Fizikia ya Ajali (The Physics of Accidents): Mabasi yetu yanaundwa/unganishwa wapi?

      Quote By Mzee Mwanakijiji View Post
      Nimejikuta na search google na yahoo kuhusu "ajali za basi" na kuangalia picha mbalimbali za ajali. Mara moja niliona pattern fulani hiyo ambayo imenifanya niulize swali kwa wenzetu wanaojua mambo ya engineering, physics and mechanics au hata metallurgy kuhusiana na mabasi yetu. Ukiondoa vijibasi vidogo vinavyoingizwa nchini mabasi mengi makubwa na malori yanaunganishwa nchini. Mengine yanatumia chasis za malori na kuwekwa body n.k Nakumbuka kulikuwepo hata na kampuni ya "Quality Bodies" or something like that. Lakini nimeangalia kidogo ajali hizi na madhara yake na nimeanza kujiuliza kama ukiiondoa tatizo la barabara yawezekana kuna matatizo ya msingi (structural problems) kwenye mabasi yetu? Na maswali mengine yakaanza:

      a. Ni chombo gani kinasimamia quality ya mabasi yanayounganishwa nchini?
      b. Viwango (standards) kinachotakiwa katika mabasi ni kwa kiasi gani kimeletwa katika uelewa wa sayansi na teknolojia ya karne hii mpya?
      c. Kabla mabasi hayajaingia kwenye huduma yanafanyiwa kwa kiasi gani majaribio ya kuhimili mikikimikiki (stress tests) ili kuhakikisha yatabehave vipi katika ajali maana baadhi ya mabasi ukiyaona unashindwa kuelwa kama ni impact peke yake inayosababisha madhara hivyo au hata structure ya basi haiko katika kuhimili mikikimikiki?
      d. Baada ya kulaumu "mwendo kasi" mara nyingi ajali zinapotokea au "kutokufuata sheria za usalama barabarani" yawezekana kuna maelezo ya kifizikia ya ajali hizi - kwa mfano uhusiano wa mwendo, uzito na impact au nguvu (force)? Yawezekana wasomi wetu kama walivyoshindwa kuukosoa ubepari (I couldn't resist that) wameshindwa kufanya utafiti wa kisayansi wa kuelewa chanzo cha ajali hizi (badala ya kukubali tu kuwa dunia ni flat) na kuja na mapendekezo ya nini kifanyike katika uungaji wa magari, maumbo yake n.k?
      e. Je muundo wetu wa barabara unachangia vipi kutokea kwa ajali hizi (kwa mfano eneo la Mikumi, Kibaha) ni kinara wa ajali kwanini?

      Ninaamini kabisa kuwa na sisi tuna uwezo na wapo watu wenye uwezo wa kuangalia mambo haya kisayansi na kuyaelewa na kuja na mapendekezo ya kisayansi badala ya "kudra" na kusema ni "mapenzi ya Mungu". Anybody?


      Angalia hizi picha na jiulize maswali yako na kama unamawazo ya majibu
      Mkuu kama kuna mtu atatokea na kujibu hayo maswali basi hili tatizo la ajali litapungua sana hapa nchini. Kuna wakati nilisikia kuwa mabasi mengi yamejengewa tu bodi za mabasi ila yalistahili kuwa malori/mafuso ya kubeba mizigo. Likatolewa tamko la kwamba mwisho wa hayo malori/mafuso kutumika kama mabasi itakuwa siku fulani (nadhani imepita miaka miwili) lakini hadi sasa hayo magari yapo barabarani!! Ilimaminika kuwa hayo malori mabasi yanakuwa yamepewa mzigo mdogo kulinganisha na yanachotakiwa bubeba yakiwa malori kwa hiyo speed huwa kubwa.

      Lakini pia kuna hili suala la barabara hasa design. Nasikia barabara zetu zimekuwa designed kwa kuhimili mwendo wa KM 100 kwa saa na si zaidi ya mwendo huo.
      CCM na CDM vyote ni vyama vya siasa vinavyoongozwa na wanasiasa; tofauti yao kubwa ni moja kwamba kimoja kina dola kingine kinataka kushika dola.

    3. #3
      Mzee Mwanakijiji's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 10th March 2006
      Location : Kijijini
      Posts : 29,614
      Rep Power : 46736
      Likes Received
      16716
      Likes Given
      8547

      Default Re: Fizikia ya Ajali (The Physics of Accidents): Mabasi yetu yanaundwa/unganishwa wapi?

      Au tuombe wazungu waje kutufikiria?
      Victim likes this.
      [email protected]
      The Best of Tanzanian Socio-Political Blogging - http://www.mwanakijiji.com

    4. #4
      Lutifya's Avatar
      Member Array
      Join Date : 6th January 2011
      Posts : 30
      Rep Power : 434
      Likes Received
      27
      Likes Given
      0

      Default Re: Fizikia ya Ajali (The Physics of Accidents): Mabasi yetu yanaundwa/unganishwa wapi?

      Mzee Mwanakijiji asante sana kwa post yako.Ni ukweli kuwa ajali zimeongezeka katika kiwango cha exponential rate kwa sasa hasa mabasi. Ni meguswa na topic hii hasa niliposhuhudia maongezi yasiyo rasmi ya madereva wa mabasi kwenye baa moja hivi. Kimsingi walisema pamoja na sababu ambazo umegususia ni kwambwa mabasi mengi pamoja na magari ya mizigo yanafungwa matairi toka chini ambayo kwa kweli sio imara. Matajiri wengi hawataki kufunga matairi kwa mfano aina ya michelin ambayo ni durable kwa sababu ya bei kuwa kubwa.
      Chukulia mfano wa basi linalosafiri toka Dar mpaka Mbeya umbali wa karibu 840km kwa mwendo kasi wa zaidi ya 80km/hr na linasimama comfort au Al jazeera restaurant kwa dk kama 10 tu, tairi linapata moto sana kwa sababu ya friction. Tairi za kichina haziwezi kuhimili tractive force ya mwendo na umbali tajwa hapo juu tene yanafungwa mbele. Madreva hao walisema ukienda na lori la mizigo kama malawi na sourth Africa,kama gari yako imefungwa tairi ambazo sio brand inayojulikana kwa ubora kama michelin huendelei na safari.
      Muhimu ni kuwa wenye mabasi wapewa na mamlaka husika kufunga tairi imara, ingawa ofcourse kuna factosr nyingi zinazosababisha ajali lakini tunaweza ku-mitigate kwa njia hiyo. Karibu ajali zilizotokea hivi karibuni za mabasi ni kwa sababu tairi za mbele zilipasuka.
      Pia mabasi mengi yanayotengenezwa hapa nchini sidhani kama body zinakuwa well balanced. wenzetu kabla ya kuunda body husika wanafanyia simulation ya body assembly kwenye design software kabla ya kupeleka kwenye production ile kucheck dynamic balance.

    5. #5
      Mzee Mwanakijiji's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 10th March 2006
      Location : Kijijini
      Posts : 29,614
      Rep Power : 46736
      Likes Received
      16716
      Likes Given
      8547

      Default Re: Fizikia ya Ajali (The Physics of Accidents): Mabasi yetu yanaundwa/unganishwa wapi?

      Yawezekana ipo haja ya kuongeza mwendo kwani naamini 80k/h ni mwendo wa pole pole sana.
      Nyambala likes this.
      [email protected]
      The Best of Tanzanian Socio-Political Blogging - http://www.mwanakijiji.com


    6. #6
      Horseshoe Arch's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 10th August 2009
      Location : Block A
      Posts : 1,316
      Rep Power : 770
      Likes Received
      171
      Likes Given
      39

      Default Re: Fizikia ya Ajali (The Physics of Accidents): Mabasi yetu yanaundwa/unganishwa wapi?

      Mkuu kufikia hapa ubongo unafreeze kabisa...imefika mahala sasa nimalizapo umbali fulani safarini namshukuru Mungu "kwa sababu sijafa"...km kuna bodi ya ukaguzi basi niisifu tu kwa kuhakikisha mabasi/malori mengi ni "video coach'' hata km body ni ya plastic..thus all
      We are what we think. With our thoughts we make the world.

    7. #7
      zumbemkuu's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 11th September 2010
      Location : street dweller
      Posts : 5,423
      Rep Power : 2023
      Likes Received
      2163
      Likes Given
      7946

      Default Re: Fizikia ya Ajali (The Physics of Accidents): Mabasi yetu yanaundwa/unganishwa wapi?

      mmmmmh! hii nchi ya kitu kidogo, ndo maana katiba mpya iweke bayana kuwa kusiwe na urafiki kati ya wafanya biashara na serikali, tatizo kama hilo litatatulika tu.
      "watakaotubeza na kututukana wasameheni wanahitaji ukombozi wa fikra" Mh.G.Lema

    8. #8
      Makfuhi's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 20th August 2008
      Posts : 147
      Rep Power : 582
      Likes Received
      24
      Likes Given
      0

      Default Re: Fizikia ya Ajali (The Physics of Accidents): Mabasi yetu yanaundwa/unganishwa wapi?

      Nilichogundua mimi ni kwamba square pipe zimetumika ambazo ni light quality ambazo basi likipigwa kofi bodi inakatika abiria wanabaki nje. mabasi ya zamani bodi zilitengenezwa kutumia angle ndiyo maana likianguka linabaki intact. Kwa kuwa serikali yetu ilienda likizo siku nyingi ikakosa nauli ya kurudi hatuna wa kutusemea.

    9. #9
      Domhome's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 28th June 2010
      Location : Chimbo
      Posts : 706
      Rep Power : 597
      Likes Received
      182
      Likes Given
      144

      Default Re: Fizikia ya Ajali (The Physics of Accidents): Mabasi yetu yanaundwa/unganishwa wapi?

      Mkuu MMKJJ,

      Utafiti huu ulipaswa uwe umeshafanyika siku nyingi sana na pengine ungesaidia kutotufikisha hapa tulipo. Nadhani, tena nasema nadhani Sumatra na Wizara ya Mambo ya Ndani walipaswa wawe na kitengo cha utafiti wa kwanini ajali zinatokea kwa wingi? nasiyo kungoja hadi wapate maoni/ushauri na au malalamiko toka kwa raia. Serikali hii imelala fofofo!

      Taasisi na mamlaka husika anzieni hapa alipoishia Mwanakijiji!
      “It’s now the moment for political baboons to see their backsides” - Time for politicians to look at themselves in the mirror! (Kenyan human right's activist)

    10. #10
      Mzee Mwanakijiji's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 10th March 2006
      Location : Kijijini
      Posts : 29,614
      Rep Power : 46736
      Likes Received
      16716
      Likes Given
      8547

      Default Re: Fizikia ya Ajali (The Physics of Accidents): Mabasi yetu yanaundwa/unganishwa wapi?

      bado sijasikia ni wapi mabasi haya yanaunganishwa na ni chombo gani kinasimamia? tuachane na ya Katiba mpya kwanza tuzungumzie right now tusije kudhania katiba mpya itatatua matatizo ya ajali au matatizo mengine yoyote yale. Kuna vitu tunaweza kuvifanya sasa hivi
      [email protected]
      The Best of Tanzanian Socio-Political Blogging - http://www.mwanakijiji.com

    11. #11
      Mzee Mwanakijiji's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 10th March 2006
      Location : Kijijini
      Posts : 29,614
      Rep Power : 46736
      Likes Received
      16716
      Likes Given
      8547

      Default Re: Fizikia ya Ajali (The Physics of Accidents): Mabasi yetu yanaundwa/unganishwa wapi?

      Au Tanzania ina matatizo ya mainjia kama ilivyo kwa wanasheria?
      [email protected]
      The Best of Tanzanian Socio-Political Blogging - http://www.mwanakijiji.com

    12. #12
      Kibunango's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th August 2006
      Location : Tampere
      Posts : 6,820
      Rep Power : 44138
      Likes Received
      375
      Likes Given
      1450

      Default Re: Fizikia ya Ajali (The Physics of Accidents): Mabasi yetu yanaundwa/unganishwa wapi?

      Quote By Mzee Mwanakijiji View Post
      Au tuombe wazungu waje kutufikiria?
      Naam, kwani miaka ya 60, 70 na mwanzoni mwa miaka ya 80, tulipokuwa na mabasi ya mashirika kama Kamata na Relwe, mabasi yao yalikuwa ya ubora sahihi wa barabara zetu na mengi yalikuwa yanaingia moja moja tuko huko kwao! Hata kampuni binafsi kama Kwacha, Rafiki, Bon City, n.k za miaka hiyo walikuwa na mabasi bora sana.

      Hata zilipoanza Garage mbalimbali za uundaji wa mabodi, bado waliendelea kufuata standards zao. Nakumbuka garage kama ya Ujamaa na Quality walivyoweza kuunda bodi zenye kuweza kuhimili ubebaji wa abiria na mizigo ya kutosha pasipo uhatarishaji wa usalama wa abiria na basi lenyewe.

      Kuja kwa garage nyingi za kuunda mabodi kunaweza kuwa ni sehemu ya matatizo haya. Siku hizi kuna mabodi toka Kenya ambayo inasemeka yana uzito mkubwa kuliko uwezo wa chasis ya basi. Kuna garage kibao bubu zinaunda mabodi yao na hata baadhi ya kampuni za mabasi zinajiundia mabodi yao. Kama ulivyodokeza hapo juu ndio maana utakuta leo hii chasis ya gari ya mizigo inatumiwa kuwa ya basi.
      Save Water Drink Beer. "Alcohol doesn't solve any problem,
      But, if you think again, neither does milk."
      Vituko Vya Zenj

    13. #13
      Kimbunga's Avatar
      JF Platinum Member Array
      Join Date : 4th October 2007
      Location : Kisiwani Juma
      Posts : 7,543
      Rep Power : 6185
      Likes Received
      3103
      Likes Given
      1025

      Default Re: Fizikia ya Ajali (The Physics of Accidents): Mabasi yetu yanaundwa/unganishwa wapi?

      Quote By Mzee Mwanakijiji View Post
      bado sijasikia ni wapi mabasi haya yanaunganishwa na ni chombo gani kinasimamia? tuachane na ya Katiba mpya kwanza tuzungumzie right now tusije kudhania katiba mpya itatatua matatizo ya ajali au matatizo mengine yoyote yale. Kuna vitu tunaweza kuvifanya sasa hivi
      Mabasi mengi yanaunganishwa Kenya. Msimamiaji ni SUMATRA na TBS
      CCM na CDM vyote ni vyama vya siasa vinavyoongozwa na wanasiasa; tofauti yao kubwa ni moja kwamba kimoja kina dola kingine kinataka kushika dola.

    14. #14
      Kibunango's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th August 2006
      Location : Tampere
      Posts : 6,820
      Rep Power : 44138
      Likes Received
      375
      Likes Given
      1450

      Default Re: Fizikia ya Ajali (The Physics of Accidents): Mabasi yetu yanaundwa/unganishwa wapi?

      Quote By Mzee Mwanakijiji View Post
      Yawezekana ipo haja ya kuongeza mwendo kwani naamini 80k/h ni mwendo wa pole pole sana.
      Mabasi mengi yanakwenda kwa speed kati ya 100km/h- 120km/h. Hiyo ya 80km/h ipo kwenye mafaili tu na imechorwa kwenye mabasi hayo. Kama unakumbuka mpango mzima wa governor ulikuwa ni kulazimisha mabasi yote yaende kwa speed ya 80km/h... Lakini umeshindikana!
      Save Water Drink Beer. "Alcohol doesn't solve any problem,
      But, if you think again, neither does milk."
      Vituko Vya Zenj

    15. #15
      Mzee Mwanakijiji's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 10th March 2006
      Location : Kijijini
      Posts : 29,614
      Rep Power : 46736
      Likes Received
      16716
      Likes Given
      8547

      Default Re: Fizikia ya Ajali (The Physics of Accidents): Mabasi yetu yanaundwa/unganishwa wapi?

      Kibunango, umenifanya nijiulize swali jingine.. what about the electronics za mabasi yetu... kuna mtu anajua ni kwa kiasi gani zimekuwa digitized?
      [email protected]
      The Best of Tanzanian Socio-Political Blogging - http://www.mwanakijiji.com

    16. #16
      Mzee Mwanakijiji's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 10th March 2006
      Location : Kijijini
      Posts : 29,614
      Rep Power : 46736
      Likes Received
      16716
      Likes Given
      8547

      Default Re: Fizikia ya Ajali (The Physics of Accidents): Mabasi yetu yanaundwa/unganishwa wapi?

      Quote By Kimbunga View Post
      Mabasi mengi yanaunganishwa Kenya. Msimamiaji ni SUMATRA na TBS
      So yanapoingia Tanzania hatuna kiwango tunachotaka kuangalia; je ajali za mabasi ziko hivyo hivyo huko Kenya au ni huku kwetu au mabodi ya Kenya ni tofauti? wao Kenya kuna chombo gani kinachosimamia ubora wa mabasi? Sumatra wamepewa majukumu ya kuregulate viwanda vya mabasi au wana majukumu ya kusimamia vyombo vikiwa tayari vimekamilika na viko barabarani?
      [email protected]
      The Best of Tanzanian Socio-Political Blogging - http://www.mwanakijiji.com

    17. #17
      Nguruvi3's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st June 2010
      Location : Kidabashi-Dongobeshi
      Posts : 3,600
      Rep Power : 2924
      Likes Received
      5001
      Likes Given
      3072

      Default Re: Fizikia ya Ajali (The Physics of Accidents): Mabasi yetu yanaundwa/unganishwa wapi?

      Tatizo ni kubwa sio upande wa engineering tu (kama ni sababu), kuna barabara, utoaji leseni, Bima, vipuri na matairi na viongozi wasiojua nini ni tatizo. Ni combination of factors.

      Miaka hiyo kulikuwa na kampuni ya Mohamed Ali ya Nairobi ndiyo ilikuwa inajenga bodi za mabasi EA nkumbuka.(Body built by Mohamed Ali & sons-Nairobi Kenya).

      Nilishtuka siku moja niliposikia mabasi yanawekewa chasis za malori kubeba mzigo wa maana!! na hakuna aliyeona hicho ni kioja.

      Ajali ni tatizo kubwa sana nchini ni kwa vile tu tunamsingizia mungu tu!

    18. #18
      Mzee Mwanakijiji's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 10th March 2006
      Location : Kijijini
      Posts : 29,614
      Rep Power : 46736
      Likes Received
      16716
      Likes Given
      8547

      Default Re: Fizikia ya Ajali (The Physics of Accidents): Mabasi yetu yanaundwa/unganishwa wapi?

      Quote By Kibunango View Post
      Mabasi mengi yanakwenda kwa speed kati ya 100km/h- 120km/h. Hiyo ya 80km/h ipo kwenye mafaili tu na imechorwa kwenye mabasi hayo. Kama unakumbuka mpango mzima wa governor ulikuwa ni kulazimisha mabasi yote yaende kwa speed ya 80km/h... Lakini umeshindikana!
      lakini hiyo ni spidi ndogo sana kwa barabara kuu.. we need to increase it.
      [email protected]
      The Best of Tanzanian Socio-Political Blogging - http://www.mwanakijiji.com

    19. #19
      Majoja's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 10th June 2011
      Posts : 613
      Rep Power : 532
      Likes Received
      167
      Likes Given
      189

      Default Re: Fizikia ya Ajali (The Physics of Accidents): Mabasi yetu yanaundwa/unganishwa wapi?

      Mkuu Mwanakijiji, somo ulilo leta leo ni la hali ya juu sana katika fani ya uhandisi na usafirishaji.
      Kwa kifupi hili ni somo katika Traffic Engineering and Management pamoja na Highway Engineering.
      Ni somo ambalo halina jibu la moja kwa moja ingawaje si sababu kubwa ya madudu tunayoyaona barabarani.
      Utengenezaji wa magari hasa mabasi ya abiria vile vile ni suala ambalo halijapewa ubunifu unaostahili kulingana na hali ya maendeleo ya sasa.
      Kuwa basi ina chassis ya lori hiyosisababu ya basi kupata ajali.
      Hebu tujikumbushe yafuatayo:
      • Kumekuwapo na a major improvement in the performance ya motor engines, engine ndogo inakuwa powerful na hivyo kubeba mzigo mzito au kwenda kasi zidi
      • Bara bara zetu hazijaendelea katika viwango kullingana na maendeleo hayo ya motor performance,Ni sehemu chache tu kamaza Chalinze-Ubena Zomozi ndio barabara zinalingana kidogo na uwezo mkubwa wa engine za kisasa.
      • Utngenezaji wa bodi za mabasi hapa Tanzania hauzingatii kabisa ubora na teknologia inayotakiwa. Hii ni licha ya mamlaka mbali mbali zilizopo katika viwango eg TBS . Kwa hapa Tanzania hata hivyo mimi sina habari kuwa kuna karakana yoyote ya serikali inayofanya research yoyote katika stress analysis kulinganana barabara zetu.
      • Kuna uchangiaji mkubwa sana kwa makosa ya binadamu katika kusababisha ajali.Aidha elimu ya usalama barabarani pamoja na ukaguzi wa ubora wa vifaa vyenyewe(magari), rushwa ya askari wa traffic na hata wasimamizi wa Tanroads mizani, vyote hivi vina mchango mkubwa sana katika ajai zinazotokea.
      Mkuu Mwanakijiji topic yako ni kubwa sana na najua kiserikali haipo chini ya wizara moja tu. Hapa kuna Wizara ya Ujenzi,Mambo ya Ndani,Tawala za Mikoa nk.
      Naomba kuwasilisha
      Mzee Mwanakijiji likes this.

    20. #20
      Mwalimu's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 21st August 2008
      Posts : 1,176
      Rep Power : 787
      Likes Received
      255
      Likes Given
      689

      Default Re: Fizikia ya Ajali (The Physics of Accidents): Mabasi yetu yanaundwa/unganishwa wapi?

      Quote By Mzee Mwanakijiji View Post
      bado sijasikia ni wapi mabasi haya yanaunganishwa na ni chombo gani kinasimamia? tuachane na ya Katiba mpya kwanza tuzungumzie right now tusije kudhania katiba mpya itatatua matatizo ya ajali au matatizo mengine yoyote yale. Kuna vitu tunaweza kuvifanya sasa hivi
      I think Quality Garage bado wanaendelea na kuunganisha mabasi, sina uhakika kama kuna washindani wengine kwenye biashara hii...
      Mzee Mwanakijiji likes this.
      I'm teaching fools some basic rules...

    Page 1 of 5 123 ... LastLast

    Similar Topics

    1. Sababu ya ajali za mabasi kukithiri
      By TUMBIRI in forum Jukwaa la Siasa
      Replies: 1
      Last Post: 20th November 2011, 14:58
    2. Yako wapi mabasi yaliyotumika kuwabeba 'watuhumiwa wa EPA'?
      By personation in forum Jukwaa la Siasa
      Replies: 11
      Last Post: 27th September 2011, 06:31
    3. Ajali ya Meli: Serikali yetu na utata wa idadi ya abiria walioangamia
      By ntamaholo in forum Habari na Hoja mchanganyiko
      Replies: 75
      Last Post: 16th September 2011, 17:49
    4. Mchanganyiko wa FDLR na CNDP unaweza kuunganishwa na Meremeta?
      By Richard in forum International Forum
      Replies: 0
      Last Post: 11th January 2010, 16:05
    5. Physics and Wireless Electricity!!!
      By MaxShimba in forum Jukwaa la Elimu (Education Forum)
      Replies: 19
      Last Post: 26th December 2008, 13:44

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...