ni kipindi kingine cha mwaka ambapo kila mwisho wa mwaka kadi za michango ya harusi inakua mingi, inakuaje mtu anataka kufanya sherehe kubwa na hana uwezo?? kwa nini usifanye hiyo harusi kutokana na uwezo wako ulionao, ni mpaka usumbue watu wakuchangie??? tena kinachoudhi ni mtu ameshakaa na mke/mme na wana watoto anataka kupasha kiporo chake nae anataka afanye sherehe kubwa na anachangisha!!! na kero nyingine mtu anakupa kadi ya mchango wa ndugu yake ambaye humjui. Sijawahi pewa au kuona mtu akichangisha kwa ajili ya maendeleo kama vile ada ya shule etc kama majirani zetu na harambee zao zenye maendeleo, sijui wenzangu mnafikiria vipi.

Reply With Quote

Follow Us Here