Maelfu ya watu nchini Israel wameandamana kupinga ughali wa maisha nchini humo. Imekadiriwa kuwa kati ya watu 250,000 hadi 350,000 walikusanyika katika maandamano makubwa kabisa kufanywa mjini Tel Aviv.
Waandamanaji wanatoa wito kwa serikali kufanya mageuzi makubwa, ili kupunguza gharama za nyumba, elimu, ulezi wa watoto na huduma za afya. Waziri Mkuu wa nchi hiyo, Benjamin Netanyahu, amekwepa kutimiza madai ya waandamanaji, lakini ameunda kamati ya mawaziri, kuchunguza madai hayo.

Reply With Quote

Follow Us Here