Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Tanzania daima wamfagilia Zitto kabwe

    Report Post
    Results 1 to 7 of 7
    1. #1
      Mkwawa's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 8th June 2011
      Location : Kalenga
      Posts : 608
      Rep Power : 3562
      Likes Received
      692
      Likes Given
      383

      Default Tanzania daima wamfagilia Zitto kabwe

      na Bakari Kimwanga

      SHEREHE za kuzaliwa upya kwa taifa la Sudan Kusini zilizofanyika juzi mjini Juba, ziliibua hisia mpya katika siasa za Tanzania baada ya Rais Jakaya Kikwete na Naibu Kiongozi wa Upinzani Bungeni, Zitto Kabwe, kuandamana kuhudhuria tukio hilo la kihistoria.
      Ziara hiyo ilifanyika baada ya Rais Kikwete kumaliza safari ya kikazi mkoani Kigoma wiki iliyopita, ambako alizindua miradi kadhaa, ikiwamo ya Barabara ya Mwandiga – Manyovu inayopita katika Jimbo la Kigoma Kaskazini linalowakilishwa na Zitto.
      Wakiwa Sudan, Kikwete na Zitto walipata fursa ya kusalimiana na kuzungumza na viongozi mbalimbali waliohudhuria sherehe hizo, akiwamo Rais wa nchi hiyo, Salva Kiir.
      Safari hiyo ya Zitto na Kikwete imezua maswali miongoni mwa wadadisi wa siasa wanaofuatilia mwenendo wa rais anayekaribia kuondoka madarakani na mwanasiasa kijana katika harakati za mageuzi nchini. Ingawa inajulikana kuwa Kikwete na Zitto wamekuwa na uhusiano mzuri kikazi, licha ya kupingana kiitikadi, ziara yao ya juzi iliongeza minong’ono, hasa baada ya Zitto kuvujisha sehemu ya mazungumzo kati ya rais na yeye (Zitto) na Mbunge wa Kigoma Kusini, David Kafulila, walipokuwa kwenye hafla ya uzinduzi wa barabara mkoani Kigoma.

      Kwa mujibu taarifa zilizobandikwa na Zitto katika ukurasa wake wa facebook siku chache zilizopita, Rais Kikwete aliwanong’oneza yeye na Kafulila kwamba asingependa baada ya kustaafu kwake nchi iongozwe na rais ‘mzee’ kama yeye.
      Rais Kikwete, ambaye aliingia madarakani kwa kampeni ya “ujana” huku akiwa na umri wa miaka 55 mwaka 2005, aliwaambia kina Zitto:
      “Msikubali atakayenirithi awe wa rika langu, sasa kizazi chenu kijiandae.”
      Wachambuzi wa masuala ya kisiasa wanasema kauli hiyo, kama ilitolewa na Rais Kikwete kweli, ililenga kuhamisha mjadala wa kisiasa kuhusu mrithi wa Kikwete nje na ndani ya CCM.
      Inafahamika kwamba wanasiasa “wakali” ambao Rais Kikwete anawaogopa, na ambao wameonyesha nia ya kuutaka urais baada yake, ni watu wa makamo kama yeye.
      Vile vile, wananchi wanapokuwa wanajadili mustakabali wa nchi, suala la umri, dini, jinsia na eneo analotoka mtu, havijawahi kuwa vigezo vinavyotumika kumuunga mkono mgombea.
      Lakini kwa taifa lililoshuhudia siasa zenye mrengo wa kijinsia katika kumpata Spika wa Bunge, na kauli za udini kwenye kampeni mara baada ya Uchaguzi Mkuu, haliwezi kupuuza kauli hizi za kigezo cha umri.
      Hata hivyo, baadhi ya wachambuzi wamekuwa wakisisitiza kuwa ujana au uzee si hoja. Wapo pia wanaosema kwa msisitizo mkubwa kwamba mgombea yeyote wa CCM atakayebebwa na Rais Kikwete ataanguka. Wanatoa sababu kadhaa.

      Kwanza, wanasema nguvu yake ndani ya mfumo inalegalega kiasi cha kumnyima uwezo wa kushinikiza wanachama wakubaliane naye katika chaguo atakalowaletea.
      Na kwa msingi wa makundi ndani ya CCM, kuna watu wamejipanga kwamba yeyote atakayeonekana kubebwa na JK lazima “apigwe chini.”
      Pili, wachunguzi wanasema historia inaonyesha kuwa hakuna aliyebebwa na rais anayeondoka madarakani, akashinda. Wanatoa mifano ya jinsi Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere mwaka 1985, alivyomtaka Dk. Salim Ahmed Salim, lakini akazidiwa kete na wajumbe waliomtaka mzee Ali Hassan Mwinyi. Hata mwaka 1995 alimtaka Dk. Salim, ikashindikana baada ya Dk. Salim mwenyewe kukataa kwa kutazama upepo wa kisiasa wa wakati huo.

      Wanasema hata Rais Mwinyi alipokuwa anaondoka, chaguo lake lilikuwa ama Cleopa Msuya au Kikwete. Alishindwa kupitisha mmoja wao.
      Hata Rais Benjamin Mkapa alikuwa na mtu wake, lakini alilazimika kumuunga mkono Kikwete baada ya kushindwa na wimbi la mtandao ndani ya chama.
      Ingawa “uhusiano” kati ya Kikwete na Zitto unajulikana kwa siku nyingi, na ingawa Zitto mwenyewe hajatamka kwamba anawania urais, kauli hizi za Kikwete na Zitto zilikuwa na ujumbe kwa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kinachomsumbua Rais Kikwete.
      Wengine wanadai anataka kumtumia Zitto kugombanisha wanaotaka urais ndani ya chama hicho. Wapo wanaodai kwamba hata Zitto mwenyewe atakuwa hajafikisha umri wa kugombea urais mwaka 2015, kwani atakuwa na miaka 39; na kwamba hata kama katiba itakuwa imebadilishwa, umri wa mgombea urais hautarajiwi kushushwa kuwa chini ya miaka 40 inayoruhusiwa sasa.
      Zaidi ya hayo, wengine wanahoji, “Kikwete anataka kurithisha urais kwa chama gani? Au ameridhika sasa kwamba CCM haiwezi kutawala tena?”
      Hata hivyo, wengine wamedai uhusiano wa Kikwete na Zitto ni mbinu ya wanasiasa hao kujijenga binafsi, kwani Kikwete anadhani akionekana na Zitto hadharani itamwongezea kukubalika na mashabiki wa Zitto na upinzani, ambao ni wengi anaowakosa.
      Wanaotetea hoja hiyo wanatoa mfano wa tukio la juzi akiwa mkoani Kigoma, ambapo rais alinong’onezwa kuwa Zitto alikuwa miongoni mwa wananchi waliokuwa mkutanoni hapo, akamwita kwa sauti aje jukwaani, na baada ya mkutano akawa anatembea na kuteta naye huku umati unawatazama.
      Wanasema Zitto naye anatumia nafasi ya Kikwete kujihalalisha kwa wana CCM na wananchi wengine kujinasibu kama mwanasiasa anayeweza kufanya kazi bila kufungwa na tofauti za kiitikadi.
      Akiwa Sudan Kusini juzi, Rais Kikwete alimtambulisha Zitto kwa Rais mpya wa nchini hiyo, Salva Kiir Mayardit, hali iliyosisimua ujumbe wa Tanzania.
      Hivi karibuni wakiwa mkoani Kigoma wakati wa ziara ya Rais Kikwete, Zitto alitoa hotuba fupi ya kumsifia Rais Kikwete, ambayo ilipokewa kwa hisia tofauti.
      Hata hivyo, Zitto ndiye anaonekana kuumizwa na uhusiano huu, maana anawakera baadhi ya wanachama wenzake, na enzi za Rais Kikwete kupendwa na kushangiliwa na watu zimepita; kwani hata wana CCM wenyewe wanadai kwamba Kikwete si kete murua ya kisiasa, kwa sababu umaarufu wake umeshuka sana, hasa baada ya serikali yake kushindwa kutekeleza majukumu ya msingi na kuibua hisia hasi kutoka kwa wananchi.
      Gazeti hili lilifanya jitihada za kumpata Zitto ili aeleze jinsi alivyoandaa safari hiyo na Kikwete, na alichozungumza na Rais Kiir wa Sudan. Hakupatikana. Lakini baadhi ya viongozi wa chama chake walikiri kufahamu ziara yake hiyo ya Juba, ingawa hawakutaka kusema iliandaliwaje.
      Zitto ni mmoja wa wanasiasa vijana machachari katika CHADEMA. Ni Waziri Kivuli wa Fedha na Uchumi, ambaye kwa kushirikiana na wabunge wenzake wa CHADEMA, ameichachafya na kuishinda serikali katika suala la kufuta posho za vikao kwa watumishi wa serikali, wakiwamo wabunge.
      Akiwa nchi Sudan Kusini juzi, Zitto alituma ujumbe kupitia mtandao wa Facebook, akasema kuzaliwa kwa taifa hilo jipya kumeamsha matumaini ya wananchi kwa serikali yao.

      Source: Gazeti la Tanzania Daima
      JUNGU MTU likes this.
      Nilijitoa mhanga kwa watu wangu; watoeni watawala wadhalimu na mafisadi kwa ustawi wa nchi yetu.

    2. Miaka 50

    3. #2
      Kombo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th October 2010
      Posts : 1,825
      Rep Power : 799
      Likes Received
      455
      Likes Given
      40

      Default Re: Tanzania daima wamfagilia zitto kabwe

      Naona kama kuna tofauti kati ya Title ya thread na contents, au pengine sijaelewa lengo la mleta thread.

    4. #3
      mmbangifingi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 9th March 2011
      Posts : 2,568
      Rep Power : 857
      Likes Received
      452
      Likes Given
      2906

      Default Re: Tanzania daima wamfagilia zitto kabwe

      yeah kuna tofauti kati nya heading na contents. cjui maana ya mleta thread.ila hakuna mlingano

    5. #4
      Narubongo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd November 2010
      Posts : 1,886
      Rep Power : 810
      Likes Received
      842
      Likes Given
      680

      Default Re: Tanzania daima wamfagilia zitto kabwe

      kama taarifa hii ndiyo iliyomfanya zitto aseme hajengwi na mtu anajijenga mwenyewe basi atakuwa na matatizo, au hii ni habari mpya baada ya ile ya mwanzo? sioni tatizo wala makosa ya tz daima
      Mkwawa likes this.
      "Chadema kinatumia alama ya vidole viwili kama manati, manati kamwe haiwezi kuua tembo" Livingstone Lusinde (2012)

    6. #5
      Apta Kayla's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 17th November 2010
      Location : Dar es salaam
      Posts : 326
      Rep Power : 496
      Likes Received
      62
      Likes Given
      33

      Default

      Quote By Narubongo
      kama taarifa hii ndiyo iliyomfanya zitto aseme hajengwi na mtu anajijenga mwenyewe basi atakuwa na matatizo, au hii ni habari mpya baada ya ile ya mwanzo? sioni tatizo wala makosa ya tz daima
      Hizi ni habari 2 tofauti Mkuu.

    7. FemaTV & Radio

    8. #6
      Remote's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 20th May 2011
      Posts : 4,247
      Rep Power : 1356
      Likes Received
      942
      Likes Given
      182

      Default Re: Tanzania daima wamfagilia zitto kabwe

      Anasumbuliwa na Zittophobiasis

    9. #7
      Mkwawa's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 8th June 2011
      Location : Kalenga
      Posts : 608
      Rep Power : 3562
      Likes Received
      692
      Likes Given
      383

      Default Re: Tanzania daima wamfagilia zitto kabwe

      Quote By Narubongo
      kama taarifa hii ndiyo iliyomfanya zitto aseme hajengwi na mtu anajijenga mwenyewe basi atakuwa na matatizo, au hii ni habari mpya baada ya ile ya mwanzo? sioni tatizo wala makosa ya tz daima
      Baada ya kusoma hii habari mara kadhaa nikishtuka sana kuwa nini kilimfanya Zitto kuhamaki. Najua wajumbe wanasema kichwa cha habari akilingani na habari. Ila ukipewa habari bila kichwa cha habari unatakiwa kukipa kichwa cha habari unachoona kinafaa. Mimi nimeona Tanzania Daima wamempamba Zitto. Ila kundi la Zitti na wafuasi wake waliona Tanzania Daima imemmaliza Zitto. Ila habari hii imeandikwa vizuri na Zitto alipewa credit za kumwaga. Nilichokugundua Zitto alitishwa na kicha cha habari ambacho kilitumika kuuza habari.
      Nilijitoa mhanga kwa watu wangu; watoeni watawala wadhalimu na mafisadi kwa ustawi wa nchi yetu.

    Similar Topics

    1. Zitto adaiwa kuhongwa kuitetea CHC -Tanzania Daima
      By MJIMPYA in forum Jukwaa la Siasa
      Replies: 38
      Last Post: 10th May 2012, 12:17
    2. Zitto Kabwe kuukosa Urais wa Tanzania
      By 2015 in forum Tanzania 2010-2015
      Replies: 33
      Last Post: 12th October 2011, 21:05
    3. Zitto kabwe yuko tayari kuiokoa tanzania??
      By The Informer in forum Habari na Hoja mchanganyiko
      Replies: 2
      Last Post: 17th June 2010, 11:07
    4. Gazeti la Tanzania Daima Vs Zitto Kabwe.
      By kanda2 in forum Habari na Hoja mchanganyiko
      Replies: 4
      Last Post: 14th December 2009, 06:10

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...