Chacha Wangwe vs CHADEMA! - JamiiForums |The Home of Great Thinkers

Go Back   JamiiForums |The Home of Great Thinkers > Public Forums > Habari na Hoja mchanganyiko


Habari na Hoja mchanganyiko Una jambo umeliona kutoka chanzo chochote cha habari? Usisite, liweke hapa uwahabarishe wenzako. Hoja binafsi pia ziwekwe hapa.


Reply
 
LinkBack Thread Tools Rate Thread Display Modes
Old 20th December 2007, 06:29 AM   #1
Chacha Wangwe vs CHADEMA!
Mtu wa Pwani Mtu wa Pwani is offline 20th December 2007, 06:29 AM

wakuu wangwe ameukwaa umakamo wa chadema.

anasema matumizi ya helikopta hayana faida na mkuu wa nyumba mbowe asema itatumika mambo hayo wakuu.

nn next?
__________________
Our job is not to make up anybody's mind, but to open minds and to make the agony of the decision-making so intense you can escape only by thinking. ~Author Unknown

 
Mtu wa Pwani's Avatar
Mtu wa Pwani
JF Senior Expert Member
Points: 917,691, Level: 100 Points: 917,691, Level: 100 Points: 917,691, Level: 100
Activity: 1% Activity: 1% Activity: 1%
Join Date: Tue Dec 2006
Posts: 2,861
Thanks: 6
Thanked 8 Times in 7 Posts
Views: 41475
Reply With Quote
  #2  
Old 20th December 2007, 07:16 AM
Asha Abdala Asha Abdala is offline
Asha Abdala has no status.
JF Senior Expert Member
Points: 656,351, Level: 100 Points: 656,351, Level: 100 Points: 656,351, Level: 100
Activity: 0% Activity: 0% Activity: 0%
 
Join Date: Wed Mar 2007
Location: Zanzibar, Sometimes DSM
Posts: 1,169
Thanks: 0
Thanked 44 Times in 22 Posts
Rep Power: 26
Asha Abdala will become famous soon enoughAsha Abdala will become famous soon enoughAsha Abdala will become famous soon enoughAsha Abdala will become famous soon enoughAsha Abdala will become famous soon enoughAsha Abdala will become famous soon enoughAsha Abdala will become famous soon enoughAsha Abdala will become famous soon enough
Default Re: wangwe makamo mwenyekiti CHADEMA, apinga chopa kutumika!!!

Quote:
View Post
wakuu wangwe ameukwaa umakamo wa chadema.

anasema matumizi ya helikopta hayana faida na mkuu wa nyumba mbowe asema itatumika mambo hayo wakuu.

nn next?
CHADEMA: Hatuna mgogoro

na Tamali Vullu

Quote:
MBUNGE wa Tarime, Chacha Wangwe (CHADEMA) jana aliyameza maneno yake mbele ya waandishi wa habari na kukana taarifa zilizomhusisha yeye akikirushia tuhuma kadhaa chama chake.

Katika siku za hivi karibuni, kuelekea uchaguzi wa kujaza nafasi ya Makamu Mwenyekiti wa chama hicho Tanzania Bara, mbunge huyo, ambaye alikuwa akiwania nafasi hiyo, alinukuliwa akikituhumu chama hicho kwa ukabila na matumizi mabaya ya ruzuku.

Chacha, ambaye alifanikiwa kuinyakua nafasi hiyo, jana alikana kuhusika na baadhi ya taarifa za vyombo vya habari na kueleza kuwa hakuna mgogoro katika chama hicho kama inavyodaiwa.

Wakati Wangwe akifanya hivyo, Baraza Kuu la chama hicho, nalo lilijibu tuhuma hizo na kueleza kuwa chama hicho hakina mgogoro na ruzuku ya sh milioni 60 inayopata kila mwezi haiwezi kukigawa, kwani chama kinaweza kuendeshwa bila ruzuku.

Kauli hiyo ilitolewa na Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa, Freeman Mbowe, alipokuwa akitoa ufafanuzi kuhusu tuhuma mbalimbali dhidi ya chama hicho zilizotolewa na baadhi ya vyombo vya habari.

“CHADEMA ni chama kimoja, hakijagawanyika na hatuna mgogoro wa aina yoyote. Kuna baadhi ya vyombo vya habari vilivyo karibu na CCM vinatumika kuandika mambo yasiyokuwepo.

“Kamwe chama hakiwezi kugombanishwa na ruzuku ya serikali, kwani kimefuzu bila ruzuku. Ruzuku inachangia asilimia ndogo sana katika chama… hata ruzuku ikifutwa, CHADEMA tutakwenda mbele,” alisema Mbowe.

Alisema sehemu kubwa ya fedha zinazotumika kukiendesha chama hicho zinatokana na michango ya baadhi ya viongozi na kwamba matumizi ya fedha ya chama yanawekwa wazi kwa kiongozi yeyote anayehitaji.

Akizungumzia tuhuma za kushamiri kwa ukabila ndani ya chama hicho, pamoja na kukanusha, Mbowe alisema kuwa chama chenye ukabila ni CCM, ambacho kina mawaziri wengi wanaotoka Mkoa wa Kilimanjaro, wakati Mkoa wa Kigoma hauna mwakilishi ambaye ni waziri.

“Mkoa wa Kilimanjaro una mawaziri wanane huku ukiwa na wakazi wapatao milioni 1.2, lakini Mkoa wa Kigoma ambao una wakazi karibu milioni 1.7 hauna waziri hata mmoja… mtu hupaswi kuzungumza kama huna takwimu,” alisema.

Hata hivyo, Daniel Nsanzugwanko, ambaye ni Naibu Waziri wa Kazi, Ajira na Maendeleo ya Vijana, ni Mbunge wa CCM kutoka Mkoa wa Kigoma. Pia, Christopher Chiza ambaye ni naibu Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika naye anatokea Mkoa wa Kigoma.

Lakini, akitetea hoja yake, Mbowe alisema kuwa ingawa wabunge hao kutoka Mkoa wa Kigoma ni manaibu mawaziri, hawaingii katika vikao vya Baraza la Mawaziri, ambamo hujadiliwa masuala yenye kupanga mustakabali wa taifa na kuwa kazi yao kubwa ni kujibu maswali bungeni.

Wangwe alisema hoja nyingi zinazotolewa katika baadhi ya vyombo vya habari si sahihi na wakati mwinigine huwa hazijasemwa kama zinavyoripotiwa.

“Ndani ya chama lazima tuzungumze ili tulete changamoto kwa Watanzania kwa lengo la kujenga chama, lakini baadhi ya vyombo vya habari wanatoa hoja hizo ‘out of contents’ (nje ya mada) au wakati mwingine hazijazungumzwa kabisa,” alisema Wangwe ambaye amechaguliwa kuwa Makamu Mwenyekiti Bara, kuziba nafasi iliyoachwa wazi na Amani Walid Kabourou aliyehamia CCM.

Alisema kwamba dhana kwamba chama hicho kina mgogoro inapandikizwa na CCM kwa lengo la kutaka kuwasambaratisha.

“Ndani ya chama hatuna mgogoro, ila tuna mdahalo na tumejenga utamaduni wa kuzungumza, na mikakati yetu tunaiweka wazi, lakini baadhi ya vyombo vya habari wanaigeuza ili kuonekana kuna mgogoro,” alisema.

Alisema kama Makamu Mwenyekiti, atakuwa na ushirikiano na viongozi wengine kwa lengo la chama kushika madaraka, ili kutoa mfano kwa vyama vingine ambavyo vinafanya mambo yake kwa siri.

Akitoa taarifa ya Baraza Kuu la chama hicho lililokutana juzi, Mbowe alisema pamoja na mambo mengine, baraza limepokea, kujadili na kupitisha taarifa ya Katibu Mkuu.

Alisema Baraza Kuu limepokea na kutathmini ziara zilizowahi kufanywa kwa kutumia helikopta katika mikutano ya kuwashukuru wananchi, kuhamasisha uwajibikaji wa serikali na kujenga chama na kubaini manufaa yaliyopatikana kutokana na ziara hiyo kwa CHADEMA na kwa taifa.

“Baraza Kuu limetafakari gharama za ziara za helikopta na kuwianisha na ziara nyingine na kuazimia kwa kauli moja kuendelea na kutumia helikopta katika awamu nyingine ya ziara za CHADEMA kama ambavyo iliazimiwa pia na Mkutano Mkuu wa CHADEMA mwaka 2006,” alisema.

Alisema baraza hilo limeridhia matumizi ya helikopta, kwani si anasa na yana tija kwa Watanzania na ufanisi katika kuendeleza chama.

Mbowe alisema Baraza Kuu pia lilipokea, kujadili na kupitisha mpango kazi na bajeti kwa mwaka 2008 na kusema mpango kazi huo utahusisha shughuli ambazo zitafanywa pia na kurugenzi mbalimbali za chama katika masuala ya utawala, uenezi, habari, sheria, bunge, halmashauri, vijana, wanawake, wazee, rasilimali, oganizesheni, mafunzo na mahusiano ya kimataifa.

Aidha, baraza limeridhia umoja wa madiwani wa CHADEMA unaojumuisha madhumuni, uanachama, muundo na masuala mengine muhimu yanayohusu taratibu za umoja wa madiwani.

“Umoja huu ambao wanachama wake ni kila diwani wa CHADEMA, utawaunganisha madiwani wa CHADEMA vizuri zaidi katika kutekeleza wajibu wao katika maeneo wanayowakilisha na kwa chama kwa ujumla,” alisema.

Sambamba na hayo, pia baraza limeazimia chama kiendelee na ushirikiano wa vyama vya upinzani vya CUF, TLP na NCCR-Mageuzi kwa lengo la kudumisha demokrasia nchini, kuunganisha nguvu katika kutetea maendeleo na hatimaye upinzani kuweza kuchukua dola.

Pia baraza hilo limetoa ratiba ya uchaguzi mkuu wa CHADEMA utakaofanyika mwakani kuanzia ngazi ya vitongoji hadi taifa.

“Mwezi Januari mwakani utakuwa wa maandalizi. Februari na Machi kutafanyika uchaguzi wa vitongoji, Mei na Juni uchaguzi wa matawi na Oktoba mosi hadi 20 uchaguzi ngazi ya majimbo.

“Novemba 20 hadi 30 utakuwa uchaguzi ngazi ya wilaya na Desemba 5 hadi 10 uchaguzi ngazi ya mikoa,” alisema mwenyekiti huyo.

Alisema kuwa Kamati Kuu itakutana Desemba 12 mwakani, Baraza Kuu, siku inayofuata na Mkutano Mkuu utafanyika Desemba 14 mwakani.
Reply With Quote
  #3  
Old 20th December 2007, 09:33 AM
djwalwa's Avatar
djwalwa djwalwa is offline
djwalwa a frustrated fellow
Member
Points: 77,349, Level: 100 Points: 77,349, Level: 100 Points: 77,349, Level: 100
Activity: 0% Activity: 0% Activity: 0%
 
Join Date: Thu Sep 2007
Posts: 39
Thanks: 0
Thanked 3 Times in 1 Post
Rep Power: 0
djwalwa will become famous soon enoughdjwalwa will become famous soon enoughdjwalwa will become famous soon enoughdjwalwa will become famous soon enoughdjwalwa will become famous soon enoughdjwalwa will become famous soon enoughdjwalwa will become famous soon enoughdjwalwa will become famous soon enough
Default Re: wangwe makamo mwenyekiti CHADEMA, apinga chopa kutumika!!!

CHADEMA nao wanaboa kweli, wakiulizwa ishu zao lazima wachomekee ishu za CCM.
Reply With Quote
  #4  
Old 20th December 2007, 12:36 PM
Engineer Mohamed Engineer Mohamed is offline
Engineer Mohamed has no status.
JF Senior Expert Member
Points: 182,615, Level: 100 Points: 182,615, Level: 100 Points: 182,615, Level: 100
Activity: 0% Activity: 0% Activity: 0%
 
Join Date: Fri Jul 2007
Posts: 544
Thanks: 0
Thanked 0 Times in 0 Posts
Rep Power: 25
Engineer Mohamed will become famous soon enoughEngineer Mohamed will become famous soon enoughEngineer Mohamed will become famous soon enoughEngineer Mohamed will become famous soon enoughEngineer Mohamed will become famous soon enoughEngineer Mohamed will become famous soon enoughEngineer Mohamed will become famous soon enoughEngineer Mohamed will become famous soon enough
Default Re: wangwe makamo mwenyekiti CHADEMA, apinga chopa kutumika!!!

Quote:
View Post
wakuu wangwe ameukwaa umakamo wa chadema.

anasema matumizi ya helikopta hayana faida na mkuu wa nyumba mbowe asema itatumika mambo hayo wakuu.

nn next?

Tuwasbiri wenyewe CHADEMA waje kujibu.

lakini mie naona itakuwa kama JACOB ZUMA na THABO MBEKI.
Reply With Quote
  #5  
Old 20th December 2007, 01:07 PM
Kasana Kasana is offline
Kasana has no status.
JF Senior Expert Member
Points: 92,855, Level: 100 Points: 92,855, Level: 100 Points: 92,855, Level: 100
Activity: 0% Activity: 0% Activity: 0%
 
Join Date: Tue Apr 2007
Posts: 501
Thanks: 0
Thanked 0 Times in 0 Posts
Rep Power: 24
Kasana will become famous soon enoughKasana will become famous soon enoughKasana will become famous soon enoughKasana will become famous soon enoughKasana will become famous soon enoughKasana will become famous soon enoughKasana will become famous soon enoughKasana will become famous soon enough
Default Re: wangwe makamo mwenyekiti CHADEMA, apinga chopa kutumika!!!

Quote:
Alisema kuwa Kamati Kuu itakutana Desemba 12 mwakani, Baraza Kuu, siku inayofuata na Mkutano Mkuu utafanyika Desemba 14 mwakani.
Na hii ndiyo itakuwa siku ya uchaguzi kwa mwenyekiti taifa? au hawa wenyeviti wa vyama vya upinzani ni wa maisha?
__________________
'Facts' in the past. 'Options' in the present. 'Possibilities' in the future.
The future can not be 'predicted' but can be 'created'.
Reply With Quote
  #6  
Old 20th December 2007, 01:48 PM
Bubu Ataka Kusema's Avatar
Bubu Ataka Kusema Bubu Ataka Kusema is offline
Bubu Ataka Kusema says life is GOOD!
JF Premium Member
Points: 12,707,061, Level: 100 Points: 12,707,061, Level: 100 Points: 12,707,061, Level: 100
Activity: 50% Activity: 50% Activity: 50%
 
Join Date: Sun Feb 2007
Location: Mfaranyaki
Posts: 12,694
Thanks: 1,055
Thanked 1,211 Times in 704 Posts
Rep Power: 2049
Bubu Ataka Kusema is one of most respected JF members!Bubu Ataka Kusema is one of most respected JF members!Bubu Ataka Kusema is one of most respected JF members!Bubu Ataka Kusema is one of most respected JF members!Bubu Ataka Kusema is one of most respected JF members!Bubu Ataka Kusema is one of most respected JF members!Bubu Ataka Kusema is one of most respected JF members!Bubu Ataka Kusema is one of most respected JF members!Bubu Ataka Kusema is one of most respected JF members!Bubu Ataka Kusema is one of most respected JF members!Bubu Ataka Kusema is one of most respected JF members!
Default Re: wangwe makamo mwenyekiti CHADEMA, apinga chopa kutumika!!!

Quote:
View Post
wakuu wangwe ameukwaa umakamo wa chadema.

anasema matumizi ya helikopta hayana faida na mkuu wa nyumba mbowe asema itatumika mambo hayo wakuu.

nn next?
Huyu naona ni pandikizi la CCM na amewekwa ili kukivuruga CHADEMA. Wasipokuwa makini kweli atawavuruga. Akiendelea kuongea upupu wake ambao hauna maslahi kwa CHADEMA ni bora kumtosa tu.
__________________
~*~Life is Good~*~
Reply With Quote
  #7  
Old 20th December 2007, 02:54 PM
Kithuku Kithuku is offline
Kithuku has successfully completed his PhD
JF Senior Expert Member
Points: 251,877, Level: 100 Points: 251,877, Level: 100 Points: 251,877, Level: 100
Activity: 1% Activity: 1% Activity: 1%
 
Join Date: Sun Nov 2006
Posts: 1,165
Thanks: 2
Thanked 19 Times in 8 Posts
Rep Power: 26
Kithuku will become famous soon enoughKithuku will become famous soon enoughKithuku will become famous soon enoughKithuku will become famous soon enoughKithuku will become famous soon enoughKithuku will become famous soon enoughKithuku will become famous soon enoughKithuku will become famous soon enough
Default Re: wangwe makamo mwenyekiti CHADEMA, apinga chopa kutumika!!!

Huyu Chacha Wangwe nilikuwa namwangalia kwenye TV akiwa anawatunishia misuli bungeni kwa misimamo yake. Nadhani anajitahidi kwa kiasi chake.
__________________
"Those who cannot remember the past are condemned to repeat it." George Santayana(1863-1952), U.S Philosopher and Poet. Life of Reason, 'Reason in Common Sense', Scribners, 1905, page 284
Reply With Quote
  #8  
Old 20th December 2007, 03:06 PM
Masatu Masatu is offline
Masatu Is Magumashi
JF Senior Expert Member
Points: 733,039, Level: 100 Points: 733,039, Level: 100 Points: 733,039, Level: 100
Activity: 4% Activity: 4% Activity: 4%
 
Join Date: Mon Jan 2007
Location: Mbagala, Jeshini
Posts: 3,741
Thanks: 0
Thanked 88 Times in 66 Posts
Rep Power: 0
Masatu is infamous around these parts
Default Re: wangwe makamo mwenyekiti CHADEMA, apinga chopa kutumika!!!

Naona shule ya HULL haijamsaidia Mh Mbowe.. sijui ndio ule msemo kila unavyosoma sana ndio unakuwa mjinga zaidi... hivi M/kiti mzima anazungumza utumbo huu... eti Kilimanjaro ina mawaziri 8 halafu anaji jibu mwenyewe kuwa naibu waziri sio waziri kwani haingii ktk kikao cha Baraza la mawaziri!

Kwa msingi huo basi hiyo hesabu ya 8 kaipata wapi? bila kujumlisha na manaibu waziri tena wengine wakiwa wabunge wa Dar Es Salaam akina Mlaki. Nadhani Quantitative Method mkuu alikuwa anaikimbia pale Hull....
__________________
Mkulima kala Mbegu......
Reply With Quote
  #9  
Old 20th December 2007, 03:14 PM
Mtu wa Pwani's Avatar
Mtu wa Pwani Mtu wa Pwani is offline
Mtu wa Pwani Si Kila Kin'garacho ni dhahabu
JF Senior Expert Member
Points: 917,691, Level: 100 Points: 917,691, Level: 100 Points: 917,691, Level: 100
Activity: 1% Activity: 1% Activity: 1%
 
Join Date: Tue Dec 2006
Posts: 2,861
Thanks: 6
Thanked 8 Times in 7 Posts
Rep Power: 28
Mtu wa Pwani will become famous soon enoughMtu wa Pwani will become famous soon enoughMtu wa Pwani will become famous soon enoughMtu wa Pwani will become famous soon enoughMtu wa Pwani will become famous soon enoughMtu wa Pwani will become famous soon enoughMtu wa Pwani will become famous soon enoughMtu wa Pwani will become famous soon enough
Default Re: wangwe makamo mwenyekiti CHADEMA, apinga chopa kutumika!!!

Quote:
View Post
Naona shule ya HULL haijamsaidia Mh Mbowe.. sijui ndio ule msemo kila unavyosoma sana ndio unakuwa mjinga zaidi... hivi M/kiti mzima anazungumza utumbo huu... eti Kilimanjaro ina mawaziri 8 halafu anaji jibu mwenyewe kuwa naibu waziri sio waziri kwani haingii ktk kikao cha Baraza la mawaziri!

Kwa msingi huo basi hiyo hesabu ya 8 kaipata wapi? bila kujumlisha na manaibu waziri tena wengine wakiwa wabunge wa Dar Es Salaam akina Mlaki. Nadhani Quantitative Method mkuu alikuwa anaikimbia pale Hull....
msanii tu huyooooo
__________________
Our job is not to make up anybody's mind, but to open minds and to make the agony of the decision-making so intense you can escape only by thinking. ~Author Unknown
Reply With Quote
  #10  
Old 20th December 2007, 03:22 PM
John Mnyika's Avatar
John Mnyika John Mnyika is offline
John Mnyika has no status.
JF Senior Expert Member
Points: 454,674, Level: 100 Points: 454,674, Level: 100 Points: 454,674, Level: 100
Activity: 2% Activity: 2% Activity: 2%
 
Join Date: Fri Jun 2006
Location: Tanzania
Posts: 788
Thanks: 4
Thanked 182 Times in 61 Posts
Rep Power: 25
John Mnyika will become famous soon enoughJohn Mnyika will become famous soon enoughJohn Mnyika will become famous soon enoughJohn Mnyika will become famous soon enoughJohn Mnyika will become famous soon enoughJohn Mnyika will become famous soon enoughJohn Mnyika will become famous soon enoughJohn Mnyika will become famous soon enough
Default Re: wangwe makamo mwenyekiti CHADEMA, apinga chopa kutumika!!!

TAARIFA KWA UMMA


DONDOO ZA MAAZIMIO YA KIKAO CHA BARAZA KUU LA CHADEMA


Taarifa hii ni kuwajulisha wanachama wa CHADEMA na watanzania kwa ujumla kuwa Baraza Kuu la CHADEMA lilifanya kikao chake katika kawaida cha kila mwaka siku ya jumanne tarehe 18 Disemba 2007 katika ukumbi wa Hoteli ya Land Mark Dar es salaam.

Ajenda katika kikao hicho zilikuwa: Kuthibitisha Muktasari wa kikao cha Baraza Kuu cha tarehe 12 Agosti 2006 na yatokanayo na muktasari huo; Taarifa ya Katibu Mkuu; Taarifa ya Fedha; Mpango Kazi na Bajeti; Kanuni za Umoja wa Madiwani; Ratiba ya Uchaguzi Mkuu wa CHADEMA mwaka 2008; Taarifa ya Ushirikiano wa Vyama na Kujaza nafasi ya Makamu Mwenyekiti(Bara).

Zifuatazo ni dondoo za msingi kuhusu maazimio yaliyofikiwa na kikao cha Baraza Kuu kuhusu ajenda mbalimbali zilizojadiliwa:

Baraza kuu limepokea, kujadili na kupitisha taarifa ya Katibu Mkuu

Taarifa hii kwa pamoja na mambo mengine imejumuisha kazi mbalimbali ambazo CHADEMA imezifanya katika mwaka 2007. Taarifa hii imehusisha pia taarifa za kurugenzi mbalimbali za makao makuu ya CHADEMA. Baraza kuu limesikitishwa na taarifa potofu za magazeti zenye kulenga kujenga taswira kwamba kuna mgogoro. Baraza kuu limepokea na kutathmini Ziara ya helikopta ya kushukuru wananchi, kuhamasisha uwajibakaji wa serikali na kujenga chama na kubaini manufaa yaliyopatikana kutokana na ziara hiyo kwa CHADEMA na kwa taifa.

Baraza kuu imejadili na kupokea taarifa ya fedha ya CHADEMA

Taarifa hii imehusisha mapato na matumizi ya CHADEMA katika kipindi cha mwaka mmoja uliopita. Baraza kuu limetafakari gharama za ziara za helikopta na kuwianisha na ziara nyingine na kuazimia kwa kauli moja kuendelea na kutumia helikopta katika za awamu nyingine za CHADEMA kama ambavyo iliazimiwa pia na Mkutano Mkuu wa CHADEMA mwaka 2006.

Baraza Kuu limepokea, kujadili na kupitisha Mpango Kazi na Bajeti kwa mwaka 2008:

Mpango Kazi na Bajeti unajumuisha Shughuli mbalimbali ambazo zimepangwa kufanya katika mwaka 2008 pamoja na bajeti ya kutekeleza mpango huo. Mpango Kazi huo utahusisha shughuli ambazo zitafanywa pia na kurugenzi mbalimbali za chama katika masuala ya utawala, uenezi, habari, sheria, bunge, halmashauri,vijana, wanawake, wazee, rasilimali, oganizesheni, mafunzo, mahusiano ya kimataifa nk.

Baraza Kuu limepokea, kujadili na kuthibitisha Taratibu Umoja wa Madiwani wa CHADEMA

Mwongozo wa Umoja wa Madiwani wa CHADEMA(UMC) unajumuisha madhumuni, uanachama, muundo na masuala mengine muhimu yanayohusu taratibu za umoja wa madiwani wa CHADEMA umeridhiwa. Umoja huu ambao wanachama wake ni kila diwani wa CHADEMA utawaunganisha madiwani wa CHADEMA vizuri zaidi katika kutekeleza wajibu wao katika maeneo wanayowakilisha na kwa chama kwa ujumla.

Baraza kuu limepokea na kujadili taarifa ya ushirikiano wa vyama

Taarifa ya ushirikiano ilijumuisha makubaliano na kazi mbalimbali ambazo zimefanywa na ushirikiano wa vyama vya siasa vya upinzani vya CHADEMA, CUF, TLP na NCCR Mageuzi imepokelewa. Baraza kuu limeazimia kuwa CHADEMA iendelee na ushirikiano wa vyama kwa lengo la kudumisha demokrasia nchini, kuunganisha nguvu katika kutetea maendeleo na hatimaye upinzani kuweza kuchukua dola.

Baraza kuu limepokea, kujadili na kupitisha Ratiba ya Uchaguzi Mkuu wa CHADEMA mwaka 2008:

Ratiba ya uchaguzi mkuu wa CHADEMA imepitishwa rasmi ambapo uchaguzi utafanyika mwaka 2008. Baraza Kuu lilipitisha azimio la kutangaza ratiba ya uchaguzi(Ratiba hiyo imeambatanishwa pamoja na Taarifa hii kwa umma, maelekezo zaidi kuhusu uchaguzi huo yatatolewa baadaye).

Baraza Kuu limefanya uchaguzi na kujaza nafasi ya Makamu Mwenyekiti(Bara).

Baraza kuu lilifanya uchaguzi wa kujaza nafasi ya Makamu Mwenyekiti(Bara). Wagombea wa nafasi hiyo walikuwa: Chacha Zakaya Wangwe(Mb) aliyepata kura-56. Na Said Amour Arfi(Mb) aliyepata kura:- 38 na hakuna kura ambayo iliharibika. Hivyo kwa matokeo hayo Chacha Wangwe(Mb) alitangazwa rasmi kuwa Makamu Mwenyekiti(Bara).



Taarifa hii imetolewa 20/12/2007 na:


Freeman Mbowe
Mwenyekiti Taifa
__________________
Kizazi Kipya, Maisha Mapya
New Generation, New Life

Mabadiliko ya Kweli, Uhuru wa Kweli
Real Change, Real Freedom

John Mnyika
Reply With Quote
Reply

Bookmarks

Tags
chacha, chadema, save chadema, save democracy, save tz, wangwe


Currently Active Users Viewing This Thread: 1 (0 members and 1 guests)
 
Thread Tools
Display Modes Rate This Thread
Rate This Thread:

Posting Rules
You may not post new threads
You may not post replies
You may not post attachments
You may not edit your posts

BB code is On
Smilies are On
[IMG] code is On
HTML code is Off
Trackbacks are Off
Pingbacks are Off
Refbacks are On


Similar Threads
Thread Thread Starter Forum Replies Last Post
CHADEMA kwawaka Moto! Mbowe arudi Dar! KadaMpinzani Jukwaa la Siasa 410 1st September 2009 01:20 PM
Baada ya Kikwete ni Mbowe Mwanaidi Jukwaa la Siasa 62 19th August 2008 11:28 AM
Walinzi Wa Kampuni Binafsi Wavunja Kwa Mara Ya Pili Tawi La Chadema Kwa Shinikizo Tok John Mnyika Jukwaa la Siasa 13 6th November 2007 08:40 PM
Chacha Wangwe Kuyafikisha Mahakamani magazeti Kwa Kumchafulia Jina John Mnyika Jukwaa la Siasa 15 24th October 2007 03:35 PM
CHADEMA Imebeba utume wa Kizazi Kipya Mwanaidi Jukwaa la Siasa 19 8th June 2007 11:48 AM

Tuma Ukurasa huu kwa rafiki yako!


All times are GMT +3. The time now is 08:50 AM.

Powered by JamiiForums.com
Copyrights reserved to JamiiForums.com