Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Tuhuma za rushwa BAVICHA zipelekwe TAKUKURU - Zitto

    Report Post
    Page 1 of 19 12311 ... LastLast
    Results 1 to 20 of 376
    1. #1
      nngu007's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 2nd August 2010
      Posts : 11,669
      Rep Power : 3652
      Likes Received
      3204
      Likes Given
      473

      Default Tuhuma za rushwa BAVICHA zipelekwe TAKUKURU - Zitto

      Na Tumaini Makene

      NAIBU Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Bw. Kabwe Zitto ametoa pongezi kwa Mwenyekiti mpya wa Baraza la Vijana (BAVICHA), huku akisema kuwa atamwandikia barua katibu mkuu wake, kushauri tuhuma za kuwepo kwa vitendo vya rushwa katika uchaguzi wa juzi, zipelekwe mbele kwa hatua zaidi.

      Akizungumza na Majira jana, Bw. Zitto alisema kuwa leo atawasilisha barua hiyo kwa Katibu Mkuu wa CHADEMA, Dkt. Willibrod Slaa, kumwomba tuhuma za rushwa zifikishwe katika Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), ili zifanyiwe uchunguzi, kisha hatua za kisheria zichukuliwe kwa watakaobainika.


      "Nafikiri nitaiwasilisha kesho hiyo barua, nitamwomba katibu mkuu hizi tuhuma zifikishwe PCCB, nafikiri hiyo itakuwa ni hatua bora zaidi, PCCB wachunguze watakaobainika na makosa wachukuliwe hatua za kisheria ili iwe fundisho kwa watu wengine wote wanaojihusisha na vitendo vya namna hiyo ndani ya chama.


      "Nitatumia nafasi yangu ya Naibu Katibu Mkuu. Kwa sababu tusipofanya hivyo itaweza kujenga hisia za kuwa walioondolewa katika uchaguzi huo kwa tuhuma za rushwa wameonewa. Italeta hisia za upendeleo...kwa sababu mwenye haki ya ku-determine rushwa ni mahakama hivyo ni bora wachukuliwe hatua zaidi," alisema Bw. Zitto, ambaye pia ni Mbunge wa Kigoma Kaskazini.


      Akizungumzia ushindi wa Mwenyekiti wa BAVICHA, Bw. John Heche, alisema kuwa changamoto kubwa aliyonayo ni kuwaunganisha vijana wote na kuwa kiongozi wao, wakiwemo wale waliokuwa washindani wake na watu waliokuwa nyuma yao wakiwasapoti.


      "Nampongeza sana Heche, kwa ushindi wake alioupata. Sasa hivi ni wakati wa kukijenga chama, uchaguzi umeisha si wakati wa kulalama tena...vijana wanamtegemea atakuwa mwenyekiti wao, mimi nafikiri moja ya changamoto zake kubwa ni pamoja na kuwaunganisha vijana, wote hata walioenguliwa," alisema Bw. Zitto.


      Juzi akizungumza na Majira juu ya uchaguzi wa BAVICHA uliofanyika mwishoni mwa wiki iliyopita, Katibu Mkuu wa CHADEMA, Dkt. Slaa alisema kuwa vitendo vyote vilivyo kinyume na maadili ya kampeni kwa mujibu wa kifungu cha 10 cha katiba ya chama hicho, pamoja na waliohusika, vitajadiliwa katika ngazi ya Kamati Kuu kwa maamuzi zaidi.


      Alisema kuwa baadhi ya wagombea, hasa walioenguliwa, walibainika kwenda kinyume na maadili ya chama hicho, hasa katika kupiga vita ufisadi wa aina yoyote kama vile kufanya hila katika uchaguzi, kujenga makundi yenye kuhatarisha chama na kutaka kuvuruga uchaguzi.


    2. #2
      Nsiande's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th July 2009
      Location : dar es salaam
      Posts : 1,530
      Rep Power : 814
      Likes Received
      742
      Likes Given
      67

      Default Re: Tuhuma za rushwa Bavicha zipelekwe TAKUKURU-Zitto

      Big up Zitto!

    3. #3
      Paulo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 5th January 2009
      Location : TZ
      Posts : 337
      Rep Power : 604
      Likes Received
      33
      Likes Given
      18

      Default Re: Tuhuma za rushwa Bavicha zipelekwe TAKUKURU-Zitto

      ZT acha unafiki wewe!
      Kwa mtu mwenye akili za kawaida kabisa hashindwi kuona undumilakuwili uliofichika ktk hoja yako kaka. Uchaguzi umekwisha na sasa wajenge chama. Mambo ya kuita PCCB eti waje kuchunguza ili kuondoa manung'uniko tusiyape nafasi bali mpeni support Heche aunganishe wote walioshindwa na walioshinda ili Chama kisonge mbele mtu wangu! Acha uchonganishi wa hila!
      IN EASY TIMES ANYONE CAN MAKE MONEY BUT IN DIFFICULT TIMES YOU CAN TELL THE MEN FROM THE BOYS.

    4. #4
      genekai's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 9th February 2010
      Location : Loitering!
      Posts : 7,680
      Rep Power : 2119
      Likes Received
      1152
      Likes Given
      1601

      Default Re: Tuhuma za rushwa Bavicha zipelekwe TAKUKURU-Zitto

      Yah ni mawazo mazuri mkuu zito ili kuondoa huu uozo kama upo!
      The future of this country is being jeopardized by the intellectual slavery of our top leaders

    5. #5
      LINCOLINMTZA's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 15th March 2011
      Location : Opposite The JF Web Page
      Posts : 1,399
      Rep Power : 706
      Likes Received
      373
      Likes Given
      224

      Default Re: Tuhuma za rushwa Bavicha zipelekwe TAKUKURU-Zitto

      Panapokuwa na Uchaguzi, minyukano haikosekani. Lakini kuiendeleza minyukano baada ya uchaguzi ni kutaka kuvuruga Chama tu. Sifikiri kama Zitto anayosema yanalengo la kushitaki waliotoa rushwa au kuwasafisha watuhumiwa.

      Naamini atakuwa upande mmoja wapo hapo juu. Yeye kama kiongozi alitakiwa kuwashauri wagombea walioshindwa kuunganisaha nguvu kujenga chama na wala siyo kuleta utengano wa kutafuta nani katoa rushwa au vipi. Nakuomba mh. Zitto uridhike na matokeo na hao wanaonung'unika washawishi wakumbali matokeo ingawa kila iliyeingia kwenye kinyang'iro aliamini atashinda, lakini anatakiwa mmoja tu.

      Naomba waeleshwe hao vijana hayo na kutumikia chama siyo lazima uwe mwenyekiti unless otherwise awe anatafuta kazi ya umwenyekiti na wala siyo cheo cha umwenyekiti.
      Haika likes this.


    6. #6
      Ibra Mo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th October 2010
      Posts : 614
      Rep Power : 564
      Likes Received
      49
      Likes Given
      3

      Default Re: Tuhuma za rushwa Bavicha zipelekwe TAKUKURU-Zitto

      Ili kukomesha hiyo Tabia na iwapo ushahidi unajitosheleza Chama moja kwa moja kupitia wanasheria wake kiwafikishe Mahakamani ila hilo lakupitia Takukuru siliafiki kwanza hii Taasisi imeoza na haiaminiki pia hawana Historia yakushinda Kesi yoyote ya Rushwa ya Mwakalebela juzi tu hapa wamechemsha sasa wa nini hawa.

    7. #7
      paulss's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th August 2009
      Posts : 3,635
      Rep Power : 4411
      Likes Received
      1105
      Likes Given
      986

      Default Re: Tuhuma za rushwa Bavicha zipelekwe TAKUKURU-Zitto

      Mvutana wa makundi mawili ndani ya chama ndio huu, kundi la akina mbowe linadaiwa kutumia rafu kumpitisha mtu wao bache ili hali kundi la akina zitto mtu wao akipigwa chini kimizengwe.

      Zitto na kundi lake hawajakubali matokeo mioyoni na ndio maana anataka baraka ili liwasilishwe takukuru, lakini katibu mkuu wake amesha sema wazi matatizo yote ya uchaguzi yatajadiliwa na kamati kuu.
      kazi kweli kweli
      Independent thinker
      Humu jf baadhi yetu wametengeneza haki miliki ya they way they think, you have to think like them and have drawn a line of where one has to belong, you are either "with us" or "against us", if you don't sail the same boat then you are an enemy!. -Pasco wa JF

    8. #8
      ngurati's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 14th February 2011
      Posts : 202
      Rep Power : 467
      Likes Received
      208
      Likes Given
      4

      Default Re: Tuhuma za rushwa Bavicha zipelekwe TAKUKURU-Zitto

      NAIBU Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Bw. Kabwe Zitto ametoa pongezi kwa Mwenyekiti mpya wa Baraza la Vijana (BAVICHA), huku akisema kuwa atamwandikia barua katibu mkuu wake, kushauri tuhuma za kuwepo kwa vitendo vya rushwa katika uchaguzi wa juzi, zipelekwe mbele kwa hatua zaidi.

      Akizungumza na Majira jana, Bw. Zitto alisema kuwa leo atawasilisha barua hiyo kwa Katibu Mkuu wa CHADEMA, Dkt. Willibrod Slaa, kumwomba tuhuma za rushwa zifikishwe katika Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), ili zifanyiwe uchunguzi, kisha hatua za kisheria zichukuliwe kwa watakaobainika.

      "Nampongeza sana Heche, kwa ushindi wake alioupata. Sasa hivi ni wakati wa kukijenga chama, uchaguzi umeisha si wakati wa kulalama tena...vijana wanamtegemea atakuwa mwenyekiti wao, mimi nafikiri moja ya changamoto zake kubwa ni pamoja na kuwaunganisha vijana, wote hata walioenguliwa," alisema Bw. Zitto.

      Alisema kuwa baadhi ya wagombea, hasa walioenguliwa, walibainika kwenda kinyume na maadili ya chama hicho, hasa katika kupiga vita ufisadi wa aina yoyote kama vile kufanya hila katika uchaguzi, kujenga makundi yenye kuhatarisha chama na kutaka kuvuruga uchaguzi.
      Acha unafiki zitto, tunaomba na wewe uangalie kwenye simu yako tarehe 3 mwezi may 2011, hii kumbukumbu namba ya MPESA uliyomtumia mmoja wa wagombea aliyeenguliwa ilikuwa ni ya nini??? Kumb namba ni hii hapa - B66FE724.

      Ukiendelea nitaweka mpaka kiasi cha pesa ulichotuma. Najua ulikuwa humuungi mkono heche tangu uchaguzi wa mwaka 2009 ulioharibika. Tafadhali sana iache BAVICHA hii ya kwanza ya kitaifa ifanye kazi.
      Masanilo, Mponjoli and eliesikia like this.

    9. #9
      ngurati's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 14th February 2011
      Posts : 202
      Rep Power : 467
      Likes Received
      208
      Likes Given
      4

      Default Re: Tuhuma za rushwa Bavicha zipelekwe TAKUKURU-Zitto

      Quote By paulss
      Mvutana wa makundi mawili ndani ya chama ndio huu, kundi la akina mbowe linadaiwa kutumia rafu kumpitisha mtu wao bache ili hali kundi la akina zitto mtu wao akipigwa chini kimizengwe.
      Zitto na kundi lake hawajakubali matokeo mioyoni na ndio maana anataka baraka ili liwasilishwe takukuru, lakini katibu mkuu wake amesha sema wazi matatizo yote ya uchaguzi yatajadiliwa na kamati kuu.
      kazi kweli kweli
      Hakuna mtu aneyeitwa bache, nahisi wewe ni mwana ccm na unafananisha heche na hussein bashe wa uvccm.

    10. #10
      TUMBIRI's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 7th May 2011
      Posts : 1,876
      Rep Power : 3641
      Likes Received
      1149
      Likes Given
      288

      Default Re: Tuhuma za rushwa Bavicha zipelekwe TAKUKURU-Zitto

      Kabla ya kujadili hoja ya Zitto, tujiulize. Mwaka jana wakati Fedrick Mwakalebela anatafuta kura za maoni za kugombea Ubunge wa Iringa Mjini na alipopatwa na tuhuma za kutoa rushwa katika minyukano ya kusaka kura za maoni, Je ni CCM iliyompeleka TAKUKURU au ni TAKUKURU ndiyo iliyomdaka?

      TAKUKURU kama taasisi ya kupambana na rushwa imesoma na kusikia kupita kwenye vyombo vya habari juu ya tuhuma za rushwa dhidi ya wagombea wa CDM. Wao ndio wanapaswa wawakamate wote wanaotuhumiwa na kuanza kufanyia kazi tuhuama dhidi yao. Au watuhumiwa wenyewe wajisalimishe TAKUKURU ili wakafanyiwe uchunguzi hatimae wasafishwe kama wanataka.

      Si kazi ya CDM kufanya kazi ya TAKUKURU unless tukubaliane kwamba TAKUKURU yetu ni SIKIO la kufa. Haisomi magazeti wala haisikilizi Radio na TV.

      Tuendelee kujadiliana!

      By TUMBIRI mtoto wa NYANI.
      mchonga and jouneGwalu like this.

    11. #11
      babap's Avatar
      Member Array
      Join Date : 22nd April 2011
      Posts : 63
      Rep Power : 425
      Likes Received
      11
      Likes Given
      0

      Default

      Quote By Paulo
      ZT acha unafiki wewe!
      Kwa mtu mwenye akili za kawaida kabisa hashindwi kuona undumilakuwili uliofichika ktk hoja yako kaka. Uchaguzi umekwisha na sasa wajenge chama. Mambo ya kuita PCCB eti waje kuchunguza ili kuondoa manung'uniko tusiyape nafasi bali mpeni support Heche aunganishe wote walioshindwa na walioshinda ili Chama kisonge mbele mtu wangu! Acha uchonganishi wa hila!
      ni kweli kabisa kuwa ZITO anayo hiden agenda ya kutaka kuleta malumbano ndani ya chama. Haihitaji mtu kufika form four kuliona hili.

    12. #12
      Galula Jr's Avatar
      Member Array
      Join Date : 15th April 2011
      Posts : 44
      Rep Power : 422
      Likes Received
      3
      Likes Given
      1

      Default Re: Tuhuma za rushwa Bavicha zipelekwe TAKUKURU-Zitto

      Ni vizuri lakini je, hao PCCB wanaaminika kwa lipi kaka Zitto? Tusije mpa mbu kazi ya kutibu maleria kaka yangu

    13. FJM
      #13
      FJM's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th April 2011
      Posts : 7,213
      Rep Power : 2580
      Likes Received
      5344
      Likes Given
      4607

      Default Re: Tuhuma za rushwa Bavicha zipelekwe TAKUKURU-Zitto

      Quote By nngu007
      Na Tumaini Makene

      NAIBU Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Bw. Kabwe Zitto ametoa pongezi kwa Mwenyekiti mpya wa Baraza la Vijana (BAVICHA), huku akisema kuwa atamwandikia barua katibu mkuu wake, kushauri tuhuma za kuwepo kwa vitendo vya rushwa katika uchaguzi wa juzi, zipelekwe mbele kwa hatua zaidi.


      "Nafikiri nitaiwasilisha kesho hiyo barua, nitamwomba katibu mkuu hizi tuhuma zifikishwe PCCB, nafikiri hiyo itakuwa ni hatua bora zaidi, PCCB wachunguze watakaobainika na makosa wachukuliwe hatua za kisheria ili iwe fundisho kwa watu wengine wote wanaojihusisha na vitendo vya namna hiyo ndani ya chama.

      "Nitatumia nafasi yangu ya Naibu Katibu Mkuu.
      I dont understand kwa nini Zitto anaongea as if hakuwepo kwenye uchaguzi. Huyu mtoto amekuwa na kasumba ya kuongea na vyombo vya habari mambo ambayo kimsingi ni Internal communications! Kama anataka kumuandikia barua kiongozi ndani ya chama chake kwa nini akasemee majira? Zitto is bad news kwa CHADEMA through & through!
      Last edited by FJM; 31st May 2011 at 16:35.

    14. #14
      Mshindo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 5th March 2009
      Location : Right Here!!
      Posts : 436
      Rep Power : 615
      Likes Received
      145
      Likes Given
      194

      Default Re: Tuhuma za rushwa Bavicha zipelekwe TAKUKURU-Zitto

      Sounds good, mature and credits for advocacy for the rule of law. But bearing in mind this TAKUKURU that I know,the level of democracy in this country and the credibility of our judicial systems; and amid the political mitafutano going on between the ruling party (practical the owner of PCCB and the judiciary) and our dear CDM.....BIG NO!! BIG NO!!!
      Kesi ya mbuzi unampelekea simba?
      lebabu11 likes this.
      Sent from @non-smart phone.....bear with me

    15. #15
      Mdau's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th March 2008
      Posts : 1,120
      Rep Power : 801
      Likes Received
      86
      Likes Given
      72

      Default Re: Tuhuma za rushwa Bavicha zipelekwe TAKUKURU-Zitto

      Ni hoja nzuri, lakini ukizingatia na historia ya PCCB katika miaka ya karibuni, sidhani kama hatua muafaka zitachukuliwa...

    16. #16
      paulss's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th August 2009
      Posts : 3,635
      Rep Power : 4411
      Likes Received
      1105
      Likes Given
      986

      Default Re: Tuhuma za rushwa Bavicha zipelekwe TAKUKURU-Zitto

      Msiwe na wasi wasi kuhusu TAKUKURU, ikihudumia kesi za ccm inaangalia maslahi ya aliyowateua, lakini kwa cdm hawana maslahi yoyote hivyo watatenda haki
      Independent thinker
      Humu jf baadhi yetu wametengeneza haki miliki ya they way they think, you have to think like them and have drawn a line of where one has to belong, you are either "with us" or "against us", if you don't sail the same boat then you are an enemy!. -Pasco wa JF

    17. #17
      TzPride's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd November 2006
      Location : Downhole
      Posts : 1,659
      Rep Power : 977
      Likes Received
      177
      Likes Given
      72

      Default Re: Tuhuma za rushwa Bavicha zipelekwe TAKUKURU-Zitto

      Kupeleka tuhuma TAKUKURU ni kupeleka kwenye Chama Cha Magamba....Takukuru ni sehemu ya vitengo vya CCM. Zitto fikiri kwa usahihi...usirukie umaarufu ukasahau kuwa sensible. Kama kulikuwa na rushwa...CDM wachunguzane wachukuliane hatua...TUKUKURU wakitaka waingie kivyao sio kuwapelekea....kijichama kichanga hiki hata GAMBA hakina....kitakula mweleka hicho...oooh!
      " Counting down on CCM downfall.

    18. #18
      Facts1's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 23rd December 2009
      Posts : 308
      Rep Power : 543
      Likes Received
      16
      Likes Given
      3

      Default Re: Tuhuma za rushwa Bavicha zipelekwe TAKUKURU-Zitto

      Zitto acha unafiki wewe ulisusia uchaguzi sasa baada ya uchaguzi kinakuhusu nini kwa nini usiseme walioandaa uchaguzi watayashughulikia, katibu mkuu ameshasema matatizo yote yatashughulikiwa na kamati kuu sasa wewe kama hukuridhika tangulia mahakamani au Takukuru mwenyewe au wape hela tena za mahakama kama ulivyowapa za kampeni.

      Mambo ya chama kwa nini unayapeleka kwenye magazeti kwanini hiyo barua usiipeleke kwenye chama hadi utangaze magazetini, Zitto my friend tumekuvumilia sana na siasa zako za makundi karibu tutafika mwisho, uchaguzi wa Bavicha uliopita ni wewe ulisababisha kuvunjika leo wenzako wamefanikisha wakati wewe umesusa unataka tena kutuletea makundi jiangalie unakokwenda.
      Democracy is a device that ensures we shall be governed no better than we deserve

    19. #19
      Lu-ma-ga's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st September 2010
      Posts : 1,916
      Rep Power : 830
      Likes Received
      540
      Likes Given
      8

      Default Re: Tuhuma za rushwa Bavicha zipelekwe TAKUKURU-Zitto

      Quote By Facts1
      Zitto acha unafiki wewe ulisusia uchaguzi sasa baada ya uchaguzi kinakuhusu nini kwa nini usiseme walioandaa uchaguzi watayashughulikia, katibu mkuu ameshasema matatizo yote yatashughulikiwa na kamati kuu sasa wewe kama hukuridhika tangulia mahakamani au Takukuru mwenyewe au wape hela tena za mahakama kama ulivyowapa za kampeni.

      Mambo ya chama kwa nini unayapeleka kwenye magazeti kwanini hiyo barua usiipeleke kwenye chama hadi utangaze magazetini, Zitto my friend tumekuvumilia sana na siasa zako za makundi karibu tutafika mwisho, uchaguzi wa Bavicha uliopita ni wewe ulisababisha kuvunjika leo wenzako wamefanikisha wakati wewe umesusa unataka tena kutuletea makundi jiangalie unakokwenda.
      Zitto kama analeta uozo wa kimagamba nadhani hataweza, intelijensia ya CDM kwa sasa ni zaidi ya ile ya magamba, ZT yuko kwenye darubini tunamcheck vizuri, akithubutu tuuuuu atashughulikiwa kama alivyoshughulikiwa yule jamaa wa FIFA.CDM ni kama FIFA ya SEpp Blater.

    20. #20
      MAFILILI's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 28th April 2011
      Posts : 1,446
      Rep Power : 461
      Likes Received
      302
      Likes Given
      64

      Default Re: Tuhuma za rushwa Bavicha zipelekwe TAKUKURU-Zitto

      Quote By Lu-ma-ga
      Zitto kama analeta uozo wa kimagamba nadhani hataweza, intelijensia ya CDM kwa sasa ni zaidi ya ile ya magamba, ZT yuko kwenye darubini tunamcheck vizuri, akithubutu tuuuuu atashughulikiwa kama alivyoshughulikiwa yule jamaa wa FIFA.CDM ni kama FIFA ya SEpp Blater.
      CDM msiwe wanafiki mwaka jana mlikuwa mnashupalia CCM walipoalila TAKUKURU katika uchaguzi wao wa ndani. Kama mpo safi kwa nini mwaogopa kuialika TAKUKURU au kwa sababu rushwa ilitolewa kama njugu kwa uwezeshaji wa mwenyekiti wa Chama HIVYO mwaona so. Kuweni na UJASIRI pelekeni maombi kwa TAKUKURU ili ukweli ujulikane, ZK mpeni pongezi kwa wazo zuri!

    Page 1 of 19 12311 ... LastLast

    Similar Topics

    1. Replies: 3
      Last Post: 19th November 2011, 06:52
    2. TAKUKURU: Chenge hahusiki na tuhuma za RADA
      By nickname in forum Jukwaa la Siasa
      Replies: 137
      Last Post: 23rd November 2010, 19:19
    3. TAKUKURU yachunguza tuhuma za Kabwe na Slaa
      By BAK in forum Jukwaa la Siasa
      Replies: 3
      Last Post: 26th August 2007, 07:51

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...