Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Propaganda Za Mitandao

    Report Post
    Results 1 to 4 of 4
    1. Shy is offline
      Shy
      #1
      Shy's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd November 2006
      Posts : 4,922
      Rep Power : 0
      Likes Received
      76
      Likes Given
      0

      Default Propaganda Za Mitandao

      PROPAGANDA ZA MITANDAO

      Mwaka jana niliwahi kuandika makala moja kuhusu propaganda za mitandao katika makala hiyo niliongelea kidogo kuhusu baadhi ya watu kwa kusukumwa na ushabiki wao wa kitu fulani , uhuni wao tu , ugonjwa tu , na matatizo yao mengine mbali mbali waliyonayo wanaamua kukaa katika computer zao na kuanza kuandika na kusambaza habari mbaya kuhusu watu wengine , vikundi au kampuni za wengine kwa makusudi kabisa bila kuwa na udhibitisho na habari hizo .

      Watu hawa wana blogu wengine ni maarufu katika forum za watanzania na wengine wanaaminika sana kiasi kwamba wakisema chochote kwa manufaa yao basi watu wote huwafuata wao na kusikiliza kile wao wanachosema hata kama sio kwa masilahi ya taifa hili tukufu la Tanzania .

      Wananchi wanaosoma blogu hizi , forum hizi na aina nyingi ya vipeperusi wawe makini sana na matangazo yao , watu hawa hawana nia njema kwa maisha ya watanzania walio wengi , wanaharifu fani ya habari na taaluma yake kwa ujumla na ndio maana wanatumia majini tofauti tofauti kujitetea au kuhalalisha hizo habari zao .

      Ni kweli mtandao hauna mipaka , kabila dini wala chama lakini wengi wao wanaonekana kuishushia hadhi serikali ya tanzania , baadhi ya viongozi wa serikali pamoja na chama tawala chama cha mapinduzi kwa propaganda zao ambazo hazina masilahi yoyote

      Tunaheshimu uhuru wa mtu kusema au kuandika chochote katika mtandao lakini mtu anapofikia kutuma habari za uwongo zinazochochea vurugu na fujo nyingine katika jamii mtu au kundi hilo la watu hatutalivumilia wala kulikalia kimya

      Watatafutwa na kufikichwa katika vyombo vya sheria ili iwe fundisho kwa wengine wenye tabia kama hizi za kusambaza habari za uwongo , chuki na visasi


    2. #2
      BabaH's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 25th January 2008
      Location : Ikulu-Magogoni
      Posts : 694
      Rep Power : 720
      Likes Received
      7
      Likes Given
      0

      Default Re: Propaganda Za Mitandao

      Usitake kutisha watu wewe kibaraka mkubwa wa Mafisadi
      Na wewe unaweza kuwa mmoja wapo wa propaganda za Mtandao, na eti unajiita Researcher??
      Haya vielelzo vya hayo maneno yako kuwa watu wanaandika habari za uongo kuhusu serikali, viongozi, na chama tawala viko wapi?

      Hivi wewe ndio unasema kweli eti unaliteta taifa na wananchi wake??
      Acha unafiki na ufaidhina wewe, wewe unawezekana punguani kabisa, unaacha kufanya mambo ya muhimu ya kuwafikisha mafisadi kwenye sheria unakuja na porojo za kutisha watu!!

      Sasa tutaendelea kuisema serikali pale inapokosea , viongozi wake, na chama chenu cha Mifisadi, ukiona kama ni uongo weka vigezo na kuwahakikishia wananchi kuwa hii sio kweli, sio kuja na kuleta porojo hapa!
      IKO SIKU BUBU WATASEMA, VIZIWI WATASIKIA NA MOTO UTAWAKA

    3. BAK is offline
      BAK
      #3
      BAK's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th February 2007
      Location : Mfaranyaki
      Posts : 26,827
      Rep Power : 45014
      Likes Received
      8683
      Likes Given
      8666

      Default Re: Propaganda Za Mitandao

      Quote By BabaH View Post
      Usitake kutisha watu wewe kibaraka mkubwa wa Mafisadi
      Na wewe unaweza kuwa mmoja wapo wa propaganda za Mtandao, na eti unajiita Researcher??
      Haya vielelzo vya hayo maneno yako kuwa watu wanaandika habari za uongo kuhusu serikali, viongozi, na chama tawala viko wapi?

      Hivi wewe ndio unasema kweli eti unaliteta taifa na wananchi wake??
      Acha unafiki na ufaidhina wewe, wewe unawezekana punguani kabisa, unaacha kufanya mambo ya muhimu ya kuwafikisha mafisadi kwenye sheria unakuja na porojo za kutisha watu!!

      Sasa tutaendelea kuisema serikali pale inapokosea , viongozi wake, na chama chenu cha Mifisadi, ukiona kama ni uongo weka vigezo na kuwahakikishia wananchi kuwa hii sio kweli, sio kuja na kuleta porojo hapa!
      Thank you BabaH. You made my day and there is nothing more to add.
      Let your graceful words fly out into the World, carried on winds of courage, imagination and joy. Let them inspire others to step into action

    4. #4
      Richard's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 23rd October 2006
      Location : LANGLEY
      Posts : 2,332
      Rep Power : 1114
      Likes Received
      502
      Likes Given
      1783

      Default Re: Propaganda Za Mitandao

      Mkuu, Shy

      Hii haijatulia kabisa na kwa maana ya jina ulilolichagua la Shy linaendana na mtindo wako wa kupachika hoja hapa jamvini na kukimbia pembeni ili uone what the reaction will be.

      Unataka kuwa jasusi? Tazama movie za "Recruit", "Training Day" na hizo ni baadhi tu na zinafundisha kuwa mwangalifu na mtindo wa kufuata mikumbo na ushawishi usio na maana, ili mradi tu unataka kuwa mtu fulani.

      Mtindo wa kutishia watu bila sababu za msingi ni ujinga kama si upumbavu. Kama hujui ni kwamba kuna tofauti kubwa kati ya mtu mjinga na yule mpumbavu. Kwa hio jinsi ukakavoendelea kuleta hoja zako zisizo kichwa wala miguu, unaweza ukajikuta una-fit katika moja ya hizo "criterias".

      Kwanza ni nani amekutuma kuleta hio ajenda yako hapa?

      Wakikutuma tena wewe changanua kwanza kabla ya kuanza kuandika hayo mambo yako ya ajabu.
      When thinking about my risk assessment, I always remember:
      HAZARD and the RISK .

    Similar Topics

    1. Mitandao Ya Jamii.
      By Jacobus in forum Habari na Hoja mchanganyiko
      Replies: 2
      Last Post: 3rd November 2011, 23:08
    2. Mitandao ya simu
      By chimala in forum Habari na Hoja mchanganyiko
      Replies: 3
      Last Post: 28th October 2011, 15:44
    3. Kabla ya mitandao
      By Mabagala in forum Jamii Photos
      Replies: 25
      Last Post: 1st October 2011, 18:13
    4. Propaganda
      By Dec in forum JF Chit-Chat
      Replies: 0
      Last Post: 11th September 2011, 20:35
    5. Mitandao ya Kijasusi
      By X-PASTER in forum Habari na Hoja mchanganyiko
      Replies: 41
      Last Post: 4th May 2009, 11:25

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...