Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Picha za Facebook Zasababisha Anyimwe Pasipoti

    Report Post
    Results 1 to 6 of 6
    1. #1
      kilimasera's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd December 2009
      Posts : 3,038
      Rep Power : 1098
      Likes Received
      184
      Likes Given
      246

      Default Picha za Facebook Zasababisha Anyimwe Pasipoti

      Mwanaume mmoja toka nchini India ambaye alijifanya yeye ni mkimbizi toka Tibet ili aweze kupata 'makaratasi' ya nchini Australia, amefikishwa mahakamani baada ya picha zake alizoziweka kwenye Facebook kuonyesha kuwa yeye ni raia wa India.
      Mwanaume huyo ambaye jina lake halikutajwa kwa sababu za kisheria, aliingia nchini Australia mwaka 2009 kwa kutumia pasipoti ya India na kisha kwenda kujilipua kwa kujifanya yeye ni mkimbizi toka Tibet.

      Mwanaume huyo alidai kuwa yeye ni mtoto wa mwanaharakati wa kutetea haki za watu wa Tibet ambaye alikimbia toka Tibet mwaka 1991 kuukimbia ukatili wa utawala wa China nchini Tibet.

      Aliendelea kusema kuwa alilelewa katika kambi ya wakimbizi nchini Nepal ambako pia alimaliza elimu yake ya msingi.

      "Kama nikirudi Nepal, serikali ya Nepal itauruhusu utawala wa China nchini Tibet unichukue hivyo watanitesa na hatimaye kuniua", alisema mwanaume huyo wakati wa kujilipua kabla ya siri zake kufichuka hivi karibuni.

      Hata hivyo picha zake kwenye mtandao wa Facebook zikimuonyesha akiwa na wanafunzi wenzake nchini India zimepelekea maombi yake ya kupewa uhalali wa kuishi Australia kukataliwa.

      Mwanaume huyo alifikishwa mahakamani ambapo mahakama ilionyeshwa picha zake kwenye Facebook zikimuonyesha akiwa amevaa unifomu za shule moja iliyopo katika mji wa Bengal nchini India.

      Katika profile yake ya Facebook mwanaume huyo alijitambulisha kuwa amemaliza masomo yake nchini India.

      Mojawapo ya picha zake kwenye facebook ilimuonyesha mwanaume huyo akiwa pamoja na dada yake wakiwa wamevaa unifomu za shule wakiwa kwenye bustani ambayo nyuma yake kulikuwa na bango lenye maandishi ya Kihindi.

      Picha zake zingine kwenye mtandao wa Hi5 zilimuonyesha akiwa amevaa unifomu za shule akiwa amepozi pamoja na wanafunzi wenzake wa nchini India.

      Mahakama iliambiwa kuwa uchunguzi wa polisi umeonyesha kuwa mwanaume huyo ni raia wa India na anamiliki pasipoti ya India na wala si mkimbizi wa Tibet kama alivyodai baada ya kuwasili nchini humo.

      Madai yake ya ukimbizi yamekataliwa huku mwanaume huyo akikabiliwa na kesi nyingine ya udanganyifu.

    2. Miaka 50

    3. #2
      Nazjaz's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 20th January 2011
      Posts : 2,865
      Rep Power : 1713
      Likes Received
      790
      Likes Given
      221

      Default Re: Picha za Facebook Zasababisha Anyimwe Pasipoti

      ukitaka kudanganya, haribu asili yako yote.

    4. #3
      kilimasera's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd December 2009
      Posts : 3,038
      Rep Power : 1098
      Likes Received
      184
      Likes Given
      246

      Default Re: Picha za Facebook Zasababisha Anyimwe Pasipoti

      asili haipotei kuna siku utadakwa tu Nazjaz
      Quote By Nazjaz
      ukitaka kudanganya, haribu asili yako yote.

    5. #4
      Katavi's Avatar
      JF Bronze Member Array
      Join Date : 31st August 2009
      Location : Lyamba Lya Mfipa
      Posts : 19,636
      Rep Power : 16776
      Likes Received
      2513
      Likes Given
      1934

      Default Re: Picha za Facebook Zasababisha Anyimwe Pasipoti

      Ukiwa muongo usiwe msahaulifu. Hakujipanga vizuri katika kudanganya!

    6. #5
      kilimasera's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd December 2009
      Posts : 3,038
      Rep Power : 1098
      Likes Received
      184
      Likes Given
      246

      Default Re: Picha za Facebook Zasababisha Anyimwe Pasipoti

      hii teknolojia ya internet inafichua mambo mengi sana hasa hizi social networks katavi we subiri tu tutajua mengi sana sema kwa nchi kama bongo wenye access ya net ni wachache sana!so informations za watu wengi hazijulikani
      Quote By Katavi
      Ukiwa muongo usiwe msahaulifu. Hakujipanga vizuri katika kudanganya!

    7. RukaaJuu Final

    8. #6
      Inkoskaz's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 6th November 2010
      Location : URT
      Posts : 4,420
      Rep Power : 7353
      Likes Received
      1073
      Likes Given
      1102

      Default Re: Picha za Facebook Zasababisha Anyimwe Pasipoti

      Thinking is the hardest work there is,which is probably the reason why so few engage in it!!

    Similar Topics

    1. Hongera kwa JK zasababisha Bushoke kuzomewa tamasha la Fiesta
      By mafinga kwetu in forum Jukwaa la Siasa
      Replies: 60
      Last Post: 1st August 2011, 14:24
    2. Pasipoti zetu
      By Ogah in forum Habari na Hoja mchanganyiko
      Replies: 8
      Last Post: 17th August 2009, 19:34

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...