Mwanaume mmoja toka nchini India ambaye alijifanya yeye ni mkimbizi toka Tibet ili aweze kupata 'makaratasi' ya nchini Australia, amefikishwa mahakamani baada ya picha zake alizoziweka kwenye Facebook kuonyesha kuwa yeye ni raia wa India.
Mwanaume huyo ambaye jina lake halikutajwa kwa sababu za kisheria, aliingia nchini Australia mwaka 2009 kwa kutumia pasipoti ya India na kisha kwenda kujilipua kwa kujifanya yeye ni mkimbizi toka Tibet.
Mwanaume huyo alidai kuwa yeye ni mtoto wa mwanaharakati wa kutetea haki za watu wa Tibet ambaye alikimbia toka Tibet mwaka 1991 kuukimbia ukatili wa utawala wa China nchini Tibet.
Aliendelea kusema kuwa alilelewa katika kambi ya wakimbizi nchini Nepal ambako pia alimaliza elimu yake ya msingi.
"Kama nikirudi Nepal, serikali ya Nepal itauruhusu utawala wa China nchini Tibet unichukue hivyo watanitesa na hatimaye kuniua", alisema mwanaume huyo wakati wa kujilipua kabla ya siri zake kufichuka hivi karibuni.
Hata hivyo picha zake kwenye mtandao wa Facebook zikimuonyesha akiwa na wanafunzi wenzake nchini India zimepelekea maombi yake ya kupewa uhalali wa kuishi Australia kukataliwa.
Mwanaume huyo alifikishwa mahakamani ambapo mahakama ilionyeshwa picha zake kwenye Facebook zikimuonyesha akiwa amevaa unifomu za shule moja iliyopo katika mji wa Bengal nchini India.
Katika profile yake ya Facebook mwanaume huyo alijitambulisha kuwa amemaliza masomo yake nchini India.
Mojawapo ya picha zake kwenye facebook ilimuonyesha mwanaume huyo akiwa pamoja na dada yake wakiwa wamevaa unifomu za shule wakiwa kwenye bustani ambayo nyuma yake kulikuwa na bango lenye maandishi ya Kihindi.
Picha zake zingine kwenye mtandao wa Hi5 zilimuonyesha akiwa amevaa unifomu za shule akiwa amepozi pamoja na wanafunzi wenzake wa nchini India.
Mahakama iliambiwa kuwa uchunguzi wa polisi umeonyesha kuwa mwanaume huyo ni raia wa India na anamiliki pasipoti ya India na wala si mkimbizi wa Tibet kama alivyodai baada ya kuwasili nchini humo.
Madai yake ya ukimbizi yamekataliwa huku mwanaume huyo akikabiliwa na kesi nyingine ya udanganyifu.

Reply With Quote



Follow Us Here