Hivi karibuni kumekuwa na matangazo mbalimbali yakitoka kwenye mabango na Television lakini hayabebi uhalisia kutokana na muonekano wa washiriki wa matangazo hayo
Mfano:
kama umebahatika kupita maeneo ya sinza Afrika sana karibu kabisa na kona baa(corner bar/Ambianze night club)
kuna bango moja kubwa lenye Tangazo la mtoto wa mwenzio ni wako,linalohamasisha watu wazima kuacha kuwatongoza watoto wa shule
Tatizo ni kwamba huyo mtoto wa shule mwenyewe hana uhalisia wa kuwa mtoto wa shule,yani kuanzia mavazi hadi muenekano wake hauendani kabisa na kinachotangazwa kwenye bango hilo
Mfano wa pili:
Kama ni muangaliaji mzuri wa Television kuna matangazo mawili moja likimuonesha mwanafunzi akitumia simu darasani wakati mwalimu akifundisha na la pili likimuonesha muhusika huyohuyo aliyekatazwa kutumia simu shuleni akiwa amerudishwa nyumbani kwa kosa la kukutwa na simu shuleni
Tatizo pia linakuja muhusiaka habebi muonekano wa kiuanafunzi,yani zaidi ya mwanafunzi
Kama umeshawahi kuona hayo matangazo niliyoyasema hapo juu,unadhani ni kweli hayo matangazo yanabeba maudhui au maana halisi ya matangazo hayo,sababu wahusika wenyewe hawabebi ujumbe kwa muonekano wao
Ni mawazo tu naomba mawazo yako tafadhari labda mimi nimekuwa rigid sana.........

Reply With Quote
Follow Us Here