Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Nyati amuua 'jangili' Hifadhi ya Taifa

    Report Post
    Page 1 of 2 12 LastLast
    Results 1 to 20 of 35
    1. #1
      kilimasera's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd December 2009
      Posts : 3,047
      Rep Power : 1103
      Likes Received
      184
      Likes Given
      257

      Default Nyati amuua 'jangili' Hifadhi ya Taifa

      MWANAMUME anayesadikiwa kuwa jangili, ameuawa kwa kukanyagwakanyagwa na nyati mwenye hasira ndani ya Hifadhi ya Taifa ya Katavi baada ya kumjeruhi mnyama huyo.

      Mauaji hayo yaligundulika juzi mchana ambapo inadaiwa kuwa mtu huyo ambaye jina lake halijajulikana mara moja anayekadiriwa kuwa na umri wa kati ya miaka 40 na 45, aliingia katika hifadhi hiyo kwa lengo la kuwinda wanyama isivyo halali.

      Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Rukwa, Isuto Mantage mwindaji huyo akiwa kwenye harakati za kufanya ujangili hifadhini humo, alishambuliwa na nyati huyo kwa kukanyagwakanyagwa na kuvunjwa mbavu zote.

      “Nyati anayedaiwa mwenye hasira baada ya kujeruhiwa, alimshambulia mwindaji huyo haramu na kufa pale pale baada ya mnyama huyo kumvunja mbavu zote kwa kumkanyagakanyaga mwili mzima,” alisema Kamanda Mantage.

      Alisema, mwili wa mwindaji huyo, uligunduliwa na askari wa wanyamapori wa hifadhi hiyo waliokuwa doria maeneo hayo kutokana na alama za nyayo za mnyama huyo walizozikuta pembeni ya mwili wa mtu huyo.

      “Pia kando ya mwili wa marehemu, askari hao walikuta silaha moja aina ya gobore na risasi zake, mwili huo umehifadhiwa chumba cha maiti katika hospitali ya wilaya mjini Mpanda kwa utambuzi,” alisema Kamanda Mantage.


    2. #2
      nziriye's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 23rd January 2011
      Posts : 689
      Rep Power : 563
      Likes Received
      32
      Likes Given
      8

      Default Re: Nyati amuua 'jangili' Hifadhi ya Taifa

      ndo dawa yao hao poachers ,nadhani hali kama hii ndo inaelekea kumpata ------ ,na yeye tutamrukia na kumvunjavunja mbavu hadi aelewe kuwa dhama hizi hatuhitaji poachers c wa wanyama wa mwituni bali pia sisi binadamu ambao ni highest rank in the group of animals,big up to that buffalo and to me that is cdm.

    3. #3
      Nyati's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 6th March 2009
      Posts : 694
      Rep Power : 662
      Likes Received
      168
      Likes Given
      65

      Default Re: Nyati amuua 'jangili' Hifadhi ya Taifa

      Du wajina ana hasira sana yaani kama ni kweli inadhihirisha ile methali ya wahenga kuwa akuanzae mmalize
      Never depend on single income. Make investment to create a second source.

    4. #4
      WomanOfSubstance's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 30th May 2008
      Posts : 5,484
      Rep Power : 1686
      Likes Received
      708
      Likes Given
      721

      Default Re: Nyati amuua 'jangili' Hifadhi ya Taifa

      Quote By Nyati
      Du wajina ana hasira sana yaani kama ni kweli inadhihirisha ile methali ya wahenga kuwa akuanzae mmalize

      Na wewe una hasira kama wajina wako?

      Ila tukiangalia vizuri tutaona kuwa hawa wawindaji haramu wanajitakia hatari wenyewe.Alikuwa amejiamini sana kwenda kuwinda mahali ambapo haruhusiwi . Watu waache kabisa kuvunja sheria makusudi tena waziwazi.
      Educating the mind without educating the heart is no education at all.... Aristotle



    5. #5
      kilimasera's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd December 2009
      Posts : 3,047
      Rep Power : 1103
      Likes Received
      184
      Likes Given
      257

      Default Re: Nyati amuua 'jangili' Hifadhi ya Taifa

      kwanini hakumchapa risasi nyingine alipoona nyati ana hasira au kwanini asingepanda kwenye mti!
      Quote By WomanOfSubstance
      Na wewe una hasira kama wajina wako?

      Ila tukiangalia vizuri tutaona kuwa hawa wawindaji haramu wanajitakia hatari wenyewe.Alikuwa amejiamini sana kwenda kuwinda mahali ambapo haruhusiwi . Watu waache kabisa kuvunja sheria makusudi tena waziwazi.


    6. #6
      WomanOfSubstance's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 30th May 2008
      Posts : 5,484
      Rep Power : 1686
      Likes Received
      708
      Likes Given
      721

      Default Re: Nyati amuua 'jangili' Hifadhi ya Taifa

      Quote By kilimasera
      kwanini hakumchapa risasi nyingine alipoona nyati ana hasira au kwanini asingepanda kwenye mti!

      Killy,
      timing labda ilikuwa mbaya akapata kigugumizi cha akili - miguu ikashindwa kukimbilia mti ( labda hakujua hata kupanda mti!) na mikono ikakosa orientation ya gobole lake!
      Educating the mind without educating the heart is no education at all.... Aristotle



    7. #7
      Popompo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 9th November 2010
      Posts : 312
      Rep Power : 498
      Likes Received
      36
      Likes Given
      34

      Default Re: Nyati amuua 'jangili' Hifadhi ya Taifa

      safi sana!ila natoa pole ya dhat kwa familia iliyompoteza baba RIP mwindaji haramu

    8. #8
      IGWE's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd February 2011
      Location : Blue Plaza Building-Arusha
      Posts : 5,312
      Rep Power : 3307
      Likes Received
      1335
      Likes Given
      1240

      Default Re: Nyati amuua 'jangili' Hifadhi ya Taifa

      r.i.p ,ni katika harakati za kujikwamua na shida ambazo zingine zimesababishwa na mfumo mbaya na mbovu wa utawala....
      "We should learn to help others,not only in our prayer but also in daily life,if we cannot help them_then,the least thing we can do is to desist from harming them"

    9. #9
      Mvaa Tai's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th August 2009
      Location : Ngudu, Mwanza
      Posts : 3,631
      Rep Power : 1227
      Likes Received
      1552
      Likes Given
      1020

      Default Re: Nyati amuua 'jangili' Hifadhi ya Taifa

      Quote By nziriye
      ndo dawa yao hao poachers ,nadhani hali kama hii ndo inaelekea kumpata ------ ,na yeye tutamrukia na kumvunjavunja mbavu hadi aelewe kuwa dhama hizi hatuhitaji poachers c wa wanyama wa mwituni bali pia sisi binadamu ambao ni highest rank in the group of animals,big up to that buffalo and to me that is cdm.
      Kweli sasa nimeamini watu hawamhitaji JK maana hapa imeletwa topic ya jangili na nyati lakini na ------ kaingizwa kidogo na mchangiaji
      Haiwezekani Kabisa Twiga kupakiwa ndani ya ndege tayari kupelekwa nje ya nchi bila Polisi na Usalama wa Taifa kujua....

    10. #10
      nziriye's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 23rd January 2011
      Posts : 689
      Rep Power : 563
      Likes Received
      32
      Likes Given
      8

      Default

      Quote By Ezan
      Kweli sasa nimeamini watu hawamhitaji JK maana hapa imeletwa topic ya jangili na nyati lakini na ------ kaingizwa kidogo na mchangiaji
      Mkuu unajua simlaumu huyu poacher bt naweza nikamlaumu ------ kwa asilimia kubwa,yeye ndo alituahidi nchi ya maziwa na asali,ajira nje nje,maisha bora lakini imekuwa mbaya,we acha ajiulie kama angewin ningempongeza ila amekosea step namwona mjinga flani ,hyo ndo hasira yangu kwa ------ na hata wanadamu wengne wa tz.

    11. #11
      kilimasera's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd December 2009
      Posts : 3,047
      Rep Power : 1103
      Likes Received
      184
      Likes Given
      257

      Default Re: Nyati amuua 'jangili' Hifadhi ya Taifa

      hapo sasa kila zigo analibeba yeye kaazi kwelikweli bora muda ukimbie tufanye uchaguzi mwingine maana watu wameshaelewa maana ya upinzani ni nini
      Quote By Ezan
      Kweli sasa nimeamini watu hawamhitaji JK maana hapa imeletwa topic ya jangili na nyati lakini na ------ kaingizwa kidogo na mchangiaji

    12. #12
      Manyanza's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 4th November 2010
      Location : Look Behind You......
      Posts : 4,424
      Rep Power : 25474
      Likes Received
      1146
      Likes Given
      913

      Default Re: Nyati amuua 'jangili' Hifadhi ya Taifa

      Hard life with fake promise from JK, me nafikiri huyo marehemu alikuwa na hamu na kitoweo na hakuwa na jinsi na akiangalia bei ya nyama buchani haikamatiki. Ikabidi ajitose ndani ya mbuga mpaka mauti yalipomkuta.RIP marehemu poleni ndugu wa marehemu
      Source ya haya yote ni JK

    13. #13
      kilimasera's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd December 2009
      Posts : 3,047
      Rep Power : 1103
      Likes Received
      184
      Likes Given
      257

      Default Re: Nyati amuua 'jangili' Hifadhi ya Taifa

      sasa angewezaje kumbeba nyati mzima peke yake hapo unaweza kukuta alikua na kundi la zaidi ya watu 70 wa kumsaidia kubeba hiyo nyama
      Quote By Manyanza
      Hard life with fake promise from JK, me nafikiri huyo marehemu alikuwa na hamu na kitoweo na hakuwa na jinsi na akiangalia bei ya nyama buchani haikamatiki. Ikabidi ajitose ndani ya mbuga mpaka mauti yalipomkuta.RIP marehemu poleni ndugu wa marehemu
      Source ya haya yote ni JK

    14. #14
      Ngongo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 20th September 2008
      Location : Mlima Meru
      Posts : 4,957
      Rep Power : 6856
      Likes Received
      2403
      Likes Given
      3159

      Default Re: Nyati amuua 'jangili' Hifadhi ya Taifa

      Quote By WomanOfSubstance
      Na wewe una hasira kama wajina wako?

      Ila tukiangalia vizuri tutaona kuwa hawa wawindaji haramu wanajitakia hatari wenyewe.Alikuwa amejiamini sana kwenda kuwinda mahali ambapo haruhusiwi . Watu waache kabisa kuvunja sheria makusudi tena waziwazi.
      Mkuu unajua Gobore ukishapiga risasi inachukua muda kuweka risasi nyingine na kukoki risasi muda wote huo Nyati hakupi nafasi ya kummaliza.Pia magobore ya aiana nyingine hayakutengenezwa kwaajili ya kuua mnyama mkubwa kama Nyati sana sana yanamjeruhi tu na kumuongezea hasira.Mara nyingi wawindaji wa aina ya marehemu wanaingia porini kuwinda wanyama wadogo wadogo kwaajili ya kitowewo unajua tena maisha siku hizi yamepanda haswa nyama ya mbuzi au kuku haishikiki.

    15. #15
      kilimasera's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd December 2009
      Posts : 3,047
      Rep Power : 1103
      Likes Received
      184
      Likes Given
      257

      Default Re: Nyati amuua 'jangili' Hifadhi ya Taifa

      ni kweli na unaweza kufyatua na likagoma kuwaka likaanza kutoa moshi tu wanasema ukiona hivyo litupe chini na ukimbie maana likifyatuka zinaweza kukurudia wewe mwenyewe!
      Quote By Ngongo
      Mkuu unajua Gobore ukishapiga risasi inachukua muda kuweka risasi nyingine na kukoki risasi muda wote huo Nyati hakupi nafasi ya kummaliza.Pia magobore ya aiana nyingine hayakutengenezwa kwaajili ya kuua mnyama mkubwa kama Nyati sana sana yanamjeruhi tu na kumuongezea hasira.Mara nyingi wawindaji wa aina ya marehemu wanaingia porini kuwinda wanyama wadogo wadogo kwaajili ya kitowewo unajua tena maisha siku hizi yamepanda haswa nyama ya mbuzi au kuku haishikiki.

    16. #16
      kilimasera's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd December 2009
      Posts : 3,047
      Rep Power : 1103
      Likes Received
      184
      Likes Given
      257

      Default Re: Nyati amuua 'jangili' Hifadhi ya Taifa

      na ukimchelewa tu umekwisha
      Quote By Nyati
      Du wajina ana hasira sana yaani kama ni kweli inadhihirisha ile methali ya wahenga kuwa akuanzae mmalize

    17. #17
      chetuntu's Avatar
      R I P Array
      Join Date : 10th January 2011
      Location : Paediatrique ward
      Posts : 956
      Rep Power : 619
      Likes Received
      100
      Likes Given
      90

      Default Re: Nyati amuua 'jangili' Hifadhi ya Taifa

      Hawa majangili kuna kitu kinaitwa roda, inawezekana nyati alishanasa kwenye roda kwa hyo marehemu akaona kazi imeisha ila nyati wananguvu sana akikuotea anakufa na wewe, huwa wanamtoboa macho kwa spoko.

    18. #18
      kilimasera's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd December 2009
      Posts : 3,047
      Rep Power : 1103
      Likes Received
      184
      Likes Given
      257

      Default Re: Nyati amuua 'jangili' Hifadhi ya Taifa

      haisee hapo wanakiuka haki za wanyama kweli uanze kwa kumtoboa macho kwa spoko huo ni uonevu wa hali ya juu sana kweli majangili ni lazima wauawe popote pale
      Quote By chetuntu
      Hawa majangili kuna kitu kinaitwa roda, inawezekana nyati alishanasa kwenye roda kwa hyo marehemu akaona kazi imeisha ila nyati wananguvu sana akikuotea anakufa na wewe, huwa wanamtoboa macho kwa spoko.

    19. #19
      mams's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 19th July 2009
      Posts : 604
      Rep Power : 625
      Likes Received
      18
      Likes Given
      0

      Default Re: Nyati amuua 'jangili' Hifadhi ya Taifa

      Chondechonde huyo Nyati apelekwe haraka Ngorongoro akawalinde wale nyati waliobaki wanne wa JK.

    20. #20
      kilimasera's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd December 2009
      Posts : 3,047
      Rep Power : 1103
      Likes Received
      184
      Likes Given
      257

      Default Re: Nyati amuua 'jangili' Hifadhi ya Taifa

      wewe utambebaje nyati aliechanganyikiwa hicho si kifo man kwanza utaanza anzaje
      Quote By mams
      Chondechonde huyo Nyati apelekwe haraka Ngorongoro akawalinde wale nyati waliobaki wanne wa JK.

    Page 1 of 2 12 LastLast

    Similar Topics

    1. Replies: 64
      Last Post: 27th October 2012, 06:52
    2. Watanzania hawaruhusiwi kutembelea hifadhi ya taifa serengeti
      By issenye in forum Habari na Hoja mchanganyiko
      Replies: 24
      Last Post: 18th November 2011, 11:53
    3. Wawindaji na nyati.
      By Jaguar in forum Jokes/Utani + Udaku/Gossips
      Replies: 2
      Last Post: 23rd April 2011, 11:39
    4. Replies: 0
      Last Post: 31st December 2010, 21:22

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...