Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Ukiritimba wa Tanesco sasa kwisha

    Report Post
    Results 1 to 6 of 6
    1. #1
      Kamanda's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 5th December 2007
      Posts : 123
      Rep Power : 610
      Likes Received
      4
      Likes Given
      3

      Lightbulb Ukiritimba wa Tanesco sasa kwisha

      WAKATI gumzo kuu nchini kwa sasa ni juu ya hali mbaya ya kifedha ya Shirika la Ugavi wa Umeme Tanzania (Tanesco) mazungumzo yanaendelea kuhusu Tanesco kukodisha sehemu ya mfumo wake wa gridi ya taifa ya usambazaji umeme kwa kampuni binafsi ya kimataifa ili iusambaze katika mikoa ya kusini.

      Mkurugenzi Mkuu wa Tanesco, Dk. Idris Rashid, aliyathibitisha hayo jana na kueleza kuwa shirika hilo kwa sasa linashauriana na kampuni ya Canada ya Artumas Group Inc., kuhusu mkataba wa muda mrefu wa ukodishaji miundombinu ya usambazaji umeme.

      Chini ya makubaliano ya miaka 20 yanayojadiliwa sasa, Artumas itakodi miundombinu ya usambazaji umeme katika mikoa ya Mtwara na Lindi na kuwapatia wateja umeme.

      Hii itakuwa mara ya kwanza Tanesco inakodisha miundombinu yake kwa kiwango kikubwa hivyo tena kwa muda mrefu kwa kampuni binafsi.

      Mtwara na Lindi ni mikoa ambayo ina eneo la Kilometa za mraba 24,000 na wakaaji wapatao milioni 2.

      Taarifa kamili za ukodishaji huo bado hazijapatikana, lakini maofisa wa serikali wamesema ukodishaji huo utaisaidia kifedha Tanesco inayokabiliwa na ukata.

      Kwa sasa Tanesco ina ukiritimba wa biashara wa sekta ya umeme na lengo hilo la serikali la kuunda taasisi tatu tofauti za kufua umeme, kuusafirisha na kuusambaza bado liko mbali kutimia.

      Haijaeleweka vizuri ni lini majadiliano baina ya Tanesco na Artumas yanatarajiwa kukamilika.

      Vilevile haijafahamika kama kampuni hiyo ya kigeni ya Artumas itaweka viwango vyake vya kulipia umeme au itaendelea kutumia viwango vinavyotozwa na Tanesco vilivyoidhinishwa na Mamlaka ya Udhibiti wa Nishati na Maji (Ewura).

      Tanesco inazalisha megawati 560 za umeme nyingi zikiwa kwa nguvu ya maji na pia inanunua megawati 200 za umeme kutoka kwa wazalishaji binafsi.

    2. Miaka 50

    3. #2
      zomba's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th November 2007
      Posts : 15,822
      Rep Power : 14621
      Likes Received
      2842
      Likes Given
      1961

      Default Re: Ukiritimba wa Tanesco sasa kwisha

      Nadhani ni wazo zuri sana ila cha kutizama ni hawa artumas wapi wanapoendesha shughuli kama hizo na kama zipo zinaendaje? na wapi wamewahi kukodisha na kuendesha shughuli za umeme? Hilo ndio muhimu isije ikawa Richmond nyingine.

      Nadhani ni wazo zuri ukichukulia kuwa, hakuna shirika katika mashirika yote tuliyokuwa nayo, tuliyotaifisha na tuliyoanzisha wenyewe ambalo limenifanikiwa, mimi silijui na kama lipo basi lipo-lipo tuu kama ilivyo Tanesco. Bora tuyakodishe kwa wenye uwezo wa kuendesha shughuli hizo kuliko kung'ang'ania kitu ambacho hatukiwezi. Alimradi tu kuwe na mikataba ya wazi na itazamwe vizuri tusije tukaishia sisi tuliokodisha ndio tunawalipa waliokodisha.

      Halafu mbona kuna wazo linakuja kuwa hatuna cha kuwakodisha ila ni kausanii kamaneno tuu haka? Tunawakodisha nini? si tuseme kweli tunawaachia waendeshe shughuli hizo, sisi zimetushinda. Nadhani hapa inaonesha neno kubinafsisha linaumiza roho za watu wengi ndio maana linaanza kutumika neno kukodisha.

      Hivi Tanesco kuna nini cha kuwakodisha hawa Artumas?

    4. #3
      Ufunuo wa Yohana's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 9th October 2007
      Posts : 327
      Rep Power : 659
      Likes Received
      1
      Likes Given
      0

      Default Re: Ukiritimba wa Tanesco sasa kwisha

      Quote By kamanda
      WAKATI gumzo kuu nchini kwa sasa ni juu ya hali mbaya ya kifedha ya Shirika la Ugavi wa Umeme Tanzania (Tanesco) mazungumzo yanaendelea kuhusu Tanesco kukodisha sehemu ya mfumo wake wa gridi ya taifa ya usambazaji umeme kwa kampuni binafsi ya kimataifa ili iusambaze katika mikoa ya kusini.

      Mkurugenzi Mkuu wa Tanesco, Dk. Idris Rashid, aliyathibitisha hayo jana na kueleza kuwa shirika hilo kwa sasa linashauriana na kampuni ya Canada ya Artumas Group Inc., kuhusu mkataba wa muda mrefu wa ukodishaji miundombinu ya usambazaji umeme.

      Chini ya makubaliano ya miaka 20 yanayojadiliwa sasa, Artumas itakodi miundombinu ya usambazaji umeme katika mikoa ya Mtwara na Lindi na kuwapatia wateja umeme.

      Hii itakuwa mara ya kwanza Tanesco inakodisha miundombinu yake kwa kiwango kikubwa hivyo tena kwa muda mrefu kwa kampuni binafsi.

      Mtwara na Lindi ni mikoa ambayo ina eneo la Kilometa za mraba 24,000 na wakaaji wapatao milioni 2.

      Taarifa kamili za ukodishaji huo bado hazijapatikana, lakini maofisa wa serikali wamesema ukodishaji huo utaisaidia kifedha Tanesco inayokabiliwa na ukata.

      Kwa sasa Tanesco ina ukiritimba wa biashara wa sekta ya umeme na lengo hilo la serikali la kuunda taasisi tatu tofauti za kufua umeme, kuusafirisha na kuusambaza bado liko mbali kutimia.

      Haijaeleweka vizuri ni lini majadiliano baina ya Tanesco na Artumas yanatarajiwa kukamilika.

      Vilevile haijafahamika kama kampuni hiyo ya kigeni ya Artumas itaweka viwango vyake vya kulipia umeme au itaendelea kutumia viwango vinavyotozwa na Tanesco vilivyoidhinishwa na Mamlaka ya Udhibiti wa Nishati na Maji (Ewura).

      Tanesco inazalisha megawati 560 za umeme nyingi zikiwa kwa nguvu ya maji na pia inanunua megawati 200 za umeme kutoka kwa wazalishaji binafsi.
      Kinachotakiwa ni mkataba ambao ni wazi, na uliojadiliwa kwa kina na wadau wa sector husika. Wananchi waelimishwa juu ya mpango husika, usiingie kinyemela na kusababisha pengine maumivu mengine kwa Watanzania. Na huu mpango utakuwa mzuri tu pale ambapo bei ya umeme itapungua kwa mtumiaji na upatikanaji wake kuwafikia watu wote million 2 wa mikoa hiyo.

    5. #4
      Semanao's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 25th July 2007
      Posts : 276
      Rep Power : 660
      Likes Received
      1
      Likes Given
      0

      Default Re: Ukiritimba wa Tanesco sasa kwisha

      Quote By UFUNUO WA YOHANA
      Kinachotakiwa ni mkataba ambao ni wazi, na uliojadiliwa kwa kina na wadau wa sector husika. Wananchi waelimishwa juu ya mpango husika, usiingie kinyemela na kusababisha pengine maumivu mengine kwa Watanzania. Na huu mpango utakuwa mzuri tu pale ambapo bei ya umeme itapungua kwa mtumiaji na upatikanaji wake kuwafikia watu wote million 2 wa mikoa hiyo.
      Ni mpango mzuri kama utasaidia wananchi wengi kumudu gharama. Tatizo la tanesco ni kushindwa kukusanya madeni sababu hawana orodha kamili ya wateja. SOmetimes private company nakuwa serious sio business as usual. Sayansi na technolojia tunakoelekea kama hatuna umeme wa wananchi wengi basi tutakuwa na maendeleo ya kurudi nyuma badala ya mbele.

    6. #5
      Lusajo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 25th February 2008
      Posts : 447
      Rep Power : 663
      Likes Received
      9
      Likes Given
      1

      Default Re: Ukiritimba wa Tanesco sasa kwisha

      Yaani mimi nilivyosikia ni Kampuni ya Canada nikajua imewahi kufanya kazi sehemu zingine za dunia, kumbe inafanya kazi zake Tanzania tuu. Wahindi wengi tuu wanakaa Canada kwa hiyo ni rahisi kwa wao kuanzisha kampuni na kuiita jina lolote halafu kuchukua tenda Tanzani. Halafu ni mkataba wa miaka 20 kwa hiyo kama kampuni ni kimeo tutaisubiri mpaka miaka 20 ipite na itakuwa inaendelea kula hela tuu, kwa sababu hao watu wenyewe ambao wana saini mikataba sijui kama wana akili nzuri au ni "special". Tanesco inabidi kuwa makini sasa hivi.

    7. RukaaJuu Final

    8. #6
      Semanao's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 25th July 2007
      Posts : 276
      Rep Power : 660
      Likes Received
      1
      Likes Given
      0

      Default Re: Ukiritimba wa Tanesco sasa kwisha

      Quote By Lusajo
      Yaani mimi nilivyosikia ni Kampuni ya Canada nikajua imewahi kufanya kazi sehemu zingine za dunia, kumbe inafanya kazi zake Tanzania tuu. Wahindi wengi tuu wanakaa Canada kwa hiyo ni rahisi kwa wao kuanzisha kampuni na kuiita jina lolote halafu kuchukua tenda Tanzani. Halafu ni mkataba wa miaka 20 kwa hiyo kama kampuni ni kimeo tutaisubiri mpaka miaka 20 ipite na itakuwa inaendelea kula hela tuu, kwa sababu hao watu wenyewe ambao wana saini mikataba sijui kama wana akili nzuri au ni "special". Tanesco inabidi kuwa makini sasa hivi.
      Akili zao kama za CHENGE

    Similar Topics

    1. Tanesco tumewachoka sasa
      By mwankuga in forum Jukwaa la Siasa
      Replies: 0
      Last Post: 25th December 2010, 08:35
    2. TANESCO wamezidi sasa
      By Ally Msangi in forum Habari na Hoja mchanganyiko
      Replies: 2
      Last Post: 7th December 2010, 21:22
    3. Tanesco na ukiritimba wa luku
      By Ami in forum Business & Economic Forum
      Replies: 0
      Last Post: 8th September 2010, 15:53
    4. Orijino Comedi - Sasa Kwisha
      By Bill in forum Entertainment
      Replies: 78
      Last Post: 20th May 2009, 16:01
    5. Huu ni ukiritimba....
      By Kibunango in forum Habari na Hoja mchanganyiko
      Replies: 1
      Last Post: 7th June 2007, 23:53

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...