Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Hapa Jk Alimaanisha Nini?

    Report Post
    Results 1 to 2 of 2
    1. #1
      Augustoons's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 31st October 2007
      Posts : 409
      Rep Power : 672
      Likes Received
      3
      Likes Given
      1

      Default Hapa Jk Alimaanisha Nini?

      Akiongea na wazee wa Dar-es-salaam pamoja na mambo mengine Rais alisema
      "Ni kweli kwamba kwa muda wa wiki nzima nchi yetu na hasa siasa na uongozi wa Taifa letu vimepata mtikisiko mkubwa. Ni hali ambayo hatukuitegemea. Imetustukiza, tumefanya maamuzi ambayo hatukuyapanga na kupata matokeo ambayo hatukuyategemea"Baada ya kufuatilia mjadala Bungeni siku iliyofuata na kusikiliza hisia za watu nchini ndipo tukafikia kwenye maamuzi yale magumu na mazito tuliyofanya. Maamuzi ambayo yalipelekea kuvunjwa kwa Baraza la Mawaziri. Ni maamuzi magumu, lakini yalikuwa hayana budi kufanyika kwa maslahi ya utangamano wa taifa letu.Ni uamuzi mgumu kwa sababu unawahusu watu ambao ni wenzangu wa karibu kimaisha na kikazi kwa miaka mingi. Na pia kwa sababu unaona wazi kuwa kama mambo fulani fulani yangefanyika mambo yasingefikia kuwa yalivyo

      Nianze na sehemu hii niliyoweka mlalo.Je,matokeo ambayo hakuyatarajia ni yapi? mmh hapana kabla ya swali hilo,kipi kilimstukiza hadi akapelekea kufanya maamuzi ambayo hakuyapanga? Nimetafakari sana kauli hii na kujiuliza,ina maana ni kweli Rais hakuwa anaona upepo wowote wa uovu ndani ya baraza lake?au je,kelele zote zilizokuwa zikipigwa na miito mbalimbali kuhusu richmonduli hakuwa anazisikia au je,zilikuwa zinaingilia sikio moja na kutokea jingine?Na hayo mambo fulani fulani ambayo yangefanyika ni yapi? Nadhani kuna haja ya kumwangalia na yeye iwapo alikuwa na nafasi yoyote kwenye richmonduli.eti wadau ninyi mwaonaje?

    2. Miaka 50

    3. #2
      Pundit's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 4th February 2007
      Posts : 3,941
      Rep Power : 2640
      Likes Received
      25
      Likes Given
      0

      Default Re: Hapa Jk Alimaanisha Nini?

      Nianze na sehemu hii niliyoweka mlalo.Je,matokeo ambayo hakuyatarajia ni yapi? mmh hapana kabla ya swali hilo,kipi kilimstukiza hadi akapelekea kufanya maamuzi ambayo hakuyapanga?
      My take ni kuwa Ikulu wanataka kuonyesha kuwa kujiuzulu kwa Lowassa ni uamuzi uliofikiwa na Lowassa mwenyewe bila hata ya kumhusisha Kikwete.Hata Lowassa amelipigia mstari hili kwamba zaidi ya mke wake hakukuwa na mwingine yeyote aliyejua hili.Kilichomstukiza ni Lowassa kuomba kujiuzulu, Maamuzi ambayo hakuyapanga ni kukubali Lowassa ajiuzulu.

      Kikwete anataka kula keki yake halafu bado ibaki mezani.Anataka kumuondoa Lowassa ili kujisafisha na kupandisha imani ya wananchi juu ya serikali, lakini hapo hapo hataki kumuudhi Lowassa na watu wake.Sasa baada ya kuuma anapuliza.


      Nimetafakari sana kauli hii na kujiuliza,ina maana ni kweli Rais hakuwa anaona upepo wowote wa uovu ndani ya baraza lake?au je,kelele zote zilizokuwa zikipigwa na miito mbalimbali kuhusu richmonduli hakuwa anazisikia au je,zilikuwa zinaingilia sikio moja na kutokea jingine?Na hayo mambo fulani fulani ambayo yangefanyika ni yapi? Nadhani kuna haja ya kumwangalia na yeye iwapo alikuwa na nafasi yoyote kwenye richmonduli.eti wadau ninyi mwaonaje?
      Tatizo ni kuwa Kikwete kwa kiasi kikubwa hajali uovu ndani ya baraza na anaweza kuwa influenced kirahisi na watu wake.Kikwete anajali public opinion kwa sababu hana performance na anategemea popularity, sasa mwanzo alifikiri issue inaweza kuzimwa ndiyo maana hakujali sana, baada ya kuona issue ni kubwa na haiwezi kuzimwa akamtoa Lowassa katika zoezi zima la kujisafisha.

      Unajua kuna maneno yameongewa katika kamati yanaonyesha kuwa mradi wa Richmond ulikuwa wa "wakubwa" siyo "mkubwa" kwa hiyo siwezi kushangaa nikisikia Kikwete naye anahusika ila kamtoa mshkaji wake kafara na anamtafutia mbinu ya kumsafisha, otherwise kama Kikwete angekuwa serious kuhusu rushwa na mismanagement Lowassa asingeongea kwa kutumia TVT na wala Kikwete asingempamba kwenye hotuba na wazee wa Dar.

    4. RukaaJuu Final

    Similar Topics

    1. Nyerere alimaanisha nini kusema hivi?
      By mzambia in forum Jukwaa la Siasa
      Replies: 2
      Last Post: 15th March 2011, 17:00
    2. Unaelewa nini hapa?
      By St. Paka Mweusi in forum Jokes/Utani + Udaku/Gossips
      Replies: 37
      Last Post: 30th November 2010, 15:30
    3. Replies: 22
      Last Post: 24th November 2010, 10:53
    4. Je, Hapa ungefanya nini?
      By Konakali in forum Mahusiano, mapenzi, urafiki
      Replies: 15
      Last Post: 2nd September 2010, 19:36

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...