Dr. Slaa, asante sana kwa kunijibu, kitendo tuu cha kuonyesha umenisoma, hiyo ni faraja tosha kwangu kuwa hata kama hamtayarekebisha mapungufu, my only defence ni kuwa tuliwaambia, mesej sent.
Kwa kuanzia, nakupongeza sana wewe binafsi kugombea, umeleta changamoto ambayo haijawahi kutokea.Ushindi wa hayo majimbo mliyoyatwaa ni uthibitisho wa the powers within you. For the first time in my life, nimehamasika na naweza kutupa karata yangu mahali 2015.
Pole kwa kutopata ushindi uliotarajiwa, ila amini usiamini, wewe bado ni mshindi kwenye roho za watu, na JK ni mshindi kwenye makatasi ya kura. Tunatakiwa kuwa wa shukrani kwa kidogo chochote tunachopata, wewe mwenye majimbo 5 hadi 22 na la 23 ni kesho, ulitakiwa kuonyesha appreciation kwa Watanzania waliokuamini, kitendo cha kususia kutangazwa matokeo for whataver reasons, ni political immaturity, na binafsi nilifadhaishwa sana, umepoteza the golden opportunity ya kuspeak out you mind, hata kama hatimaye utakuja kuita waandishi na kuyasema ya moyoni, never will they have the impact kama ungejitokeza pale na kusema nimekuja siyakubali matokeo kwa sababu yamechakachuliwa.
Nakubaliana na wewe kuhusu weakneses kwenye analysis yangu, infact kitu nilichokisema hapa, its only my observation. True analysis inapatikana baada ya kufanya research, nakiri sijafanya research yoyote serious zaidi ya observation tuu, ila hili jicho langu ndilo la mwananchi wa kawaida kule kijijini na sio jicho la reseacher as a member of academia.
La kambi ya upinzani, nimelisemea, if you go by the books, it is ok kwa vile nyinyi peke yenu mnaconstitute ile quoram kwa mujibu wa kanuni, don't play by the book, just play by reality, logic and moderation. Umimi wenu Chadema, haujaanza leo, msipokubali weaknesses zenu, you can not turn them ito streghths. Naomba nisiende tena kwenye personalities zaidi, tunakuomba kaa siti ya mbele, shika usukani, pangeni safu yenu vizuri, futeni dhana zote zilizojengeka dhidi yenu ziwe za kweli au za kizushi, 2015 ikulu ni yenu, maana wale milioni 12 waliojiandikisha halafu hawakupiga kura, ndio mtaji wenu wa 2015 haswa ukizingatia vijana wa shule za kata ndio watakuwa vyuoni!.
Asante tena.
Follow Us Here