Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Kuhatarisha usalama wa Taifa? Give me a Break!

    Report Post
    Page 11 of 11 FirstFirst ... 91011
    Results 201 to 217 of 217
    1. #1
      Baija Bolobi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 25th February 2009
      Location : Bosnia
      Posts : 612
      Rep Power : 719
      Likes Received
      325
      Likes Given
      0

      Default Kuhatarisha usalama wa Taifa? Give me a Break!

      Madudu mengi na ya hatari yanayotokea katika siasa za nchi yetu yanaashiria kuwa idara yetu ya Usalama wa Taifa imefika mwisho kiutendaji. Ebu ona:-

      -Rais akamteua Chenge baada ya kuvunjwa kwa Baraza la mawaziri. Watu wakapiga kelele, yeye akakaidi. Baada ya muda mfupi akalazimika kumwondoa kwa aibu!

      -Nape na Malisa wakavutana kuhusu uongozi wa UVCCM; Rais akawatosa wote na kumchukua Masauni. Amegundulika alifoji umri, akaondoka, lakini aibu ikabaki kwa Rais. Hakuna aliyewajibishwa katika idara ya Usalama.

      -Sasa tunaambiwa Bashe si raia. Amekuwa katika nafasi nyingi ikiwamo NEC. Chiligati anasema walipitiwa tu. Wamepitiwa mangapi?

      La kujiuliza, hivi tuna ile Idara ya Usalama wa Taifa au sasa ni Idara ya Uhasama wa Taifa? Kinachoonekana kujengeka sasa ni kuwa uhasama katika mahusiano ya watawala ni mkubwa sana. Leteni maoni ya nini mwisho wa uhasama huu.

      Kwa wasiojua majukumu ya taasisi hii wa-download attachment hii:


      Quote By KAPONGO
      Kazi ya Usalama wa Taifa pia imegawika katika mafungu haya:
      1. Kulinda Viongozi Wakuu- Rais, Makamu wa Rais, Waziri Mkuu, na Viongozi wa staafu wa ngazi hizo, (pamoja na kulinda viongozi wakuu wa UWT km mkurugenzi wake mkuu).
      2. Kukusanya taarifa za usalama kwa lengo la kujua mood ya wananchi kuhusiana na kila tukio linalotokea ama lisilotokea nchini ili kuiwezesha serikali kufanya maamuzi sahihi, na mara zote kulinda maslahi ya taifa.
      3. Kutafuta intelligensia kutoka nje ya mipaka zenye kuiwezesha nchi kujua siri za ndani za nchi nyingine, rafiki ama shindani, ama hasimu, ili ziweze kuisaidia kufikia maamuzi sahihi (informed decisions) kuhusiana na mambo mbalimbali ya kitaifa na kimataifa.
      Quote By Derimto
      Kufanya mauaji ni sehemu ya kazi ya TISS na idara yoyote ile ya kijasusi katika nchi mbalimbali ila haiwi wazi inaweza kufanyika kwa kuwekewa sumu ambayo mtu anaweza kufa hapohapo au baada ya siku tatu au hata zaidi kutegemea na aina ya sumu na kiwango chake na pia kuna ajali ya gari ambayo inaweza kuonekana kama ya kawaida kabisa au ya kusababishwa na aina ya hila yoyote ile kama ilivyotokea kwa Diana ionekane alikuwa anawakimbia wapiga picha na kuna ambayo wengi wamezoea ambayo ni ya kumfuata mlengwa na kumpiga risasi mahali popote nyumbani kwake, kwenye mkutano au sehemu yoyote inapopatikana nafasi hiyo.

      Ni kweli kuwa kazi ya usalama wa Taifa ni kulinda masilahi ya Taifa lakini na raia wakeila kuna nyakati huwa ni kwaajili ya kulinda wakubwa wachache au serikali husika na masilahi yake na hapa inaweza kufikia hata kuua kiongozi mkubwa na mwandamizi au hata kundi la watu kwa mfano aliyekua waziri mkuu wa Israel Yitzak Rabin huyu alipigwa risasi na ikasemekana ni raia ila ukweli ulivyo yule hakuwa raia wa kawaida alikuwa alinda kile ambacho Waisrael wanakiamini siku zote na PM. Yeyote anapochukua nchi ile anatakiwa akifuate akikiuka siyo mwenzao tena atatolewa kafara kwa namna yoyote ile kuhakikisha Israel inabaki kuwa ilivyo kama wanavyoamini wayahudi na ni wakatili mawako tayari kuona mwarabu anapata anachokitaka okay basi tufanye hivi kule midle east kuna waarabu kibao tena ambao ni wazaliwa Israel kwa nini asitumwe kwenda kufanya yale mauaji lakini yakafanywa na myahudi mwenzake? Angalia wengine kama Rafik Harir wa Syria, na hata marehemu Kombe aliuawa na Polisi wakimtuhumu kuwa ni Jambazi pamoja na kuwa alijitambulisha kuwa yeye ni nani!

      Ngoja nikupe mfano mwingine ambao huu utawachanganya wengi na wavivu wa kusoma na kuchunguza tutawaacha mbali sana WTC huko New York ambapo walikufa zaidi ya watu 3000 na kuwasingizia magaidi na kuzua vita ambavyo vimedhulumu maisha ya wanyonge wengi bila kujali aina ya dini kabila au hata utaifa maana walikufa wamarekani na waisilamu wa Iraq na kwingineko duniani na hata kumnyonga Sadam na hali ikawa mbaya Iraq kuliko alivyokuwepo Sadam Hussein na pia kubadilisha mambo mengi duniani ikiwemo kuvujiana heshima na kutuhumiana ugaidi kwa kumpima mtu kwa itikadi yake tu na hata kumdhalilisha

      Ni matumain yangu humu JF. Kuna wakandarasi ambao wanaweza kutoa ufafanuzi wa jinsi gorofa linaweza kujengwa namna gani halafu ligongwe na ndege lishuke kama ice cream juani na kuwa vumbi na wanahabari watoe picha ambazo nyingi zinafanana na hasa ukizingatia kwa wenzetu suala TEKNOHAMA wako mbali wana vyombo vingi vya kudugundua mambo mengi HEBU WANAJF.TUSIWE WATU WA MALUMBANO MENGI HUMU NDANI TUPATE MUDA WA KUSOMA NA KUCHUNGUZA MAMBO KWA KINA UTANIELEWA NASEMA NINI HAYA NINAYOYANGEA HUMU

      ANGALIZO: Hapa simaanishi magaidi hawapo laa ila magaidi wapo na wanafanya kazi zao na wengine kibao tunao hata hapa kwetu tena wanajishikamanisha vizuri sana wakubwa wa serikali zetu kwa kuifadhili na kutoa michango mbalimbali kwenye serikali na jamii kwa ujumla na ukijidai kuwafuatilia yaweza kukuta makubwa maana baadhi ya wakubwa wana masilahi yao huko.

      Hivyo basi moja ya kazi ya idara yoyote ya ujajusi ni kufanya ujasusi na project za siri katika nchi mbalimbali tatizo ni kuwa hapa kwetu na baadhi ya nchi nyingi zinatumia vibaya Idara hizo badala ya kujiletea maendeleo kama Nchi za urusi na Asia na hivyo sehemu kubwa kuishia kulinda kundi la watu wachache na madaraka yao maana hao ndiyo wenye uwezo wa kumpoint mkurugenzi na wengine katika kazi nyeti za serikali iliyoko madarakani.

      Idara hii ina watu wengi sana tena wengine hawathaminiki katika jamii kabisa na wanafanya kazi kizalendo zaidi na kutanguliza masilahi ya Taifa mbele lakini wanakwamishwa na urasimu na kutokuchukuliwa hatua kwa wahusika (watu hatarishi wa usalama) na ikumbukwe kuwa idara hizi kwenye nchi nyingi huingia maeneo mengi sana mbalimbali unaweza kumkuta waziri,Mchungaji, sheikhe, mhadhiri,mwana habari, mfagiaji, dereva wa dalala au tax, fundi viatu, mwalimu, padre,mwanamuziki, makahaba na kwa hapa Dsm. Hata muuza samaki (pweza) kwenye sinia anaweza akawa na akafanya kazi kwa ufanisi mzuri kabisa ila mwana usalama wa kweli hana na habebi bango la kujitangaza waziwazi kuwa yeye ni mwana usalama na ndiyo maana ukimwona mtu anajigamba sana ujue huyo ni feki na ana masilahi yake binafsi ukiacha wale ambao wanafanya kazi za wazi za kuwalinda viongozi Top5 kingine kazi ya kukamata wahalifu mara nyingi huwa ni kazi ya polisi na kama kuna ofisa usalam akitaka kukamata anaweza kukamata kama raia mwingine yeyote kulingana na sheria za nchi MZISOME! raia anaweza kumkamata mhalifu ila ikiwa ni lazima sana kwa mwanausalama kufanya hivyo kimabavu anaweza kufanya hivyo akishirikiana na polisi na vyombo vingine vya dola kama vile PCCB, Uhamiaji, TFDA, Jeshi nk. TENA IKUMBUKWE KUWA OFISA WA IDARA YA USALAMA WA TAIFA HAKAMATI MVUTA BANGI MARA NYINGI ATAKUWA RAFIKI YAKE ILI AWEZE KUJUA BANGI INALIMWA WAPI NA KUPELEKWA KUUZWA WAPI HAWAKURUPUKI TU. Lakini sio mbwembwe ambazo watu wengi wanapenda kujionyesha nazo kuwa wao ni wana usalama na kuwakera wengine.

      Kwa kwa kuongezea ni kuwa hakuna jambo lolote la hasara na aibu ambalo linaipata nchi hii ambalo vyombo husika na Rais mwenyewe hana Taarifa nalo kila kitu kinajulikana na kutolewa ufanunuzi na hasra zake LAKINI KIKUBWA NI KWAMBA HUPUZWA KWANI WASIKA WENGI HUWA NI MASWAIHIBA WA RAIS AU WAZIRI MHUSIKA NA HATA VIONGOZI WAANDAMIZI Na ndiyo maana mara nyingi Rais anashindwa kuchukua maamuzi magumu maana yanaweza kumgusa yeye mwaneyewe au yalianzia kwake mwenyewe. Lakini idara ina heshima zake na kukusanya taarifa mbalimbali za kiulinzi na usalama na hata kiuchumi lakini hazitiliwi maanani zinawekwa kapuni na kama unabisha mtafute rafiki yako yeyote wa karibu muulize kiundani kama hawahui mambo yanyoendela nchi hii lakini hana namna ya kufanya.

      OMBI NA TAHADHARI:
      IDARA HII ISIBEZWE NA KULAUMIWA KWA KUWABEBA WANASIASA NA KUTOKUFANYA KAZI YAKE IPASAVYO NI KWA SABABU YA MFUMO WENYEWE ULIVYO KAMA NDANI YA JESHI NA IKUBUKWE KWA WALE WALIOPITIA HOJA ZANGU ZA MWANZO NILIONYESHA JINSI WANAVYOTOA KAZI KUANZIA NATIONAL SERVICE KWA MAANA HIYO IDARA HII NI PARAMILITARY NA KUNA CHAN OF COMMAND AMBAYO KILA MTU ANAIFUTA KULINGA NA ORDER ALIYOPEWA NA AMIRI JESHI MKUU WA MAJESHI NI RAIS MWENYEWE WA JMT.

      ILA NA WAO WAMECHOKA NA UOVO UNAOENDELEA SERIKALINI MPAKA HUKO KWENYE MAJESHI NA HII NI HATARI SANA INAWEZA KUJA KULETA MACHUFUKO SIKU ZA USONI KAMA IVORY COAST NA KWINGINEKO MAANA HAWANA UHAKIKA NA MAISHA YAO YA BAADAYE YA WATOTO WAO NA NDUGU ZAO MAANA KILA KITU KIZURI NA CHENYE MASILAHI KIMESHIKWA NA WAKUBWA NA WAJANJA WACHACHE.
      jmushi1, luck, MpigaKelele and 5 others like this.
      HERI KUFIA MAWAZO YANAYOISHI KULIKO KUISHI KWA MAWAZO YALIYOKUFA.

    2. FemaTV & Radio

    3. #201
      Ndinani's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th August 2010
      Posts : 2,947
      Rep Power : 1531
      Likes Received
      745
      Likes Given
      237

      Default re: Hivi Usalama wa Taifa ni Haki ya Serikali au ni Haki ya Umma?

      Ili kuirudisha taasisi hii kwenye kazi /hadhi yake ya kulinda mali za nchi na watu wake kutoka kwa maadui wa ndani na nje ya nchi, kuna umuhimu wa kuiangalia upya sheria iliyounda UWT [TISS] with special emphasis ya majuku yake na jinsi mkuu wa taasisi hii anavyopatikana.

      Hivi sasa mkuu wa hii taasisi anateuliwa na Rais kwa vigezo visivyoeleweka wazi wazi na mara nyingi the basisi of appointment ni nepotism ili akiwa kazini alinde maslahi ya yule aliyemteua hivyo basi kubadili mfumo wa uteuzi unaweza kusaidia kuirudishia intergrity ya TISS.
      DSN likes this.

    4. DSN
      #202
      DSN's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 1st April 2011
      Location : Home Tanzania
      Posts : 1,443
      Rep Power : 4452
      Likes Received
      690
      Likes Given
      576

      Default re: Hivi Usalama wa Taifa ni Haki ya Serikali au ni Haki ya Umma?

      Quote By uwemba1
      Kwa nionavyo mimi, ww ni mmoja Wao ila umekuja kujaribu kuona tunawaonaje coz JFK ni kioo sana Kifupi ni kuwa u r nothing good for citizen wa kawaida but a threat kama vile nyie ndio wa kwanza kuwapora haki zao ktk uchaguzi, kusaidia wezi wa raslimali zetu kama wale twiga, kusaidia wauzaji unga ambao wanatuua kwa madawa hayo huku mkitumia kodi zetu. Kinauma sana kwa usaliti wenu
      Mkuu uwemba mjenga nchi ni mwananchi mwenyewe na mbomoa nchi ni mwananchi mwenyewe,wewe unavyoona kwa mtizamo wako sikuzuii kwa kuwa siwezi kuingia ndani ya mawazo na kuyatoa huko unakoyapeleka ila thread yangu ilitaka kukushirikisha kama mwanajf [Great thinker] ndani ya Jamii Forum a place where people dare to talk openly for the good of the country and better for all.

      Ila wewe umekataa kwa kutanguliza hisia na kuinyima haki yake nafasi yako ya kuwa great thinker kutafakari na kuchambua maswali ya thread hii kama walivyofanya wanajf ambao ni great thinker either wako Positive or Negative lakini hawakutazama kumzungumzia mtu binafsi bali issues za taasisi umma kama zilivyowakilisha, kwa nia njema ya kujenga kwa kuwa UTAKI UNATAKA NI LAZIMA IWEPO NA ITAENDELEA KUWEPO TAASISI HIYO KWA FAIDA YA UMMA.

      Cha msingi ni sisi kupima na kukubaliana kama umma kuwa JE tunalidhika na utendaji wake na umma wote uwe na mtizamo chanya [Positive] na si hasi [Negative] kama ulio nao wewe.Niko/tupo kama wanajf hapa kama walivyo wengine humu kwa kusudio la kujenga siko/hatuko hapa kubomoa?Wewe hapa uko upande gani?Na kwa taarifa raia yoyote halali wa United Republic of Tanzania ni Mwanausalama wa Taifa lake!!!

      Watu wa fani ya biashara za masoko [Marketers] wanasema hivi kama mteja/mwananchi [customer] akihudumiwa vizuri na kuondoka na bidhaa/huduma [Product or Service] akiwa AMELIZIKA [SATISFIED] basi mteja huyo atasambaza taarifa kwa WATU WENGINE WATATU atakaokutana nao kwamba bidhaa/huduma ile aliyonunua ni NZURI na BORA kwa matumizi husika.Lakini kama mteja huyo huyo akiondoka na bidhaa akiwa HAKULIZIKA [NOT SATISFIED] basi atawaambia WATU WENGINE TISA kuwa bidhaa/huduma ile SI BORA/HAIFAI.Accusation zako hazijengi kwa mwendo wako huo!!tunaitaji constructive idea kutibu sio kubomoa.

    5. #203
      Kasimba G's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 19th January 2011
      Location : Dar es Salaam
      Posts : 852
      Rep Power : 593
      Likes Received
      252
      Likes Given
      265

      Default re: Hivi Usalama wa Taifa ni Haki ya Serikali au ni Haki ya Umma?

      Unajua TISS wengine wanafikiri watu hawajui majukumu yaTISS, Tanzania ni kanchi kadooo saana TZ, watu wanajua majukumu ya CIA, KGB,MOSAD na mashirika makubwa mengine ya kijasusi, TISS kwa vyovyote wameiga huko!Sasa visemina vya wanaTISS wanaambiwa labda! Watanzania wengine hawaju majukumuya TISS, Watu wanafahamu na wanawaangalia mnavyochemsha!

      Kwa taarifa yako TISS number 1 sio Rais ila ni akili kamili ya mtu binafsi(Mwenye akili kamili), ninavyosema kamili ni utashi wa mtu mwenye akili nyingialiyekamilika! Hujui hilo? Mawazo kama haya ndio yana haribu utendaji wa TISS,Tunajua TISS wanafikili wao ndio, wanatakiwa kuweka Rais, Kuchaguwa mawazir,kuchagulia watu wabungei on which wanaweka watu wasio na uwezo, kwa kuwa TISS 1yao haiko okay!

      jinsi ilivyo kwa utashi kamili na akili zetu kamili i mean TISS 1, mnadanganywa kuwa watu hawafahamu, ukiclaim utaamini, ila ukiwa na TISS1 Kichwani utaelewa kitu ninacho kisema,

    6. #204
      Masabaja's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 4th March 2012
      Posts : 139
      Rep Power : 391
      Likes Received
      18
      Likes Given
      13

      Default re: Hivi Usalama wa Taifa ni Haki ya Serikali au ni Haki ya Umma?

      Kwa kweli ndugu zangu mmenigusa kwenye jambo moja la msingi ambalo nimekuwa nikijiuliza kila siku, hivi hii idara ina muhimu gani kwa taifa letu kwa
      sasa fuatilia vizuri wizi wa pesa EPA,DEEP GREEN FINANCE,MEREMETA,RICHMOND na madudu mengine mengi baadhi ya maafisa wa idara hii wanausika moja kwa moja, kuna wizi wa mizigo bandarini wanahusika na ndiyo wanatumika. Haiwezekani matukio makubwa ya wizi na mikataba feki ifanyike bila baraka zao utaweza ni mpaka uwe mtu wao. Ikifika mahali rais anasema haijui kagoda kampuni iliyoiba pesa BOT halafu unasema una usalama wa taifa ni bora kuifuta taasisi hii isiendelee kutumia hela ya walipa kodi yetu bure hawatusaidii chochote wizi mtupu.

    7. DSN
      #205
      DSN's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 1st April 2011
      Location : Home Tanzania
      Posts : 1,443
      Rep Power : 4452
      Likes Received
      690
      Likes Given
      576

      Default re: Hivi Usalama wa Taifa ni Haki ya Serikali au ni Haki ya Umma?

      Quote By Kasimba G
      Unajua TISS wengine wanafikiri watu hawajui majukumu yaTISS, Tanzania ni kanchi kadooo saana TZ, watu wanajua majukumu ya CIA, KGB,MOSAD na mashirika makubwa mengine ya kijasusi, TISS kwa vyovyote wameiga huko!Sasa visemina vya wanaTISS wanaambiwa labda! Watanzania wengine hawaju majukumuya TISS, Watu wanafahamu na wanawaangalia mnavyochemsha!

      Kwa taarifa yako TISS number 1 sio Rais ila ni akili kamili ya mtu binafsi(Mwenye akili kamili), ninavyosema kamili ni utashi wa mtu mwenye akili nyingialiyekamilika! Hujui hilo? Mawazo kama haya ndio yana haribu utendaji wa TISS,Tunajua TISS wanafikili wao ndio, wanatakiwa kuweka Rais, Kuchaguwa mawazir,kuchagulia watu wabungei on which wanaweka watu wasio na uwezo, kwa kuwa TISS 1yao haiko okay!

      jinsi ilivyo kwa utashi kamili na akili zetu kamili i mean TISS 1, mnadanganywa kuwa watu hawafahamu, ukiclaim utaamini, ila ukiwa na TISS1 Kichwani utaelewa kitu ninacho kisema,
      Tunajua wenzenu wanavyoshabikia vyombo vyao katika kulinda mali zao na Taifa lao kwa ujumla na kuliweka Taifa lao kwenye ramani ya Duniani,uwezi kuwa raia wa Marekani mwenye upeo wa wastani asijue CIA iko kwa kazi gani na ndio maana wako tayri kuitetea popote pale nani na nje ya mipaka yao.Vivyo hivyo Waisrael na MOSAD nao kwa nguvu ile ile ya sawa ya wamarekani wananchi wanajengwa kuthamini nguvu na uwezo wa vyombo vyao vya umma kuwapa msaada wa kuwa wanajua dhahili mashirika hayo yako kwa faida ya Taifa lao.Je sisi watanzania kwanini tujijenge kweye sura hasi [negative] kifanyike nini nasi kila anaezaliwa ndani ya Tanzania anakuwa mzalendo wa Taifa lake kwa kuwa mwishi wa yote kila ria ni Mwanausalama wa Taifa lake kadri ninavyoamini mimi kwa upeo wangu.

    8. Miaka 50

    9. #206
      Kibunago's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th January 2008
      Location : MWANZA
      Posts : 286
      Rep Power : 637
      Likes Received
      84
      Likes Given
      23

      Default re: Hivi Usalama wa Taifa ni Haki ya Serikali au ni Haki ya Umma?

      Ninaelewa nchi nyingi ambazo ili ufanyiwe vetting kuwa katika Shirika / Taasisi ya Usalama wa Taifa si tu kuwa wewe ni Mwaminifu na Mzalendo kwelikweli bali lazima uwe na AKILI MAONO NA PIA AKILI NYINGI (uwezo wa kutambua, kuhisi na kushughulikia mambo kwa ufanisi zaidi kuliko binadamu wengine wa kawaida).

      Sasa kila aliye TISS sasa anayenisoma hapa ajipime hapo na aseme na roho yake kama anafaa kuwa humo!!

      Idara hii ni ya muhimu sana na niseme bado inafanya kazi nzuri lakini ingetakuwa kuwa inafanya zaidi ya hapo kwa sababu ajira ya baadhi ya walioko humo hawana hizo sifa zinazotakiwa au wamekiuka na kukosa uzalendo.

      Hata kama wewe ni mkubwa wangu ukinipa amri ambayo inakiuka uzalendo na maendeleo ya Mtanzania niko tayari kukukatalia na huwezi nifanya chochote! Kiapo chao na cha Mabosi wao wote hatimaye ni kuilinda na kuitetea KATIBA YA NCHI. Sasa nionyeshe ambapo Katiba inasema kuwa kuna bosi wako (haijalishi ana rank gani )ambaye yuko juu ya Katiba?

      Tuwasaidie ili TISS iweze kuwa na mabadiliko, iwe ya kisasa na yenye ufanisi zaidi. Na zaidi ya yote wapewe meno ya kungáta !!! sio kuchunguza tu na kuripoti!
      Ogah and DSN like this.
      Have you ever wondered which hurts the most: saying something and wishing you had not, or saying nothing, and wishing you had?

    10. #207
      KULWA MAKONO's Avatar
      Junior Member Array
      Join Date : 11th March 2012
      Posts : 5
      Rep Power : 364
      Likes Received
      0
      Likes Given
      3

      Default re: Hivi Usalama wa Taifa ni Haki ya Serikali au ni Haki ya Umma?

      Usalama wa Taifa kokote duniani ni jukumu la kila raia na sio serikali

    11. #208
      K.Msese's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 1st April 2012
      Posts : 238
      Rep Power : 407
      Likes Received
      145
      Likes Given
      219

      Default re: Hivi Usalama wa Taifa ni Haki ya Serikali au ni Haki ya Umma?

      1: Je Usalama wa Taifa ni haki ya Serikali au ni Haki ya Umma?
      JIBU- Usalama wa taifa ni haki ya umma unaoratibiwa na kuongozwa na serikali kwa niaba ya umma.

      2: Je raia wa kawaida wa Tanzania kujua taarifa za msingi kuhusu kazi [Basic Information] ya usalama wa Taifa lake ni kosa?
      JIBU - Sio kosa kwa raia kujua kazi za usalama wa taifa, ambayo ni kulinda na kusimamia usalama wa nchi nje na ndani ya mipaka ya nchi.


      3: Je nini objectives and role za Usalama wa Taifa kwa Serikali inayokuwa Madarakani?
      JIBU; Usalama wa taifa upo blank katika role zilizo nje ya kulinda na kusimamia usalama wa nchi, lakini utatekeleza role inayopewa na serikali kwa niaba ya umma, na hapa ndiyo serikali iliyopo madarakani huchukua fursa ya kutumia TISS kujiwekea mizizi.

      4: Je nini objective and role za Usalama wa Taifa kwa Wananchi yani Umma wa Watanzania.
      JIBU: Ni kuwahakikishia usalama umma wa watanzania sasa na baadaye.


      5: Je majukumu na kazi za Usalama wa Taifa zinapaswa kuogopwa [Tisha] Wananchi au zinapaswa kuheshimiwa na hata kusaidiwa na raia wema [wazalendo] kama njia sahihi ya kulinda Taifa na mali zake?
      JIBU; Sheria iliyopo inayounda usalama wa taifa haina direct link kati ya raia na idara hii, kwani sheria hii inadhani rai anaweza kuwasilisha anachoona hatarishi kwa idara nyingine kama polisi n.k
      ! Yes, kwa raia na asiye raia inamlazimu aiogope idara hii endapo atashiriki kutoa siri za nchi, atahatarisha usalama wa nchi au/na viongozi wakuu wa nchi, kufanya jinai ambazo zinafuatiliwa na idara hii, tofauti na uvunjifu wa hivyo idara hiyo haipaswi kuogopwa.

      #CIA kwa marekani ni kitengo cha kijasusi kinacho linda na ktafuta masilahi yao nje ya nchi, mbali ya kulinda usalama wa nchi yao. Wanayo FBI na idara yao ya usalama pia. Kuna Mi5 na Mi6 in UK, mbali na inteligncy agncy dept nchini mwao.
      -Ndiyo maana nimeshauri kuwa badala ya TISS kunyooshewa kidole kwa kufanya shughuli wasizo tarajiwa na umma, au kutofanya majukumu yaliyo tarajiwa na umma, ni vyema turekebishe kwanza sheria inayoiunda idara yenyewe.
      -Nafikiri katika muundo wa katiba, tupendekeze Tiss iundwe na kitengo cha biashara na sheria za kimataifa, propaganda na masoko, halafu na usalama wa nchi kwa maana ya ulinzi. Katika idara ya propaganda Tiss iweke Contacts zake na baadhi ya shughuli zao kwa wananchi via websites n.k!

      Kibanga Msese
      Kasimba G and DSN like this.

    12. #209
      MKALIMOTTO's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 7th April 2012
      Posts : 136
      Rep Power : 386
      Likes Received
      9
      Likes Given
      8

      Default re: Hivi Usalama wa Taifa ni Haki ya Serikali au ni Haki ya Umma?

      Ninapofuatilia mada hii, nakumbuka usemi usemao ukicheka na nyani utavuna mabua na mchelea mwana hulia mwenyewe. Hivi ndugu zangu watanzania wenzangu, mimi binafsi sioni hata sababu ya kukichokonoa saaaaaaaaaana chombo hiki mhimu sana kwa usalama wa nchi yetu.

      Ni kweli kuwa huenda wapo wachache wa members wake ambao siyo diligent, hii haimaanishi kuwa chombo kizima ni rotten! Bado usalama wa taifa ndicho chombo pekee kinachosimamia mstakabali wa taifa hili. Wengi wetu hatujui majukumu yao na pengine ndiyo maana hata tunadodosa weeeeee, eti kwa kulinganisha na intelligenge agency ya Kenya!

      Tukumbuke kuwa kila nchi ina mfumo wake wa kuendesha shughuli za kijasusi na si kwambwa kwasababu wakenya wameainisha majukumu ya intelligence agency yao kwa uwazi basi na Tanzania ifanye hivyo, hapana. Ninashauri kuwa tuchezee vitu na idara zote lakini hii hebu tuiache ieendelee na kazi zake. Huu ndiyo moyo wa nchi yoyote ile duniani, tunapokichezea chombo hiki tunachezea hatima ya taifa letu.

      Ndugu zangu hebu tuwe na uzalendo, tuwaamini hawa jamaa kuwa hawalali usiku kucha kwaajili yetu. Mimi kitaaluma ni mwalimu lakini nina ndugu rafiki yangu anayefanya kazi TISS, ninajua namna jamaa anavyokuwa busy na kazi kiasi hata familia yake hakai nayo muda mwingi. Kiukweli jamaa wanapiga kazi jamani.
      K.Msese likes this.

    13. #210
      Bongolander's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 10th July 2007
      Location : Tandale
      Posts : 4,034
      Rep Power : 1417
      Likes Received
      610
      Likes Given
      44

      Default Re: Hivi Usalama wa Taifa ni Haki ya Serikali au ni Haki ya Umma?

      Quote By DSN
      Tunajua wenzenu wanavyoshabikia vyombo vyao katika kulinda mali zao na Taifa lao kwa ujumla na kuliweka Taifa lao kwenye ramani ya Duniani,uwezi kuwa raia wa Marekani mwenye upeo wa wastani asijue CIA iko kwa kazi gani na ndio maana wako tayri kuitetea popote pale nani na nje ya mipaka yao.Vivyo hivyo Waisrael na MOSAD nao kwa nguvu ile ile ya sawa ya wamarekani wananchi wanajengwa kuthamini nguvu na uwezo wa vyombo vyao vya umma kuwapa msaada wa kuwa wanajua dhahili mashirika hayo yako kwa faida ya Taifa lao.Je sisi watanzania kwanini tujijenge kweye sura hasi [negative] kifanyike nini nasi kila anaezaliwa ndani ya Tanzania anakuwa mzalendo wa Taifa lake kwa kuwa mwishi wa yote kila ria ni Mwanausalama wa Taifa lake kadri ninavyoamini mimi kwa upeo wangu.
      Mkuu kama unakumbuka mabadiliko aliyofanya Mkapa, alifanya decision making zote kuhusu operation ya issue kubwa za nchi zinafanywa na political establishment, wao TISS ni kutekeleza tu yale wanayoambiwa na politicians. Kama kweli TISS wangekuwa wanafanya utekekelezaji wenyewe mambo yasingekuwa kama yalivyo sasa, wako kama aylivyo kwa sababu sio TISS wanafanya hivyo. TISS wanaripoti kwa TISS 1 yaani Rais na yeye ndiye anayewateua kwenye nyadhifa mbalimbali, na sio kuwa Rais anaripoti kwa TISS.

      Sasa ni kipindi amcho TISS ina opportunity kubwa ya kujenga imani yake kwa watanzania, lakini haiwezi kufanya hivyo kwa kuwa ya sasa imegawanyika mara mbili au tatu, (Tiss-Mwang'onda, Tiss Kitine na Tiss Othmam) nayo iko very politicised, sio ile iliyokuwa inafahamika, iliyokuwa inafanya kazi ya usalama wa taifa. sasa hivi majibu mpaka yanafanya hata uhalifu karibu na Tiss HQ. au hata ndani ya HQ kwenyewe zamani ujinga huo haukuwepo.

    14. #211
      Bisek's Avatar
      Member Array
      Join Date : 2nd April 2012
      Posts : 71
      Rep Power : 374
      Likes Received
      10
      Likes Given
      3

      Default Ni nini hasa kazi ya Usalama wa Taifa?

      Naomba kujua jaman...maana tangu nizaliwe nachosikia na ninachokijua ni kuwa TISS inahusika zaidi na
      1.Kuiba kura halali za wananchi hasa wakati wa uchaguzi wa wabunge na rais na kuzipachika kwa CCM wakishirikiana na tume ya wachakachuaji(tume ya uchaguzi

      2.Kupeleleza taarifa za siri kutoka kwa viongozi wa kisiasa mf.kuweka vinasa sauti kwenye hoteli zao

      3.Kupanga na kutekeleza mauaji ya viongozi wanaokosoa serikali mf kombe,kolimba nk

      4.Kuuhadaa umma wa watanzania kuwa viongozi wanaoshukiwa na makosa makubwa ya jinai wamefariki mfano Balali,Dito

      Naomba kujua kama hizi ndio kazi zao msingi na wanatumia kodi zetu kuzitekeleza na zipo kwa mujibu wa sheria,kama sio hizi,basi kazi zao hasa ni nini?

    15. #212
      MAMA POROJO's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 22nd November 2007
      Posts : 4,858
      Rep Power : 1843
      Likes Received
      592
      Likes Given
      413

      Default Re: Ni nini hasa kazi ya Usalama wa Taifa?

      pole kwa ulimbukeni wako na kutokujua kwako majukumu ya chombo hicho.... hakuna hata moja kati ya hayo ni jukumu lake. Soma sheria ya TISS ya 1996 inapatikana kwenye mtandao.

      hali yote hii imekutokea kwa sababu ya uwezo wako wa kuelewa mabo na kuchanganua bila kushirisha siasa kwenye mambo makuu ya kitaifa
      Ndumbayeye likes this.

    16. #213
      SJUMAA26's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 25th January 2012
      Posts : 327
      Rep Power : 623
      Likes Received
      69
      Likes Given
      2

      Default Re: Ni nini hasa kazi ya Usalama wa Taifa?

      Quote By MAMA POROJO
      pole kwa ulimbukeni wako na kutokujua kwako majukumu ya chombo hicho.... hakuna hata moja kati ya hayo ni jukumu lake. Soma sheria ya TISS ya 1966 inapatikana kwenye mtandao
      Hii sheria bado iko valid kweli even after 46 years? Labda tu cha kumkumbusha mtoa mada ni kuwa kazi kubwa ya Idara ya Usalama wa Taifa ni KUHAKIKISHA TAIFA LIKO SALAMA. Baaaaasi!!!!!!!!
      MAMA POROJO likes this.

    17. #214
      MAMA POROJO's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 22nd November 2007
      Posts : 4,858
      Rep Power : 1843
      Likes Received
      592
      Likes Given
      413

      Default Re: Ni nini hasa kazi ya Usalama wa Taifa?

      Quote By SJUMAA26
      Hii sheria bado iko valid kweli even after 46 years? Labda tu cha kumkumbusha mtoa mada ni kuwa kazi kubwa ya Idara ya Usalama wa Taifa ni KUHAKIKISHA TAIFA LIKO SALAMA. Baaaaasi!!!!!!!!

      sheria ya 1996 sio 1966 .

    18. #215
      thinktank's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 11th March 2008
      Posts : 132
      Rep Power : 598
      Likes Received
      6
      Likes Given
      4

      Default Re: Ni nini hasa kazi ya Usalama wa Taifa?

      Kazi ya usalama wa taifa ni usalama wa taifa, maswali mengine bhana.

    19. #216
      Sumba-Wanga's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 2nd February 2011
      Location : Gambushi
      Posts : 4,000
      Rep Power : 1221
      Likes Received
      776
      Likes Given
      680

      Default Re: Hivi Usalama wa Taifa ni Haki ya Serikali au ni Haki ya Umma?

      Mkuu nimekuunga mkono. Lakini, kama utasoma sheria iya kuunda TISS, utaona ni jinsi gari rais amepewa madaraka makubwa katika kuteua na kusimamia utendaji wa idara hiyo.

      Sasa kama rais akichagua shoga yake kuongoza idara hiyo, unategemea atampinga? Si ndio maana TISS wanaaacha majukumu yao ya msingi na kuanza kushughulika na mgomo wa madaktari na CHADEMA!

      Jamani, piganieni mabadiliko ya sheria ya kuunda TISS.

    20. #217
      Sumba-Wanga's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 2nd February 2011
      Location : Gambushi
      Posts : 4,000
      Rep Power : 1221
      Likes Received
      776
      Likes Given
      680

      Default Re: Ni nini hasa kazi ya Usalama wa Taifa?

      Quote By thinktank
      Kazi ya usalama wa taifa ni usalama wa taifa, maswali mengine bhana.
      What do you mean ny usalama wa Taifa????
      "A man's or woman's best or worst choice in life is his or her spouse"

    Page 11 of 11 FirstFirst ... 91011

    Similar Topics

    1. Replies: 78
      Last Post: 12th April 2012, 08:10
    2. Nyerere give us a break...Tshs 4 Millions cannot build 2 classrooms..........
      By Rutashubanyuma in forum Jukwaa la Elimu (Education Forum)
      Replies: 2
      Last Post: 12th December 2010, 19:08
    3. Kuhatarisha usalama wa Taifa? Give me a Break!
      By Mtanzania in forum Jamii Intelligence
      Replies: 8
      Last Post: 30th September 2007, 09:03

    User Tag List

    Tags for this Topic

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...